Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Zakumi.

Naona wewe ndio umepondanga kabisa ingawa umejitahidi kukieleza kile nilichobainisha mimi katika maelezo yangu kuhusu rule of law.

kifupi nimesema hivi NCHI yoyote inayofuata utawala bora na utawala wa sharia ( rule of law) kama TZ inakuwa na mihimili mitatu mikuu inayofanya kazi huru kabisa kila mmoja. Nayo ni Serikali, bunge na mahakama.

Kazi za bunge ni kutunga sharia na mkuu wa bunge anaitwa SPEAKER.

Kazi ya mahakama ni kutafsiri sharia zinazotungwa na bunge na kiongozi mkuu wa mahakama anaitwa JAJI MKUU .

Kazi ya serikali ni kutekeleza sharia zinazotungwa na Bunge na mkuu wa serikali ni RAIS.

Na wakuu wote wa mihimili hiyo ni wa NCHI.

Sijui unataka ziada gani tena hapo.

pole sana
Speaker siyo mkuu wa bunge Kama unavyoamini. Speaker ni kiongozi wa baraza LA taifa (national assembly) ambayo ni sehemu ya bunge. Rais pia ni mkuu wa sehemu nyingine ya bunge ambayo inaitwa "raisi".
Kwa nchi Kama US,speaker ni kiongozi wa lower house na seneti inaongozwa na seneta atayechaguliwa na maseneta wenzake.
Kwa hiyo hapo umeteleza kidogo.Rais ni mbunge mwenye nguvu sawa na wajumbe wa baraza LA taifa ambao pia ni wabunge Kama yeye.
 
Speaker siyo mkuu wa bunge Kama unavyoamini. Speaker ni kiongozi wa baraza LA taifa (national assembly) ambayo ni sehemu ya bunge. Rais pia ni mkuu wa sehemu nyingine ya bunge ambayo inaitwa "raisi".
Kwa nchi Kama US,speaker ni kiongozi wa lower house na seneti inaongozwa na seneta atayechaguliwa na maseneta wenzake.
Kwa hiyo hapo umeteleza kidogo.Rais ni mbunge mwenye nguvu sawa na wajumbe wa baraza LA taifa ambao pia ni wabunge Kama yeye.

Kobello.

Hapa tunaizungumzia Tanzania na sio nchi nyingine.

Na kama unataka tuongee katika level ya kimataifa twende jukwaa la kimatataifa nitakupa mengi sana kuhusu utaratibu huo uweze kulinganisha na Tz.Soma mada mkuu na maelezo kabla kukurupuka.


By the way vipi serikali ya mtaa ya manispaa ya nchi ya temeke. vipi umetembelea bunge na mahakama yao pale uwanja wa Taifa?
Hivi jina la Rais na Speaker wao ni nani vile?
 
Ndio tunarudi pale pale katika masuala yangu.

Serikali ni nini?
Nchi ni nini?
Dola ni nini?

Kwani wengi wanasahau tofauti za maneno hayo na kutumia udhaifu wa kiswahili kujenga hoja mfano kutumia neno Executive bila kujua hilo linaingia kama serikali.
Kwani kiongozi wa Executive branch ni raisi wa nchi.

Serikali au (Government) is nothing more than an institution (taasisi)
ambayo jukumu lake kubwa ni kutunga na kutekeleza sheria na sera mbalimbali ndani ya jamii husika. Serikali kama taasisi ina nguvu na pia mamlaka ya kutawala eneo husika la kijiografia pamoja na wakazi wanaoishi katika eneo hilo. MUHIMU: Uhusiano wa Serikali na mihimili mingine (bunge na mahakama) ipo katika muktadha wa “MAMLAKA” tu, basi. Mamlaka na nguvu hii ya serikali imegawanyika katika maeneo makuu matatu:

1. Bunge (lenye mamlaka ya kutunga sheria mbalimbali).
2. Executive - yenye mamlaka ya kushurutisha? (Enforce) utiifu wa sheria.
3. Judiciary - yenye mamlaka ya kufafanua au kuainisha sheria mbalimbali ili kuongoza shughuli za kila siku katika uendeshaji wa serikali - kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Watu wengi huchanganya dhana ya ‘state’ vis a vis ‘government’ kama vile ni kitu kile kile. Dhana hizi zina uhusiano wa karibu lakini havimaanishi kitu kimoja. Na hapo mchanganyiko kama wa Mkandara na wengine ndio hujitokeza.

Wakati Serikali ni “Taasisi”, state ni dhana ya kijiographia zaidi i.e. a state is a geographic entity. Any modern state inalazimika kuijunga na jumuiya ya kimataifa. Lakini ili "state" husika iweze kujiunga na mfumo wa kimataifa, ni lazima itambulike na states nyenzake duniani kwamba it’s a sovereign state. State itatambulika as a state ikiwa na haya:

1. It must have her fiscal system.
2 It must have her own constitution and
3. It must have her own sovereignty (freedom from external control).

Vile vile sifa kuu za any state ni hizi tatu:

1. Ina watu wa aina mbalimbali bila ya kujalisha idadi/wingi wao au utofauti wao kijinsia, kidini, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni n.k.

2. Huwa na eneo lake la ardhi bila ya kujalisha ukubwa eneo husika ili mradi eneo hilo lina uwezo wa kukidhi "mahitaji ya makazi" kwa watu wake.

3. Huwa na uhuru wa kutekeleza sera na sheria mbalimbali bila ya kuingiliwa na mataifa ya nje.

Watu wengi wanachanganya mjadala wa state and government kwamba ni kitu kimoja hasa kwa sababu kwa nchi ambazo zina practice ‘presidential system’, the head of STATE also tends to be the head of GOVERNMENT.
 
Last edited by a moderator:
Serikali au (Government) is nothing more than an institution (taasisi)
ambayo jukumu lake kubwa ni kutunga na kutekeleza sheria na sera mbalimbali ndani ya jamii husika. Serikali kama taasisi ina nguvu na pia mamlaka ya kutawala eneo husika la kijiografia pamoja na wakazi wanaoishi katika eneo hilo. MUHIMU: Uhusiano wa Serikali na mihimili mingine (bunge na mahakama) ipo katika muktadha wa "MAMLAKA" tu, basi. Mamlaka na nguvu hii ya serikali imegawanyika katika maeneo makuu matatu:

1. Bunge (lenye mamlaka ya kutunga sheria mbalimbali).
2. Executive - yenye mamlaka ya kushurutisha? (Enforce) utiifu wa sheria.
3. Judiciary - yenye mamlaka ya kufafanua au kuainisha sheria mbalimbali ili kuongoza shughuli za kila siku katika uendeshaji wa serikali - kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Watu wengi huchanganya dhana ya ‘state' vis a vis ‘government' kama vile ni kitu kile kile. Dhana hizi zina uhusiano wa karibu lakini havimaanishi kitu kimoja. Na hapo mchanganyiko kama wa Mkandara na wengine ndio hujitokeza.

Wakati Serikali ni "Taasisi", state ni dhana ya kijiographia zaidi i.e. a state is a geographic entity. Any modern state inalazimika kuijunga na jumuiya ya kimataifa. Lakini ili "state" husika iweze kujiunga na mfumo wa kimataifa, ni lazima itambulike na states nyenzake duniani kwamba it's a sovereign state. State itatambulika as a state ikiwa na haya:

1. It must have her fiscal system.
2 It must have her own constitution and
3. It must have her own sovereignty (freedom from external control).

Vile vile sifa kuu za any state ni hizi tatu:

1. Ina watu wa aina mbalimbali bila ya kujalisha idadi/wingi wao au utofauti wao kijinsia, kidini, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni n.k.

2. Huwa na eneo lake la ardhi bila ya kujalisha ukubwa eneo husika ili mradi eneo hilo lina uwezo wa kukidhi "mahitaji ya makazi" kwa watu wake.

3. Huwa na uhuru wa kutekeleza sera na sheria mbalimbali bila ya kuingiliwa na mataifa ya nje.

Watu wengi wanachanganya mjadala wa state and government kwamba ni kitu kimoja hasa kwa sababu kwa nchi ambazo zina practice ‘presidential system', the head of STATE also tends to be the head of GOVERNMENT.
Mkuu yote haya tunayafahamu ila tunazungumzia kinachoeleweka. Niaposema Serikali ya Mitaa haina maana kuna Bunge na Mahakama, hivyo neno serikali lazima tulitumie kwa maelewano mnapokuwa mkijadili. Hayo ndio mawazo yangu ya kwamba Tuna mihimili mitatu 1.Serikali, 2. Bunge na 3. Mahakama na kila mmoja una functions zake.

Hivyo basi mtu anapozungumzia serikali hana maana mnayotaka kuisema kwa sababu nchi nyinginezo mfumo wetu sisi rais angekuwa kiongozi wa NCHI na Waziri mkuu ndiye kiongozi wa Serikali, rais anakuwa kama Ceremonial tu lakini sisi tumemfanya Rais kuwa ndio kila kitu na waziri mkuu kuwa msimamizi wa mambo ya Bara. Rais humchagua waziri mkuu kama mwakilishi wake Bungeni katika mambo ya Bara kitu ambacho leo hii sijui kama bado ndivyo ilivyo au imebadilika, na kwa nini rais asimchague pia Waziri mkuu wa Zanzibar hilo sijui?. Nchi nyingine Waziri mkuu huchaguliwa na Wananchi hali sisi huteuliwa na rais.

Hivyo, tuelewane tunazungumzia kitu gani laa sivyo tutapoteza kabisa maana kwa sababu Ukisema Pinda ni waziri mkuu wa Tanzania wasomi wa nchi nyingine watatafsiri tofauti kabisa. Sina sababu ya kuingilia ubishi huu ambao kwangu haunisaidii kitu zaidi ya watu kubishana juu ya Tafsiri..
 
Mkuu yote haya tunayafahamu ila tunazungumzia kinachoeleweka. Niaposema Serikali ya Mitaa haina maana kuna Bunge na Mahakama, hivyo neno serikali lazima tulitumie kwa maelewano mnapokuwa mkijadili. Hayo ndio mawazo yangu ya kwamba Tuna mihimili mitatu 1.Serikali, 2. Bunge na 3. Mahakama na kila mmoja una functions zake.
Mkandara, naona unapenda tu ubishi, basi. Unatumiaje neno 'mhimili' bila ya kusema ni wa nini? Hivi kweli unamweleza mtu kwamba kwa mfano - 'kuna matawi matatu' bila ya kusema ni matawi ya kitu gani? bila ya kusema shina ni nini? mhimili unawezaje to exist in a vacuum?

Hivyo basi mtu anapozungumzia serikali hana maana mnayotaka kuisema kwa sababu nchi nyinginezo mfumo wetu sisi rais angekuwa kiongozi wa NCHI na Waziri mkuu ndiye kiongozi wa Serikali, rais anakuwa kama Ceremonial tu lakini sisi tumemfanya Rais kuwa ndio kila kitu na waziri mkuu kuwa msimamizi wa mambo ya Bara. Rais humchagua waziri mkuu kama mwakilishi wake Bungeni katika mambo ya Bara kitu ambacho leo hii sijui kama bado ndivyo ilivyo au imebadilika, na kwa nini rais asimchague pia Waziri mkuu wa Zanzibar hilo sijui?. Nchi nyingine Waziri kkuu huchaguliwa na Wananchi hali sisi huteuliwa na rais.

Hivyo, tuelewane tunazungumzia kitu gani laa sivyo tutapoteza kabisa maana kwa sababu Ukisema Pinda ni waziri mkuu wa Tanzania nchi nyingine watatafrisi tofauti kabisa. Sina sababu ya kuingilia ubishi huu ambao kwangu haunisaidii kitu zaidi ya watu kubiishanajuu ya Tafsiri..

Unachanganya tu mambo. Dhana ya serikali haipo context specific. Serikali ni serikali tu. Serikali ya mtaa ni subordinate to central government (serikali kuu). Serikali ya mtaa haina katiba. Rejea mjadala wangu wa awali kuhusu vigezo vya 'state'.

Yote unayojadili hapo, kwa kujua au kwa kutojua, common denominator ni SERIKALI. Kuna aina nyingi za serikali lakini zinazotambulika zaidi ni pamoja na hizi zifuatazo:

1. A monarchy (absolute monarchy)-huu ni utawala wa serikali hii unatokana na haki za kurithi- basically ni hereditary rights ambapo mfalme au malkia anakuwa na absolute power, hakuna katiba inayomzuia kufanya lolote.

2. Constitutional monarchy - hii ni serikali, na hapa kunakuwepo na katiba ambayo inaanisha na kuamua madaraka ya malkia/mfalme ni yepi na mipaka ya madaraka husika.

3. Theocracy - utawala wa serikali ya aina hii hufuata imani fulani ya dini.

4. Oligarchy - utawala wa serikali ya aina hii unahodhiwa na watu wachache sana ndani ya jamii.

5. Dictatorship - utawala wa serikali ya aina hii haujali katiba, sheria na hauruhusu mawazo mbadala hasa upinzani.

6. Constitutional republic - hapa supreme power ipo mikononi mwa wananchi ambao huchagua viongozi wao wa kuwawakilisha katika ngazi mbalimbali.

Serikali ni ALPHA na OMEGA.

Je sasa tunaweza kurudi kwenye mada juu ya ACT Mpini wa CCM Kumaliza Upinzani?
 
Serikali au (Government) is nothing more than an institution (taasisi)
ambayo jukumu lake kubwa ni kutunga na kutekeleza sheria na sera mbalimbali ndani ya jamii husika. Serikali kama taasisi ina nguvu na pia mamlaka ya kutawala eneo husika la kijiografia pamoja na wakazi wanaoishi katika eneo hilo. MUHIMU: Uhusiano wa Serikali na mihimili mingine (bunge na mahakama) ipo katika muktadha wa “MAMLAKA” tu, basi. Mamlaka na nguvu hii ya serikali imegawanyika katika maeneo makuu matatu:

1. Bunge (lenye mamlaka ya kutunga sheria mbalimbali).
2. Executive - yenye mamlaka ya kushurutisha? (Enforce) utiifu wa sheria.
3. Judiciary - yenye mamlaka ya kufafanua au kuainisha sheria mbalimbali ili kuongoza shughuli za kila siku katika uendeshaji wa serikali - kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Watu wengi huchanganya dhana ya ‘state’ vis a vis ‘government’ kama vile ni kitu kile kile. Dhana hizi zina uhusiano wa karibu lakini havimaanishi kitu kimoja. Na hapo mchanganyiko kama wa Mkandara na wengine ndio hujitokeza.

Wakati Serikali ni “Taasisi”, state ni dhana ya kijiographia zaidi i.e. a state is a geographic entity. Any modern state inalazimika kuijunga na jumuiya ya kimataifa. Lakini ili "state" husika iweze kujiunga na mfumo wa kimataifa, ni lazima itambulike na states nyenzake duniani kwamba it’s a sovereign state. State itatambulika as a state ikiwa na haya:

1. It must have her fiscal system.
2 It must have her own constitution and
3. It must have her own sovereignty (freedom from external control).

Vile vile sifa kuu za any state ni hizi tatu:

1. Ina watu wa aina mbalimbali bila ya kujalisha idadi/wingi wao au utofauti wao kijinsia, kidini, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni n.k.

2. Huwa na eneo lake la ardhi bila ya kujalisha ukubwa eneo husika ili mradi eneo hilo lina uwezo wa kukidhi "mahitaji ya makazi" kwa watu wake.

3. Huwa na uhuru wa kutekeleza sera na sheria mbalimbali bila ya kuingiliwa na mataifa ya nje.

Watu wengi wanachanganya mjadala wa state and government kwamba ni kitu kimoja hasa kwa sababu kwa nchi ambazo zina practice ‘presidential system’, the head of STATE also tends to be the head of GOVERNMENT.

Mchambuzi.

Ahsantum kwa ufafanuzi wako.

Mimi suala langu lilelile nini Executive huko Tz na CEO wake ni nani?

kwa mimi ninavyojuwa Executive huko Tz ni baraza la mawaziri na mwenyekiti wake ni Rais wa nchi.

Vile vile kuna AG ambaye ni mwanasharia mkuu wa serikali nae anaingia bungeni je huyu vile vile anakuwa mwanasheria au mshauri wa bunge mambo ya sharia.

Waziri mkuu anaitwa kiongozi wa serikali bungeni. je kama bunge ni muhimili wa serikali ina masna PM ni kiongozi wa bunge?

Lakin wabunge wanapouliza maswali bungeni je wale wanaotoa majibu ni executive au serikali.

Naomba ufafanuzi wako.

Ahsantum
 
Last edited by a moderator:
Mkandara, naona unapenda tu ubishi, basi. Unatumiaje neno 'mhimili' bila ya kusema ni wa nini? Hivi kweli unamweleza mtu kwamba kwa mfano - 'kuna matawi matatu' bila ya kusema ni matawi ya kitu gani? bila ya kusema shina ni nini? mhimili unawezaje to exist in a vacuum?



Unachanganya tu mambo. Dhana ya serikali haipo context specific. Serikali ni serikali tu. Serikali ya mtaa ni subordinate to central government (serikali kuu). Serikali ya mtaa haina katiba. Rejea mjadala wangu wa awali kuhusu vigezo vya 'state'.

Yote unayojadili hapo, kwa kujua au kwa kutojua, common denominator ni SERIKALI. Kuna aina nyingi za serikali lakini zinazotambulika zaidi ni pamoja na hizi zifuatazo:

1. A monarchy (absolute monarchy)-huu ni utawala wa serikali hii unatokana na haki za kurithi- basically ni hereditary rights ambapo mfalme au malkia anakuwa na absolute power, hakuna katiba inayomzuia kufanya lolote.

2. Constitutional monarchy - hii ni serikali, na hapa kunakuwepo na katiba ambayo inaanisha na kuamua madaraka ya malkia/mfalme ni yepi na mipaka ya madaraka husika.

3. Theocracy - utawala wa serikali ya aina hii hufuata imani fulani ya dini.

4. Oligarchy - utawala wa serikali ya aina hii unahodhiwa na watu wachache sana ndani ya jamii.

5. Dictatorship - utawala wa serikali ya aina hii haujali katiba, sheria na hauruhusu mawazo mbadala hasa upinzani.

6. Constitutional republic - hapa supreme power ipo mikononi mwa wananchi ambao huchagua viongozi wao wa kuwawakilisha katika ngazi mbalimbali.

Serikali ni ALPHA na OMEGA.

Je sasa tunaweza kurudi kwenye mada juu ya ACT Mpini wa CCM Kumaliza Upinzani?
Nitazidi kusema Ubishi mwingine siuwezi, maana alichoandika Barubaru kinaeleweka. Ndio maana mimi hukataa watu wanahoji Chadema imetuletea nini? wakati sii chama tawala wala hawaundi serikali ya CCM. Bunge ni wawakilishi wa wananchi tu na ndio maana kazi yao imesema ni pamoja na kuisimamia serikali kwa maana kamili ya kwamba kuna mhimili (serikali) unaotakiwa kusimamiwa.

Laa sivyo utawezaje kutunga sheria ya Bunge Kuisimamia serikali kumbe ina maana wajisimamie wenyewe. Vile vile kwa nchi nyingine hiyo serikali utakuwa ina viongozi wake (mawaziri) sio Wabunge. Hivyo kwa kukosa neno la matumizi ya kiswahili kinachoeleweka neno serikali limechukua nafasi ya Utendaji katika mijadala mingi kama sio yote nchini.

Na kama wewe unakubali serikali ya Mitaa ni sehemu ya serikali, kwa nini unakataa kuwa serikali hii inayozungumziwa ya (Utendaji) ni sehemu pia ya Serikali kuu unayoijua wewe. Hata wadhungu wenyewe husema - A Majority party will form a Government?
 
Nitazidi kusema Ubishi mwingine siuwezi, maana alichoandika Barubaru kinaeleweka. Ndio maana mimi hukataa watu wanahoji Chadema imetuletea nini? wakati sii chama tawala wala hawaundi serikali ya CCM. Bunge ni wawakilishi wa wananchi tu na ndio maana kazi yao imesema ni pamoja na kuisimamia serikali kwa maana kamili ya kwamba kuna mhimili (serikali) unaotakiwa kusimamiwa.

Laa sivyo utawezaje kutunga sheria ya Bunge Kuisimamia serikali kumbe ina maana wajisimamie wenyewe. Vile vile kwa nchi nyingine hiyo serikali utakuwa ina viongozi wake (mawaziri) sio Wabunge. Hivyo kwa kukosa neno la matumizi ya kiswahili kinachoeleweka neno serikali limechukua nafasi ya Utendaji katika mijadala mingi kama sio yote nchini.

Na kama wewe unakubali serikali ya Mitaa ni sehemu ya serikali, kwa nini unakataa kuwa serikali hii inayozungumziwa ya (Utendaji) ni sehemu pia ya Serikali kuu unayoijua wewe. Hata wadhungu wenyewe husema - A Majority party will form a Government?
Mkandara,
Inawezekana Sina uelewa wa kutosha kuhusu Suala hili, Pengine nibaki msomaji kuliko mchangiaji. Nitashiriki Zaidi Kwenye hoja Ya ACT mpini wa CCM, hasa kusuburia Majibu yenu kuhusiana Na maswali Yangu kufuatia clip Ya TUJITEGEMEE iliyohusu hotuba Ya Zitto Tabora.
 
Last edited by a moderator:
Mkandara,
Inawezekana Sina uelewa wa kutosha kuhusu Suala hili, Pengine nibaki msomaji kuliko mchangiaji. Nitashiriki Zaidi Kwenye hoja Ya ACT mpini wa CCM, hasa kusuburia Majibu yenu kuhusiana Na maswali Yangu kufuatia clip Ya TUJITEGEMEE iliyohusu hotuba Ya Zitto Tabora.
Mkuu sijasema huna uelewa wa kutosha isipokuwa mnataka kusahihisha kitu mnachojua kabisa Barubaru alikuwa na maana gani na ndio maana nikauliza kwani inaposemwa Majority party will form a Government isiwe kosa wangesema form Executive?.. Kwa sababu neno hili linatumika hata kuichambua CCM, hatusemi Mhimili wa Utendaji bali serikali ya CCM na inaeleweka.

Kwa hiyo mmetoka Shinyanga sasa ni Tabora mtachambua hotuba ngapi ili kuthibitisha kuwa ACT ni mpini wa CCM au tumetoka na huko sasa ni Zitto mtenganishi ili hali hotuba za Mbowe ya sera za Chadema zinahusu Majimbo? katika utekelezaji wa sera hizo huwa wanamaanisha nini? Ukisema Zitto kachukua sera za Chadema na kizifanya madaraka mikoani nitakusikiliza tuangalie tofauti iliyopo kati ya Majimbo na Madaraka mikoani.
 
Ndio tunarudi pale pale katika masuala yangu.

Serikali ni nini?
Nchi ni nini?
Dola ni nini?

Kwani wengi wanasahau tofauti za maneno hayo na kutumia udhaifu wa kiswahili kujenga hoja mfano kutumia neno Executive bila kujua hilo linaingia kama serikali.
Kwani kiongozi wa Executive branch ni raisi wa nchi.

Barubaru:

Sikutumia udhaifu wa kiswahili kujenga hoja. Umeleta hoja ya mihimili mitatu ya serikali na kusema kuwa Tanzania ina mihimili mitatu na iliyo huru.

Ukweli wa mambo mfumo wa utawala wa Tanzania sio wa mihimili mitatu japokuwa kuna watendaji wa utawala (executive branch), wabunge, na mahakama.

Kinadharia tunaambiwa ni mfumo wa mihimili mitatu kwa kufananisha na mfumo wa utawala wa Marekani. Lakini kiutendaji hakuna ukweli huo.

Katiba ya Marekani inatoa moja kwa moja vipengele vya kuwa na mihimili mitatu na uhuru wa mihimili hiyo ya serikali. Katiba ya Tanzania inayotumika sasa haisemi kitu chochote kuhusu serikali au mfumo wa utawala wa mihimili mitatu yenye uhuru.

Hivyo kiswahili sio tatizo kwa sababu lugha yoyote ni lazima ijitosheleze katika mazingira yake. Tatizo ni kujadili mfumo wa utawala wa Tanzania wa kutoka hewani. Tanzania sio nchi ya utawala wa mihimili matatu.
 
Barubaru:

Sikutumia udhaifu wa kiswahili kujenga hoja. Umeleta hoja ya mihimili mitatu ya serikali na kusema kuwa Tanzania ina mihimili mitatu na iliyo huru.

Ukweli wa mambo mfumo wa utawala wa Tanzania sio wa mihimili mitatu japokuwa kuna watendaji wa utawala (executive branch), wabunge, na mahakama.

Kinadharia tunaambiwa ni mfumo wa mihimili mitatu kwa kufananisha na mfumo wa utawala wa Marekani. Lakini kiutendaji hakuna ukweli huo.

Katiba ya Marekani inatoa moja kwa moja vipengele vya kuwa na mihimili mitatu na uhuru wa mihimili hiyo ya serikali. Katiba ya Tanzania inayotumika sasa haisemi kitu chochote kuhusu serikali au mfumo wa utawala wa mihimili mitatu yenye uhuru.

Hivyo kiswahili sio tatizo kwa sababu lugha yoyote ni lazima ijitosheleze katika mazingira yake. Tatizo ni kujadili mfumo wa utawala wa Tanzania wa kutoka hewani. Tanzania sio nchi ya utawala wa mihimili matatu.
Hiyo kweli kabisa, na ndio yawezekana tatizo kubwa la mambo mengine yoote ya kimfumo linaanzia hapo.
 
Mkandara, Waberoya, Zakumi, Ritz, Adharusi. Nawaombeni tuache siasa za kinafiki na kishabiki, nawaombeni msuze nyuso zenu zilizojaa masizi hivyo kutoweza kuona jinsi gani Zitto ni tapeli na mlaghai mkubwa kwa wananchi. Tutafafanua hoja kwa hoja:

Katika uzinduzi wa ACT Wazalendo kufuatia ZItto na akina kitila mkumbo kuwapora watanzania wengine chama chao cha ACT Tanzania, Zitto alitamka kwamba amejiunga na chama cha ACT Wazalendo kwa kuwa chama hicho ndiyo chama pekee nchini kinachokubaliana na itikadi ya ujamaa na kinaamini katika falsafa ya Nyerere. Ndugu zangu, sijui kwanini hamtaki kukubali kwamba hakuna ukweli wowote katika kauli hizi za supreme leader zitto. Zitto analenga kutapeli na kudanganya umma kwa maslahi binafsi. Kwanza, Zitto sio mjamaa, na pili, hakuna jambo hata moja ambalo tunaweza kumfananisha Zitto na Mwalimu Nyerere. Hakuna! Kwa mfano:

· Tofauti na zitto, nyerere alikuwa na maono; zitto hana maono.
· Tofauti na zitto, nyerere hakuwa msaliti; zitto ni msaliti,
· Tofauti na zitto, nyerere alitenganisha maisha yake binafsi na uongozi; zitto anatumia uongozi wake kujikweza na kujinufaisha kibinafsi.
· Tofauti na zitto, kwa Mwalimu uongozi ulikuwa ni utumishi kwa wananchi, uongozi haukuwa ni kujikweza, kujinufaisha binafsi, na kujitafutia sifa kwa nguvu;
· Tofauti na zitto, Mwalimu hakuwa kujiingiza katika mgongano wa maslahi;
· Tofauti na Zitto, Mwalimu, aliweka taifa lake mbele kwanza;
· Tofauti na zitto, mwalimu hakuwahi kugonganisha wanachama wa chama chake cha CCM kwa maslahi ya watu wengine waliopo nje ya chama.

Tukiangalia hata kwa macho ya usingizi, ni rahisi sana kubaini kwamba hakuna ujamaa katika Zitto, na hakuna Azimio la Arusha katika ACT. Zitto ni tapeli na mlaghai mkubwa kwa wananchi. Cha ajabu ni kwamba hata nyinyi mmeamua kwa akili zenu timamu kabisa kujiunga na utapeli huu na ulaghai huu. Mnautetea usiku na mchana.

Tulitazame kwa undani kidogo Azimio la Arusha. Azimio la Arusha katika sehemu inayozungumzia viongozi linasema yafuatayo:

1. “Kiongozi wa TANU au wa Serikali sharti awe mkulima aumfanyakazi na asishiriki katika jambo lo lote la kibepari au kikabaila.”

· Je Zitto anatosha hapa? Kati ya ubepari na ujamaa, Zitto anaishi maisha ya namna gani zaidi?

2. “Asiwe na hisa katika makampuni yo yote”.

Je, zitto anatosha katika hili? Tusisahau sakata la Leka Tukige Limited na Gombe Advisors Limited.

3. “Asiwe mkurugenzi katika kampuni ya kikabaila au kibepari”.

Rejea hoja ya hapo juu.

4. “Asiwe na mishahara miwili au zaidi”.

Je, zitto anatosha katika hili? Tusisahau ulaghai wake katika sakata la posho za wabunge. Vile vile, tusisahau jinsi gani ametuhumiwa kujinufaisha mara kwa mara na fedha za walipa kodi kupitia taasisi zilizokuwa chini ya kamati yake ya PAC, Tanapa na NSSF.

5. “Asiwe na nyumba ya kupangisha”.

Je anatosha katika hili?

6. “Viongozi tunaofikiria hapa ni wajumbe wa Halmashauri Kuu
ya Taifa, Mawaziri, Wabunge, Wakuu wa Vyama vilivyoshirikishwa na TANU, Wakuu wa Mashirika ya Kiserikali.”

Je si yumo humu kama mbunge (aliyejiuzulu)?

Katika madhumuni, Azimio la Arusha linasema hivi:

· “…Kuona kwamba Serikali inatoa nafasi zilizo sawa kwa wote,
wake kwa waume, bila kujali rangi, kabila, dini au hali.”

· “…Kuona kwamba Serikali inaondoa kila namna ya dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa na upotofu.”

Katika haya, zitto hatoshi kwani akiwa ACT amekuwa mstari wa mbele kuwagawa watanzania kwa makabila yao na hali zao za maisha.

Kwanini tumuamini tapeli, laghai na mchonganishi Zitto kwa kumpa dhamana ya uongozi?

Tumeshuhudia jinsi gani Zitto amekuwa mstari wa mbele akihubiri siasa za kibaguzi.

Kwanini tufanye kosa la kumpa mtu hatari kama huyu dhamana ya uongozi?

Pia zitto ametuhumiwa kujipatia fedha kutoka TANAPA na NSSF kwa njia za rushwa na ujanja ujanja. Hajawahi kukanusha tuhuma hii kwa hoja,

Azimio la Arusha pia linasema haya kuhusiana na Siasa ya Ujamaa, siasa ambayo Zitto analaghai wananchi kwamba yeye na ACT ndio inafuata misingi yake:

“Katika nchi ya Ujamaa kamili mtu hamnyonyi mtu, bali kila awezaye kufanya kazi hufanya kazi, na kila mfanya kazi hupata pato la haki kwa kazi aifanyayo na wala mapato ya wafanyakazi mbali mbali hayapitani mno.”

Hii ndio Tanzania ambayo tuliiona kupitia Azimio la Arusha, Tanzania ambayo Mwalimu alipigana usiku na mchana kuijenga kwa maslahi ya watanzania wote. Tofauti na hayo, tumeona jinsi gani Zitto amekuwa akilaghai watanzania kwa kuleta takwimu zilizojaa upotoshaji kwamba ipo baadhi ya mikoa ambayo inanyonya mikoa mingine. Kupitia takwimu za kodi ya mapato nchini, tumeona kwamba mikoa ambayo zitto amekuwa akiichonganisha na mikoa mingine kwa viel tu imepiga hatua kimaendeleo, kumbe ni mikoa ambayo imekuwa inapata mgao kutokana na jasho la wananchi wa mikoa hiyo (Makusanyo ya Kodi).

Azimio la arusha linazidi kulinda wananchi wa mikoa ya Kilimanjao na Arusha inayobaguliwa na ZItto pale linaposema kwamba:

MASHARTI YA MAENDELEO:

1. Juhudi:
“Kila mwananchi anataka maendeleo, lakini si kila mwananchi
anaelewa na kukubali masharti ya maendeleo. Sharti moja
kubwa ni JUHUDI”.

2. Maarifa:
“Sharti la pili la maendeleo ni MAARIFA. Juhudi bila maarifa haiwezi
kutoa matunda bora kama juhudi na maarifa.”

Nguruvi3 na wengine wamejadili suala hili kwa kina pale walipokuwa wanapingana na hoja za zitto za kuwabagua wananchi wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro. Hoja ya msingi ya Nguruvi3 katiak suala hili imekuwa kwamba maendeleo ya wananchi wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro ni matokeo ya “juhudi” na “maarifa” yao, kama jinsi azimio la arusha linavyoelekeza.

Tutazidi kuonyesha kwa hoja jinsi gani supreme leader Zitto ni tapeli na laghai wa kisiasa na kwamba, kama hatajirekebisha, basi huu ni wakati kwa watanzania kukaa mbali nae kama ukoma.

Hivi Mwalimu Nyerere alipokua na umri kama wa Zitto alikuaje...thamani yake imekua kubwa baada ya kuwa waziri mkuu wa Tanganyika,na baadae Rais,kwahiyo Zitto anatengeneza historia yake
 
Anatengeneza historia yake kilaghai na ya kugawa wananchi
Nyie tatizo lenu mnafikira mbaya sana, yaani kwa Mkristu kumfuata Yesu basi tayari unataka alingane na Yesu jambo ambalo haliwezekani isipokuwa hoja ya mtu ni kufuata mafundisho yake. Leo Zitto anatangaza kufuata mafundishio ya Nyerere tayari mnataka kumfananisha, wapi na wapi... Swala hapa jamani ni ACT mpini wa CCM haya ya kweli? Sio kwamba CDM wamechonga mpini wenyewe! ama ndio yale yale ya kwa mwoga huenda kicheko, kwa shujaa kilio!
 
Hivi Mwalimu Nyerere alipokua na umri kama wa Zitto alikuaje...thamani yake imekua kubwa baada ya kuwa waziri mkuu wa Tanganyika,na baadae Rais,kwahiyo Zitto anatengeneza historia yake
Hata Hitler alitengeneza historia.
 
Waswahili wanasema kila kitu na zama zake.

Hata siku moja huwezi kumfananisha Zitto na Nyerere kwa kigezo chochote kile kwani hawa watu wapo katika zama na nyakati tofauti. Hii ni sawa na kufananisha chumvi na Sukari.

Nyerere alikuwa mbabe na alipendwa kuogopwa na enzi zake hakuruhusiwa mtu yoyote kuhoji maamuzi ya Nyerere na aliyediriki kuhoji alipelekwa Exile kama si kupotezwa jambo ambalo leo hii kila kitu kipo wazi na kila mtu ana haki kuhoji lolote ilimuradi kufuata sharia na taratibu.

Enzi za Nyerere hakukuwa na uhuru wa kujieleza wala uhuru mpana wa kupata habari jambo ambalo leo kila kitu kipo wazi.

Zitto anachofuata nyayo za Nyerere ni katika tarbia na mwenendo wake kulingana na nyakati hizi.

Lakin mimi nashangaa mpaka sasa KWANINI ZITO ANAANDAMWA HIVI KWA KILA ANALONENA AU KUTENDA? AU CHADEMA WALIFIKIRI KUMVUA UANACHAMA NDIO UTAKUWA MWISHO WAKE KISIASAA?
 
Waswahili wanasema kila kitu na zama zake.

Hata siku moja huwezi kumfananisha Zitto na Nyerere kwa kigezo chochote kile kwani hawa watu wapo katika zama na nyakati tofauti. Hii ni sawa na kufananisha chumvi na Sukari.

Nyerere alikuwa mbabe na alipendwa kuogopwa na enzi zake hakuruhusiwa mtu yoyote kuhoji maamuzi ya Nyerere na aliyediriki kuhoji alipelekwa Exile kama si kupotezwa jambo ambalo leo hii kila kitu kipo wazi na kila mtu ana haki kuhoji lolote ilimuradi kufuata sharia na taratibu.

Enzi za Nyerere hakukuwa na uhuru wa kujieleza wala uhuru mpana wa kupata habari jambo ambalo leo kila kitu kipo wazi.

Zitto anachofuata nyayo za Nyerere ni katika tarbia na mwenendo wake kulingana na nyakati hizi.

Lakin mimi nashangaa mpaka sasa KWANINI ZITO ANAANDAMWA HIVI KWA KILA ANALONENA AU KUTENDA? AU CHADEMA WALIFIKIRI KUMVUA UANACHAMA NDIO UTAKUWA MWISHO WAKE KISIASAA?
Kifupi naambia hawa jamaa zangu kuwa kwa mwoga huenda kicheko kwa shujaa kilio, sisi wengine hiki ni kilio kwetu...
 
Hiyo video inafuguliwa na browser gani maana youtube inakataa.
 
https://www.youtube.com/watch?v=AddzBZS1Eu8k

Leo katika pekua pekua nimekumbana na hiyo clip ya Zitto akiwa Kigoma.. Hebu pateni kiduchu kuhussu huyu Mzalendo wetu wa karne.

Nimevutiwa na dk 5:19 mpk 6:35 pia dk ya 14:17 mpaka mwisho. Its very very interesting..
https://www.youtube.com/watch?v=AddzBZS1Eu8k

Leo katika pekua pekua nimekumbana na hiyo clip ya Zitto akiwa Kigoma.. Hebu pateni kiduchu kuhussu huyu Mzalendo wetu wa karne.

Nimevutiwa na dk 5:19 mpk 6:35 pia dk ya 14:17 mpaka mwisho. Its very very interesting..
@Alinda umemjibu Barubaru vizuri sana. Hapo nyuma Barubaru kasema Zitto anaandamwa.

Tulikaa kimya tukijua majibu yapo, ndiyo hayo!


Kiongozi mkuu ameitaja Arusha kama sehemu moja ya watu walioweka miguu juu.

Hawezi kusema jambo baya bila kutaja mikoa ya kaskazini kama Arusha

Huyu ndiye kiongozi anatarajiwa kuongoza taifa akijenga nyufa za chuki jukwaani


Kuanzia dakika 14.17 anaeleza uenyekiti ndio tatizo.

Hakuwaeleza wananchi wake juu ya
Waraka!

Hakueleza juu yauchochezi aliousimamia miaka yote ukiwemo wa masalia, akina Shonzy n.k.

Supreme huwa anakaribisha mijadala bila kujua. Akiwa na vipaza sauti anahitaji washauri.

Ukisikiliza hiyo hotuba ukaanganisha na madudu yaliyofuata ya ACT utaweza kupata picha halisi ya mwenzetu.


Bado anahitaji muda mwingi kukua kiakili na fikra.
 
Back
Top Bottom