Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

UnaweZa kutusaidia Katika haya mkuu:

Lini watanganyika Walisema hayo.

Watanganyika wangapi kwa takwimu Zipi.

Na Walisema hayo kwa hoja zipi.

Kumbuka matumizi ya Neno "fact" Katika majibu yako, be consistent na Neno hii;

Sent from my iPhone using JamiiForums
Mchambuzi mimi hapo ndipo ninapowashangaa hawa watu na haya matamko yao...angalau Tume hata kama hukubaliani na mapendekezo yake lakini fact ni kwamba ilizunguka nchi nzima ikikusanya maoni ya wananchi bila kuwabagua watoa maoni kwa kabila, nasaba, itikadi, dini, rangi, jinsia wala umri.

Lakini pia zaidi ya theluthi ya waliopitisha rasimu ya Chenge/Sitta walichaguliwa na mtu moja, Raisi, na waliobaki walichaguliwa na Watanzania 5,000,000 katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kati ya 20,000,000 waliojiandikisha kupiga kura (sawa na asilimia 25%)...hii pia ni fact.

Hata hivyo linaloshangaza zaidi ni kwamba tukiacha walioteuliwa na Raisi (walikuwa 201) kwa kazi ya kupitia, kuboresha na kupitisha rasimu kama ilivyopendekezwa na tume, waliobaki hakuna hata moja aliyetumwa na wanachi specifically kufanya kazi hiyo na hii pia ni fact.

Sasa anapotokea mtu na akili zake timamu anabeza mapendekezo ya Tume huku akitetea uhuni uliofanyika ndani ya hilo Bunge Maalum La Katiba likiongozwa na watu ambao kulingana na matendo yao hawafai hata kusimama mbele ya Umma, huo ni ulimbukeni.

Mtu haitambui Tanganyika lakini hapo hapo anadai Watanganyika hawahiitaji Tanganyika, je hao Watanganyika wasioitaka Tanganyika aliongea nao lini na wapi? Does this really make sense? Halafu anathubutu kulibatiza hilo dai lake kwamba ni fact! Akipewa ukweli anadai katukanwa! Shame shame shame!
 
Mkuu Mag3 , hao wengine wanasema sisi ni Watanzania.
Well, wana maana Watanganyika na wazanzibar ni Watanzania.That's ok

Ukiwauliza kama ni hivyo kwanini tuwe na Tanzania na Zanzibar? Hawana jibu
Wanatuambia Tanzania ni muungano wa nchi ya Tanzania bara kama wasemavyo akina(Mkandara, Happy feet, Mtanganyika)

Ukiwauliza kama Tanzania ni zao la Tanganyika na Zanzibar, nini kimeua Tanganyika na kuwa Tanzania ambayo znz ipo? Hawana jibu.

Ukiwauliza, ni vipi unaweza kutenga mambo ya Tanzania yenye Tanganyika kama znz inavyoweza kutenga mambo ya Tanzania na ya znz. Hakuna jibu.

Ukiwauliza kwanini Tanzania itumiwe na znz na znz isiwajibike kwa Tanzania, hawana jibu.

Ukisoma maoni yao kama ninavyomsoma Mtanganyika(kada) na Kobello, ni wazi wanataka jina Tanzania kwasababu ni tamu, linatamakika vizuri katika lahaja na lafudhi kadha wa kadha. Hawana political au economic justification.

Wakati huo huo hawawezi kutetea mfumo wa Tanzania ambao Mtanganyika amegeuzwa jalala la matatizo ya wznz.

Hatuwezi kuwa na fiscal autonomy bila ya kuwa na Tanganyika.
Na kama tumeamua kuwa Watanzania, uzanzibar unatoka wapi tena ukiwa na fiscal autonomy yake?

Labda niwakumbushe Watanganyika jambo moja. Akiwa BBC, Pinda anasema, IPTL imelitia doa taifa, wahisani wameondoa misaada. Well, uzembe huo ataulipia Mtanganyika.

Wakati huo huo mzanzibar ana 4.5 ya chochote kile kitakachopataikana Tanganyika kwa jina la Tanzania.
Sasa hapa tunaambiwa 4.5% ni pesa za misaada.
Sijui @mkandara anaweza kuja hapa na kutuonyesha jinsi misaada hiyo itakavyoiathiri znz? Maana 4.5 yao ipo tu.

Hoja kubwa ni kuwa kiuchumi, znz imekuwa mzigo mzito sana kwa Mtanganyika.

Na Mtanganyika anabeba mzigo huo kwa jina la Tanzania.
Hata watetezi wa Tanzania wanajua ukweli huo ingawaje wanalazimika kujitoa ufahamu.
Suala ni kuwa uvumilivu huu wa Watanganyika ni hadi lini?

Kwanini tubebe muungano wenyewe kwa gharama zetu, tubebe gharama za SMZ na kisha tuwape mafao ya binus kwa kuwa katika muungano?
Bonus ni hizi:
Ulinzi na usalama bureee
Mambo ya ndani na nje , buree
Bajeti ya SMZ, kutoka hazina ya Watanganyika
Elimu ya juu, bureee
Mishahara ya SMZ, kutoka hazina ya Tanganyika kwa jina la Tanzania
Kazi za wabunge wao, ni mzigo wa Mtanganyika kwao ni buree
Ajira zao 21 halafu waje kuchukua 79% ya Watanganyika kwa jina la Tanzania.
Ardhi ya Tanganyika ni ya Tanzania, ya znz ni ya znz
n.k.

Tukifika hapa tunauliza, huu uvumilivu utaendelea hadi lini?

Je, watu hawaoni hatari ya Watanganyika kuamka siku moja na kusema, wznz rejeeni kwenu tumechoka tena katika vurugu?

Hili kweli linahitaji diploma kujua? Nani asiyejua ni bomu linalosubiri muda?

Mkuu Mag3 , don't give up, wapo wanaosoma na kuelewa unachosema. Uki give up hawa wasio na hoja watapoteza kizazi chetu.
Ni vema kuwaonyesha vijana ubabaishaji kuliko kuacha waambiwe kuna nchi inaitwa Tanzania bara.

Na wala wasidharauliwe hawa wapotoshaji, fikiria kuwa mtu anaweza kuandika bila aibu, haya au chembe ya soni kuwa kuna taifa lililowahi kuwepo linaitwa Tanzania bara, huyu ni hatari kuliko asiyejua. Huyu keshajitoa ufahamu na akikabidhiwa mkoba wowote atabeba. Wme determine kweli kweli.

Masikini ya mungu, leo tuna nchi inaitwa Tanzania bara! Eeeh mola tunusuru! manani tuokoe na utuongoe ili nasi tukinusuru kizazi chako kinachofundishwa nchi ya Tanzania bara iliwahi kuwepo duniani. Mwenyezi! tusaidie yarabi!
 
Nguruvi, unarudia rudia argument za gharama over and over wakati tangu mwanzo niliweza kuweka side by side matumizi ya serikali ya Zanzibar na Tanzania, nikakwambia kwamba argument ya gharama haina sababu the cost is insignificant na hata ufanye IF analysis yoyote huwezi kuwa na significant cost.

Nimekwambia kwamba from security standpoint benefit outperform the cost. Na hapa ndio wengi hawapendi kupazungumzia lakini that is a fact.
 
Akina Kobello Wanachojaribu kufanya ni kuhalalisha uhuni wa kisiasa. Mwisho wa siku watakuja na hoja Kwamba katiba ya JMT 1977 ni katiba halali. Hii ni kwa sababu muda sio mrefu umma utagundua Kwamba hakuna katiba mpya, Bali katiba ya 1977 iliyopakwa wanja.

Kuna haja ya kuwaweka akina Kobello, Mtanganyika, Mkandara, MwanaDiwani sawa mapema Kabla hawajazidi potosha umma, huku Wengine Kama akina chama, zomba, ZeMarcopolo wakiwa wamesha salimu amri siku nyingi.

Kama nilivyosema, Katiba inayopendekezwa, hii sio katiba mpya Bali ni katiba ya 1977 iliyofanyiwa cosmetics za Hapa na pale kwani nguzo kuu za katiba ya 1977 zilikuwa ni Mfumo wa chama kimoja na Mfumo wa serikali Mbili. Haya yote hayajabadilika, kwani Mfumo wa chama kimoja umebadilika only in theory, kwani in practice, tunaona jinsi gani CCM inaendelea kuongoza nchi Kama vile we are still living in the party- state era. Na Mfumo wa muungano Kama ilivyo dhahiri, mfumo ni ule ule iliyofeli kwa miaka zaidi ya 50 sasa.

Katika historia ya taifa letu, hatujawahi kuwa na bunge la katiba ambalo ni genuine. EMT na Wengine wameeleza Hili kwa mapana. Kwa mfano katiba ya 1962 iliyozaa jamhuri ya tanganyika, katiba hii ilitungwa by the then or "existing National Assembly". Bunge lile likajibadilisha na kuwa bunge la katiba, yani likapitisha Sheria ya kuligeuza kuwa la katiba kisha likaketi na kuandika katiba mpya ya jamhuri ya Tanganyika. Hapa tukumbuke Kwamba bunge lile la "katiba" la mwaka 1962 lilipata mamlaka yake ya kisheria kutoka kwenye Sheria zilizopitishwa na bunge la jamhuri ya Tanganyika, bunge ambalo lilipata mamlaka yake kutoka kwenye Sheria ya kawaida iliyopitishwa na bunge la "Uingereza".

Katiba ya JMT 1977 je? Katiba hii ilipitishwa na bunge la katiba ambalo liliundwa mwaka huo huo ndani ya masaa machache kwa kufanya Yale Yale ya 1962 - kugeuza wabunge wa jamhuri kuwa wajumbe wa bunge la katiba. Hapa tukumbuke Kwamba rais nyerere alipewa mamlaka ya kuita bunge la katiba na mkataba wa muungano (1964), mkataba ambao inasemekana ulipitishwa na mabunge ya pande zote Mbili za muungano as stipulated ndani ya mkataba ule, ingawa kwa Zanzibar, bado hapakuwa na bunge la wananchi, kwahiyo waliopitisha mkataba huo kwa upande wa Zanzibar walikuwa ni wajumbe wa baraza la mapinduzi.

Kwahiyo kwa katiba mpya ya 1977, Kama alivyofanya kwa katiba ya 1962, mwalimu nyerere aliita wabunge wa bunge la JMT na akawateua hapo hapo kuwa wajumbe we bunge la katiba. Hoja ya msingi Hapa ni Kwamba - kwa katiba mpya ya 1962 kuhusu jamhuri mpya ya Tangayika na kwa katiba mpya ya 1977 kuhusu jamhuri ya muungano wa Tanzania, rais nyerere aligeuza wabunge wa mabunge husika kuwa wajumbe wa bunge la katiba. Hii ilikuwa ni Kinyume cha utaratibu.

Pia ni muhimu tukasema Kwamba katiba ya mwaka 1977 ilikiuka mkataba wa muungano (1964), kwani the legal foundations of the union ni articles of the union, hili halikwepeki. Lakini pia, mkataba wa muungano haukuwahi kupigiwa kura ya maoni na wananchi, hivyo kuleta kila justifications za wananchi kuamua Kama wanautaka muungano au hapana, na Kama wanautaka, uwe ni wa aina gani.

Pia katiba ya JMT 1977 haikuwahi kupigiwa kura na wananchi. Kilichotokea ni viongozi wa jamhuri Mbili huru kutia Saini Nyaraka za muungano, na baadae Kamati ya chama cha siasa (CCM), sat and drafted the constitution. Na Ndio maana ilipotokea kwa Mara ya kwanza fursa ya kujadili katiba, matokeo yake ikawa ni kuchafuka kwa Hali ya hewa ya kisiasa 1983-84. Rasimu ya Chenge ni Katiba Ile Ile mbovu ya mwaka 1977, lakini sasa CCM inaitafutia uhalali kwa Mara ya kwanza. Kitendo cha wananchi kuipa uhalali katiba hii maana yake ni kukubali sasa Kwamba historia, hadhi, mamlaka na utambulisho wa Tanganyika na hata Zanzibar sasa ni halali kuchakachuliwa, Tena kwa Mujibu wa Sheria, na ole wao watakaothubutu Kuhoji Hilo baada ya hapo.

Kulazimisha rasimu ya Chenge kuwa Ndio katiba mpya ya JMT kwa kusingizia Kwamba uhalali wake umetokana na wananchi, huku ni kutengeneza mazingira ya kuchafuka kwa Hali ya hewa kisiasa Tena kwa kiwango ambacho hakijapata tokea. Hii ni kwa sababu, wananchi, hasa wa Tanganyika wanaweza wakaingizwa Mjini na CCM kupitia kura ya maoni lakini muda sio mrefu watakuja kuyaona haya tunayojadili humu. Wakati huo ukifika, Watu aina ya kina Kobello, hawa hawatapata Madhara yoyote kwani wameshakana uraia wao humu na kusema Kwamba Hawana mpango Tena wa kuishi Katika upande huu wa dunia, upande ambao wapo busy kuuangamiza kupitia vitufe vyao vya computer.



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Akina Kobello Wanachojaribu kufanya ni kuhalalisha uhuni wa kisiasa. Mwisho wa siku watakuja na hoja Kwamba katiba ya JMT 1977 ni katiba halali. Hii ni kwa sababu muda sio mrefu umma utagundua Kwamba hakuna katiba mpya, Bali katiba ya 1977 iliyopakwa wanja.

Kuna haja ya kuwaweka akina Kobello, Mtanganyika, Mkandara, MwanaDiwani sawa mapema Kabla hawajazidi potosha umma, huku Wengine Kama akina chama, zomba, ZeMarcopolo wakiwa wamesha salimu amri siku nyingi.

Kama nilivyosema, Katiba inayopendekezwa, hii sio katiba mpya Bali ni katiba ya 1977 iliyofanyiwa cosmetics za Hapa na pale kwani nguzo kuu za katiba ya 1977 zilikuwa ni Mfumo wa chama kimoja na Mfumo wa serikali Mbili. Haya yote hayajabadilika, kwani Mfumo wa chama kimoja umebadilika only in theory, kwani in practice, tunaona jinsi gani CCM inaendelea kuongoza nchi Kama vile we are still living in the party- state era. Na Mfumo wa muungano Kama ilivyo dhahiri, mfumo ni ule ule iliyofeli kwa miaka zaidi ya 50 sasa.

Katika historia ya taifa letu, hatujawahi kuwa na bunge la katiba ambalo ni genuine. EMT na Wengine wameeleza Hili kwa mapana. Kwa mfano katiba ya 1962 iliyozaa jamhuri ya tanganyika, katiba hii ilitungwa by the then or "existing National Assembly". Bunge lile likajibadilisha na kuwa bunge la katiba, yani likapitisha Sheria ya kuligeuza kuwa la katiba kisha likaketi na kuandika katiba mpya ya jamhuri ya Tanganyika. Hapa tukumbuke Kwamba bunge lile la "katiba" la mwaka 1962 lilipata mamlaka yake ya kisheria kutoka kwenye Sheria zilizopitishwa na bunge la jamhuri ya Tanganyika, bunge ambalo lilipata mamlaka yake kutoka kwenye Sheria ya kawaida iliyopitishwa na bunge la "Uingereza".

Katiba ya JMT 1977 je? Katiba hii ilipitishwa na bunge la katiba ambalo liliundwa mwaka huo huo ndani ya masaa machache kwa kufanya Yale Yale ya 1962 - kugeuza wabunge wa jamhuri kuwa wajumbe wa bunge la katiba. Hapa tukumbuke Kwamba rais nyerere alipewa mamlaka ya kuita bunge la katiba na mkataba wa muungano (1964), mkataba ambao inasemekana ulipitishwa na mabunge ya pande zote Mbili za muungano as stipulated ndani ya mkataba ule, ingawa kwa Zanzibar, bado hapakuwa na bunge la wananchi, kwahiyo waliopitisha mkataba huo kwa upande wa Zanzibar walikuwa ni wajumbe wa baraza la mapinduzi.

Kwahiyo kwa katiba mpya ya 1977, Kama alivyofanya kwa katiba ya 1962, mwalimu nyerere aliita wabunge wa bunge la JMT na akawateua hapo hapo kuwa wajumbe we bunge la katiba. Hoja ya msingi Hapa ni Kwamba - kwa katiba mpya ya 1962 kuhusu jamhuri mpya ya Tangayika na kwa katiba mpya ya 1977 kuhusu jamhuri ya muungano wa Tanzania, rais nyerere aligeuza wabunge wa mabunge husika kuwa wajumbe wa bunge la katiba. Hii ilikuwa ni Kinyume cha utaratibu.

Pia ni muhimu tukasema Kwamba katiba ya mwaka 1977 ilikiuka mkataba wa muungano (1964), kwani the legal foundations of the union ni articles of the union, hili halikwepeki. Lakini pia, mkataba wa muungano haukuwahi kupigiwa kura ya maoni na wananchi, hivyo kuleta kila justifications za wananchi kuamua Kama wanautaka muungano au hapana, na Kama wanautaka, uwe ni wa aina gani.

Pia katiba ya JMT 1977 haikuwahi kupigiwa kura na wananchi. Kilichotokea ni viongozi wa jamhuri Mbili huru kutia Saini Nyaraka za muungano, na baadae Kamati ya chama cha siasa (CCM), sat and drafted the constitution. Na Ndio maana ilipotokea kwa Mara ya kwanza fursa ya kujadili katiba, matokeo yake ikawa ni kuchafuka kwa Hali ya hewa ya kisiasa 1983-84. Rasimu ya Chenge ni Katika Ile Ile mbovu ya mwaka 1977, lakini sasa CCM inaitafutia uhalali kwa Mara ya kwanza. Kitendo cha wananchi kuipa uhalali katiba hii maana yake ni kukubali sasa Kwamba historia, hadhi, mamlaka na utambulisho wa Tanganyika na hata Zanzibar sasa ni halali kuchakachuliwa, Tena kwa Mujibu wa Sheria, na ole wao watakaothubutu Kuhoji Hilo baada ya hapo.

Kulazimisha rasimu ya Chenge kuwa Ndio katiba mpya ya JMT kwa kusingizia Kwamba uhalali wake umetokana na wananchi, huku ni kutengeneza mazingira ya kuchafuka kwa Hali ya hewa kisiasa Tena kwa kiwango ambacho hakijapata tokea. Hii ni kwa sababu, wananchi, hasa wa Tanganyika wanaweza wakaingizwa Mjini na CCM kupitia kura ya maoni lakini muda sio mrefu watakuja kuyaona haya tunayojadili humu. Wakati huo ukifika, Watu aina ya kina Kobello, hawa hawatapata Madhara yoyote kwani wameshakana uraia wao humu na kusema Kwamba Hawana mpango Tena wa kuishi Katika upande huu wa dunia, upande ambao wapo busy kuuangamiza kupitia vitufe vyao vya computer.



Sent from my iPhone using JamiiForums
Japan ni nchi ya kidemokrasia kuliko Tanzania?? Nani alitunga katiba yao?
 
Japan ni nchi ya kidemokrasia kuliko Tanzania?? Nani alitunga katiba yao?

Tuelimishe wewe unayejua, kisha tutachangia Katika muktadha wa utapeli unaoendelea kwetu kwa miaka 50 sasa;


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Wakuu Nguruvi3, Mchambuzi, Mag3 na wengineo, pls msikate tamaa kutoa michango yenu yenye manufaa kwetu na vizazi vyetu vijavyo, msikatishwe tamaa na hawa watu wanaotaka nchi iende bila mwelekeo wowote ilimradi tu lipo kundi fulani linanufaika,

Na ninaomba niwatie moyo wapo wengi sana wanabadilishwa fikra zao na kupata maono mapya kupitia elimu ya jukwaa na mabandiko yenu, tuzidi kuelimishana.

Nirudi kwenye mada kidogo, Nina Swali moja kubwa linanitesa sana moyo wangu na fikra zangu kila wakati, enyi great thinkers mnisaidie kujibu, Tuliungana nchi mbili Tanganyika na Zanzibar tukaunda Tanzania nchi mpya. Lakini kila wakati watu wa Tanganyika watajitanbulisha kama Tanzania Bara ( not Tanganyikan, wameua kabisa asili yao), while wenzetu wa Visiwani wao kila mara na hadi bunge la katiba nimeona wakijiita Wazanziba/ Tanzania Zanziba, Why?? Kwa nini wabara wanaua asili yao na wengine bado wanaitukuza?

Msinishangae kwa swali langu hili, kwamba huyu jamaa mbona hajagusia facts za kiuchumi na kifedha? Nimeona kabla sijaenda huko labda tuanziea hapa, hivi Watanganyika na viongozi wetu wa Tanganyika tunajielewa kweli? Why tunashidwa kutetea asili yetu?? Je viongozi wetu wataweza kweli kututetea kwenye maslahi mapana ya kiuchumi na kijamii wakati hawataki hata kujulikana kama watanganyika kama wenzao wa upande wa pili, wao hujikana asili zao na kujiita watanzania bara, loooh inaumiza sana.

Nilisikitika viongozi fulani wakubwa eti wanasema vijana wengi wamezaliwa baada ya muungano hivyo hawaijui tanganyika, huu ni upotoshaji wa hali ya juu sana, kwani wazazibar wote wazee? Mbona wao wanaitambua zanziba yao hata baada ya muungano, hiii inasikitisha sana. Wanasahau asili haina uzee wala vijana, taifa la Israel liligawanyika vipande vipande, lakini hata siku moja hawasahau asili yao, ndg zetu Rwanda hata iweje wao huikumbuka Rwanda,

Tusemezane great thinkers labda mm sielewi, maana naona kuna tatizo kuanzia kwenye fikra zetu juu ya nchi yetu na tumekubali kukandamizwa katika kufikiri kwetu kuhusu nchi yetu, tunaaminishwa yale watakayo watu fulani tuyaamini
 
Wakuu Nguruvi3, Mchambuzi, Mag3 na wengineo, pls msikate tamaa kutoa michango yenu yenye manufaa kwetu na vizazi vyetu vijavyo, msikatishwe tamaa na hawa watu wanaotaka nchi iende bila mwelekeo wowote ilimradi tu lipo kundi fulani linanufaika,

Na ninaomba niwatie moyo wapo wengi sana wanabadilishwa fikra zao na kupata maono mapya kupitia elimu ya jukwaa na mabandiko yenu, tuzidi kuelimishana.

Nirudi kwenye mada kidogo, Nina Swali moja kubwa linanitesa sana moyo wangu na fikra zangu kila wakati, enyi great thinkers mnisaidie kujibu, Tuliungana nchi mbili Tanganyika na Zanzibar tukaunda Tanzania nchi mpya. Lakini kila wakati watu wa Tanganyika watajitanbulisha kama Tanzania Bara ( not Tanganyikan, wameua kabisa asili yao), while wenzetu wa Visiwani wao kila mara na hadi bunge la katiba nimeona wakijiita Wazanziba/ Tanzania Zanziba, Why?? Kwa nini wabara wanaua asili yao na wengine bado wanaitukuza?

Msinishangae kwa swali langu hili, kwamba huyu jamaa mbona hajagusia facts za kiuchumi na kifedha? Nimeona kabla sijaenda huko labda tuanziea hapa, hivi Watanganyika na viongozi wetu wa Tanganyika tunajielewa kweli? Why tunashidwa kutetea asili yetu?? Je viongozi wetu wataweza kweli kututetea kwenye maslahi mapana ya kiuchumi na kijamii wakati hawataki hata kujulikana kama watanganyika kama wenzao wa upande wa pili, wao hujikana asili zao na kujiita watanzania bara, loooh inaumiza sana.

Nilisikitika viongozi fulani wakubwa eti wanasema vijana wengi wamezaliwa baada ya muungano hivyo hawaijui tanganyika, huu ni upotoshaji wa hali ya juu sana, kwani wazazibar wote wazee? Mbona wao wanaitambua zanziba yao hata baada ya muungano, hiii inasikitisha sana. Wanasahau asili haina uzee wala vijana, taifa la Israel liligawanyika vipande vipande, lakini hata siku moja hawasahau asili yao, ndg zetu Rwanda hata iweje wao huikumbuka Rwanda,

Tusemezane great thinkers labda mm sielewi, maana naona kuna tatizo kuanzia kwenye fikra zetu juu ya nchi yetu na tumekubali kukandamizwa katika kufikiri kwetu kuhusu nchi yetu, tunaaminishwa yale watakayo watu fulani tuyaamini

Mkuu King Suleiman,

Naomba nichokoze mada zaidi badala ya kuja na majibu.

Una hoja za msingi sana. Miaka 20 iliyopita, Christopher Mtikila alikuja na hoja ya Tanganyika, and I must confess, Nikiwa secondary, nilimuona ni comedy. Je ni kwanini? Vijana wengi ambao Ndio tunawahitaji sasa kwa ajili ya ukombozi wa Tanganyika, wengi wao bado wana mentality yangu ya Enzi za mtikila na Tanganyika, je ni kwanini? Je ni kwanini wapo walio badilika, na wapo wenye fikra mgando? Tunawabadilishaje ili waokoke na upofu unaojengwa na akina Mtanganyika, MwanaDiwani, Kobello, Mkandara na wenzao?

Utanzania awali ulikuwa ni ufahari na Sifa kubwa sana Katika miaka ya awali ya muungano, lakini baadae Hali ikaanza badilika kutokana na usaliti wa Zanzibar, aliyebakia na utanzania ni mtanganyika tu, je ni kwa Sifa na ufahari gani?

Leo hii utanzania una maana na faida gani kwa mtanganyika? Kobello, Mtanganyika, Mkandara, MwanaDiwani, tafadhali tusaidiane majibu. Kwa mzanzibari tunajua ni pale tu linapokuja suala la uchumi, ulinzi na usalama.




Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Barubaru,

Unazungumziaje uamuzi wa watanganyika wa kufuta utaifa wao kwa maslahi ya utaifa wa Tanzania na kuishia kusalitiwa na wazanzibari ambao kwa miaka 50, utaifa wao muhimu zaidi ni Uzanzibari, huku utanzania ukiwa na maana kwa ajili ya uchumi, ulinzi na usalama?

Unazungumziaje uamuzi wa watanganyika wa kuhamishia Mapato Yao kuwa ni ya watanzania mwaka 1964 kwa sababu wenzao wazanzibari hawakuwa na Mapato ya maana ya kuchangia muungano zaidi ya excise duty ya karafuu?

Haya Ndio yamejenga utanzania, ni gharama kubwa sana watanganyika wameingia, lakini sasa wanasema, "basi imetosha."






Sent from my iPhone using JamiiForums

Mchambuzi,

Inaweza kuwa kweli ulichoandika ingawa mimi kama mchumi naamini NO FREE IN LIFE na ndio maana waZnz wamelibaini hilo wanataka uhuru kamili wa kiuchumi.

Ok tujaalie ulichoongea ni sahihi, sasa nikuulize MBONA MNAKUWA VINARA WA KULALAMIKA NA KUNUNG'UNIKA ikiwa wenyewe kwa hiari zenu mmeamua kuubeba mzigo mzito wa Mzanzibar?

Lakin la pili kama Mznz amechoka kubebwa kwanini mnamlazimisha abebwe na ninyi huku mkinung'unika.

Lakin mlitakiwa mjue muungano ni kama koti ukiona linakutatiza mnalivua kwanini msifane hivyo badala ya kuleta manung'uniko hapa barzani. Kumbuka Tanzania na ana uzoefu mkubwa wa kuvunja muungano kwani wamejifunza mengu katika mbinu hizo kwa kuvunjika kwa EAC

Binafsi huwa nikisoma manung'uniko yenu wewe na nguruvi3 hususan mnapoelekeza tuhuma zenu kwa waZnz na sio wenyewe ima kwa kujikomba au kujipendekeza nafikia kipindi nawaweka kundi la Mh Keissy na vituko vyake lakin akija kwenye kura anaufyata.

Pole sana
 
Mimi nimeshakuupuza, naomba wenzangu wakupuuze. Jasusi zlishasema hakuna mjadala unaoingia ukwa na mchango wa maana.

Ahsante tumekusoma, tunaomba upunzike tukikuhitaji tutakualika.

Ahali yangu niliwahi kukubainishia uwe unafanya utafiti kidogo kabla kuandika KWANI SASA NAKUHUKUMU KWA MAANDIKO YAKO ya kubainisha waTGK wamechoka kuwabeba waZnz kiuchumi wakti SIVYO hivyo bali wanawataka kwa kula hali.

Nakushauri ufanye utafiti kidogo kabla kuandika kwani maandiko hayo watu wataweza kukusuta hata baada ya miaka 50 ijayo.

Pole sana
 
Mkuu Barubaru,

Unazungumziaje uamuzi wa watanganyika wa kufuta utaifa wao kwa maslahi ya utaifa wa Tanzania na kuishia kusalitiwa na wazanzibari ambao kwa miaka 50, utaifa wao muhimu zaidi ni Uzanzibari, huku utanzania ukiwa na maana kwa ajili ya uchumi, ulinzi na usalama?

Unazungumziaje uamuzi wa watanganyika wa kuhamishia Mapato Yao kuwa ni ya watanzania mwaka 1964 kwa sababu wenzao wazanzibari hawakuwa na Mapato ya maana ya kuchangia muungano zaidi ya excise duty ya karafuu?

Haya Ndio yamejenga utanzania, ni gharama kubwa sana watanganyika wameingia, lakini sasa wanasema, "basi imetosha."






Sent from my iPhone using JamiiForums

Mchambuzi,

Nilipo BLUE.

Hapo ndipo ninaposhangaaa hata mimi NA KUJIULIZA JE NI WATANGANYIKA GANI HAO WANAOSEMA BASI IMETOSHA?

Mimi nilitegemea msemee bungeni katika Bunge la KATIBA especially katika kura ya maamuzi ya kupitisha rasimu hiyo. Huko wawakilishi wenu wameipitisha kwa kura ya NDIO kwa kishindo kikubwa.

Labda utudadavulie ni wapi hapo wanaposema wamechoka au JF?

Na nakuhakikishia kuwa hata katika kura za wananchi kuipitisha rasimu hiyo UPANDE WA BARA WATAPATA KURA ZA NDIO ZAIDI YA 80% na upande wa Znz mmh mtihani kupata .

Sasa najiuliza aliyechoka kunyonywa ni Mtanganyika au Mznz kutokana na maamuzi ya Bunge la Katiba?

Nakushauri unapo nung'unika kumbuka watu wanakusoma hapa barzani na kila neno lako linapimwa wakti ukifika. Angalia usije kuumbuka kama Nguruvi3 na maneno yake niliyombainishia huko juu.


Pole sana.
 
Tuelimishe wewe unayejua, kisha tutachangia Katika muktadha wa utapeli unaoendelea kwetu kwa miaka 50 sasa;


Sent from my iPhone using JamiiForums
Ndiyo, na katiba yake iliandikwa na wanasheria 12 kutoka Marekani.

The point is, watu kuikubali katiba na marekebisho yatayofuata kulingana na hali halisi. Katiba ya 1977 siyo ya kidikteta just because wananchi hawakuipigia referendum. Katiba nyingi za nchi za kidemokrasia hazijapitia referrendum, mfano US Constitution.
 
Nguruvi, unarudia rudia argument za gharama over and over wakati tangu mwanzo niliweza kuweka side by side matumizi ya serikali ya Zanzibar na Tanzania, nikakwambia kwamba argument ya gharama haina sababu the cost is insignificant na hata ufanye IF analysis yoyote huwezi kuwa na significant cost.

Nimekwambia kwamba from security standpoint benefit outperform the cost. Na hapa ndio wengi hawapendi kupazungumzia lakini that is a fact.
Kwanza, elewa hakuna gharama za znz na Tanzania. Unapoongelea Tanzania unaongelea Tanganyika na Zanzibar. Huwezi kuwa na gharama za znz halafu za Tanzania. Logic inalazimisha usema gharama za Tanganyika na Zanzibar

Pili, ni makosa sana kutoangalia gharama za znz na kusema ni insignificant.Mifano kidogo
Zanzibar kama sehemu nyingine ya Tanzania inapata 4.5% ya pato la Tanganyika kwa jina la Tanzania.

Ukiacha mambo mengine, pato la Tanganyika tu ni Trilioni 12 kwa mwaka.
4.5 ya Trilioni 12 ni takribani Bilioni 400.Pato la znz ni bilioni 400 kwa mwaka.
Hivyo znz inaweza kuishi bila kufanya kazi kutegemeana na pato la Tanzania.
Ndio maana hawakusanyi kodi kwasababu mjomba Tanganyika atafidia uzembe wao

Kiasi hicho ni kikubwa kuliko pesa za wizara moja ya Tanganyika katika bajeti. Unawezaje kusema ni insignificant

2. Katika mikoa inayochangia pato la taifa Sumbawanga inachangia takribani Trilioni 1 kwa mwaka.
Pesa za maendeleo kwenda Sumbawanga ni chini ya bilioni 20, wakati znz inachukua zaidi ya bilioni 300.
Hayo yote yanatokea wakati znz ikiwa haichangii chochote katika muungano. Unawezaje kusema ni insignificant

3. Gharama za ulinzi na usalama, znz haijui. Ukichukua mfano mmoja tu wa kikosi kimoja cha jeshi kinachotumia bilioni 50 kwa mwaka, kwa znz hiyo ni sawa na asilimia 7. Yaani asilimia 7 hutoka Tanganyika.Ndivyo ilivyo kwa shughuli nyingine na wizara.

In short znz inachukua nusu ya bajeti ya wizara ya mambo ya ndani ya Tanganyika.
Unawezeje kusema ni indignificant.Hebu jiulize ni mkoa gani katika Tanganyika unaochukua kisasi hicho.

Mfano rahisi sana, Znz inaleta wanafunzi 1700 kwa jina la Tanzania,hudhaminiwa bure.
Kwa hesabu za mjadala, kama gharama ya mwanafunzi mmoja ni milioni 5 tu kwa mwaka hiyo ni sawa na 8.5 Bilioni.
Kumbuka hizi ni gharama za kodi, Tanganyika inabeba.

Watanganyika wanarudisha mikopo. Kwa wanafunzi 1,700 wa Tanganyika hilo ni deni na inabidi walipe.
Unawezaje kusema ni insignificant wakati haijawa insignificant kwa Tanganyika.

ZNZ haina uwezo wa kudhamini wanafunzi 1000,wanaokota mitaani 1,700 kwa kuwa hawana gharama, unawezaje kudharau kiasi hicho. Kama si kuokota kwanini SMZ idhamini wazanzibar tu 800 na kuleta 1,700 kwa gharama za kodi za Mtanganyika

Endapo kijana, ndugu au jamaa yako wa Tanganyika amekosa mikopo kwasababu pesa zimeelekezwa kwa wanafunzi 1.700 wa znz hiyo ni 100% maumivu na huwezi kusema ni insignificant.

Kwamba mwanafunzi amekosa masomo kwa haki ya mkopo, wakati yule wa nchi jirani ya zanzibar amepewa buree ikiwa ni kodi za mzazi wa Tanganyika. Insane!

Fikiria, mbunge mmoja tu wa znz asiye na manufaa yoyote Dodoma analipwa milioni 15.
Wapo wabunge 84, Kwa mwezi tu, achilia posho na gharama nyingine, ni takribani milioni 120.
Hawa wamekuja kuwakilisha znz si Tanganyika hivyo walipaswa kulipwa na SMZ.

Leo kuna Hospitali haina X-ray ya milioni 50 tu kwa mfano wakati pesa zinaelekezwa kwa watu 84 wasiotuhusu.
Unawezaje kusema ni gharama ndogo. Kwanini wasilipiwe gharama zao za matibabu na wake zao na SMZ iliyowaleta kutetea znz tu

Mwezi January, JMT ambayo ni Tanganyika imetoa bilioni 11 kupeleka umeme nchi jirani ya znz kule Pemba.
Fikiria, kiasi hicho kingeweza kudhamini wanafunzi wangapi wa Tanganyika wasio na mikopo.
Unawezaje kusema ni kiasi kidogo sana.

Gharama za bajeti ya SMZ anazibeba Mtanganyika, kwa tune ya bilioni zaidi ya 300.
Jiulize kiasi gani kinakwenda hospitali ya Muhimbili kwa miezi 3 halafu utumabie ni insignificant.

Orodha ni ndefu sana, ninachoweza kusema ni kuwa wakati znz haina machango wowote wa maana kiuchumi, uchukuaji wake umekuwa mkubwa kuliko mkoa wa DSM.

Leo unatuambia kiasi hicho ni kidogo. Halafu angalia idadi ya watu kama laki 600 tu wanapewa kiasi hicho huku wengine wakiishi bara na kuleta social constrains katika services kama Watanzania, ukweli ukiwa Mtanganyika ndiye mbeba mzigo huo.

Hivyo jaribu kuangalia kutoka kona mbali mbali uone jinsi watu 1.2M wanavyochota tu bila kuchangia halafu utazame watu milioni 45 wanaochangia jinsi wanavypopata. Hili unasema ni dogo sana! real

Kutoka security point of view, labda utueleze kwa dunia ya sasa ni security gani unayozungumzia.
Hatuna sababu za kuficha mambo, weka hadharani kwanini unadhani znz ni muhimu kwa security ya nchi.
Kama ni muhimu, huo umuhimu kwa katiba ya Chenge umelindwa vipi.

Tunachotaka wengine, kwanza, znz iwajibike kuchangia muungano.
Znz iache kudai misaada kutoka Tanganyika kama haki yao.

Na pili Tanganyika ipate fiscal autonomy yake bila kufungwa mikono na uwepo wa znz.
Tunataka znz iwajibike kwa gharama zinzaowahusu, kwa mfano wabunge wao walipwe na kodi zao kwa ajili yao.

Hatutaki kuwa na muungano ambao znz inatumia jina la Tanzania inapohitaji kukidhi dhiki zao.

Hilo sasa lazima lifike mwisho. Na pia watambue kuwa muungano wa dunia ya leo ni kiuchumi si kuchota na kulilia hovyo.

Hebu tuambie kuhusu security, nini kinachokutisha.
 
Nianze kwa kutoa asante, pongezi na shukhrani kwa Mchambuzi, Barubaru na Nguruvi3 kwa michango yao iliyojikita kwenye takwimu na namba. Mimi kwa upande wangu nimejikita zaidi kwenye lojiki na mantiki na katika msingi huo nina swali kwa Mtanganyika; mara nyingi umekuwa ukitumia maneno Tanzania na Zanzibar kama vile yako kwenye mizani sawa; mara mchango wa Tanzania dhidi ya Zanzibar, serikali ya Tanzania dhidi ya serikali ya Zanzibar au wananchi wa Tanzania dhidi ya watu wa Zanzibar...hivi inapotajwa Tanzania, Zanzibar haimo? Wanapotajwa Watanzania, Wazanzibari hawamo? Inapotajwa serikali ya Tanzania, Zanzibar haimo? Na mwisho, katika msingi huo huo inapotajwa Katiba ya Tanzania ina maana hiyo Katiba haihusu Zanzibar? Does this make sense to you or to any right thinking individual? Hili dude Tanzania ni nini hasa?

Ajabu ni kwamba upuuzi wote huu umewezekana kwa sababu moja tu, muundo wa Muungano eti wa serikali mbili. Mchakato wa katiba mpya ulitupa fursa ya kuondokana na huu upuuzi na kweli Watanzania walipendekeza kupitia Tume namna ya kurekebisha hali hiyo lakini wahafidhina wanaonufaika na upuuzi huo wameamua kuyapuuza maoni yao. Katiba ya mwaka 1977 haikuweza kuzuia uhaini uliofanyika huko Zanzibar, na mpaka dakika hii katiba ya Chenge/Sitta inapitishwa na BMLK, Katiba ya Zanzibar iko pale pale imetulia. Je Katiba mpya, iliyojikita kwenye muundo ule ule wa serikali mbili na zote zikiwa na masharubu, itatumia njia zipi kuhakikisha kwamba yaliyotokea huko nyuma hayajirudii? Nasema hivi kwa sababu hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa dhidi ya kitendo cha kihaini kilichofanyika cha kuisigina Katiba ya Jamhuri ya Muungano! Again I ask, does any of this make sense to a right thinking individual?

Kwa nini kama kweli kuna nia njema, kabla ya hii katiba ya Chenge/Sitta kuletwa kwa wananchi kwa kura ya maoni, Katiba ya Zanzibar isifanyiwe marekebisho ikaeleweka wazi kuwa Katiba ya Muungano itakuwa supreme? Tutazidi kuwa wapuuzi kama tutaendelea kutumia mabilioni ya fedha za walipa kodi bila kwanza kuwa na uhakika wa BLW la Zanzibar kuafiki hii katiba ya Chenge/Sitta. Maana tupende tusipende Watanganyika tumebaki kama mateka wa katiba ya Zanzibar, it is all subject to Watu wa Zanzibar wanataka nini; hasa kama watakubali kufuta vipengele vya Katiba waliyoipitisha kwa kura ya maoni kwa asilimia kubwa tu (zaidi ya theluthi mbili) huku ikiwa na ibara inayotamka wazi kwamba; nanukuu;
Katiba ya Zanzibar sehemu ya kwanza ibara ya (4) said:
Katiba hii ni Katiba ya Zanzibar na itakuwa na nguvu za kisheria nchini kote na isipokuwa kutokana na kifungu 80 ikiwa sheria yoyote inatofautiana na Katiba hii, basi Katiba hii ndiyo itayokuwa na nguvu na sheria hiyo itakuwa batili kwa kiwango kile ambacho kinahitilafiana.
Kifungu 80 kinasema hivi nanukuu;
Katiba ya Zanzibar kifungu 80A. (1) said:
Bila ya kuathiri masharti ya kifungu cha 80 cha Katiba, Baraza la Wawakilishi halitaweza kufanya mabadiliko ya Katiba kuhusiana na sharti lolote liliomo katika kifungu chochote kilichoainishwa katika kijifungu cha (2) cha kifungu hiki, mpaka kwanza mabadiliko hayo yakubaliwe na wananchi kwa Kura ya Maoni
Sasa kama si uhuni na ulaghai uliofanyika ndani ya Bunge Maalum La Katiba, hiyo kura ya maoni ni lazima kwanza ifanyike huko Zanzibar na marekebisho ya Katiba ama yakubalike au yakataliwe. Kama serikali ya Muungano ingekuwa na ujasiri, ingeanza kwa kuiwajibisha serikali ya Zanzibar lakini maadam hata hilo dogo halikuwezekana nani hasa anamdanganya nani hapa. Uongozi legelege huzaa serikali legelege isiyoweza kulinda, kutetea na kusimamia sheria kuu ya nchi, Katiba; na mpaka sasa huo uongozi haujaonekana huku muda wa serikali kubaki madarakani ukizidi kuyoyoma. Jamani tuwe serious angalau kwa issue kama hii ya Katiba; hakuna njia yoyote ile itakayoweza kutuondoa kwenye hili dimbwi lililojaa tope zaidi ya Katiba inayowatambua rasmi wahusika wa Muungano huu...nafasi zao na wajibu wao katika kuulinda.
 
Mkuu Mag3 hapo juu, kuna neno! tena neno zito. Kama ulivyosema logic haiwezi kuwekwa pembeni.
Kuna maswali mazito, narudia kuna neno zito. Nitarudi kuchangia.
 
Last edited by a moderator:
Kifungu 80 kinasema hivi nanukuu;

Sasa kama si uhuni na ulaghai uliofanyika ndani ya Bunge Maalum La Katiba, hiyo kura ya maoni ni lazima kwanza ifanyike huko Zanzibar na marekebisho ya Katiba ama yakubalike au yakataliwe. Kama serikali ya Muungano ingekuwa na ujasiri, ingeanza kwa kuiwajibisha serikali ya Zanzibar lakini maadam hata hilo dogo halikuwezekana nani hasa anamdanganya nani hapa. Uongozi legelege huzaa serikali legelege isiyoweza kulinda, kutetea na kusimamia sheria kuu ya nchi, Katiba; na mpaka sasa huo uongozi haujaonekana huku muda wa serikali kubaki madarakani ukizidi kuyoyoma. Jamani tuwe serious angalau kwa issue kama hii ya Katiba; hakuna njia yoyote ile itakayoweza kutuondoa kwenye hili dimbwi lililojaa tope zaidi ya Katiba inayowatambua rasmi wahusika wa Muungano huu...nafasi zao na wajibu wao katika kuulinda.
SURA YA KUMI NA TISA
MASHARTI YATOKANAYO NA MASHARTI YA MPITO

Muda wa Mpito
293.-(1) Muda wa Mpito utakuwa muda wote kuanzia tarehe ya kuanza kutumika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 2014 hadi kupita miaka minne baada ya kuanza kutumika kwa Katiba hii.

(2) Bunge linaweza, kwa azimio litakaloungwa mkono na theluthi mbili ya Wabunge wote, kuongeza muda wa mpito uliotajwa katika ibara ndogo ya (1) kwa kipindi kisichozidi miaka miwili ili kukamilisha Mambo ya Mpito yatakayokuwa hayajafanyika au kukamilika.

Utekelezaji wa masharti ya Katiba Mpya

294. Mambo yafuatayo yatafanyika na kukamilika katika Muda wa Mpito:

(a) kurekebisha Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 ili kuwiana na masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 2014;

(b) kutunga na kurekebisha sheria mbalimbali za Jamhuri ya Muungano, sheria ambazo si za Muungano zinazohusu Tanzania Bara na sheria za Zanzibar ili kuwiana na masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 2014;

(c) kuanzishwa kwa Mahakama ya Juu;

(d) kuundwa kwa Tume na Taasisi nyingine za kikatiba zilizoainishwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 2014 na kwa kuzingatia masharti ya Katiba hii;
 
SURA YA KUMI NA TISA
MASHARTI YATOKANAYO NA MASHARTI YA MPITO

Muda wa Mpito
293.-(1) Muda wa Mpito utakuwa muda wote kuanzia tarehe ya kuanza kutumika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 2014 hadi kupita miaka minne baada ya kuanza kutumika kwa Katiba hii.

(2) Bunge linaweza, kwa azimio litakaloungwa mkono na theluthi mbili ya Wabunge wote, kuongeza muda wa mpito uliotajwa katika ibara ndogo ya (1) kwa kipindi kisichozidi miaka miwili ili kukamilisha Mambo ya Mpito yatakayokuwa hayajafanyika au kukamilika.

Utekelezaji wa masharti ya Katiba Mpya

294. Mambo yafuatayo yatafanyika na kukamilika katika Muda wa Mpito:

(a) kurekebisha Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 ili kuwiana na masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 2014;

(b) kutunga na kurekebisha sheria mbalimbali za Jamhuri ya Muungano, sheria ambazo si za Muungano zinazohusu Tanzania Bara na sheria za Zanzibar ili kuwiana na masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 2014;

(c) kuanzishwa kwa Mahakama ya Juu;

(d) kuundwa kwa Tume na Taasisi nyingine za kikatiba zilizoainishwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 2014 na kwa kuzingatia masharti ya Katiba hii;

MwanaDiwani[/USER] , acha kupotosha. Hayo yalikuwa maelezo ya tumeya Warioba kwa kuzingatia kuwa muungano ungekuwa na S3 na hivyo kuwe na kipindicha mpito cha kuundwa kwa serikali za nchi husika.

enge ni ile mwaka 1977iliyoongezwa marais tu, hakukuwa na sababu zozote za kuwa na kipindi cha mpito.

Kipindi hicho kimewekwa kwa hoja za Mag3 kuwa, itakuwa ningumu sana, na Chenge anafahamu hivyo kubadili katiba ya uhaini ya znz iwianena ile ya JMT.

Hivyo lazima uelewe uhuni wa Chenge/Sitta si kila mmoja anaumeza. Wengine tupo huru tukitumikia umma na si kulamba miguu ya mafisadi.

Ahsante
 
Last edited by a moderator:
MwanaDiwani , acha kupotosha. Hayo yalikuwa maelezo ya tumeya Warioba kwa kuzingatia kuwa muungano ungekuwa na S3 na hivyo kuwe na kipindicha mpito cha kuundwa kwa serikali za nchi husika.

Kwavile Katiba pendekezwa ya Chenge ni ile mwaka 1977iliyoongezwa marais tu, hakukuwa na sababu zozote za kuwa na kipindi cha mpito.
Kipindi hicho kimewekwa kwa hoja za Mag3 kuwa, itakuwa ningumu sana, na Chenge anafahamu hivyo kubadili katiba ya uhaini ya znz iwianena ile ya JMT.

Hivyo lazima uelewe uhuni wa Chenge/Sitta si kila mmoja anaumeza. Wengine tupo huru tukitumikia umma na si kulamba miguu ya mafisadi.


Ahsante
Ndugu Nguruvi3

Upotoshaji wangu uko wapi?

Nimekuwekea mpaka Sura ya Katiba Inayopendekezwa, ambayo utalipata andiko lakini cha kushangaza bado unasema ninapotosha.

Huwezi kuanza kupingana na ukweli au kuanzisha ubishi kwa matakwa yako ya kisiasa.

Kama utapata muda nenda ukaisome Katiba Inayopendekezwa lakini kama unadhani Proposed Constitution is still not worth reading, basi ni bora ukanyamaza tu kuliko kuanza kupiga kelele bila back up!.

Ubishi usio na msingi ni kupoteza muda!

''You are better that this''!
 
Ndugu Nguruvi3

Upotoshaji wangu uko wapi?

Nimekuwekea mpaka Sura ya Katiba Inayopendekezwa, ambayo utalipata andiko lakini cha kushangaza bado unasema ninapotosha.

Huwezi kuanza kupingana na ukweli au kuanzisha ubishi kwa matakwa yako ya kisiasa.

Kama utapata muda nenda ukaisome Katiba Inayopendekezwa lakini kama unadhani Proposed Constitution is still not worth reading, basi ni bora ukanyamaza tu kuliko kuanza kupiga kelele bila back up!.

Ubishi usio na msingi ni kupoteza muda!

''You are better that this''!
Kusoma ni jambo moja, kuelewa ni jambo jingine, kutafsirini jambo tofauti.
Weweumesoma na ndivyo Chenge alivyoandika, upo sahihi kabisa. Umesoma!

Umeamua kuja katika propaganda ili tuamini alichoandika Chenge ni kweli wakati tunajuaukweli.

Hakuna sababu za kuwa na kipindi cha mpito wakati mfumowa katiba ni ule ule. Katiba ya Chenge/Sitta nimarekebisho ya katiba ya 1977. Kama umeielewa, tuambie katiba ya 1977 na ya Chengezimetofautiana nini.
Au una maana kutaja makundi yaakina mama na vijana?

Tunachofanya hapa si copy and paste, ni tafakuri kuhusuhoja.
Hivyo,hatuwezi kumeza tu kwasababu hatufanyi kazi za chama wala hatuamini fisadianaweza kuwa mwema katika nyaraka ya taifa achilia mbali uhuni uliofanywa.

Hayo uliyonukuu ni yale yaliyotokana uhuni waSitta/Chenge na kina Zakhia Meghjikutangazwa wajumbe wa bara na kupiga kura wajumbe wa znz. Ukifanya copy and paste ya gazeti la serikaliZakhia yupo katika 201 kutoka bara.

Ukifanya tafakuri kidogo kama tunavyofanya wenzako,utajiuliza iweje alipiga kura znz katika uhuni wa bunge la CCM?
Haibadilishi ukwelikuwa ule ni uhuni

Tulikuuliza ukakaimbia, sasa unakuja na copy and pasteili kutuondoa katika tafakuri na tuanze kujadili uhuni wa Dodoma.

Mkuu, tunatumia maarifa, hiyo inatuweka huru katikajamii. Hatulazimiki kulamba miguu mkate uje mezani. Copy and paste, mhhh nadhani si mahala pake. Gazeti laUhuru wangekushukuru, hapa tunasema tafakauri mbele copy and paste baadaye mkuu
 
Mkuu Mag3 , katika bandiko 194 umeuliza maswali wasiyotakakuyasikia. Nakuhaikishia Mtanganyika na wenzake hawataweza kuyagusa. Hili lakusema Tanzania bara ni sawa na lile swali la King Suleiman

Hawataki Tanganyika itajwe kwasababu kutajwa tukunairudishia hadhi.
Hivyo inaundwa nchi ya Tanzania bara ambayo historia yakeinaanzia mwaka 1977.
Ni aibu kwamba watu wanadai Tanzania Vs Zanzibar

Ulisema tatizo lote lipo katika mfumo wa serikali mbili. Nakwamba, znz haitaweza kubadili katiba yao ya uhaini ya 2010 kuwiana na JMT. Hilo ni kweli kabisa ukizingatia unafiki wa wazanzibar

Ingawa wao hupenda kuitwa waungwana, sifa ya unafiki ni sehemu ya utamaduni wao.
Naomba nifafanunue

Mwaka 2010 aliyekuwa Spika wa Bunge ni Pandu Kificho. Woteakina Idd Seif, Nahodha, Seif Khatibu, Mohamed Aboud walikuwa ndani ya BLW wakati znz inakamilisha udhalilishaji wa katiba ya JMT.

Aliyesaini uhuni huo ni Karume. Wale watalii 84 wanaokujaDodoma waliunga mkono uhuni huo wa kuvunjwa katiba ya JMT inayowalaza na kuwapaposho bila kazi pale Dodoma.

Wote hao ndio tumewaona Dodoma wakishirikiana na Chenge/Sitta kuhalalisha katiba ya mafichoni kwa kutetea muundo wa S2 naMuungano. Hoja yao kubwa ni kuwa S2 zinaimarisha muungano.

Tayari wamegeuga nakusahau kuwa ile katiba ya znz 2010 ilivunja muungano wala si kudhoofisha.
Nikatiba hiyo ya znz ndiyo imezaa mengi tunayoyaona leo.

Hapa kuna unafiki, yaani manafiki wa kizanzibar wakiwa znz wanasema jambo moja, wakivuka bahari wanasema jingine. Hawataki muungano wakiwaUnguja, wakija Dodoma wanataka uimarishwe.

Jamani huu kama si unafiki wa daraja jema ni kitu gani?

Hivyo, kwasasa wanaunga mkono katiba ya mafichoni ya Chenge/Sitta iliyoandikwa kwa maoni ya wafugaji 23 na wakulima 14. Wakirudi znz, hawawezi kubadili hiyo katiba iwiane nay a JMT? Si hao hao walivunjakatiba ya JMT mwaka 2010 na ndio wamekuja kuandika katiba ya JMT nyingine. Hivi wataachaje unafiki ikiwa ni utamaduni wao.

Na hapa ndipo hoja kubwa inapokuja kuwa Watanganyika, hivikwanini watu 1.2M ambao kichumi, kisiasa na kijamii hawana impact yoyote waendelee kuwa superior kwa taratibu zetu tena wakiwa mgongoni wananyonya madole?
Is it not a wake up call to act
 
Back
Top Bottom