Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

ZITTO AENDELEZA UTAPELI WA KISIASA, SASA AMEUHAMISHIA KIGOMA

Zitto ametangaza rasmi nia yake kugombea ubunge Kigoma Mjini Kupitia ACT Wazalendo, chama ambacho ameshiriki kukipora huku kukiwa na kesi mahakamani. Kwa maana nyingine, wananchi wa Kigoma Kaskazini wanajiandaa kupigia kura chama ambacho matokeo ya uchaguzi yanaweza kutenguliwa huko mbeleni na mahakama kutokana na chama hicho kuwa ni cha kiujanja janja.

Akizungumza mara baada tu ya kuchukua fomu ya kuwania ubunge, zitto alitamka kwamba ameamua kuwania ubunge jimbo la Kigoma mjini kwa sababu wananchi wa jimbo hilo “wameshindwa kupata haki zao za msingi wanazostahili”. Zitto akaenda mbali zaidi na kusema kwamba – amemaliza kazi ya kuwahudumia wananchi wa Kigoma Kaskazini na kudai kwamba katika jimbo hilo hakuna shida tena ya maendeleo. Haya ni matusi makubwa sana kwa wananchi wa Kigoma Kaskazini. Zitto anadanganya na ushahidi upo. Maendeleo ni huduma bora za afya, elimu bora, miundo mbinu, kutaja machache. Maswali:

1. Je kuna hospitali ngapi zenye ubora wa kukidhi mahitaji kama vile upasuaji ndani ya jimbo la Kigoma Kaskazini? Jibu ni Hakuna hata moja.
2. Je, kuna barabara ngapi za lami ambazo zinazoweza kupitika mwaka mzima? Jibu ni Barabara ni moja tu, barabara ya Mwandiga – Manyovu.
3. Je, Kigoma Kaskazini ina shule ngapi za sekondari zenye vidato vya tano na sita? Jibu ni Hakuna hata shule moja.
4. Je, wananchi wa Kigoma Kaskazini wamefanikiwa kumaliza tatizo la magonjwa ya milipuko? Jibu ni hapana kwani Kigoma Kaskazini ni eneo linalojulikana sana kama chanzo cha ugonjwa Kipindu Pindu.
5. Je Kigoma Kaskazini kuna soko kubwa la kusaidia wananchi kuuza mazao ya kibiashara (cash crops)? Hakuna soko hata moja.

Hivi karibuni katika ziara zake kama kiongozi mkuu wa ACT Tanzania, Zitto alitoa matamshi ya kubagua na kuchonganisha wananchi wa mikoa mbalimbali. Zitto aliwashambulia wananchi wa mikoa ya Kaskazini (Arusha na Kilimanjaro) kwamba wanawanyonya wananchi wa mikoa mingine kama vile Mwanza na Shinyanga. Zitto alitumia takwimu za GDP kama kipimo cha michango ya mikoa, na takwimu za HDI kama kipimo cha kuangalia returns za michango husika. Kwa vile Zitto anasema kwamba tatizo la umaskini kwa wananchi wa Kigoma Kaskazini halipo tena, je:

· Umaskini huo umetokomezwa kwa kutumia rasilimali zipi – GDP?
· Kufuatia mafanikio hayo, Kigoma Kaskazini sasa ni jimbo hilo ni la ngapi kitaifa kimaendeleo?
Mchambuzi.

Hii habari umeipata wapi mkuu wangu wakati Zitto anachukuwa fomu Kigoma Mjini wala akuita vyombo vya habari.
 
Last edited by a moderator:
Bunge ni mhimili wa nini?

Nafikiri nimeeleza vizuri sana. Kuwa NCHI yoyote inayofuata UTAWALA WA SHARIA (Rule of Law) basi nchi inaongozwa na mihimili mitatu nayo ni Bunge, Mahakama na Serikali.

Kazi ya Bunge ni kutunga sharia
Kazi ya Mahakama ni Kutafsiri sharia
Kazi ya Serikali ni kutekeleza Sharia ambazo zimetungwa na Bunge..

Kwa mujibu wa Suala lako BUNGE ni Muhimili wa nchi ,kama ilivyo kwa Serikali na Mahakama kuwa navyo ni mihimili ya nchi katika utekelezaji wa Utawala bora.J

Je una zaidi? Basi Bismillah!
 
Yes upo sahihi kwa mtazam huo. Ni kweli ipo mihimili 3 kama ulivyosema
Pengine ningesema Zitto alikuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania

Pamoja na ukweli huo, pia elewa kuwa mihimili hiyo hufanya kazi kwa kutegemeana ingawa ni huru katika maamuzi

Bunge lina kazi muhimu ya kuisimamia serikali iliyopo madarakani. Zitto alikuwa Mbunge, akiwa na nafasi ya kueleza duku duku lake dhidi ya mikoa ya kaskazini kupendelewa au kuwezeshwa kama anavyosema Mkandara

Pia alikuwa mwenyekiti wa PAC akishughulikia sana mambo ya serikali. Kwa mtazamo huo Zitto alikuwa ''in a way'' sehemu ya serikali ingawa hakuwa mtu wa serikali. Unaposimamia serikali kwa kuichunguza na kutoa mapendekezo ya kuisimami, hapo unakuwa sehemu ya'' na sio kuwa ni serikali

All in all, sikumaanisha kuwa alikuwa waziri, mkuu wa mkoa au vinginevyo

Nguruvi3,

Kama nilivyofafanua huko Juu kwa Kobello maaana halisi ya mihimili mitatu ya utawala bora katika Nchi.U

Ukitaka kujua watu ambao ni Sehemu ya Serikali ni mawaziri na wakuu wa wilaya na mikoa wanaoingia bungeni. Na Swifa kubwa ya watu hao ni kuwa wanaapishwa na wakuu wa mihimili hiyo.

Mfano mawaziri woote kwanza wanaapishwa na Rais kuwa ni watendaji wa Serikali na wanapoingia Bungeni wanaapishwa tena na Spika wakimaanisha kuwa ni wabunge. Hivyo kwa kuwa wameapishwa na wakuu wa mihimili miwili tofauti ya nchi moja, hivyo wao ndio wanakuwa ni sehemu ya Serikali na vile vile Sehemu ya Bunge.

Lakin kumbuka hakuna mkuu wa muhimili anayeweza kujiapisha mwenyewe bali anaapishwa na Mkuu wa muhimili
mwingine.


Hivyo Zitto hajawahi kuwa waziri au Mkuu wa wilaya au mkoa, HIVYO HAJAWAHI KUWA SEHEMU YA SERIKALI BUNGENI AU SEHEMU YA YA MBUNGE KATIKA SERIKALI..

Pole sana
 
Mkandara,

Bunge ni mhimili wa kidemokrasia? Umesoma Wapi hili.
Do you really know what "government" means? Kwanini unataka kuanzisha ubishi kwamba bunge sio sehemu Ya serikali? Do you know anything about separation of powers? Serikali ina mihimili mitatu - executive, legislative and judiciary. That's the bottom line.

Mchambuzi,
K
Kumbuka kuna Tofauti kubwa sana baina ya Serikali, Nchi na Doula?

Je unaweza kutuambia mkuu wa Executive anaitwa nani?


Je unazijua? Tudadavulie
 
ZITTO AENDELEZA UTAPELI WA KISIASA, SASA AMEUHAMISHIA KIGOMA

Zitto ametangaza rasmi nia yake kugombea ubunge Kigoma Mjini Kupitia ACT Wazalendo, chama ambacho ameshiriki kukipora huku kukiwa na kesi mahakamani. Kwa maana nyingine, wananchi wa Kigoma Kaskazini wanajiandaa kupigia kura chama ambacho matokeo ya uchaguzi yanaweza kutenguliwa huko mbeleni na mahakama kutokana na chama hicho kuwa ni cha kiujanja janja.

Akizungumza mara baada tu ya kuchukua fomu ya kuwania ubunge, zitto alitamka kwamba ameamua kuwania ubunge jimbo la Kigoma mjini kwa sababu wananchi wa jimbo hilo “wameshindwa kupata haki zao za msingi wanazostahili”. Zitto akaenda mbali zaidi na kusema kwamba – amemaliza kazi ya kuwahudumia wananchi wa Kigoma Kaskazini na kudai kwamba katika jimbo hilo hakuna shida tena ya maendeleo. Haya ni matusi makubwa sana kwa wananchi wa Kigoma Kaskazini. Zitto anadanganya na ushahidi upo. Maendeleo ni huduma bora za afya, elimu bora, miundo mbinu, kutaja machache. Maswali:

1. Je kuna hospitali ngapi zenye ubora wa kukidhi mahitaji kama vile upasuaji ndani ya jimbo la Kigoma Kaskazini? Jibu ni Hakuna hata moja.
2. Je, kuna barabara ngapi za lami ambazo zinazoweza kupitika mwaka mzima? Jibu ni Barabara ni moja tu, barabara ya Mwandiga – Manyovu.
3. Je, Kigoma Kaskazini ina shule ngapi za sekondari zenye vidato vya tano na sita? Jibu ni Hakuna hata shule moja.
4. Je, wananchi wa Kigoma Kaskazini wamefanikiwa kumaliza tatizo la magonjwa ya milipuko? Jibu ni hapana kwani Kigoma Kaskazini ni eneo linalojulikana sana kama chanzo cha ugonjwa Kipindu Pindu.
5. Je Kigoma Kaskazini kuna soko kubwa la kusaidia wananchi kuuza mazao ya kibiashara (cash crops)? Hakuna soko hata moja.

Hivi karibuni katika ziara zake kama kiongozi mkuu wa ACT Tanzania, Zitto alitoa matamshi ya kubagua na kuchonganisha wananchi wa mikoa mbalimbali. Zitto aliwashambulia wananchi wa mikoa ya Kaskazini (Arusha na Kilimanjaro) kwamba wanawanyonya wananchi wa mikoa mingine kama vile Mwanza na Shinyanga. Zitto alitumia takwimu za GDP kama kipimo cha michango ya mikoa, na takwimu za HDI kama kipimo cha kuangalia returns za michango husika. Kwa vile Zitto anasema kwamba tatizo la umaskini kwa wananchi wa Kigoma Kaskazini halipo tena, je:

· Umaskini huo umetokomezwa kwa kutumia rasilimali zipi – GDP?
· Kufuatia mafanikio hayo, Kigoma Kaskazini sasa ni jimbo hilo ni la ngapi kitaifa kimaendeleo?


Mchambuzi,

Mimi nimemsoma vizuri hapo Zitto amesema kuwa amemaliza kazi ya kuwahudumia watu wa kigoma Kaskazini lakin hakupambanua ni huduma zipi amemaliza.


Sasa suala langu kwako . Hivi kazi za mbunge ni kujenga Hospitali, barabara, skuli na marikiti? Je fedhwa za kujenga hayo yote Mbunge huyo anazipata wapi?

Je unaweza kunipa mfano halisi wa mbunge yoyote ambaye amejenga skuli pamoja na Hospitali na marikiti kwa pesa zake binafsi huko Tgk?



Nasubiri ufafanuzi wako kwayo.

Ahsantum

 
Mkandara,

Bunge ni mhimili wa kidemokrasia? Umesoma Wapi hili.
Do you really know what "government" means? Kwanini unataka kuanzisha ubishi kwamba bunge sio sehemu Ya serikali? Do you know anything about separation of powers? Serikali ina mihimili mitatu - executive, legislative and judiciary. That's the bottom line.
Mkuu labda wewe tuambie hilo neno executive mbona hulitumii unapozungumzia serikali ya JK. Maana tunapojadili jambo ni muhimu tuwe na picha moja. Hakuna Mtanzania yeyote anayetumia Mtendaji mkuu akiwa na maana executive, sote tunatumia neno serikali kama chombo cha muhimili..Hivyo maneno mengine ya kiingereza huwa hatuyatumii katika tafsiri ya mazungumzo yetu. Tukielewana lugha husaidia zaidi ktk mjadala badala ya kuanza kutafutana.
 
Nafikiri nimeeleza vizuri sana. Kuwa NCHI yoyote inayofuata UTAWALA WA SHARIA (Rule of Law) basi nchi inaongozwa na mihimili mitatu nayo ni Bunge, Mahakama na Serikali.

Kazi ya Bunge ni kutunga sharia
Kazi ya Mahakama ni Kutafsiri sharia
Kazi ya Serikali ni kutekeleza Sharia ambazo zimetungwa na Bunge..

Kwa mujibu wa Suala lako BUNGE ni Muhimili wa nchi ,kama ilivyo kwa Serikali na Mahakama kuwa navyo ni mihimili ya nchi katika utekelezaji wa Utawala bora.J

Je una zaidi? Basi Bismillah!
Manispaa ya Temeke (serikali ya mitaa) ni nchi?
Je ina mihimili mitatu?

Wabillahi taufiq walhidayah!
 
Manispaa ya Temeke (serikali ya mitaa) ni nchi?
Je ina mihimili mitatu?

Wabillahi taufiq walhidayah!
Mkuu jamani mwee tuelewane. sasa ukisema pia Serikali ya Temeke, tayari unarudisha swali kuwa ina mihimili mitatu maana kwa maelezo yenu bunge ni sehemu ya serikali yenye mihimili mitatu. Tusiende huko tutapotezana wakuu ila tufahamu mtu anaposema serikali ana maana chombo cha Utendaji basi mjadala uendelee.
 
Mkuu jamani mwee tuelewane. sasa ukisema pia Serikali ya Temeke, tayari unarudisha swali kuwa ina mihimili mitatu maana kwa maelezo yenu bunge ni sehemu ya serikali yenye mihimili mitatu. Tusiende huko tutapotezana wakuu ila tufahamu mtu anaposema serikali ana maana chombo cha Utendaji basi mjadala uendelee.
Sawa kaka.
Ila naomba huyu ndugu Barubaru uniachie mmi, tunaweza kwenda naye kwenye dhana Fulani ambayo uelewa wetu unahitilafiana.
 
Last edited by a moderator:
Manispaa ya Temeke (serikali ya mitaa) ni nchi?
Je ina mihimili mitatu?

Wabillahi taufiq walhidayah!

Mwee!!! Kobello.

Vuta subra kidogo wakti Mchambuzi akija tupa darsa hapa tofauti baina ya SERIKALI, NCHI na DOLA. Nafikiri utajifunza mengi sana.

Lakin vile vile ujifunze zaidi kuhusu muundo wa Serikali yenu especially madaraka ya
1. Serikali kuu.
2. Serikali za mitaa. etc.

Pole sana.
 
Mwee!!! Kobello.

Vuta subra kidogo wakti Mchambuzi akija tupa darsa hapa tofauti baina ya SERIKALI, NCHI na DOLA. Nafikiri utajifunza mengi sana.

Lakin vile vile ujifunze zaidi kuhusu muundo wa Serikali yenu especially madaraka ya
1. Serikali kuu.
2. Serikali za mitaa. etc.

Pole sana.
Shukran, ila naomba wewe uliyesema bunge ni mhimili wa nchi utupe maana ya hiyo nchi uliyoisema. Kuhusu serikali kuu na serikali za mitaa wala usiwe na wasiwasi, mimi ndiye gwiji au kikwetu unaweza kuniita mwamba.

Tafadhali fafanua dhana hii ya doulat, nchi na serikali ... Kisiasa.
 
Mchambuzi,

Mimi nimemsoma vizuri hapo Zitto amesema kuwa amemaliza kazi ya kuwahudumia watu wa kigoma Kaskazini lakin hakupambanua ni huduma zipi amemaliza.


Sasa suala langu kwako . Hivi kazi za mbunge ni kujenga Hospitali, barabara, skuli na marikiti? Je fedhwa za kujenga hayo yote Mbunge huyo anazipata wapi?

Je unaweza kunipa mfano halisi wa mbunge yoyote ambaye amejenga skuli pamoja na Hospitali na marikiti kwa pesa zake binafsi huko Tgk?



Nasubiri ufafanuzi wako kwayo.

Ahsantum


Barux2;

Kwanza ningependa kutoa mchango kuhusu mihimili au matawi ya serikali. Kuna mifumo miwili mikubwa ya uendeshaji wa demokrasia. Mfumo wa kwanza ni wa matawi mawili na mfumo wa pili ni wa matawi matatu.

Katika mfumo wa matawi mawili, vyombo muhimu ni bunge na mahakama. Bunge linakuwa na jukumu la kutunga sheria na vilevile kuwa kuendesha utendaji wa serikali. Katika mfumo huu waziri mkuu ndio kiongozi wa serikali na ni lazima awe mbunge wa kupitisha na kundi la wabunge wengi. Kazi ya mahakama ni kulinda haki kwa mujibu wa sheria.

Katika mfumo wa matawi matatu, kuna bunge, mahakama, Ofisi ya utendaji wa shughuli za serikali (executive branch). Bunge linatunga sheria. Mahakama inalinda haki kwa mujibu wa sheria. Ofisi ya utendaji wa shughuli za serikali ambayo hipo chini ya rais inapanga na kufuatilia shughuli za serikali kutokana na sera zilizopo na kwa mujibu wa sheria.

Matawi ya serikali yanakuwepo kwa nia kuu mbili. Kwanza mgawanyo wa kazi hili kurahisisha ufanisi. Na pili kuweka mizani ya kuwajibika (Check and balance).

Tukirudi kwa muundo wa serikali ya Tanzania, pande zote mbili za muungano zilianza na serikali za matawi mawili. Kwa kudanganyana, tunaamini tuna mfumo wa matawi matatu. Lakini kiutendaji serikali ina matawi 2.5, 2, au 1.5. Hii yote inategemea na wakati.

Tukirudi kwenye maswali ya posti yako, sio kazi ya mbunge kujenga shule, barabara au vitu vingine. Kazi ya mbunge ni kutunga sheria. Katika nchi zingine (sina uhakika na Tanzania), bajeti ya serikali ambayo ndio inayojenga shule, barabara na kutoa huduma zingine ni sheria ya nchi. Bajeti inapitiswa bungeni na kusainiwa na rais kwa kutumia utaratibu wa utunzi wa sheria.

Hivyo mbunge anaweza kusema amejenga shule au barabara kwa kutoa hoja ambazo zitaifanya serikali kutenga bajeti ya kujenga shule au barabara katika jimbo lake.


Tukirudi tena kwenye mada ya mkoa wa Shinyinga na Kilimanjaro, mikoa hii inapata mgao wa matumizi kwa kupitia bajeti zilizopitishwa na bunge. Hivyo rais anaposaini bajeti, sheria inakuwa imepita. Kama Kilimanjaro wanapata pesa nyingi kuliko Shinyanga, wanapata hivyo kwa mujibu wa sheria na sio mapato ya tax.
 
Shukran, ila naomba wewe uliyesema bunge ni mhimili wa nchi utupe maana ya hiyo nchi uliyoisema. Kuhusu serikali kuu na serikali za mitaa wala usiwe na wasiwasi, mimi ndiye gwiji au kikwetu unaweza kuniita mwamba.

Tafadhali fafanua dhana hii ya doulat, nchi na serikali ... Kisiasa.
Kobello, tumetofautiana kwa mengi lakini kwa hapa nakuunga mkono 100%. Kabla sijachangia lolote nasubiri Barubaru na Mkandara watuambie Bunge ni mhimili wa nini, nchi au serikali...a very interesting and healthy debate na napendekeza mjadala huu ufunguliwe thread ya peke yake?

Samahani wote kwa kuwatoa kwenye mada; Chama cha ACT - Mpini wa CCM kumaliza upinzani.
 
Niende tena kwa Zakumi ulisema kuwa kwanini wachagga hawachangii maendeleo ya wasukuma na nk..

Sijui hapa ulisema kuchangia maendeleo wa jinsi gani.. Ila ninavyoelewa ni kuwa kila mtanzania ambaye ni mfanyakazi, mfanyabiashara, mkulima au mfugaji anawajibu wa kulipa kodi, na Serikali yake ambayo inakusanya hizi kodi inawajibu wa kuwaletea wananchi wake huduma ambazo zitafanya kuwa kichocheo cha wananchi wa eneo husika kujiletea maendeleo.

Ni wajibu wa serikali inayokusanya kodi, kujenga barabara, kujenga mashule,kujenga vyuo, kutengeneza ajira kwa waitimu wake,kujenga mahospital, kuleta umeme, kuvuta maji na nk. Pale serikali inaposhindwa kupeleka hivi vitu katika mikoa husika either kwa kutokuwa na pesa ya kutosha ua kwa ufisadi jambo ambalo limezooeleka hapa nchini mwetu hilo si kosa la mchanga au mhaya au kabila lolote lile. Maana wao kwa umoja wao kama watanzania wametimiza wajibu wao wa kulipa kodi. Na iwepo ikotoke mkoa fulani kwa kona muhimu wa barabara, na kuona kuwa serikali haina uwezo, au haioni muhimu wa kujenga barabara mkoa husika,na watu wa mkoa ule wakaamua wao kuchangishana pesa, na wakajenga barbara kwa nguvu zao basi ili ni jambo la kujivunia na jambo la kuigwa. Si lazima wa mtu kutoka mkoa fulani kwenda mkoa mwingine kwa minajiri ya kujengea watu wa mkoa husika barabara, au kisima cha maji, au kuwaimiza kupeleka watoto wao bali ni wajibu wa watu wa mkoa fulani kuona muhimu wa kujiletea wao maendeleo kwa kuiga mkoa uliofanya hivyo. (ok hapa viongozi wanahusika zaidi katika kushawishi watu kujiletea maendeleo). Hiyo basi utaona kuwa Mchagga /msukuma/Mhaya anasaidia maendeleo pale anapotimiza wajibu wake wa kulipa kod.


Linapokuja swala la nchi za nje kutusaidia kuleta maendeleo hili nalo linahitaji uzi wake, Maana kwa uelewa wangu hakuna nchi yeyote ile ambayo imewahi kupata maendeleo kwa misaada. Hawa watu wanachofanya ni kutupa pesa, hii haitusaidi bali inatufanya kuwa na akili tegemezi, (ni kama unapokuwa nyumbani kuna akiba fulani hiko kabati, basi utakapopata shida yeyote ya pesa akili itakutuma kwenda kwenye kabati kuchua hiyo pesa, huwezi kuwaza zaidi ya hapo) wanatakiwa kutupa ujuzi, kutufundisha jinsi ya kupata pesa si kwa kutuletea pesa. Hebu angalia miaka 50 kila siku ya Mungu tunapokea misaada ya pesa kutoka mataifa mbali mbali hebu niambie mbona bado matatizo yetu yako pale pale? Sasa kama 50 yumepewa misaaada/tumesaidiwa katika maendeleo na mpaka sana safari bado ni ndefu je hii misaada ni muhimu wowote katika swal zima la kujiletea maendeleo? Kwanini wasitupe ujuzi, wakatujengea viwanda,wakatujenga vyou na nk? si kwamba hawawezi bali wakikujengea viwanda na kukupa elimu hawataweza kukutalawa tena kupita mlango wa misaada.

Alinda:

Kwa mujibu wa ushahidi uliotoa, hitimisho ni kuwa mluguru, mpemba, mmakonde naye anachangia maendeleo ya msukuma. Ukweli wa mambo naona vigumu kuamini kuwa kila kabila Tanzania linachangia maendeleo ya msukuma.

Kodi sio chachu za maendeleo. Na wakati mwingine kodi ni chachu ya umasikini. Hivyo tusijenge hoja ya maendeleo kwa kutumia miwani ya kodi pekee yake.

Maendeleo yanatokana na matumizi mazuri ya local resources.
 
Kobello, tumetofautiana kwa mengi lakini kwa hapa nakuunga mkono 100%. Kabla sijachangia lolote nasubiri Barubaru na Mkandara watuambie Bunge ni mhimili wa nini, nchi au serikali...a very interesting and healthy debate na napendekeza mjadala huu ufunguliwe thread ya peke yake?

Samahani wote kwa kuwatoa kwenye mada; Chama cha ACT - Mpini wa CCM kumaliza upinzani.

Mag3.

Tuliza munkar nimeshafafanua kwa kina sana suala lako. Naomba soma vizuri post zangu za hapo juu na kama utakuwa ujatosheka basi Bismillah.

Pole sana.
 
Barux2;

Kwanza ningependa kutoa mchango kuhusu mihimili au matawi ya serikali. Kuna mifumo miwili mikubwa ya uendeshaji wa demokrasia. Mfumo wa kwanza ni wa matawi mawili na mfumo wa pili ni wa matawi matatu.

Katika mfumo wa matawi mawili, vyombo muhimu ni bunge na mahakama. Bunge linakuwa na jukumu la kutunga sheria na vilevile kuwa kuendesha utendaji wa serikali. Katika mfumo huu waziri mkuu ndio kiongozi wa serikali na ni lazima awe mbunge wa kupitisha na kundi la wabunge wengi. Kazi ya mahakama ni kulinda haki kwa mujibu wa sheria.

Katika mfumo wa matawi matatu, kuna bunge, mahakama, Ofisi ya utendaji wa shughuli za serikali (executive branch). Bunge linatunga sheria. Mahakama inalinda haki kwa mujibu wa sheria. Ofisi ya utendaji wa shughuli za serikali ambayo hipo chini ya rais inapanga na kufuatilia shughuli za serikali kutokana na sera zilizopo na kwa mujibu wa sheria.

Matawi ya serikali yanakuwepo kwa nia kuu mbili. Kwanza mgawanyo wa kazi hili kurahisisha ufanisi. Na pili kuweka mizani ya kuwajibika (Check and balance).

Tukirudi kwa muundo wa serikali ya Tanzania, pande zote mbili za muungano zilianza na serikali za matawi mawili. Kwa kudanganyana, tunaamini tuna mfumo wa matawi matatu. Lakini kiutendaji serikali ina matawi 2.5, 2, au 1.5. Hii yote inategemea na wakati.

Tukirudi kwenye maswali ya posti yako, sio kazi ya mbunge kujenga shule, barabara au vitu vingine. Kazi ya mbunge ni kutunga sheria. Katika nchi zingine (sina uhakika na Tanzania), bajeti ya serikali ambayo ndio inayojenga shule, barabara na kutoa huduma zingine ni sheria ya nchi. Bajeti inapitiswa bungeni na kusainiwa na rais kwa kutumia utaratibu wa utunzi wa sheria.

Hivyo mbunge anaweza kusema amejenga shule au barabara kwa kutoa hoja ambazo zitaifanya serikali kutenga bajeti ya kujenga shule au barabara katika jimbo lake.


Tukirudi tena kwenye mada ya mkoa wa Shinyinga na Kilimanjaro, mikoa hii inapata mgao wa matumizi kwa kupitia bajeti zilizopitishwa na bunge. Hivyo rais anaposaini bajeti, sheria inakuwa imepita. Kama Kilimanjaro wanapata pesa nyingi kuliko Shinyanga, wanapata hivyo kwa mujibu wa sheria na sio mapato ya tax.

Zakumi.

Naona wewe ndio umepondanga kabisa ingawa umejitahidi kukieleza kile nilichobainisha mimi katika maelezo yangu kuhusu rule of law.

kifupi nimesema hivi NCHI yoyote inayofuata utawala bora na utawala wa sharia ( rule of law) kama TZ inakuwa na mihimili mitatu mikuu inayofanya kazi huru kabisa kila mmoja. Nayo ni Serikali, bunge na mahakama.

Kazi za bunge ni kutunga sharia na mkuu wa bunge anaitwa SPEAKER.

Kazi ya mahakama ni kutafsiri sharia zinazotungwa na bunge na kiongozi mkuu wa mahakama anaitwa JAJI MKUU .

Kazi ya serikali ni kutekeleza sharia zinazotungwa na Bunge na mkuu wa serikali ni RAIS.

Na wakuu wote wa mihimili hiyo ni wa NCHI.

Sijui unataka ziada gani tena hapo.

pole sana
 
Mag3.

Tuliza munkar nimeshafafanua kwa kina sana suala lako. Naomba soma vizuri post zangu za hapo juu na kama utakuwa ujatosheka basi Bismillah.

Pole sana.
Kuna watu hutafuta Ubishani kwa hiyo zoea tabia hii itakufuata hata kwa maandishi tu ukikosea.
 
Zakumi.

Naona wewe ndio umepondanga kabisa ingawa umejitahidi kukieleza kile nilichobainisha mimi katika maelezo yangu kuhusu rule of law.

kifupi nimesema hivi NCHI yoyote inayofuata utawala bora na utawala wa sharia ( rule of law) kama TZ inakuwa na mihimili mitatu mikuu inayofanya kazi huru kabisa kila mmoja. Nayo ni Serikali, bunge na mahakama.

Kazi za bunge ni kutunga sharia na mkuu wa bunge anaitwa SPEAKER.

Kazi ya mahakama ni kutafsiri sharia zinazotungwa na bunge na kiongozi mkuu wa mahakama anaitwa JAJI MKUU .

Kazi ya serikali ni kutekeleza sharia zinazotungwa na Bunge na mkuu wa serikali ni RAIS.

Na wakuu wote wa mihimili hiyo ni wa NCHI.

Sijui unataka ziada gani tena hapo.

pole sana


Inawezekana lugha ya kiswahili ina upungufu wa misamiati. Chombo cha utendaji (Ofisi ya rais, makamu wa rais na baraza la mawaziri) ni sehemu ya serikali. Au kwa jina jingine executive branch of the government. Chombo hiki pamoja na bunge na mahakama vinafanya serikali.

By the way sio lazima nchi iwe na mihimili hiyo mitatu hili iwe nchi ya kufuata sheria. Hiyo system ya mihimili mitatu ni muundo ulioanza Marekani hili kuwe na check and balance. Wengine tunaiga kwa mafanikio yanayotofautiana.

Kwa mfano kwa Tanzania, baraza la mawaziri linaundwa na wabunge. Hivyo kwa Tanzania huwezi kuwa na serikali bila kuwa na bunge. Na kwa mantiki hiyo Tanzania haina mihimili mitatu. Ina mihimili 2 au 2.5.

Kuhusiana na bunge, chombo hicho kinaongozwa kwa kura za wengi. Mamlaka ya speaker yapo kwenye kuongoza taratibu za bunge. Lakini hana sauti.

Kuhusiana na utunzi wa sheria, mpaka rais apige saini, ndipo mswada unakuwa sheria. Hivyo sio wabunge pekee yao wanaotunga sheria. Rais naye yumo kwenye process.

Kuhusu majaji ni rais anayefanya uteuzi wa majaji. Hivyo huwezi kusema kuwa mihimili ya kiserikali ni huru. Hata nchini Marekani majaji wamegawanyika kutokana siasa za warais waliowateua.

Kuhusiana na mahakama, Tanzania nayo inafuata common law. Hivyo sio kila sheria imo kitabuni.
 
Kuna watu hutafuta Ubishani kwa hiyo zoea tabia hii itakufuata hata kwa maandishi tu ukikosea.
Granted, sasa twende taratibu Mkandara, naanza na Kobello;
Bunge ni mhimili wa nini?
Kobello please. Bunge ni muhimuli wa Kidemokrasia wenye uwakilishi wa matakwa ya wananchi. Na ndani yake, matakwa ya wengi ndio huwa represented. Upande mwingine Serikali hushughulikia mambo ya utawala kulingana na mahitaji ya wananchi.
Mkandara,
Bunge ni mhimili wa kidemokrasia? Umesoma Wapi hili.
Do you really know what "government" means? Kwanini unataka kuanzisha ubishi kwamba bunge sio sehemu Ya serikali? Do you know anything about separation of powers? Serikali ina mihimili mitatu - executive, legislative and judiciary. That's the bottom line.
Mkandara kapata upenyo mwingine wa kujadili mihimili ya serikali badala ya hoja ya Chama cha ACT ni mpini wa CCM kuumaliza upinzani.
BUNGE ni Muhimili wa nchi ,kama ilivyo kwa Serikali na Mahakama kuwa navyo ni mihimili ya nchi katika utekelezaji wa Utawala bora.
Je una zaidi? Basi Bismillah!
Akifafanua anaendelea;
Nguruvi3,
Kama nilivyofafanua huko Juu kwa Kobello maaana halisi ya mihimili mitatu ya utawala bora katika Nchi.
Ukitaka kujua watu ambao ni Sehemu ya Serikali ni mawaziri na wakuu wa wilaya na mikoa wanaoingia bungeni.
Pole sana
Kobello, tumetofautiana kwa mengi lakini kwa hapa nakuunga mkono 100%. Kabla sijachangia lolote nasubiri Barubaru na Mkandara watuambie Bunge ni mhimili wa nini, nchi au serikali...a very interesting and healthy debate na napendekeza mjadala huu ufunguliwe thread ya peke yake?
Mag3.

Tuliza munkar nimeshafafanua kwa kina sana suala lako. Naomba soma vizuri post zangu za hapo juu na kama utakuwa ujatosheka basi Bismillah.

Pole sana.
Barux2;
Kwanza ningependa kutoa mchango kuhusu mihimili au matawi ya serikali. Kuna mifumo miwili mikubwa ya uendeshaji wa demokrasia. Mfumo wa kwanza ni wa matawi mawili na mfumo wa pili ni wa matawi matatu.

Matawi ya serikali yanakuwepo kwa nia kuu mbili. Kwanza mgawanyo wa kazi hili kurahisisha ufanisi. Na pili kuweka mizani ya kuwajibika (Check and balance).
Zakumi.
Naona wewe ndio umepondanga kabisa ingawa umejitahidi kukieleza kile nilichobainisha mimi katika maelezo yangu kuhusu rule of law.

kifupi nimesema hivi NCHI yoyote inayofuata utawala bora na utawala wa sharia ( rule of law) kama TZ inakuwa na mihimili mitatu mikuu inayofanya kazi huru kabisa kila mmoja. Nayo ni Serikali, bunge na mahakama.

Sijui unataka ziada gani tena hapo.
pole sana
Inawezekana lugha ya kiswahili ina upungufu wa misamiati. Chombo cha utendaji (Ofisi ya rais, makamu wa rais na baraza la mawaziri) ni sehemu ya serikali. Au kwa jina jingine executive branch of the government. Chombo hiki pamoja na bunge na mahakama vinafanya serikali.
Bravo kwa wote, a very healthy debate indeed! How I wish it had its own thread! Nadhani kinachogomba ni swali, je serikali ni nini? Je bila mhimili mojawapo kati ya hizi tatu tunaweza kuwa na serikali? Je kuna chombo chochote mfano serikali kinaweza kuendeshwa bila sheria? Nawatakia mjadala mwema.
3-legged-stool.jpg
 
Last edited by a moderator:
Granted, sasa twende taratibu Mkandara, naanza na Kobello;





Akifafanua anaendelea;






Bravo kwa wote, a very healthy debate indeed! How I wish it had its own thread! Nadhani kinachogomba ni swali, je serikali ni nini? Je bila mhimili mojawapo kati ya hizi tatu tunaweza kuwa na serikali? Je kuna chombo chochote mfano serikali kinaweza kuendeshwa bila sheria? Nawatakia mjadala mwema.
View attachment 255445

Ndio tunarudi pale pale katika masuala yangu.

Serikali ni nini?
Nchi ni nini?
Dola ni nini?

Kwani wengi wanasahau tofauti za maneno hayo na kutumia udhaifu wa kiswahili kujenga hoja mfano kutumia neno Executive bila kujua hilo linaingia kama serikali.
Kwani kiongozi wa Executive branch ni raisi wa nchi.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom