Dunia yashangazwa na kubadilika ghafla kwa Rais Samia kutoka kuwa mtenda haki na kuanza uonevu

Dunia yashangazwa na kubadilika ghafla kwa Rais Samia kutoka kuwa mtenda haki na kuanza uonevu

Dunia ipi iliyostaarabika? Ile ambayo raia wake weusi wanauwawa kama mbwa na polisi wazungu huku hakuna hatua ya maana iliyochukuliwa ili kukomesha mambo hayo yasiendelee kutokea au unazungumzia dunia ipi?
Naweza sema wew ni mpumbavu. Samahani kama utaelewa vibaya
 
Nchi haimshindi KATU.....

Haikumshinda Hayati kipenzi chetu JPM kupelekea Mh.Mbowe kuishi DUBAI..... pamoja na ninyi KUMSHAMBULIA VYA KUTOSHA bado wengi wa WALALAHOI wanamkumbuka mpaka sasa.....

Serikali ni mfumo.....

Pamoja na yote....mh.Kagame bado yupo.....

Pamoja na yote.....mh.Museveni bado yupo.....

CCM si Sawa na CHADEMA....endeleeni KUJIOTESHA NDOTO MPENDAZO


#NchiKwanza
#AmaniKwanza
#JMTKwanza
#PundaAfeMzigoUfike
#KaziInaendelea
Hakuna mtu timamu aliyemkubali jiwe. Lazima uwe mjinga au masikini usiyejielewa ndipo ungeweza kumwelewa jiwe.
 
Hakuna mtu timamu aliyemkubali jiwe. Lazima uwe mjinga au masikini usiyejielewa ndipo ungeweza kumwelewa jiwe.
Vigezo gani au Instruments gania zinatumika katika kumtambua mtu aambaye ni timamu na asiye kuwa timamu?
 
Kinachonisikitisha, huyu mama alikuwa na nafasi ya kipekee ya kupendwa na kukong'a nyoyo za watanzania.
Alitakiwa afanye mambo. matatu tu

1. Kuachana na pia kurekebisha mambo ya kijingajinga ya mtangulizi wake

2. Kuyafanyia kazi mazuri ya mtangulizi wake ikiwemo miradi mikubwa

3. Kufanya reforms za msingi za kiuchumi na kisiasa ili yale yaliyojitokeza kwa mwendazake yasijitokeze tena

Sasa unfortunately kaanza kukumbatia hata yale ya kijinga ya mwendazake kama kuonea, kutoheshimu katiba na kiapo alichokula.

Asipobadilika, wananchi watamchukia vibaya sana!
Uwezo wao wa akili ni mdogo
 
Kinachonisikitisha, huyu mama alikuwa na nafasi ya kipekee ya kupendwa na kukong'a nyoyo za watanzania.
Alitakiwa afanye mambo. matatu tu

1. Kuachana na pia kurekebisha mambo ya kijingajinga ya mtangulizi wake

2. Kuyafanyia kazi mazuri ya mtangulizi wake ikiwemo miradi mikubwa

3. Kufanya reforms za msingi za kiuchumi na kisiasa ili yale yaliyojitokeza kwa mwendazake yasijitokeze tena

Sasa unfortunately kaanza kukumbatia hata yale ya kijinga ya mwendazake kama kuonea, kutoheshimu katiba na kiapo alichokula.

Asipobadilika, wananchi watamchukia vibaya sana!
Uwezo wao wa akili ni mdogo
Vigezo gani au Instruments gania zinatumika katika kumtambua mtu aambaye ni timamu na asiye kuwa timamu?
Kigezo ni kumkubali kichaa aliyeenda zake
 
Nimegundua hawa jamaa wanaelewa kila kitu kinachoendelea nchi hii.

Ukiacha hili la Mbowe,huyo Prof. anajua mpaka habari ya hizi tozo za laini za simu na wanasema kabisa ni za kututia watanzania umasikini.

Tuko uchi!
Dunia ya leo, nchi za dunia ya tatu lolote ufanyalo wanaliona, inakuwa unajidanganya kwa kuuficha uso wakati mwili wote uko wazi. Tozo ni wizi wa kuhamisha hela za watu kwa nguvu kuzipeleka hazina. Weka tozo kwenye umiliki wa simcard, hata sh 100000 kwa mwaka, uko sahihi, kuna wenye pesa wanamiliki zaidi ya line 3. Hela inayotumwa ni pato ambalo tayari limekatwa kodi, kuweka tozo ni unyang'anyi wa kidola.
 
Kama kweli n watenda haki Waaanze na kwao pia Waaanze kuangalia uchafu uliofanyika Zimbabwe, Uganda Juz apa Rwanda huko ndo wanapotezwa kabisa Burundi ndo kabisa hawasikiki Kenya apo wasaniii tu misri pale wamenyongwa wote hao mabeberu wanaangalia Tanzania tu
 
Kuwaeliminate Wasaliti wote unamaanisha nini? Kuwaua???
Yes. Kwasababu hawako jwa ajili ya maslahi ya nchi. Wao ni vibaraka tu wa wazungu. Kwa maneno mengi ni opener au Keys wa milango yao ya kutuibia.

Mzungu hawezi kukusaidia wewe kama hakuna maslahi. Kama unajidanganya hivyo basi endelea.

Kwao kuna demokrasia gani?

Ulimwengu wana siasa hawana chao. Wanasiasa wako kwa ajili ya Investors.
 
Aisee ndugu yangu...., kumbuka hata Mugabe-Zimbabwe alikuwa anazungumza propaganda na maneno kama haya unayosema......haya ndugu yangu, sie watazamaji tu......
Tutapambana na mabeberu mpaka tone la mwisho la damu,hawatuwezi
 
Kelele za CHURA hazimzuii TEMBO kunywa maji.....

Hiyo CNN na hiyo DUNIA imeshaongea sana kuhusu RWANDA....Mh.Kagame bado yupo.....M7 yupo....

CNN hawajapewa kibali cha KUWAAMULIA WENGINE WAISHI VIPI.....

TANZANIA IS A SOVEREIGN COUNTRY ,WE AS THE PEOPLE KNOW MUCH ABOUT OURSELVES THAN FOREIGNERS

#KaziIendelee
#NchiKwanza
#AmaniKwanza
Sovereign country kwa nchi inayotegemea donors zaidi ya 30% ya budget, dumping place ya bidhaa zao unaweza nini huna mitaji,technologia wala wataalam lazima wakubane tuu
 
Sidhani kama mama SSH ana 'ma- informer' wazuri wa kumpa taarifa, inaonekana bado 'amezungukwa' na wale wa mwendazake!

Atambue kuwa wapo kwa ajili ya kumwangusha ili 2025 asiweze kabisa kuteuliwa. Akina mwigulu na ndugai ambao sio watu wenye ushawishi ktk siasa za Tz wanaongea maneno ya kumporomosha mama SSH bila yeye kujua. Muda ni mwalimu mzuri sana atakuja kugundua hilo na itakuwa too late.
 
Watanzania tunapaswa kuwa makini kwani kila kiongozi huwa ana
Huyo Mbowe ana nia ya kuleta vurugu nchi hii.Huwezi kuvitisha vyombo vya dola kisha ubaki wewe ndiye mshindi.
Hii ni serikali siyo muvi ya kihindi eti mtu kama Mbowe anajipa u starring
Kipaumbele chake.

Hivyo Mh.Mbowe asubili hadi siku sera ya katiba mpya itakuwepo kwenye ilani ya uchaguzi ndo atauliza kama inafanyiwa kazi.

Huu siyo wakati wake, anataka kuwachanganya watanzania na sera zake ambazo haziko specific na periodic.

Na chakushangaza watanzania tunaendelea kujazwa sumu na nchi za nje wakati na wao wana shida ambazo zinazidi hata gaya yetu.

Take care.
 
Sovereign country kwa nchi inayotegemea donors zaidi ya 30% ya budget, dumping place ya bidhaa zao unaweza nini huna mitaji,technologia wala wataalam lazima wakubane tuu
Kuwa mwanamme. Usidanganyike wala kuogopeshwa na hela zao. Technology hata wewe unaweza kuipata. Ninkujiamini tu na kike unachokifanya.
 
She is Magufuli wannabe!

Ndiyo maana mtaani raia hawamuelewi kabisa na hizi series za makosa yake anayoyafanya.
Mtaa gani unaousemea? huku mtaani mbona mambo shwari tu?

Shida yenu CDM ni kutaka kuwin sympathy za watu wa nje,badala ya kupambana mpate sympathy ya wananchi wa Tanzania ambao kimsingi ndo waamuzi wa hatima yenu.Kwa kufanya hivyo mnaonekana kama chama cha vibaraka.
 
Mtaa gani unaousemea? huku mtaani mbona mambo shwari tu?

Shida yenu CDM ni kutaka kuwin sympathy za watu wa nje,badala ya kupambana mpate sympathy ya wananchi wa Tanzania ambao kimsingi ndo waamuzi wa hatima yenu.Kwa kufanya hivyo mnaonekana kama chama cha vibaraka.
Wewe unadhani watu lazima wafanye mivuruguvurugu ndo ujue wamekasirishwa na jambo
Watanzania siyo watu wa mivurugu lakini wakikasirshwa wanazungumza, wanasema wanatoa rai
Sasa kama wewe ni kiongozi mbabe unaweza kuamua kupuuza, lakini hii haimaanishi kuwa raia hawasemi
 
Back
Top Bottom