Dubai tumesaini nao mikataba ya maendeleo zaidi ya 30. Watanzania wanaopenda Maendeleo tumieni fursa alizotuletea Rais Samia

Fursa tunazo waTanzania wenyewe.
Hakuna mtu mwingine yeyote toka nje atakayetuletea maendeleo hapa.

Huku ni kukosa akili kichwani.
Nakusikitikia sana. Hivi hizo fursa ulizonazo utaendelea bila kuingiza kipato cha kutoka nje?

Hebu rundika pesa zako nyunbani, usitoke nje ya nyumba wslsmudikaribishe wageni kufanya kazi au biashara na wewe, uone kama pesa zako zitaongezeka au zitakwisha.

Dunia nzima, hata nchi zilizoendelea duniani zinashindana kutafuta wawekezaji kutoka nje, unawaona wote hao wajinga?

Tanzania kwa watu wenye fikra kama zako, tuna safari ndefu sana ya kwenda.

Sasa naelewa kwanini Wakenya hawana mali asili kama sisi lakini wanatupiga bao kiuchumi.

Hakika hizo shule mlienda kusomea ujinga.
 
Hiyo hatujawahi kuiona, hatuna comments..

Huu wenyewe uko wazi, Kila mtu kauona. Ni mkataba wa hovyo, mbaya, wa kijinga na hautufai sisi Watanganyika..

Pelekeni takataka hiyo kwenu Zanzibar..!

Ujinga wenu ni mmoja tu. Kuuweka nyeti zenu wazi..

Laiti mngefanya kimya kimya tu, tungehisi maumivu kwa matokeo yake tu..

Lakini mmetuonesha ujinga wenu halafu tuwaache kimya kimya tu???

No way!!!
 
Hebu tutajie hizo hasara na faida ? ili watu wajinga wazijue toa darasa kidogo

wewe ni mtumwa wa mawazo yako mwenyewe
 
Mbona sikuhizi unakosea sana kuandika? Kulikoni? Au akaunti imedukuliwa nini
 
Na amejtahidi kuuweka uwazi lakini hofu tu ya baadhi ya watu muhimu kuboresha vipengele vyenye utata.
Kuna watu walikuwa na hofu kama hii wakati hayati Mkapa alivyoleta FDI za SA lakini nyingi zinafanya vizuri mpaka leo

Tunangoja bahari ikauke
 
Jisikitikie mwenyewe na huyo unayemtumikia anayelazimisha tuwe watega bakuli kwa kila kitu.

Mtu kama wewe mwenye akili iliyoishia kutegemea wengine, hata huwezi kutambua kwamba sijasema kuwa wawekezaji wote hatuwataki.
Ni wawekezaji matapeli na wanaotafuta kudhalilisha nchi zetu ndio tusiowataka.

Wawekezaji, hata hao wanaotafuta kuvuna kwa manufaa yao na yetu ni msaada tu wa kuunga juhudi zetu za kujiletea maendeleo.
Hatuwezi kuacha nchi yetu ije ijengwe na watu toka nje

Hakuna nchi yoyote duniani iliyotegemea watu waje wailetee mandeleo, wao wamebaki wanatembeza tu midomo kama mnavyofanya nyinyi.

Mwambie huyo mama afanye kazi na wananchi wake, asipoteze muda wote akishughulika na uwekezaji wenye masharti ya kutudhalilisha.
 
Why Dubai??
 
Mbona mmekazana "wa hovyo" lakini mkiambiwa onesheni huo uhovyo uko kifungu kipi, hamsemi?


Mimi nakwambiani mkataba mzuri sana na unajijibu wenyewe maswali yote. Usidanganywe na wajinga wachache wasioitakia mema Tanzania ya mama Samia. Kwa chuki tu za agenda zao siri.


Upitie. Mkataba hapa👇🏾 halafu tuambie nini cha hovyo. Bofya chini hapo 👇🏾

 
Weka nakala halisi ya mkataba, siyo hiyo tafsiri yako.
 
Why Dubai??
Dubai ni jiji la connections za uwekezaji mkubwa duniani kwa sasa.

Hivi dunia ya leo ni nani asiyetaka kufanya biashara na kitovu cha biashara duniani?

Dubai ndiyo nchi yenye mkusanyiko mkubwa wa wawekezaji kutoja kila pembe ya dunia. Ukiwekeza na mwekezaji tajiri mmoja wa Dubai ujuwe umewekeza na dunia.
 
Niliona habari moja inasema Dubai na Tanzania wamesaini MOU kuhusu misitu. Kwa hiyo hadi misitu tutegemee Dubai??
 
Weka nakala halisi ya mkataba, siyo hiyo tafsiri yako.
Weka wewe wako ulionao kama unaona waangu siyo sahihi. Unangoja nini? Upinge wewe ushahidi nikupe mimi?


Hakika shule mlienda kusomea ujinga.
 
NBC ipo?, CRDB, migodi?
 
Niliona habari moja inasema Dubai na Tanzania wamesaini MOU kuhusu misitu. Kwa hiyo hadi misitu tutegemee Dubai??
Ndugu yangu kitu usichokielewa ni kuwa suala la kulinda mazingira duniani ni jukumu la kila mtu lipo chini ya UNEP, makao makuu ya UNEP yapo Nairobi, Kenya. Tanzania na Dubai zote ni wadau wa kulinda mazingira. Na nchi zinazozalisha kaboni kwa wingi duniani zimekubaliana zilinde misitu ya duniani. Sasa kama mama kaweza kuwa convince adilimua yao ya ulibdaji misitu ya dubia waulete Tanzanua, tatizo. Liko wapi? Mbona nchi nyingi zinafanya hivyo?

Halafu huelewi kuwa katika Uislam kulinda mazingira ni ibada.


Umewahi wenda dubai?






Soma zaidi kuhusu UNEP: unep full form headquarters - Google Suche
 

Attachments

  • 1687377443194.png
    15 KB · Views: 4
Maswali ya msingi ukiulizwq unakimbia nakuuliza moja la mwisho

Je dubai wanakuja kusaidia Tanzania au kujenga maslai yao kiuwekezaji?

Kwa akili yako unahisi Dubai wanahangaikia ya kwao au ya kwetu?
 
Na amejtahidi kuuweka uwazi lakini hofu tu ya baadhi ya watu muhimu kuboresha vipengele vyenye utata.
Kuna watu walikuwa na hofu kama hii wakati hayati Mkapa alivyoleta FDI za SA lakini nyingi zinafanya vizuri mpaka leo
Vipi kuhusu net group solution aliowaingiza Kwa mtutu wa bunduki Tanesco? Walikuja wakakusanya madeni ya Tanesco wakakata umeme mpaka kwenye mawizara ya serikali. Walipomaliza kukusanya pesa kazi ikawashinda wakarudi kwao
Kwa kifupi watanzania mabwege ndo maana mnaowachagua hawa waogopi wanafanya watakavyo
 
Wewe hukulazimishwa kuzitumia fursa, lakini usije kusema hukuambiwa. Au serikali haikuleta fursa.


Hivi kiwanda cha kuuunda sindano za Kushonea nguo kiko wapi vileTanzania? Kumbuka siulizii za kushonea viatu kwa mkono.

Unafahamu kuwa hilo jina lako "kalamu" limetokea ndani ya Qur'an?


Sikio la kufa halisikii dawa.
 
Maswali ya msingi ukiulizwq unakimbia nakuuliza moja la mwisho

Je dubai wanakuja kusaidia Tanzania au kujenga maslai yao kiuwekezaji?

Kwa akili yako unahisi Dubai wanahangaikia ya kwao au ya kwetu?
Sijawahi kukimbia swali. Labda sijaliona au umeuliza maswali mengi kwa pamoja. Naamini kuwa aulizae ataka kujuwa, mpaka nimeweka uzi miaka sasa wa yeyote kuniuliza swali lilote. Ntakuwekea link chini hapo.


Umeukiza maswali mawili. Siyo moja kama ulivyosema. Ssi kitu, majibu:

1) Mikataba iliyoingiwa ni ya ushiriano kimaendeleo na uwekezaji. Siyo uwekezaji wa Dubai tu kuwekeza Tanzania bali pia kwa Tanzania kuwekeza Duba tunakaribishwa na runawakaribisha. Mbona kuna Watanzania wengi tu wamewekeza Dubai.

2) Kwa "akili" yangu hakuna anaehangaika. Dubai ni wafanya biashara kubwa kubwa duniani na ndogo ndogo pia, hakuna biashara ya halali wasiyoifanya kwao. Fikiri, ikiws kazi yao kubwa ni biashara yao kwanini iwe kuhangaiska?


Kama wameziona fursa za biashara Tanzania na mitaji wanayo mimi naona hiyo nayo ni fursa kwetu, au wewe unsmaonaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…