Duru za siasa: Gharama za muungano (siri isiyozungumzwa)

Duru za siasa: Gharama za muungano (siri isiyozungumzwa)

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
15,773
Reaction score
32,431
ZANZIBAR INAJIBANZA KWA MGONGO WA MUUNGANO
MTANGANYIKA ANALIPA KWA KILE ASICHOTUMIA
ZIGO LA UENDESHAJI WA SMZ NI LA MTANGANYIKA

Sehemu ya I


Wanajamvi
Katika mambo yasiyozungumzwa au kugusiwa katika suala la muungano ni gharama. Gharama hazimaanishi kuendesha muungano tu, zinaenda mbali na kugusa kila sehemu ya nchi na mtu binafasi.

Prof Shivji katika uzi amezungumzia msingi wa muungano ni KUGAWANA MADARAKA. Hii ndiyo dhana ya wazanzibar katika suala la muungano

Ukweli ni kuwa msingi wa muungano ni uchumi.
Mijadala yote imejikita katika dhana ya uchumi na laiti mambo ya uchumi yasingekuwepo tusingekuwa na mjadala mrefu kiasi hiki

Kwanini uchumi? Kwanza ni kutokana na mabadiliko ya kisiasa duniani ambayo uchumi ndiyo siasa. Tanzania na Afrika imeshapita kipindi cha ukombozi na mambo ya kisiasa na sasa tunakwenda katika uchumi.

Muungano wa EU, NAFTA, BRICKS, ASIAN n.k yote imekikita katika uchumi na si siasa. Hata NATO imejiondoa katika ulinzi zaidi kwa kuelewa ulinzi mahdubuti uliopo dunia ya sasa ni uchumi.

Kwetu sisi ni kutokana na upande mmoja kuona unaonewa au una haki zaidi ya upande usiokuwepo( Tanganyika)

Zanzibar wanadhani wanayo haki zaidi katika mambo ya uchumi, kwabahati mbaya Mtanganyika hana kauli kwasababu yeye ni Mtanzania ambaye ndani yake yupo mzanzibar.

Hii maana yake ni kitu kimoja kinachoitwa kwa lugha ya kigeni 'fiscal autonomy' kwamba, ni uwezo na uhakika wa sehemu ya jamii kupewa uhakika huo kwa kuamua mambo yao kwa kuhakikishiwa na serikali au katiba(kwa tafsiri isiyo rasmi)

Prof Shivji jana kasema suala la uvuvi halikuwa la muungano na hivyo JMT iliingilia mamlaka ya znz. Hapo ndipo fiscal autonomy inapokuja kuwa Zanzibar wana haki kikatiba ya kutumia maliasili zao kiuchumi kwa kuhakikishiwa na katiba ya JMT na katiba ya Zanzibar.

Kwa upande mwingine Tanzania bara haina fiscal autonomy kwasababu mambo yote yanayohusu Tanzania yanahusu Zanzibar.

Ni kwa msingi huo watalii(wabunge) kutoka znz wanapokuja Dodoma, wanalipwa kwa pesa ya Tanzania ambayo ni ya Mtanganyika.

Zanzibar ina uwezo wa kuamua idadi ya wajumbe wa BLW kwasababu ina fiscal autonomy.

Ni kwa msingi huo, BLW lina wajumbe 50 na Watalii wa znz katika bunge la JMT ni 81.

Hii maana yake ni kuwa Tanganyika haina fiscal autonomy katika mambo yake. Imeuza autonomy kwa muungano ili hali znz ina autonomy katika mambo yanayoihusu na yanayomhusu Mtanganyika

Mfano wa pili katika kufafanua mada hii, pesa za madini zinatumika katika mambo ya muungano bila kujali lipi la muungano na lipi lisilo kwasababu Tanzania ndiyo Tanganyika ambapo znz ina mkono wake.

Tunapokuja katika suala la kodi, Tanganyika inachangia kodi zake katika muungano ambapo kodi hizo zinaitwa za Tanzania na znz ikidai haki kwasababu ni sehemu ya Tanzania. Hilo ndilo linapelekea znz ipewe 4% ya pato la taifa kwasababu ni sehemu ya Tanzania.
Kwasasa wanadai wapewe 11% ya pato la taifa kwasababu nao ni sehemu ya Tanzania. Haki hiyo wanapewa na katiba kwasababu ni sehemu ya JMT na ndicho kinaitwa fiscal autonomy kwa upande wao.

Kwa upande mwingine, znz ina ZRA inayokusanya kodi zake na kubaki huko huko hivyo kuwa na fiscal autonomy iliyopewa na katiba yao au kuchakachua kama ilivyotokea mwaka 2010.

Hili linaeleza kwa undani kabisa namna kodi za Mtanganyika zinavyovuka bahari kwenda kuendeleza nchi jirani.
Zaidi zinaeleza matumizi mbaya ya kodi za Watanganyika. Nitoe mfano;

Watalii 81 wa znz katika bunge la JMT wanalipwa takribani milioni 10 kwa mwezi, sawa na jumla ya milioni 810 kwa mwenzi na bilioni 9.6 kwa mwaka kama mishahara na marupu rupu.

Ukiweka na viinua mgongo kiasi kinakwenda na kufikia bilioni 9.6 kwa kiwango rahisi sana cha Ts Milioni 100 kwa kila mmoja.

Jumla ya fedha kwa miaka mitano inakwenda kwa hesabu za makadirio ya 9.6 B x 5 + 9.6 ambayo ni karibu na Bilioni 50 Ths

Bilioni 50 zinatoka katika JMT inayochangiwa na Tanganyika 100% kwasababu znz haijachangia kwa miaka mingi at least 10 iliyopita.

Rais Kikwete akiwa Muheza Tanga alitangaza serikali kutenga kiasi cha sh milioni 500 kwa halmashauri 41 nchini kujenga nyumba za Walimu

Hadi hapo unaweza kujiuliza iweje kwa miaka mitano watalii 81 kutoka znz wapokee bilioni 50 halafu halmashauri 41 zipewe bilioni 500 kwa pamoja.

Hii maana yake ni kuwa Tanganyika haina fiscal autonomy ya resources zake kiasi cha kutoa mabilioni kwa watu 81 wasio na mchango wowote katika bunge la JMT zaidi ya utalii huku walipa kodi wa halmashauri 41 wakipewa milioni 500 ambazo ni pungufu ukilinganisha na milioni 800 kwa mwezi wanazopewa watalii 81.

Tuangalie muungano kama wa Scotland na UK unakuwaje

Inaendelea

 
Sehemu ya II

Tukiangalia mfumo wa Scotaland na UK tunaona kuwa Scotland imepewa uwezo wa kukusanya kodi zake na kupanga matumizi yake. Kinachotokea ni Scotland kupeleka kiasi cha makusanyo ya kodi zao katika serikali ya UK ili kushughulikia mambo ya pamoja kama ulinzi na mambo ya kidiplomasia.

Kwa upande wetu Zanzibar imepewa fiscal autonomy ya kukusanya kodi zake na kuoanga maendeleo yake kwa kupitia BLW na SMZ. Kama tujuavyo miaka kadhaa znz haijachangia katika muungano kwa namna yoyote.

Hivyo wao wana uwezo huo na uwezo wa kuingia katika fuko la Tanzania ambayo ni Tanganyika na kujichotea chochote wanachodhani wanahitaji. Gurantee hiyo wamepewa na katiba ya JMT na SMZ.

Kwa upande wa Tanganyika , hakuna fiscal autonomy na kila kilicho chao kinaingia katika fuko kubwa la muungano. Hii ina maana kubwa sana kiuchumi.

Kwamba pamoja na resource chache JMT inawajibika kupanga resource zake kwa kuangalia sehemu zote za muungano. Hapo hakuna fiscal autonomy kwa Tanganyika kwasababu kile chao ni cha wote na hawawezi kupanga mipango tofauti.
Kuna kuwa na strains katika ku allocate budget na resources zinazohitajiwa.

Mfano, Tanzania ambayo ni Tanganyika ikipanaga kudhamini wanafunzi wa elimu ya juu, inatoa nafasi 1,000 kwa znz kama gurantee kwavile ni sehemu ya muungano. Kiasi hicho hakirudishwi na kama kinarudishwa basi ni kwa serikali ya mapinduzi.

Mwaka jana Tanganyika ilitenga nafasi 1,000 wakati SMZ kwakutumia fiscal autonomy yao walidhamini wanafunzi 800. Hivyo resource ambazo zilipaswa kutumika Tanganyika kwa wanafunzi wa Tanganyika zimelekezwa znz kweye fiscal autonomy.

Matokeo ya hili ni JMT kuweka viwango vya ufaulu ili wanafunzi wapate mikopo. Watanganyika wamegombea nafasi hizo huku wenzi wao wa znz hata kama wana viwango hafifu wamepata dhamana ya mikopo kwasababu tu ni wznz.

Wanafunzi wa znz whawapaswi kurdisha mikopo, wale wa Tanganyika ambapo baba, mama , dada zao ndio hasa walipa kodi wanalazimika kulipia mikopo hiyo baada ya kumaliza masomo.

Ni kwanini? Ni kwasababu moja znz ina fiscal autonomy na Tanganyika haina. Hivyo ni makosa kulalamika kwa Mtanganyika hadi pale atakapokuwa na chombo cha kumsimamia ambayo ni serikali yake.

Katika mlolongo huo yapo mambo makubwa zaidi. Znz ina budget yake ambayo haiingiliana na ya JMT.

Bajeti ya znz inafidiwa na pesa kutoka hazina ambazo ni kodi za Mtanganyika. Hakuna kiasi kilichotengwa kutoka budget ya znz kwa Mtanganyika. Tunarudi pale pale kuwa Tanganyika ikiwa ni Tanzania haina fiscal autonomy wakati wenzao wanayo. Hiyo inafanya SMZ kuja kuchukua hata mishahara hazina kwasababu ni sehemu ya Tanzania, wakivuka bahari ni znz na fiscal autonomy.

Katika mashirika ya umma kuna wafanyakazi wa znz ambao hawapaswi kuwepo pale. Mfano, TBS ina wafanyakazi na wajumbe wa bodi kutoka znz. Lakini Znz ina ZBS. Mishahara na mafao ya wafanyakazi wa TBS yanalipwa na Mtanganyika wakati ZBS haina Mtanganyika hata mmoja.

Inaendelea....
 
Ndivyo ilivyo kwa Tanzania Maritime ambapo kodi za Mtanzania a.k.a Mtanganyika zinalipa ada kule IMO.

Zanzibar wana ZMO ambayo hukusanya mapato bila kuyaingiza katika muungano.
Hata wafanyakazi wa Maritime walioko Tanganyika kutoka znz nao hulipwa mafao yao hadi ya uzeeni na kodi za Watanganyika.

Hali hiyo ipo hadi katika huduma kama za umeme. Tanesco ni ya Tanzania, na hivyo deni la Tanesco ni la Tanzania. Znz imeshindwa kulipa mabilioni ya deni la Tanesco. Kinachofuata ni Tanzania ambayo ni Tanganyika kuchukua deni hilo na mzigo kuupitisha kwa mwananchi wa Kidatu Morogoro anayeishi mita chache kutoka chanzo.

Zanzibar wameanzisha ZESCO, ambayo kazi yake ni kukusanya makusanyo na kuyaacha kwa SMZ huku deni hilo akikabidhiwa Mtanganyika kwasababu tu Tanganyika ndiyo Tanzania na haina fiscal autonomy katika mipango yake.

Gharama zinaendelea hadi katika ulinzi na usalama ambako znz imejificha kama Tanzania na gharama zote zinabebwa na Mtanganyika.

Katika mfano kama wa Scotland znz ilipaswa kuchangia katika suala la muungano hata kama ina fiscal autonomy yake.
Hilo halitokei na Mtanganyika wa Mtimbira na Kadewele anabeba gharama hizo.

Kwa kadri tunavyoendelea tutaeleza mifano na kufafanua jinsi ambavyo misaada na mikopo inayodaiwa kuchukuliwa na Tanganyika inavyogawanywa kwa njia zisizo sawa na Mtanganyika kujikuta anabeba zigo kubwa kwasababu ya kukosa fiscal autonomy.

Wana duru ni kwa mantiki hii utaona hata prof Shivji amekwepa suala la gharama na kueleza msingi wa muungano ni kugawana madaraka.

Maana yake ni kuwa madaraka wanayotaka ni ili waweze kusimamia rasilimali za Mtanganyika zisizo na fiscal autonomy kuiendeleza na kuikwamua nchi yao.

Madaraka wanayotaka ni kuhakikisha kuwa wanaweka watu wao kuendelea kuitumia Tanganyika kama soko lao la ajira,bishara na chanzouhakika cha mapato.
Jiulize waziri wa afya anafanya nini pale Dar ikiwa afya si jambo la muungano.

Htapa hatujaongelea kabisa gharama za kuendesha muungano alizobeba Mtanganyika mgongoni wala mambo 22 ayliyoingizwa katika muungano nje ya Mkataba. Hatujagusia huduma za jamii na kimataifa.

Inatosha kusema hutasikia Mzanzibar akiongelea gharama hata siku moja. Hapo Dodoma macho na akili zao ni kama alivyowashauri Shivji kufikiria madaraka na mgawanyo wake, ingawa hawajui gharama za madaraka au mgawanyo huo.

Wewe Mtanganyika unapswa kujiuliza, nani atasimama kwa ajili yako na maendeleo yako? Hadi lini wewe utakuwa mtoaji na si mokeaji? Nini unachovuna katika muungano huu unakutia kodi za juu, kulipa madeni na hata kumnyima mtoto wako nafasi kwasababu tu unampenda mtoto wa jirani?

Hebu tusemezane kwanza kabla hatujaendelea..

Karibuni
 
Mkuu Nguruvi3:

Katika masuala ya muungano. Ni lazima nchi itakayokubali kuwa engine ya muungano iwe Bold na kuchukua gharama za muungano.

Mimi ni mtanganyika through and through. Na nataka Tanganyika iwe BOLD na iwe na watu wenye kuchukua majukumu na kuyaweza kuyagharimia.

Kulialia na gharama ulizotoa hapo juu, haionyeshi kuwa Tanganyika ipo tayari kwenye project yoyote ya integration ya nchi za kiafrika. Na itakapotokea nchi yoyote ya Afrika mashariki yenye uwezo wa kiuchumi, tutabuluzwa kwa kuogopa gharama zisizo gharama.
 
Zakumi , haya ni baadhi ya mambo znz imekuwa inalalamikia kuhusu misaada na mikopo kutoka nje. Haiwezekani useme Tanganyika ni kubwa ibebe dhamana na wakati huo huo ikitupiwa lawama za kunufaika na muungano na si kutoa zaidi.

Nitakuwa mtu wa kwanza kuilaani Tanzania kama haitachangia katika mashirika, taasisi na umoja wowote wa dunia ya leo. Pamoja na umasikini tuna haki na ni wajibu wetu kuchangia UN, AU, SADC, EAC n.k.


Burundi na Rwanda ndani ya EA ni ndogo lakini zinachangia katika jumuiya bila kujali udogo wake. Ndivyo itakavyokuwa kwa znz ikijiunga na EAC kama nchi kwa mujibu wa katiba yao ya 2010.


Hapa tunaonyesha jinsi ambavyo Watanganyika wamebeba muungano na uzito wote kwa ujira wa matusi, lawama na kashfa.


Nikupe mfano, Znz wameondoa baraza la mitihani katika JMT ambayo Tanganyika ilikuwa inabeba mzigo. Kwa sasa wana BMZ ambalo ni ''fiscal autonomy'

Kwanini kuwe na wajumbe wa bodi ya NECTA kutoka Zanz mbao si kuwa hawana interest na chombo hicho bali wanalipwa mishahara na mafao yao yote kwa huduma hewa!


Nimekuonyesha watalii 81 wanavyokula pesa kuliko halmashauri 41 za Tanganyika.

Shivji kasema halmashauri si suala la muungano. Swali linakuja kwanini watalii hao 81

Kwanza, wajihusishe na mambo yasiyo ya muungano

Pili, walipwe kiasi cha mabilioni badala ya kuyaelekeza katika halamshauri zetu


Kumbuka pesa wanazopewa Watalii wa znz ni za Tanganyika, niambie kwa mchango gani unaoweza kuufanyia extrapolation na kupata matokeo katika halmashauri zetu.


Inasikitisha watu 81 wanakula bilioni 50 kwa mwaka na halmashauri 41 zinapewa milioni 500. Ni watu kiasi gani wapo katika halmashauri hizo 41, kwamba kwa pesa zilizotolewa kila mmoja kwa average anapata senti ngapi as opposed to bilioni ngapi wanazokula watalii 81 kutoka Unguja na Pemba


Tunataka Tanganyika ili kuwe na fiscal autonomy. Yale ya pamoja tutachangia kwa kadri ya uwezo wa kila mmoja. Warioba kasema ni 7 si 22 ya sasa. Hapo tatizo lipo wapi?

 
Last edited by a moderator:
Zakumi , Tanganyika imechukua majukumu hayo kwa miaka 50 na siyo kulia lia. Nimekupa mfano wa SCotland, hukusuanya mapato yake na kutoa sehemu kwa huduma za muungano kama jeshi na mambo ya nje.

Kelele za misaada na mikopo zimepigiwa, Watanganyika kuonekana maharamia dhidi ya Ukarimu wao. Ubaguzi uliojaa zanzibar ni kielelezo cha kutokuwa na uchungu na muungano

Nikupe kwanza vielelezo halafu tunyambulishe. Kabla ya hapo nikutanabaishe kuwa muungano ulilenga katika 'win-win situation' na siyo mmoja kubeba majukumu. Kama ni kubeba majukumu muungano hauna maana. Waasisi walikusudia kujenga muungano wa 'win-win' situation.

Mchambuzi;3383940]
Pato la kila mtanzania kwa mwaka (GDP Per Capita) kwa kila mkoa wa Tanzania.
Table 2: Vipato Vya Watanzania Kulingana na Mikoa Wanayotoka (GDP Per Capita)
[TABLE="width: 0"]
[TR]
[TD]MKOA
[/TD]
[TD]PATO LA KILA MWANANCHI KWA MWAKA (T.Shillings) (2010)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1. Dar-es-salaam
[/TD]
[TD]1,740,947 (million)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2. Iringa
[/TD]
[TD]979,882 (laki)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]3. Arusha
[/TD]
[TD]945,437
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]4. Mbeya
[/TD]
[TD]892,877
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]5. Kilimanjaro
[/TD]
[TD]879,432
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]6. Ruvuma
[/TD]
[TD]866,191
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]7. Mwanza
[/TD]
[TD]829,647
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]8. Tanga
[/TD]
[TD]763,203
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]9. Morogoro
[/TD]
[TD]744,234
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]10. Rukwa
[/TD]
[TD]726,658
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Table 4: Kumi Bora Kwa Uzalishaji Wa Bidhaa na Huduma (GDP).
[TABLE="width: 0"]
[TR]
[TD]MKOA
[/TD]
[TD]UZALISHAJI WA BIDHAA NA HUDUMA (GDP) T.shillings (2010)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1. Dar-es-salaam
[/TD]
[TD]T.sh 5.4 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2. Mwanza
[/TD]
[TD]T.sh 3.0 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]3. Mbeya
[/TD]
[TD]T.sh 2.3 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]4. Shinyanga
[/TD]
[TD]T.sh 1.9 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]5. Iringa
[/TD]
[TD]T.sh 1.7 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]6. Morogoro
[/TD]
[TD]T.sh 1.6 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]7. Arusha
[/TD]
[TD]T.sh 1.5 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]8. Kilimanjaro
[/TD]
[TD]T.sh 1.3 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]9. Kagera
[/TD]
[TD]T.sh 1.3 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]10. Ruvuma
[/TD]
[TD]T.sh 1.2 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]11. Tabora
[/TD]
[TD]T.sh 1.2 trillioni
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]12. Rukwa
[/TD]
[TD]T.sh 1.1 trillioni
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Mikoa yenye michango midogo zaidi kwenye pato la taifa/uzalishaji mdogo zaidi wa bidhaa na huduma Tanzania?
Table 5: Mikoa Yenye Michango Midogo Katika Uzalishaji/Pato la Taifa (bottom 5).
[TABLE="width: 0"]
[TR]
[TD]MKOA
[/TD]
[TD]UZALISHAJI WA BIDHAA NA HUDUMA (GDP) T.shillings (2010)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1. Singida
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 661
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2. Pwani
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 608
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]3. Lindi
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 621
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]4. Kigoma
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 906
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]5. Mtwara
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 927
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Table 6: Orodha ya kumi bora – vipaumbele katika Bajeti Ya Serikali.
[TABLE="width: 0"]
[TR]
[TD]MKOA
[/TD]
[TD]BAJETI YA MWAKA (T.sh)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1. Dar-es-salaam
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 154
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2. Mwanza
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 135
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]3. Mbeya
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 109
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]4. Shinyanga
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 104
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]5. Kilimanjaro
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 100
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]6. Tanga
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 92
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]7. Kagera
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 88
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]8. Morogoro
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 86
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]9. Iringa
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 85
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]10. Arusha
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 81
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Table 7: Mikoa Isiyopewa Kipaumbele Katika Bajeti Ya Serikali (Bottom five).
[TABLE="width: 0"]
[TR]
[TD]MKOA
[/TD]
[TD]BAJETI YA MWAKA (T.sh)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1. Mtwara
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 57
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2. Kigoma
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 56
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]3. Singida
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 50
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]4. Manyara
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 54
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]5. Rukwa
[/TD]
[TD]T.sh Billioni 49
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Kwa hisani ya Mchambuzi
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,

Tunashukuru kwa uzi huu muhimu. Kwa kweli mjadala juu ya gharama za muungano pamoja unahitaji uzi wake maalum ili kutoa fursa kwa wananchi ‘to focus' katika suala hili badala ya kulichanganya na masuala mengine hivyo kupotezea suala la gharama za muungano, nguvu na umuhimu wake katika mazingira ya sasa.

Mijadala mingi juu ya gharama za muungano zimekuwa na mapungufu kadhaa. Moja wapo, ni mijadaka kukosa "an analytical framework", ambayo inasaidia watu kufuatilia vizuri zaidi hoja zinazotolewa. Umekuja na jibu katika hili kwa kuleta dhana ya "FISCAL AUTONOMY". Wadau kama Mtanganyika, Gamba la Nyoka, Mkandara na wengine wamekuwa na utamaduni wa kutetea mfumo wa serikali mbili kwamba una gharama nafuu kuliko serikali tatu, lakini mara nyingi, hoja zao huishia kuwa too random, erratic, inconsistence and incoherent, kwa vile they don't base on any analytical framework, constructed by them au borrowed elsewhere. Pamoja na kuwakumbushia juu ya umuhimu wa kufanya hivyo, ni kawaida yao kukimbia mijadala, na wakirudi siku chache baadae, wanaanzia pale pale walipokosea. Ni matumaini yangu kwamba "FISCAL AUTONOMY" as a framework of analysis sasa itawapa fursa waeleweke vizuri zaidi kwa wananchi. Lakini pia bado wana fursa ya kutuletea an alternative framework wanayoona inafaa kutumika katika mijadala juu ya suala zima la ufanisi wa mapato (taxation) na matumizi (expenditure ) ya fedha za umma kwa ajili ya wananchi wa nchi shiriki ndani ya muungano.

Lipo pungufu linguine kubwa kwa upande wa wenzetu wa hoja. Nalo ni kwamba, aidha kwa kujua au kutojua, wenzetu hawa wanakuja na hoja za kisiasa kuteta hoja za kiuchumi, hali inayowapelekea kushindwa kufikisha hoja zao kwa "nguvu za hoja", na badala yake kuishia kufikisha hoja zao kwa "hoja za nguvu". Hii ni kwa sababu, lengo lao kuu ni kulinda "the status quo" au ‘the establishment", kuliko kumlinda mwananchi. Wanashindwa kuelewa kwamba haiwezekani kutetea muungano na kujadili faida zake kwa wananchi kwa mafanikio kwa kuweka "politics" at the centre of discussion. Kinachotakiwa kuwa at the centre ni UCHUMI (kama alivyojadili nguruvi3 awali), kwa lugha na mifano rahisi ambayo mwananchi wa kawaida ataelewa.

Kwa lugha rahisi - "fiscal autonomy" maana yake ni mamlaka kamili/uhuru kamili (unaotambulika kikatiba) wa taifa (huru/sovereign) kujiamulia juu masuala ya fedha za umma (taxes/mapato & expenditures/ matumizi) katika kuhudumia uchumi na jamii iliyopo ndani ya eneo lake la utawala linalotuambulika kwa mujibu wa taifa hilo. Tutajadili kwa undani zaidi dhana nzima ya "fiscal autonomy" na kuihusisha na mfumo wa muungano wetu, lakini kwa sasa ningependa kujadili japo kwa uchache masuala yafuatayo:

Kwanza – wale wote wanaotetea muungano wa serikali mbili wanasahau kwamba muungano wa Tanganyika na Zanzibar haukuwa muungano wa KIUCHUMI bali ulikuwa ni muungano wa KISIASA. Katika kundi hili, wapo pia watu kama Profesa Issa Shivji na makada wengi wa chama tawala (CCM). Profesa Shivji, kwa mfano, wakati wote katika maandiko yake, amekuwa akiujadili muungano wa Tanganyika na Zanzibar kama muungano wa Kisiasa huku akikosoa dhamira nzima ya panafricanism inayoongozwa na dira ya aina hiyo. Kutokana na muungano tulionao kutawaliwa na siasa zaidi kuliko uchumi, ndio maana Shivji wakati wote huwa anapata wakati mgumu katika uchambuzi wake, kujadili kwa ufasaha juu ya "gharama za serikali tatu" dhidi ya serikali mbili. Muhimu zaidi ni kwamba Shivji ni mwanazuoni ambae wakati wote amejadili muungano huu kwamba hauna uhalali wowote wa kisheria.

Tukirudi katika hoja juu ya muungano unaosukumwa na nguvu za kisiasa kuliko kiuchumi, historia inatueleza kwamba Mwalimu Nyerere alipendelea Zanzibar iwe sehemu ya Shirikisho la Afrika mashariki. Ndio maana wakati ule wa harakai za PAFMECA akiwa na kina Marais Kenyetta na Obote, Nyerere alidhamiria kuisubiri Zanzibar ipate uhuru wake ili shirikisho la Afrika mashariki lizaliwe Zanzibar ikiwa ni sehemu ya shirikisho hilo. Lakini baadae kidogo, Kenyatta na Obote wakawa wagumu kukubaliana na Mwalimu juu ya shirikisho hilo, kwahiyo Mwalimu akaona aanze na Zanzibar kufungua njia ya shirikisho hilo. Tujiulize maswai yafuatayo: ·

Kwanini majirani zetu Kenya na Uganda walisita kukubali wazo la Mwalimu Nyerere juu ya shirikisho la kisiasa la afrika mashariki miaka zaidi ya 50 iliyopita? Jibu ni kwamba hawakuona maslahi ya uchumi zaidi ya maslahi ya kisiasa. Waligundua kwamba muungano huu ungekuja kuwaletea matatizo ya kisiasa baadae kutokanana suala zima la uchumi kutopewa umuhimu wa kutosha. Panafricanism was more of a Political Agenda than an economic agenda, na mafanikio yake yalikuwa short lived. Issa Shivji anajadili suala hili katika kitabu chake cha Pragmatism or Panafricanism: Lessons of Tanganyika and Zanzibar Union (2008), na anajadili kwamba muungano wa Tanganyika na Zanzibar is a failed panafricanism project kwa vile siasa zimetangulia uchumi. Lakini cha kushangaza ni kwamba, juzi katika kongamano la wanavyuo wa CCM, Shivji akabadili msimamo wake wa awali na kuwaeleza Vijana wale kwamba muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni mfano mzuri wa mafanikio ya Panafricanism agenda, hivyo hawana budi kuulinda chini ya serikali mbili.

Swali linguine la kujiuliza ni je: Kwanini Jumuiya ya Afrika Mashariki ilikufa miaka kumi tu baada ya kuanzishwa kwake? Jibu kwa swali hili pia ni three words - UCHUMI UCHUMI UCHUMI. Siasa zilitawala uchumi badala ya siasa kutumikia uchumi. Hata leo hii, sababu kubwa juu ya kwanini muungano wa Tanganyika na Zanzibar utakuja vunjika ni ile ile – UCHUMI UCHUMI UCHUMI. Tutajadili kwa undani zaidi baadae.

Pili – kama alivyojadili Nguruvi3, Tanzania Bara (Tanganyika) haina "fiscal autonomy" (rejea definition hapo juu). Haya yamejadiliwa kwa kina na tume ya warioba. Kwa mfano, chini ya mfumo wa serikali mbili, yapo:-Masuala ya Muungano.-Masuala ya Tanzania Bara.-Masuala mchanganyiko ya Tanzania Bara na Muungano.

Yaliyo mengi zaidi ni masuala ya muungano na masuala mchanganyiko ya Tanzania bara na muungano. Mchanganyiko kuu ni moja ya sababu za msingi juu ya kero za muungano zisizokwisha. Na kwa hatua ya Zanzibar kikatiba (2010), kero hizi haziwezi kutatuliwa chini ya mfumo wa serikali mbili.

· Chini ya mfumo wa sasa wa serikali mbili, nchi mbili, Zanzibar wanasimamia mambo yao yote ya kisiasa na kiuchumi. Lakini kwa upande wa Tanzania bara, hali hii haipo. Suala la fedha linatofautiana na suala la uchumi, tutafafanua baadae kidogo.

· Chini ya mfumo wa serikali mbili, nchi mbili, Zanzibar wana mihimili yote mitatu ya dola (Rais, Bunge na Mahakama). Lakini kwa upande wa Tanzania bara, hali hii haipo. Badala yake, Tanzania Bara ndio jamhuri ya muungano wa Tanzania. Kama mikakati wa kulinda mfumo uliopo kwa hali na mali, CCM imependekeza kuanzishwa kwa baraza la wawakilishi la Tanzania bara ambalo litakuwa linasimamia masuala ya Tanzania bara tu. Wananchi wanabaki kujiuliza – ni serikali ipi katika ya mbili (ya Zanzibar na ya muungano) ndio itakayosimamia bunge la wawakilishi la Tanzania bara? Muungano utaendeshwa vipi na serikali mbili yenye mabunge matatu? Hapa wananchi wengi ndio wanazidi kuelewa kwamba CCM inaelewa umuhimu wa serikali tatu lakini inalikataa wazo kwa sababu za kisiasa na zisizo na tija kwa wananchi. Mabunge matatu, serikali mbili, itakuwa ni moja ya njia kuu za kuvunja muungano muda sio mrefu. Tutafafanua baadae.

Pamoja na mapungufu yote haya ambayo kimsingi yanainyima Tanganyika HAKI yake ya Kikatiba, Kidemokrasia na Kirasilimali (fiscal autonomy), kwa upande wa wazanzibari, wao kero yao leo imebakia katika maeneo machache kama vile madaraka/nafasi za uongozi lakini muhimu pia, suala la fedha za nje. Katika hili, Wazanzibari wanalalamika kwamba hawana uwezo wa ku-negotiate on Loans and Grants moja kwa moja na wahisani, na badala yake, masuala haya yanasimamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya fedha ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kama tulivyokwisha ona, suala la Fedha za nje (loans and grants) ni suala la muungano. Lakini kama alivyojadili Nguruvi3, suala la fedha za ndani, Zanzibar ina mamlaka/uhuru juu ya mapato na matumizi yake ya ndani. Chini ya mfumo huu, Tanzania Bara hawaonji hata senti moja ya wazanzibari, badala yake yanaingizwa katika kapu la muungano na kufanywa kuwa ni matumizi kwa ajili ya WATANZANIA (Tanzania Bara na Zanzibar), kama alivyojadili Nguruvi3. Tunachoona hapa sasa ni kwamba, Zanzibar sasa wanataka kuwa ‘in full control' na vyanzo vyote vya fedha:

1. Fedha za ndani (mapato yanayokusanywa Zanzibar).
2. Fedha za nje (loans and grants).
3. Fedha za Tanganyika (zinazotupwa katika kapu la muungano chini ya serikali mbili).

Tuangalie kwa undani kidogo juu ya fedha za NJE (Loans and Grants), ambapo ndiko kwenye msingi Wa Malalamiko Ya Wazanzibari. Kama tulivyokwisha ona, msingi wa malalamiko ya wazanzibari ni kutokuwa na mamlaka to negotiate with donors on grants & loans (fedha za nje). Hali hii ni matokeo ya Sheria ya mwaka 1974 (The Ministry Of Finance of United Republic of Tanzania Loans and Grant and Guarantee Act of the 1974) inayotamka kwamba – jukumu la kufanya negotiations na wahisani ‘on provision of all external aid', ni jukumu la Serikali ya Muungano, Kupitia Wizara ya Fedha ya muungano. Sheria hiyo inaelekeza kwamba Wizara ya fedha ya Zanzibar inatakiwa to submit project funding proposals to donors kupitia wizara ya fedha ya muungano, badala ya kuwa na direct Negotiations with donors.

Mamlaka ya Zanzibar Juu Ya Uchumi na Mipango.

Ni muhimu tufahamu kwamba, tofauti na Tanzania bara, Zanzibar ina mamlaka kamili juu ya mikakati ya maendeleo ya taifa pamoja na mipango yake kisera. Haya yote hayawi implemented na serikali ya muungano, bali na serikali ya Zanzibar, kwa mfano masuala ya kilimo, afya, n.k. Tukitazama kwa makini hapa tunagundua kwamba – tofauti na Tanzania Bara ambayo haina full autonomy katika suala zima la mikakati ya maendeleo ya taifa na mipango kisera, Zanzibar wanayo full autonomy lakini wanakuwa defeated na tatizo ambalo tumeshalijadili, nalo ni kwamba: pamoja na kuwa na mamlaka ya kujipangia mikakati yao uchumi, maendeleo pamoja na sera husika, ili haya yatekelezeke, Zanzibar haina uwezo wa kifedha kutona vyanzo vyake vya ndani kukidhi mahitaji haya, kwahiyo wanahitaji vyanzo vya fedha kutoka nje (loans and grants). Tatizo linakuja pale ambapo kupitia sheria ya 1974 (tuliyoijadili), ili wapate fedha hizi kutoka kwa wahisani, ni lazima watume maombi kwenye serikali ya Muungano (Wizara ya Fedha). Hii haijalishi hata kama Waziri wa Fedha anatokea Zanzibari. Msumeno wa sheria hii ni ule ule.

HITIMISHO

Zinazojadiliwa kama kero za muungano, kwa bahati mbaya zimekuwa zikipotoshwa kama vile ni kero za upande mmoja tu wa muungano (Zanzibar). Katika mazingira ya namna hii, CCM ipo tayari kufanya lolote lile at the expense of Tanganyika ili kuwaridhisha Zanzibar na mfumo wa serikali mbili. Ndio maana upo mpango madhubuti wa CCM kupitia bunge la katiba kuhakikisha kwamba wazanzibari wanapewa yale yote wanayo yalalamikia, likiwepo suala la kuwa na mamlaka to negotiate moja kwa moja na donors on loans and grants badala ya kutegemea Wizara ya Fedha ya Muungano. From the looks of it, Zanzibar wakipata hili (pamoja na sustenance yao on self determination and political autonomy kupitia katiba yao ya 2010), Zanzibar wataridhika na kupunguza kunung'unika.

Tunaweza kutoa tafsiri moja tu kwa wanasiasa wa Zanzibar and their march towards mabadiliko ya sheria ya 1974 (see above): They Want AID Money; They Don't want to be self reliant. Vinginevyo kwa taifa lenye viongozi makini, mikakati ilitakiwa iwe ni jitiada za kuepuka kuingia katika mtego wa AID – Dependency. Lakini kama nilivyokwisha sema, tyrants LOVE AID. They can hardly survive without it. Ndio maana hata wagombea urais (CCM) 2015 wanafanya kila njia kuzuia serikali tatu kwani serikali ya muungano haitakuwa na uwezo wa kukopa nje. Jukumu hilo litakuwa ni la nchi shiriki (Tanganyika na Zanzibar). Rais wa muungano kazi yake itakuwa ni kutafuta vyanzo vingine vya ndani, lakini zaidi, kutegemea michango ya nchi shiriki za muungano. Chini ya mazingira haya, fedha chafu, vyeo vya fadhila, na madudu yote ya kumgharimu mwananchi, yatakuwa put to rest. Ni jukumu letu kuwaelimisha wananchi juu ya hatari iliyopo mbele yao iwapo watakubali kupotoshwa juu ya faida za serikali tatu, kwa faida yao na vizazi vyao vya baadae. Itaendelea kwa kuingia kwa undani juu ya haja, faida, na umuhimu wa fiscal autonomy kwa nchi shiriki za muungano, hivyo kwanini mfumo wa serikali tatu utakuwa na maslahi zaidi kwa pande zote mbili za muungano kuliko mfumo mbovu wa sasa wa CCM (serikali mbili).


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.
 
Mkuu Mchambuzi
Kuna mambo kadhaa umeyagusia ningependa niyachangie kwa uchache sana.

Umoja wa Ulaya (EU) una wakati mgumu, baadhi ya nchi zikitaka kujitoa.
Sababu kubwa ni suala la uchumi

Ujerumani ndiye mkubwa anayedhamini akina Greece, Italy n.k. Sababu kubwa si za kiusalama au kisiasa bali kiuchumi

Greece kwa eneo na ukubwa wa uchumi ni muhimu kwa Europe kuliko political influence yake
Nchi za BRICS zinaungaishwa na uchumi si siasa. Ndivyo ilivyo kwa blocks zingine duniani.
Muungano wa Tanzania umeshavuka hatua ya kisiasa, kinachogomba ni uchumi.

Kwa maana hii kuutazama muungano kwa jicho la kisiasa kama alivyofanya Shivji ni kujidanganya.

Malalamiko ya znz kuhusu Loans and grants yanafikirisha. Tanzania inapewa mikopo(IMF) kwasababu ya assets zake. Kwa njia hiyo znz inakuwa collateral.
Inapotokea default anayeulizwa ni Tanzania siyo znz.

Wale wanaosema znz haipati misaada wajiulize, jana Rais Shein kafungua marine cable kuongeza umeme Znz kutoka Bara kupitia msaada wa milleninium wa US.
Barabara aliyozindua Pemba nayo ni kupitia msaada huo huo.

Tatizo la wajenga hoja za misaada (wazo baya sana katika maendeleo) ni kuwa znz haipati kiasi sawa cha misaada.

Wanachotaka ni kugawana misaada 50%. Wasichokijua ni kuwa nje ya Tanzania znz haiwezi kupata loans au grants ambazo ni kubwa kuliko assets zake.
Kwa uchumi wa znz kiasi wanachopata kutoka Tanganyika ni zaidi ya wanachotarajia nje ya muungano.

Wanojenga hoja ya misaada, hawakumbuki kuna mambo mengine yanayohusiana na misaada hata kama hayaitwi hivyo. Kwa mfano, deni la ndani la znz linamezwa na Tanganyika ingawa znz ina fiscal autonomy.

SMZ inaposhindwa kulipa mishahara hukimbilia hazina. Mwaka 200Tanganyika ilimeza deni la bilioni 20 za umemeznz kwa Tanesco, hku deni hilo likiendelea kukua na sasa kukaribia Bilioni 70.

Wajenge hoja za serikali 2 wanashindwa kutueleza namna gharama za kawaida za JMT zinavyogharamiwa huku znz ikiwa na control alizosema Mchambuzi na nikumbushe
1. fiscal autonomy
2. Fedha za makusanyo ya kodi ambayo tume ya Amina ilipiga marufuku zisivuke bahari
3.Fedha za loans and grants
4. Fedha za kapu la mama Tanzania ambazo ni za Tanganyika isipokuwa tu kama kuna hoja za kisiasa.

Kwasasa znz inataka kitu kimoja tu ambacho kwa bahati mbaya prof Shivji kakisema 'KUGAWANA MADARAKA' ili izidi kuwa na uwezo wa kuitumia Tanganyika kikamilifu.

Ipo hoja kuwa Zanzibar haiwezi kuchangia katika serikali ya muungano au shirikisho.
Hoja haina ukweli kwasababu tukiangalia fiscal autonomy ya Scotland tunaona uwezo huo upo. Znz inakusanya kodi kupitia vyanzo vyake.
Kinachotakiwa ni kuchangia mambo machache ya muungano ili kuleta maana ya muungano na si kubebana.
Scotland wanafanya hivyo kwanini znz ishindwe ikiwa ni dola yenye miaka 200 kwa mujibu wa Shivji.

CCM ya akina Nape Nnauye wanatambua ukweli kuwa Tanganyika inamenyeka katika muungano. Kwasasa wanasema liwepo bunge la Tanzania bara. Kwa maneno mengine wanataka kuwe na fiscal autonomy kwa Tanganyika. Wanapo fall short ni pale wasipoweza ku justify bunge hilo linasimamiwa na nani.

Ni kituko kama si maono kuwa na bunge lisilowajibika au wajibisha pengine. I meana utakuwaje na bunge lisiloweza kujibu hoja za wabunge? Bunge la Tanzania bara halina waziri wa kiongozi wa serikali, litafanya kazi gani kwa maono ya CCM.

Hata uwepo wa bunge hilo hautajibu manung'uniko ya Watanganyika. Manung'uniko ya Watanganyika ni kukosa fiscal autonomy kiasi kwamba hawawezi ku negotiate kati ya resource zao na priority zao. Kwamba kinachoingia Tanganyika kinagawanywa hadi Zanzibar.

Tume ya Warioba imeliona tatizo hilo na kuja na mambo 7 tu ambayo huduma zake zinaweza kuchangiwa na washirika.
Kwanini tunasema kuchangiwa?
Kwavile znz takes everything for granted haina uchungu wa muungano na wala haioni thamani yake. Wanapata zaidi wanachotoa na kila wakiomba wanapewa zaidi kama CCM wanavyojiandaa kuwapa zaidi Dodoma wakati huu.

Matokeo ya kutokuwa na uchungu na muungano ni znz kufanya mambo kwa mtindo hovyo ukipewa baraka na Shivji alilaani muungano huu siku za nyuma. Hakuna namna ya kuwafanya wawe responsible kama wataendelea kupata handouts kila wakilia. Ni lazima wachangie kile wanachoweza kwasababu hii ni win win situation.

Kuchangia kutaimarisha muungano na kutoa fursa kwa washirika kuhudumia maeneo yao kutokana na income/expenditure etc etc. Kwasasa hilo halipo kilichopo ni Yananyika kubeba mzigo wa kuendesha nchi jirani.
Nimalizie kwa hesabu rahisi sana
Kwa majedwali hapo juu bandiko #6 Mkoa wa Rukwa unachangia uzalishaji na huduma (GDP) ya 1.1 Trillion.
Rukwa inapata Bilioni 49 kutoka katika bajeti ya taifa.

Tujiulize Znz inachangia kiasi gani katika muungano na inapata kiasi gani kwa huduma na uzalishaji kama vipo.
 
Last edited by a moderator:
Sehemu ya II

Tukiangalia mfumo wa Scotaland na UK tunaona kuwa Scotland imepewa uwezo wa kukusanya kodi zake na kupanga matumizi yake. Kinachotokea ni Scotland kupeleka kiasi cha makusanyo ya kodi zao katika serikali ya UK ili kushughulikia mambo ya pamoja kama ulinzi na mambo ya kidiplomasia.
Mkuu Nguruvi3 Naona hujautendea haki huu mlinganisho wako.

Naomba tukubali kutokubaliana katika haya yafuatayo.
1) Scotland haijapewa uwezo wa kukusanya kodi zake kama unavyosema. Tax policy zinafanyika Westminster na Kodi za UK ukiondoa council tax zinakusanywa na kitengo cha Her Majesty's Revenue and Custom (HMRC). Bunge la Scotland linaweza kuweka viwango vya kodi katika mambo fulani fulani tu lakini pesa za kodi hizo Scotland haizikusanyi.
2) Makusanyo ya pesa ya UK yanapofanyika, mgawanyo wake unafanyika kwa njia iliyokubaliwa kipindi cha miaka ya 1970's unaoitwa Bernet formula baada ya kutokea ukata na manung'uniko mengi ya watu wa Scotland wakitaka kuanzisha Bunge lao katika mtazamo wa kutaka kujitawala. Kwa sasa takwimu zinaonyesha kuwa nchi ambazo ziko kwenye UK ukiondoa England, huwa zinapata mrejesho wa pesa wa kiasi cha asilimia 12 zaidi ya matumizi kwa kila mwananchi wa England baada ya kukusanywa na HMRC na kugawiwa back kwa njia ya fungu. Kwa maana nyingine, hii ni kama hongo ya kisiasa kuwafanya waendelee kuwa kwenye UK.
3) Kuweka mfumo wa Scotland katika ujengaji wa hoja yako ni kutoitendea haki hoja yako na pia ni kuweka dhana kuwa mfumo wa UK katika maswala ya fiscal rules and fiscal policy uko fair kwa nchi zake zote wakati kila siku Scotland inapiga kelele ikitaka iwe na full fiscal autonomy achila mbali independent.

Nimalizie kwa kusema, Katika nchi karibia zote ambazo zimeungana lakini ndoa zake za muungano zina economic inequality. Lazima nchi moja isaidiwe, na katika huu msaada huwa mara nyingi ni kama mojawapo ya union incentives ili kupata political legitimacy kwa wananchi ili iendelee kuwepo kwenye muungano. Ndiyo maana hata nchi za Scotland, Wales and Northern Ireland zinapewa fungu kubwa la pesa ukilinganisha na England lakini hatuelewi kiundani faida ya England kuendelea kutotaka Scotland ipate uhuru wake.

Ukiangalia kwa undani utagundua kuwa, Tanganyika ndiyo ilitaka sana kuwa kwenye muungano zaidi ya Zanzibar. Kutaka huko mpaka leo lazima kuje/kuwepo na political, economy and social incentives inayoonekana kwa watu wa Zanzibar.

Benefit hata tunazoziona kwa sasa ni zile ambazo zinaonekana kwa macho, na katika kuonekana huko, ndiyo maana tunaona kama Zanzibar wanapata faida zaidi lakini cha kushangaza, viongozi wetu hawataki kuiachia Zanzibar kutoka kwenye Muungano. Why?. Lazima kuna kitu kimejificha!.
 
Mkuu Nguruvi3 Naona hujautendea haki huu mlinganisho wako.

Naomba tukubali kutokubaliana kama haya yafuatayo.
1) Scotland haijapewa uwezo wa kukusanya kodi zake kama unavyosema. Kodi za UK ukiondoa council tax zinakusanywa na kitengo cha Her Majesty's Revenue and Custom (HMRC). Bunge la Scotland linaweza kuweka viwango vya kodi katika mambo fulani fulani tu lakini pesa za kodi hizo Scotland haizikusanyi.
2) Makusanyo ya pesa ya UK yanapofanyika, mgawanyo wake unafanyika kwa njia iliyokubaliwa kipindi cha miaka ya 1970's unaoitwa Bernet formula baada ya kutokea ukata na manung'uniko mengi ya watu wa Scotland wakitaka kuanzisha Bunge lao katika mtazamo wa kutaka kujitawala. Kwa sasa takwimu zinaonyesha kuwa nchi ambazo ziko kwenye UK ukiondoa England, huwa zinapata mrejesho wa pesa wa kiasi cha asilimia 12 zaidi ya matumizi kwa kila mwananchi wa England baada ya kukusanywa na HMRC na kugawiwa back kwa njia ya fungu. Kwa maana nyingine, hii ni kama hongo kuwafanya waendelee kuwa kwenye UK.
3) Kuweka mfumo wa Scotland katika ujengaji wa hoja yako ni kutoitendea haki hoja yako na pia ni kuweka dhana kuwa mfumo wa UK katika maswala ya fiscal rules and foscal policy uko fair kwa nchi zake zote wakati kila siku Scotland inapiga kelele ikitaka iwe na full fiscal autonomy achila mbali independent.

Nimalizie kwa kusema, Katika nchi karibia zote ambazo zimeungana lakini ndoa zake za muungano zina economic inequality. Lazima nchi moja isaidiwe, na katika huu msaada huwa mara nyingi ni kama mojawapo ya union incentives ili kupata political legitimacy kwa wananchi ili iendelee kuwepo kwenye muungano. Ndiyo maana hata nchi za Scotland, Wales and Northern Ireland zinapewa fungu kubwa la pesa ukilinganisha na England lakini hatuelewi kiundani faida ya England kuendelea kutotaka Scotland ipate uhuru wake.

Ukiangalia kwa undani utagundua kuwa, Tanganyika ndiyo ilitaka sana kuwa kwenye muungano zaidi ya Zanzibar. Kutaka huko mpaka leo lazima kuje/kuwepo na political, economy and social incentives inayoonekana kwa watu wa Zanzibar.

Benefit hata tunazoziona kwa sasa ni zile ambazo zinaonekana kwa macho, na katika kuonekana huko, ndiyo maana tunaona kama Zanzibar wanapata faida zaidi lakini cha kushangaza, viongozi wetu hawataki kuiachia Zanzibar kutoka kwenye Muungano. Why?. Lazima kuna kitu kimejificha!.
Mkuu labda nikuulize kidogo, una uhakika kuwa UK ndiyo inafanya taxation kule Scotland?

Pili, Hoja ya kuchangia haina maana kusiwe na muungano. Ina maana lazima tugawane muungano kwa kiwango kinachowina. Hivi mkuu unakubali kuwa ni lazima tulipe Bilioni 9.6 kwa mwaka kwa watu 81 walizuru Dodoma kaama Watalii

Tatu, ni kiasi gani Wales inachangia katika Uk kuliko England na kiasi inacpewa kutoka UK

Nne, muungano mkubwa utabeba mdogo, ndivyo Warioba amependekeza na tume yake. Rasimu imeeleza wazi, je hilo linaifanya znz isichangie lolote huku tukidai zaidi kutoka Rukwa inayochangia zaidi ya trillioni 1 kwa huduma na bidhaa.

Tano, kama uchumi mkubwa unabeba mdogo, malalamiko ya znz kuhusu misaada yapo katika misingi gani.

Sita, Je unaamini msingi wa muungano ni kugawana madaraka

Saba, kwa kutumia serikali 2 nani anayebeba mzigo wa muungano na kwanini abebe

Nane, Unaamini uchumi wa znz hauwezi kuchangia katika muungano kwa uwiano wake
 
Mkuu Nguruvi3 naomba kwanza uelewe kuwa mimi ni muumini wa serikali moja au kuvunja muungano na fikra zangu zinaweza kubadilika kama nitapata hoja mbadala za nadharia na kiuhalisia kama aina zingine za muungano zinafaa.
Mkuu labda nikuulize kidogo, una uhakika kuwa UK ndiyo inafanya taxation kule Scotland?
Nguvu waliyonayo kwa sasa katika bunge la Scotland ni uwezo wa kurekebisha kiwango cha tax mpaka kwenye 3pence kwa kila Pound ukilinganisha na tax ya England.

Kutokana na vuguvugu la Wascotland kutaka uhuru wao, Serikali ya Westminster iliwahonga kuanzia mwaka 2015 waweze kujiamulia wenyewe maswala ya kodi ya mapato na ardhi kwa masharti fulani fulani.
Pili, Hoja ya kuchangia haina maana kusiwe na muungano. Ina maana lazima tugawane muungano kwa kiwango kinachowina. Hivi mkuu unakubali kuwa ni lazima tulipe Bilioni 9.6 kwa mwaka kwa watu 81 walizuru Dodoma kaama Watalii
Ninakubaliana na wewe. Matatizo ya Muungano kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na usiri wa wanasiasa and very unequal katika nyanja mbali mbali za Muungano.

Kuna gharama zingine ni muhimu katika Muungano na haziwezi kuepukwa kama hii ya wabunge kulingana na nature ya muungano wetu. Hata kwenye Muungano wa UK. Kuna Bunge la Scotland lenye Wabunge wa nchi hiyo halafu pia kuna bunge la Westminster lenye Wabunge pia tena wa Kutoka Scotland.

Kwenye mambo ya shule. Wanafunzi wa elimu ya juu kutoka Scotland hawalipi Tuition fees ambayo ni kiasi cha £9,000 kulinganisha na wale wa England kama ilivyo kwa Tanzania kuhusiana na wanafunzi kutoka Zanzibar.
Tatu, ni kiasi gani Wales inachangia katika Uk kuliko England na kiasi inacpewa kutoka UK
Data za mwaka 2012/13 zinaonyesha kuwa, Wales iliweka mapato kwa kila mwananchi kwenye hazina kiasi cha 26% less than mwananchi wa UK. Kwa maana kuwa, mapato UK kwa ujumla kwa kila mwananchi ukiondoa North Sea Oil na Gas ilikuwa ni £7,300 wakati Wales ilikuwa £5,400.

Kwenye mgawo wake, Wales huwa inapata kiasi kama 12+% more than England per person. Kama kila mwananchi wa England akipewa £1, basi mwananchi wa Wales anapewa £1.12.
Nne, muungano mkubwa utabeba mdogo, ndivyo Warioba amependekeza na tume yake. Rasimu imeeleza wazi, je hilo linaifanya znz isichangie lolote huku tukidai zaidi kutoka Rukwa inayochangia zaidi ya trillioni 1 kwa huduma na bidhaa.
Zanzibar kutokuchangia kwenye Muungano kumesababishwa na nature ya Muungano wetu. Sisi toka kuasisiwa kwa Muungano tulionekana kama tunauhitaji sana huu Muungano na matokeo yake, Zanzibar ikajiona kuwa ina "pendeka" na ina "more value" katika Muungano zaidi ya Tanganyika. Matokeo yake, ikaanza "kudeka na kulinga" ikifahamu kuwa Tanganyika itaibembeleza tu. Hata kwenye maisha ya ndoa huwa mara nyingi, mmoja katika wana ndoa anapogundua kuwa anahitajika sana, basi mara nyingi huanza "kulinga na kudeka".
Tano, kama uchumi mkubwa unabeba mdogo, malalamiko ya znz kuhusu misaada yapo katika misingi gani.
Kuibeba Zanzibar kiuchumi siyo vibaya kama critea za kiuchumi zinabainisha hivyo, lakini kuibeba Zanzibar wakati uwezo inao ila haina nia ya kutokubebwa ni kujenga Muungano tegemezi.

Zanzibar is a free rider na mpaka pale tutakapofahamu kilichoko nyuma ya Viongozi wetu kukubali Tanzania Bara kuwa Provider, tutaendelea kuumiza vichwa bure kwa ajenda zilizojificha.

Hizi hoja za kusema Zanzibar haina uwezo ni hoja muflisi kwa sababu binadamu na kama taifa tumepewa uwezo wa kupambana na mazingira yoyote yale. Muungano ukivunjika kesho, Zanzibar itaendelea kuwa ni Zanzibar.

Kuna gharama zingine ni muhimu katika Muungano na haziwezi kuepukika kama hii ya wabunge kulingana na nature ya muungano wetu mpaka pale utakapo vunjika. Hata kwenye Muungano wa UK. Kuna Bunge la Scotland lenye Wabunge wa nchi hiyo halafu pia kuna bunge la Westminster lenye Wabunge pia tena wa Wascotland.

Kwenye mambo ya shule. Wanafunzi wa elimu ya juu kutoka Scotland hawalipi Tuition fees ambayo ni kiasi cha £9,000 kulinganisha na wale wa England kama ilivyo kwa wanafunzi wa Zanzibar.
Nane, Unaamini uchumi wa znz hauwezi kuchangia katika muungano kwa uwiano wake
Ninaamini kabisa Zanzibar kama nchi ikiwa inataka kuwepo kwenye Muungano, bila wasiwasi itaweza kuchangia gharama zote za muungano kama Tanganyika inavyofanya kwa sababu inauhitaji sana huu Muungano.
Sita, Je unaamini msingi wa muungano ni kugawana madaraka
Msingi wa Muungano haukuwa kugawana madaraka bali ilikuwa ni kuboresha madaraka kwa faida ya ukuaji wa Mataifa yaliyoungana.

Inawezekana kabisa kuna sababu nyingine kuu nje ya hizi tunazozifahamu lakini hizo sababu ninaamini hakuna ya kugawana Madaraka.

Malalamiko ya Muungano kwa upande wa Wazanzibari kwa sasa yanachagizwa na ubinafsi wa Uroho wa Madaraka na nation economic opportunities.

Malalamiko kwa upande wa Tanganyika yanachagizwa na kutokuelewa kwa undani faida na hasara za Muungano kwa sababu hata viongozi wetu hawataki kuziweka juu ya meza ili zichambuliwe.
 
@ng'awamapalala,

Nadhani unajua kwamba kutokana na changamoto za unitary system ya UK, kuna mjadala unaoendelea ambao unatazama uwezekano wa kuanzisha shirikisho litakalohusisha nchi za Uingereza, Scotland na Wales. Tukumbuke kwamba Wales and Scotland make up 15 percent of the UK population.

Naomba nipingane na wewe unapokataa kwamba hoja ya Nguruvi3 kuhusiana na mfumo wa Serikali mbili kutumika kama kichaka cha kuwapa wazanzibari madaraka ili waridhike na muungano wa sasa. Katika kitabu chake cha "our leadership and the destiny of Tanzania, uk 35 anasema hivi:

Our fear had been that if we would have one government it would appear that Tanganyika had swallowed up Zanzibar, we had to find a system that would remove from zanzibar this fear of being swallowed up, without heaping on Tanganyika the burden of running two governments of comparable size

Vile vile Mwalimu ananukuliwa na Dash (1963), The Constitution of India: A comparative study:

When Tanganyika and Zanzibar agreed to form one sovereign state, we could have adopted one of these usual structures of unity. But we felt unable to do so because of the small size of Zanzibar relative to that of Tanganyika. Zanzibar had at that time 300,000 people and Tanganyika 12,000,000. Tanganyika had swallowed up Zanzibar.

Mwalimu pia ananukuliwa na Srinivastan (1983) akizugumza kabla tu ya uhuru wa Tanganyika kwamba:

I fear Zanzibar will be a big headache for us.

Mwalimu ananukuliwa na shivji in pan-africanism or pragmatism:Lessons of Tanganyika and Zanzibar union akisema miaka ya mwanzo ya 1960s kwamba:

Ningekuwa na uwezo, ningekisukumia kisiwa cha zanzibar mbali kabisa katikatika ya bahari ya Hindi

Indeed, Miaka 50 baadae, Zanzibar is still not just a headache for us, bali pia mfumo wa serikali mbili unaongeza "handouts" kwao, na "handcuffs" kwetu; huu ndio msingi wa hoja ya nguruvi3.

Nikirudi kwenye hoja ya msingi juu ya suala la madaraka kwa wazanzibari, ili kuwahakikishia wazanzibari kwamba muungano hautawaweza kutokana na udogo wa taifa lao relative to Tanganyika, Mwalimu akahakikisha kwamba Serikali ya Muungano pia iwe ni ya Tanzania bara, wabunge wa zanzibar washiriki katika kuendesha mambo ya bara kupitia muungano, vile vile mawaziri wa zanzibar wapewe wizara za muungano. Na utaratibu huu ulianza mara tu baada ya muungano ambapo mawaziri kadhaa kutoka zanzibar wakapewa kazi kuongoza wizara ambazo hazikuwa za muungano bali za bara, kwa mfano Kassim Hanga (waziri wa viwanda, nishati na madini), Aburahaman Babu (waziri wa nchi ofisi ya rais, mipango), Hassan Nassor Moyo (Waziri wa sheria), na Idrisa Wakili (waziri wa habari na utalii).

Utamaduni huu ukaendelea kwa miaka mingi ambapo hata nafasi za Rais wa Muungano na Makamo wa rais ambao walikuwa pia ni marais na makamo marais wa Tanzania bara kwa koti la muungano, nafasi hizi zilienda kwa wazanzibari. Lakini kwa watanganyika, ni kama marufuku kushiriki mijadala ya bunge la wazanzibari, ni kama marufuku kuwa mawaziri upande wa zanzibar, na urais ndio haitakaa itokee. Huo ndio muungano wetu ambao hakika kwa wazanzibari ni "handouts", kwa watanganyika ni "handcuffs".

Kwa kweli logic iliyopo ni serikali tatu, lakini tatizo ni hoja za udogo wa zanzibar, huku wanasiasa wakitumia upenyo huo kuingiza hoja ya "gharama", hoja ambayo tutaijadili kwa kina katika uzi huu.

Hakuna kiongozi wa CCM au mwanazuoni mwenye haki ya kuwaamulia watanzania mfumo unaofaa. Katika kitabu chake cha Freedom and Unity (1966), Nyerere anasema:
No one person has the right to say "I am The People. No Tanzanian has the right to say I know what is good for Tanzania and others must do it. All Tanzanians have to make decisions for Tanzania.

Tume ya Katiba imekuja na maoni ya watanzania, na sisi tunaojenga hoja juu ya mfumo wa serikali tatu tunafanya hivyo baada ya kuelewa watanzania wanataka nini, sio makada wa CCM au Profesa Shivji wanataka nini.

Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,

Hoja yako kuhusu mabilioni ya fedha za walipa kodi wa Tanganyika kugharamia watalii Wa Zanzibar kule Dodoma ina mashiko ingawa Mtanganyika anapingana nayo bila hoja yoyote ya maana. Nikupe mfano mdogo tu:

Katika Study ya Malyamkono et al (2000): "The Political Plight of Zanzibar", Malyamkono et al anasema kwamba:

Katika vipindi viwili tu, 1984/5 na 1998/9, ambayo literally ni miaka miwili tu, direct dependence of Zanzibar on Tanzania Mainland ilikuwa karibia dollar za kimarekani milioni 835. Hii ni zaidi ya shillingi TRILIONI MOJA Kwa miaka miwili tu (curret value). Malyamkono et al wanaeleza kwamba hizi ni direct transfer from watanganyika to wazanzibari. Yani ni karibia sawa kama unapoitumia familia yako Tanzania fedha kwa Western Union.

Ni kwa mantiki hii Malyamkono et al wanaelezea jinsi gani Zanzibar drains the Union economy. Na kama tunavyofahamu, kwa vile Tanzania Bara ndio iliyovaa koti la muungano, draining the union economy maana yake ni draining the mainland economy, for that matter uchumi wa Tanganyika.

Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Zakumi , haya ni baadhi ya mambo znz imekuwa inalalamikia kuhusu misaada na mikopo kutoka nje. Haiwezekani useme Tanganyika ni kubwa ibebe dhamana na wakati huo huo ikitupiwa lawama za kunufaika na muungano na si kutoa zaidi.

Nitakuwa mtu wa kwanza kuilaani Tanzania kama haitachangia katika mashirika, taasisi na umoja wowote wa dunia ya leo. Pamoja na umasikini tuna haki na ni wajibu wetu kuchangia UN, AU, SADC, EAC n.k.


Burundi na Rwanda ndani ya EA ni ndogo lakini zinachangia katika jumuiya bila kujali udogo wake. Ndivyo itakavyokuwa kwa znz ikijiunga na EAC kama nchi kwa mujibu wa katiba yao ya 2010.


Hapa tunaonyesha jinsi ambavyo Watanganyika wamebeba muungano na uzito wote kwa ujira wa matusi, lawama na kashfa.


Nikupe mfano, Znz wameondoa baraza la mitihani katika JMT ambayo Tanganyika ilikuwa inabeba mzigo. Kwa sasa wana BMZ ambalo ni ''fiscal autonomy'

Kwanini kuwe na wajumbe wa bodi ya NECTA kutoka Zanz mbao si kuwa hawana interest na chombo hicho bali wanalipwa mishahara na mafao yao yote kwa huduma hewa!


Nimekuonyesha watalii 81 wanavyokula pesa kuliko halmashauri 41 za Tanganyika.

Shivji kasema halmashauri si suala la muungano. Swali linakuja kwanini watalii hao 81

Kwanza, wajihusishe na mambo yasiyo ya muungano

Pili, walipwe kiasi cha mabilioni badala ya kuyaelekeza katika halamshauri zetu


Kumbuka pesa wanazopewa Watalii wa znz ni za Tanganyika, niambie kwa mchango gani unaoweza kuufanyia extrapolation na kupata matokeo katika halmashauri zetu.


Inasikitisha watu 81 wanakula bilioni 50 kwa mwaka na halmashauri 41 zinapewa milioni 500. Ni watu kiasi gani wapo katika halmashauri hizo 41, kwamba kwa pesa zilizotolewa kila mmoja kwa average anapata senti ngapi as opposed to bilioni ngapi wanazokula watalii 81 kutoka Unguja na Pemba


Tunataka Tanganyika ili kuwe na fiscal autonomy. Yale ya pamoja tutachangia kwa kadri ya uwezo wa kila mmoja. Warioba kasema ni 7 si 22 ya sasa. Hapo tatizo lipo wapi?



Nguruv3:

Kuna gharama za muungano na nchi inayokubali kuwa engine ya muungano ni lazima ichukue gharama hizo. Kama hutaki kuchukua gharama hizo acheni hoja za muungano au integration yoyote na nchi jirani.

Mifano: Ujerumani Magharibi bado inachukua gharama za kuunganisha nchi. Kuna majimbo Marekani ambayo yanapata pesa nyingi kutoka federal government kuliko michango yao kwa federal government. Ujerumani inatumia pesa kubwa katika EU kuliko nchi zingine.

Wabunge wa Zanzibar katika bunge la muungano wanakuja kwa kigezo cha muungano. Bila muungano, Zanzibar haiitaji wabunge hao. Ni mfumo wa utawala tunaotaka watanganyika ndani ya muungano ndio unaofanya Zanzibar ilete wabunge hao 81. Hivyo usilalamikie gharama wakati ni kitu umekitaka.

Toka miaka ya mwanzoni mwa 80 wazanzibar wanataka serikali tatu. Ni mtanganyika anayetaka serikali mbili ambayo ina bunge linalowapa viti 81. Hilo sio kosa lao.

Wabunge wa kutoka Zanzibar wanalipwa kama wabunge wengine wa bunge la Jamuhuri la Muungano. Ni job description yao inayowalipa pesa hizo. Wafanyakazi wa mashirika ya kimataifa wanaotoka Tanzania wanalipwa kwa kutumia scale za mashirika hayo na sio uwiano wa mchango wa Tanzania katika mashirika hayo.

Kwa mtaji huu, wabunge 81 wa kutoka Tanganyika nao wanatumia bilioni 50 wakati halmashauri 41 zinatumia milioni 400. Hivyo hoja ya matumizi ya wabunge wa Zanzibar haina mshiko.
 
Nguruvi3,

Hoja yako kuhusu mabilioni ya fedha za walipa kodi wa Tanganyika kugharamia watalii Wa Zanzibar kule Dodoma ina mashiko ingawa Mtanganyika anapingana nayo bila hoja yoyote ya maana. Nikupe mfano mdogo tu:

Katika Study ya Malyamkono et al (2000): "The Political Plight of Zanzibar", Malyamkono et al anasema kwamba:

Katika vipindi viwili tu, 1984/5 na 1998/9, ambayo literally ni miaka miwili tu, direct dependence of Zanzibar on Tanzania Mainland ilikuwa karibia dollar za kimarekani milioni 835. Hii ni zaidi ya shillingi TRILIONI MOJA Kwa miaka miwili tu (curret value). Malyamkono et al wanaeleza kwamba hizi ni direct transfer from watanganyika to wazanzibari. Yani ni karibia sawa kama unapoitumia familia yako Tanzania fedha kwa Western Union.

Ni kwa mantiki hii Malyamkono et al wanaelezea jinsi gani Zanzibar drains the Union economy. Na kama tunavyofahamu, kwa vile Tanzania Bara ndio iliyovaa koti la muungano, draining the union economy maana yake ni draining the mainland economy, for that matter uchumi wa Tanganyika.

Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla
Mkuu kwa hesabu za darasa la IIB ni kuwa dollar milioni 845 ni sawa na Tsh Trilioni 1.33. Ukigawa kwa miaka miwili ni sawa na Bilioni 660 kwa mwaka mmoja.

Bajeti ya znz ni sawa na Tsh Bilioni 700. Mapato ya znz kwa exchange rate ya leo ni bilion 320 kwa mwaka. Hivyo kwa mwaka mmoja Tanganyika ilitoa mara mbili ya mapato ya miaka 2 ya znz.
Na kwa mwaka mmoja Tanganyika ilipeleka bajeti ya znz kama ilivyo.

Wasichokitanbua Watanganyika ni kuwa wafanyakazi wa muungano si kwamba wanalipwa mishahara tu bali Mtanganyika ataendelea kulipa kodi wakati wote wa mafao ya uzeeni ya mfanyakazi husika. Swali, ni wangapi wanaofanya kazi Tanganyika na ambao ni mzigo wa kizazi kijacho.

Kuhusu Watalii (wabunge wa znz) endapo SMZ ingewagharamia hilo lisingekuwa tatizo. Wanaweza kuja kuhudhuria vikao kama sehemu ya utalii.
Hata waandishi wapo Dodoma wakitenda majukumu yao.
Tatizo ni pale watu 81 wanapopewa bajeti kubwa kuliko halamashuri 41. Inasikitisha sana.

Angalia jedwali hapo juu uone jinsi Rukwa ilivyochangia kwa huduma na bidhaa katika pato la taifa. Ukiangalia majedwali zaidi utaona Rukwa imepewa bilioni 49 kwa shughuli za maendeleo. Mwaka huo huo Zanzibar ilipewa Bilioni 32 kupitia ofisi ya makamu wa Rais achilia mbali jambo jingine unalolijua.

Kwamba Rukwa inayochangia inapewa kidogo kuliko mgao wa papo kwa papo kuipitia ofisi moja tu ya makamu wa Rais.Swali ni kuwa hivi Rais akitoka znz Tanganyika itapata nini kutoka ofisi ya Makamu wa Rais?

Kwasababu ya kubebwa wznz hawana uchungu na muungano, wanaudharau kwavile kwao ni granted watapata wanachotaka. Wanakaa na kubadili katiba tu ili kukidhi matakwa yao.

Hivi kama Tanganyika inalipa bilioni 9.6 kwa ajili ya Watalii 81 wajao Dodoma, kuna sababu gani za msingi za mswada kupelkwa tena Baraza la Wawakilishi?
Hapa si tayari znz ina uwakilishi wa Watalii vipi tena yanayojadiliwa Dodoma yapelekwe kupata idhini BLW

Prof Shivji anapotosha kuwa ni procedure, lakini hakusema kuwa procedure hiyo inafungwa na vifungu vya katiba ya znz ya mwaka 2010 inayosema, pale penye mgongano wa jambo katiba ya znz itakuwa juu.

Hii maana yake ni kuwa mswada kutoka Bunge la JMT ukipelekwa BLW na kuleta utata basi katiba ya Zanzibar itakuwa juu kwa maamuzi.

Leo Shivji anasema lengo la muungano ni kugawana madaraka, madaraka ndiyo hayo ya kuidhalilisha Tanganyika?

Lakini pia mgawanyo wa madaraka siyo kitu kama hewa, ni jambo linalohusu gharama.
Kwa miaka mingi na at least 10 iliyopita znz haijachangia katika muungano.

Sasa wanataka madaraka ya kutawala nini, misitu au wanyama Serengeti?
Kama ni kutawala nchi, huyo rais wa znz atakuja na nini kutoka kwao!

Sijui kwanini Watanganyika hawaoni mambo rahisi kama haya.

CCM wnaolinda znz kwa kumbebesha Mtanganyika gharama ikiwa ni pamoja na kodi nzito hawatambui kuwa sehemu ya kodi za wznz zinakwenda kuchangia maendeleo ya nchi jirani ya znz
Hali hiyo itaendelea na tutarithisha watoto wetu ufukara uliopo kwa kuwatia ufukura zaidi.

Tanganyika ni masikini haina rsource za kutosha, vipi leo tuone tunawajibu wa kuumiza watu wetu ili kuwapendeza Raia wa nchi jirani ya znz(katiba ya znz 2010)



 
Mkuu Nguruvi3 naomba kwanza uelewe kuwa mimi ni muumini wa serikali moja au kuvunja muungano na fikra zangu zinaweza kubadilika kama nitapata hoja mbadala za nadharia na kiuhalisia kama aina zingine za muungano zinafaa.
Nguvu waliyonayo kwa sasa katika bunge la Scotland ni uwezo wa kurekebisha kiwango cha tax mpaka kwenye 3pence kwa kila Pound ukilinganisha na tax ya England.

Kutokana na vuguvugu la Wascotland kutaka uhuru wao, Serikali ya Westminster iliwahonga kuanzia mwaka 2015 waweze kujiamulia wenyewe maswala ya kodi ya mapato na ardhi kwa masharti fulani fulani.

Ninakubaliana na wewe. Matatizo ya Muungano kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na usiri wa wanasiasa and very unequal katika nyanja mbali mbali za Muungano.

Kuna gharama zingine ni muhimu katika Muungano na haziwezi kuepukwa kama hii ya wabunge kulingana na nature ya muungano wetu. Hata kwenye Muungano wa UK. Kuna Bunge la Scotland lenye Wabunge wa nchi hiyo halafu pia kuna bunge la Westminster lenye Wabunge pia tena wa Kutoka Scotland.

Kwenye mambo ya shule. Wanafunzi wa elimu ya juu kutoka Scotland hawalipi Tuition fees ambayo ni kiasi cha £9,000 kulinganisha na wale wa England kama ilivyo kwa Tanzania kuhusiana na wanafunzi kutoka Zanzibar.

Data za mwaka 2012/13 zinaonyesha kuwa, Wales iliweka mapato kwa kila mwananchi kwenye hazina kiasi cha 26% less than mwananchi wa UK. Kwa maana kuwa, mapato UK kwa ujumla kwa kila mwananchi ukiondoa North Sea Oil na Gas ilikuwa ni £7,300 wakati Wales ilikuwa £5,400.

Kwenye mgawo wake, Wales huwa inapata kiasi kama 12+% more than England per person. Kama kila mwananchi wa England akipewa £1, basi mwananchi wa Wales anapewa £1.12.

Zanzibar kutokuchangia kwenye Muungano kumesababishwa na nature ya Muungano wetu. Sisi toka kuasisiwa kwa Muungano tulionekana kama tunauhitaji sana huu Muungano na matokeo yake, Zanzibar ikajiona kuwa ina "pendeka" na ina "more value" katika Muungano zaidi ya Tanganyika. Matokeo yake, ikaanza "kudeka na kulinga" ikifahamu kuwa Tanganyika itaibembeleza tu. Hata kwenye maisha ya ndoa huwa mara nyingi, mmoja katika wana ndoa anapogundua kuwa anahitajika sana, basi mara nyingi huanza "kulinga na kudeka".

Kuibeba Zanzibar kiuchumi siyo vibaya kama critea za kiuchumi zinabainisha hivyo, lakini kuibeba Zanzibar wakati uwezo inao ila haina nia ya kutokubebwa ni kujenga Muungano tegemezi.

Zanzibar is a free rider na mpaka pale tutakapofahamu kilichoko nyuma ya Viongozi wetu kukubali Tanzania Bara kuwa Provider, tutaendelea kuumiza vichwa bure kwa ajenda zilizojificha.

Hizi hoja za kusema Zanzibar haina uwezo ni hoja muflisi kwa sababu binadamu na kama taifa tumepewa uwezo wa kupambana na mazingira yoyote yale. Muungano ukivunjika kesho, Zanzibar itaendelea kuwa ni Zanzibar.

Kuna gharama zingine ni muhimu katika Muungano na haziwezi kuepukika kama hii ya wabunge kulingana na nature ya muungano wetu mpaka pale utakapo vunjika. Hata kwenye Muungano wa UK. Kuna Bunge la Scotland lenye Wabunge wa nchi hiyo halafu pia kuna bunge la Westminster lenye Wabunge pia tena wa Wascotland.

Kwenye mambo ya shule. Wanafunzi wa elimu ya juu kutoka Scotland hawalipi Tuition fees ambayo ni kiasi cha £9,000 kulinganisha na wale wa England kama ilivyo kwa wanafunzi wa Zanzibar.

Ninaamini kabisa Zanzibar kama nchi ikiwa inataka kuwepo kwenye Muungano, bila wasiwasi itaweza kuchangia gharama zote za muungano kama Tanganyika inavyofanya kwa sababu inauhitaji sana huu Muungano.

Msingi wa Muungano haukuwa kugawana madaraka bali ilikuwa ni kuboresha madaraka kwa faida ya ukuaji wa Mataifa yaliyoungana.

Inawezekana kabisa kuna sababu nyingine kuu nje ya hizi tunazozifahamu lakini hizo sababu ninaamini hakuna ya kugawana Madaraka.

Malalamiko ya Muungano kwa upande wa Wazanzibari kwa sasa yanachagizwa na ubinafsi wa Uroho wa Madaraka na nation economic opportunities.

Malalamiko kwa upande wa Tanganyika yanachagizwa na kutokuelewa kwa undani faida na hasara za Muungano kwa sababu hata viongozi wetu hawataki kuziweka juu ya meza ili zichambuliwe.

Ng'wamapalala:

Mimi ni muumini wa federal government. Kama muungano wa sasa utavunjika, ndani ya Tanganyika nishabikia kuwepo kwa majimbo yenye mamlaka kamili na kuwa na federal government ya majimbo hayo. Sababu kubwa ni kuwa Tanzania ni kubwa na idadi ya watu wake ni wengi. Hivyo kutegemea viongozi wa serikali kuu kutatua matatizo ya wananchi ni kitu kisichowezekana. Wamejaribu kwa zaidi ya miaka 50 wameshindwa.

Tatizo kubwa hapa ni kuwa watanganyika sio BOLD. Muungano ulikuja kwa sababu ya usalama. Lakini zaidi ya hapo tumeshindwa kuwa engine ya maendeleo ya jamii. Huwezi kuendelea kutetea mfumo wa utawala unaotaka katika serikali ya muungano wakati huonyeshi maendeleo yoyote.
 
Nguruv3:

Kuna gharama za muungano na nchi inayokubali kuwa engine ya muungano ni lazima ichukue gharama hizo. Kama hutaki kuchukua gharama hizo acheni hoja za muungano au integration yoyote na nchi jirani.

Mifano: Ujerumani Magharibi bado inachukua gharama za kuunganisha nchi. Kuna majimbo Marekani ambayo yanapata pesa nyingi kutoka federal government kuliko michango yao kwa federal government. Ujerumani inatumia pesa kubwa katika EU kuliko nchi zingine.

Wabunge wa Zanzibar katika bunge la muungano wanakuja kwa kigezo cha muungano. Bila muungano, Zanzibar haiitaji wabunge hao. Ni mfumo wa utawala tunaotaka watanganyika ndani ya muungano ndio unaofanya Zanzibar ilete wabunge hao 81. Hivyo usilalamikie gharama wakati ni kitu umekitaka.

Toka miaka ya mwanzoni mwa 80 wazanzibar wanataka serikali tatu. Ni mtanganyika anayetaka serikali mbili ambayo ina bunge linalowapa viti 81. Hilo sio kosa lao.

Wabunge wa kutoka Zanzibar wanalipwa kama wabunge wengine wa bunge la Jamuhuri la Muungano. Ni job description yao inayowalipa pesa hizo. Wafanyakazi wa mashirika ya kimataifa wanaotoka Tanzania wanalipwa kwa kutumia scale za mashirika hayo na sio uwiano wa mchango wa Tanzania katika mashirika hayo.

Kwa mtaji huu, wabunge 81 wa kutoka Tanganyika nao wanatumia bilioni 50 wakati halmashauri 41 zinatumia milioni 400. Hivyo hoja ya matumizi ya wabunge wa Zanzibar haina mshiko.
Katika integration yoyote huwezi kuwa mtazamaji.

Yes,kuna udogo lakini lazima mkono uwepo. Burundi na Rwanda zinachangia EAC hakuna udogo. Znz inaenda EAC lazima ichangie haiwezi kuwa msikilizaji wa kudai madaraka eti Kenya iwahudumie kwasababu ya Integration.

Tunasema hivi, mambo yamebaki 7 ya muungano, katika hayo kila mmoja atie mkono mfukoni na kuweka japo senti.

Mfano, kuna tatizo gani SMZ ikuhudumia watalii 81 wanaokuja kuwakilisha nchi yao?
Hawana maana wala mafao na Tanganyika, wapo kwa ajili ya znz.

Kunasababu gani ada za Tanzania kule International Maritime(IMO) organization zilipwe na Tanganyika, znz ikusanye kodi(ZMO) bila kufanya remittance hata ya senti tano.
Udogo upo wapi, kuchukua na si kuweka.

Kuhusu Ujerumani, Ujerumani mashariki inachangia katika shirikisho.
Mchango wa Magharibi ni mkubwa lakini haiondoi ukweli kuwa mashariki wanachangia pia.
Sisi kwa ata least miaka 10 znz haina mchango, unawezaje kuweka katika mizani nchi hizo na sisi

Ujerumani na EU:
Ujerumani inafanya bail out ya Greece, Italy etc. Haitoi pesa kama msaada, ipo siku zitarudishwa tena na interest. Ujerumani ina bail out nchi hizo kwasababu investors wengi wamewekeza huko kutoka Ujerumani.

Kuziacha zifilisike maana yake ni kuacha mitaji ya mabenki na makampuni ya magari izame.
Impact ya hilo itaathiri sana uchumi wa Ujerumani kwa kuzingati wawekezaji hao ndio wenye mitaji katika masoko ya Ujerumani na ndio wanaochangia katika mabenki kwa uwekezaji.
Hivyo Ujerumani si Tanganyika, Tanganyika inatoa sadaka.

Wazanzibar anaotaka serikali 3 wapo Dodoma. Katika kura wamesema 'ndiyo'
Wao ndio vinara wa kuandika kanuni na kuzisimamia wakati Sitta anachakachua.
wznz hawasimami na Warioba wanasimama na CCM na wengine wakiwa CUF wamejificha.

Kuhusu wabunge kinachogomba si kiasi wanacholipwa.
Tatizo ni kuwa ni wataliim, kwasababu mambo yanayozungumzwa Dodoma hayawahusu.
Kwa mfano, lini umemsikia Pinda amekwenda znz kukagua shughuli za maendeleo?
Wakiwa Dodoma wanamsikiliza Pinda kama PM lakini inabaki kuwa hadithi kwasababu hawagusi kwa lolote.

Tunachosema ni kuwa badala ya kupeleka 9.6 bilioni kwa watu 81 gharama hizo zichukuliwe na SMZ kwasababu wanawakilisha znz.

Hatuna tatizo hata kama watalipwa milioni 50 kwa siku provided hizo ni pesa za Zanzibar siyo za mlala hoi wa Mtimbira, Kinesi au Isevya.

Mlipa kodi wa Kadewele, Magoroto au Viwanjasitini hana faida na uwepo wa watalii wa znz kwasababu wao hawamjui na hawana sababu za kumuongelea.

Lini umsesikia Pinda kaenda kukagua shughuliz znz.
Lini umesikia wabunge wa bunge la JMT wapo znz wakikagua shughuli.
Hata hao watalii 81 hawana kazi kwao kwanini sisi tuingie gharama za kuwahudumia?
 
YAH: YASIYOSEMWA KUHUSU GHARAMA ZA MUUNGANO

Kuna haja ya kuanza kuwaelimisha wananchi wa Tanganyika juu ya nini kinaendelea chini ya mfumo wa serikali mbili, na sasa nchi mbili, na jinsi gani hali zao za kiuchumi zinaathirika/zitazidi kuathirika wasipoanza kudai mabadiliko sasa. Nguruvi3 amejadili mengi ya msingi. Ningependa kuongezea maoni yangu zaidi kwa kuliweka suala la "fiscal autonomy" katikati kama framework of analysis. Itakuwa vizuri zaidi iwapo pia watetezi wa hoja kwamba serikali mbili una unafuu wa gharama kwa wananchi kuliko mfumo wa serikali tatu, wakajitokeza ili tupimane kwa hoja wakati tunapasha misuli kwenda kuwafafanulia wananchi kuelekea kura ya maoni kwanini wamechagua mfumo sahihi wa serikali tatu. Mtanganyika, Nape Nnauye, Gamba la Nyoka, ZeMarcopolo, Mwigulu Nchemba, MwanaDiwani, Ritz, Pasco, Zakumi, na wengine wa upande wa pili wa hoja, karibuni katika mjadala tupimane kwa "hoja".

Ø Dhana ya "Fiscal Autonomy" na umuhimu wake katika muungano wa nchi mbili au zaidi.

Kwa lugha rahisi, neno"Fiscal" linahusiana na "fedha za serikali", ambazo literary ni "fedha za umma". Katika muktadha huu, kinachoangalia ni "role" ya serikali katika uchumi wa taifa husika, ambapo mapato na matumizi ya serikali na taasisi zake/za umma, vinakuwa assessed. Kwa kawaida, linapokuja suala la matumizi na mapato, serikali inatarajiwa kuwa na "desired outcomes", huku pia ikihakikisha kwamba inaepuka "undesired outcomes." Kwa kawaida, kodi huwa ni suala unpopular kwa wananchi, lakini kwa vile kodi ni necessary evil kwa serikali kulipia huduma za kijamii na kiuchumi kwa ujumla, matumizi ya kodi lazima yawe ni popular with the electorate. In the eyes of any government, desired outcomes ni pale inapotokea kwamba matumizi ya fedha za umma ni popular with the electorate. Kinyume cha hapo huwa ni "undesired outcomes".

Kama tulivyokwisha jadili, maana rahisi ya kuelewa dhana ya - "fiscal autonomy", ni kwamba - ni mamlaka kamili au uhuru kamili wa taifa huru (sovereign state) wa kujiamulia juu masuala ya suala zima la public finance (rejea hapo juu) bila ya kuingiliwa na taifa linguine. Na mamlaka haya ni lazima yatambulike kwa mujibu wa katiba ya taifa husika.

Ø Fiscal Relationship Baina ya Serikali ya Jamhuri ya Tanzania na Serikali Ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Kama alivyojadili Nguruvi3 awali, kwa mujibu wa katiba ya JMT (1977), serikali ya mapinduzi ya zanzibar has almost complete "political and fiscal autonomy". Na ukweli juu ya hili unazidi thibitishwa na mabadiliko ya katiba ya Zanzibar (2010) ambayo, tofauti na awali ambapo Zanzibar ilikuwa ikitambuliwa kama sehemu ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania, hivi tunavyozungumza, Zanzibar inatambulika kama moja ya nchi zinazounda Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Nchi nyingine ambayo inastahili kuitwa Tanganyika, inaendelea kuitwa "Tanzania Bara" kufuatia sheria ya serikali, sheria namba 24 ya mwaka 1967 ambayo iliifuta Tanganyika kimya kimya. Kwahiyo, baina ya serikali hizi mbili (Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania), serikali ya Zanzibar ina "fiscal autonomy", huku serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania (ambayo pia ni serikali ya Tanzania bara), yenyewe ikiwa haina "fiscal autonomy".

Katika mazingira haya, kilicho cha Zanzibar ni cha Zanzibar, na kilicho cha Tanzania Bara/Tanganyika, ni cha wote (wazanzibari na watanzania bara). Huu ndio mfumo ambao CCM imeamua kwamba ni lazima uendelee kuwepo katika katiba mpya, huku advocates wa mfumu huo wakina ni pamoja na Mtanganyika, Nape Nnauye, Gamba la Nyoka, ZeMarcopolo, Mwigulu Nchemba, MwanaDiwani, Ritz, Pasco, Zakumi, Professa Issa Shivji, na wengine wengi.

Leo, Katiba ya Zanzibar nchi hii mpya ndani ya muungano:
· Kuunda serikali
· Kuunda Baraza la wawakilishi
· Kuunda Baraza la mapinduzi
· Kuwa na bendera yake
· Kuwa na wimbo wake wa taifa
· Kuwa na vikosi vyake vya ulinzi na usalama, n.k.

Katika haya, hakuna ambalo serikali ya Zanzibar inatakiwa kuripoti kwa serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Mbali ya hili, kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, baraza la wawakilishi (bunge la Zanzibar) ndio lenye mamlaka ya mwisho juu ya hatima ya sera na sheria ambazo zinapitisha na bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania. Mamlaka haya hayajalishi iwapo sera au sheria husika zinahusu mambo yasiyokuwa ya Zanzibar, kwa mfano masuala yanayohusu shughuli za kiuchumi au kijamii Tanzania bara kama vile Ukerewe, Tukuyu, Chalinze na maeneo mengine ya ardhi ya Tanzania Bara. Huu ndio mfumo ambao CCM imeamua kwamba ni lazima uendelee kuwepo katika katiba mpya, huku advocates wa mfumu huo wakina ni pamoja na Mtanganyika, Nape Nnauye, Gamba la Nyoka, ZeMarcopolo, Mwigulu Nchemba, MwanaDiwani, Ritz, Pasco, Zakumi, Professa Issa Shivji, na wengine wengi.

Miaka kadhaa iliyopita, kiliundwa chombo kinachoitwa "Joint Finance Commission" (JFC), chombo ambacho jukumu lake ni ‘to determine zanzibar's contribution to and allocation from the Government of the United Republic, lakini hadi leo, chombo hiki hakina influence yoyote juu ya masuala ilichopewa kuyasimamia.

Leo, finances za Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zipo independent of one another kama tulivyojadili huko nyuma (rejea bandiko #7 la uzi huu). The only significant agreements baina ya serikali hizi mbili ni hizi zifuatazo:
1. Serikali ya Zanzibar kupewa 4.5% share ya fedha ambazo vyanzo vyake ni vya nje (Loans and Grants). Tunasikia wanasema gawio hili haliwatoshi.
2. Serikali ya Zanzibar kupewa 4.5% of the dividends za Benki Kuu ya Tanzania (BOT).
3. Serikali ya Zanzibar kulipwa excise taxes kwa bidhaa zilizozalishwa Tanzania bara lakini ambazo hazijawa consumed Zanzibar.

Madhara ya "Fiscal Autonomy Kwa Muungano Chini ya Mfumo wa Serikali Mbali.

CCM inatumia maprofesa kuidhalilisha tume ya katiba (kwa mfano matumizi ya Profesa issa shivji) huku maprofesa hawa wakijikita katika hoja za kisiasa kutisha na kupotosha wananchi wasichague serikali tatu, huku wakiacha hoja muhimu za kiuchumi, aidha kwa makusudi au kwa kutozielewa vizuri. Wananchi wengi wa Tanzania Bara (Tanganyika) ambao hawana ufahamu kwamba inachofanya CCM ni propaganda, wanaishia kushawishika kwamba kwa kuwasikilza makada wa CCM with their new recruit "Profes Shivji", kuikataa Tanganyika, ASHAKUM SIO MATUSI – basi ni kuruka na kuepuka kukanyaga "haja ndogo", lakini maskini wa watu wanashindwa kuelewa kwamba, wanapoenda kutua ni kwenye "haja kubwa". Nitafafanua:

Chini ya mazingira ya sasa ambapo muungano ni wa serikali mbili na nchi mbili, huku serikali ya Zanzibar ikuwa na "fiscal autonomy", muda sio mrefu, wazanzibari wakiamua kutumia fiscal autonomy waliyonayo under their revolutionary government to adopt changes to its tax bases and rates vis a vis zile zilizo chini ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndugu zangu wa upande wa pili wa hoja Mtanganyika, Nape Nnauye, Gamba la Nyoka, ZeMarcopolo, Mwigulu Nchemba, MwanaDiwani, Ritz, Pasco, Zakumi, Professa Issa Shivji, na makada wengine wengi wa ccm], madhara yatakuwa ni haya yafuatayo:

1. Kuongezeka kwa gharama za tax compliance and administration.
2. Creation of opportunities for tax arbitrage for Zanzibar i.e. take advantage of a price difference between the two jurisdictions (Zanzibar and Tanzania (Tanzania Bara).
3. Itachochea ushindani wa kodi baina ya Zanzibar na Tanzania Bara (ushindani usio na tija kwa ‘Tanzania Bara' (kutokana na kukosa ‘fiscal autonomy' kama ya Zanzibar). Hali hii itakwaza internal trade, lakini mbaya zaidi ni kwamba, it will create difficulties katika jumuiya ya afrika mashariki (EAC) with respect to Customs Union.

Athari hii kwa EAC, Msomi kama Profesa Shivji aidha kwa kujua au kutojua, haizungumzii, huku hapo hapo akihimiza Vijana waunge mkono mfumo wa sasa wa serikali mbili, nchi mbili kwa hoja kwamba hivyo ndivyo tutaingia katika shirikisho la afrika la mashariki kwa kishindo!

Waziri wa EAC, Samuel Sitta ambaye suala hili linamgusa moja kwa moja kwa dhamana yake ya uwaziri, hana dalili yoyote ya kutumia fursa aliyonayo kama mwenyekiti wa bunge la katiba kurekebisha tatizo hili kwa kutetea mfumo wa serikali tatu kwa manufaa ya Tanzania Bara kwenye muktadha wa shirikisho la Jumuiya ya Afrika mashariki. Katika hili, linapokuja suala la Jumuiya ya Afrika mashariki, nimekuwa najadili sana juu ya haja ya viongozi wetu kuachana na "POLITICAL MOBILIZATION NA BADALA YAKE KUJIKITA KATIKA ECONOMIC CALCULATIONS." Lakini tunaishia kuambiwa kwamba hatuna hoja bali viroja na kina Mtanganyika, Nape Nnauye, Gamba la Nyoka, ZeMarcopolo, Mwigulu Nchemba, MwanaDiwani, Ritz, Pasco, Zakumi na wengine wengi.

· Zanzibar's Fiscal Autonomy As a TIMING BOMB

So far we are lucky (if this is the right word) kwamba hadi sasa, Zanzibar bado hawajaamua kutumia their "fiscal autonomy" kujitofautisha na Tanzania bara (kwenye suala la KODI), na badala yake, zanzibar bado wanaendelea to act somewhat responsibly kwa ku-adopt conforming tax legislations – kwa maana ya kwamba – tax bases and rates za Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania (Tanzania Bara/Tanganyika), ambapo, generally, Income Tax, VAT & Customs Duties za kwao (Zanzibar) bado zipo consistent na zile za serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania (Tanzania Bara/Tanganyika).

Awali (rejea bandiko #7 ), tulijadili kwamba zanzibar wana mamlaka kamili juu ya mikakati yake ya maendeleo kama taifa pamoja na mipando ya sera kuendana na mikakati hiyo. Kwa maana hii, Zanzibar imekuwa ikitumia her "borrowing autonomy" – yani they come with their own development/sectoral priorities, and then submit them HAZINA kwa kina Mwigulu Nchemba, kisha ule mgao wao wa 4.5% kutoka. Katika hili, kuna matatizo mawili: Kwanza, Fedha wanazopewa Zanzibar sio project specific, na pili, serikali ya Jamhuri ya Muungano haina mamlaka ya kuhoji fedha hizi (za walipa kodi wa Tanganyika) zinaenda kwenye miradi gani. Hali hii inapelekea timing bomb ya pili ambapo:

Risk ya kuruhusu a subnational government to borrow ni kwamba – serikali hii ya Zanzibar doesn't take into account madhara yanayotokana na "their borrowing" on the credit worthiness ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Tanzania Bara/Tanganyika). Mbaya zaidi ni kwamba, serikali kuu (serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Tanzania Bara/Tanganyika) haina uwezo to adopt sera ya "no bail out", ambayo ni credible. Hali hii ya Zanzibar kuwa na "borrowing autonomy", huku serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Tanzania Bara/Tanganyika) ikiwa haina uwezo wa kuja na sera ya kuzuia "bail out", ambayo ni credible inapelekea serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Tanzania Bara/Tanganyika) kuja na very soft budget constraints ambapo hata zanzibar wavurunde vipi, walipa kodi wa Tanganyika will bail them out. Hali hii inachochea tatizo la ukosefu wa "fiscal discipline" ambalo tumelipigia sana kelele elsewhere. In the final analysis, yote haya huko mbeleni yatatupeleka into "macroeconomic instability". Such instability ni matokeo ya serikali kukopesha hela ambazo haziendi katika uwekezaji (public investment) katika maeneo yenye kuongeza uzalishaji, kukuza ajira, na kupunguza mfumuko wa bei, among other things, badala yake nyingi ya fedha za walipa kodi zinaenda kwenye matumizi ya kawaida ikiwa ni pamoja na kugharamia watalii wa zanzibar kule Dodoma kama nguruvi3 anavyojadili.

Tusichoke kuwaelimisha wananchi na kuwaondoa upofu wa upotoshaji juu ya umuhimu wa kuizindua Tanganyika.


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.
 
Mchambuzi, mzee hapa umechanganya mambo mengi sana kujaza paragraph. Bandiko lako hili umejikita sana kwenye Gharama za Muungano na kama unavyosimamia kwamba njia mbadala yake ni kuongeza serikali ya tatu, yenye Ikulu yake na Ving'ora vyake. Naomba twende taratibu, na tuchambue namba moja baada ya nyingine. Taratibu:

Kwa sasa Budget ya Tanzania ni 10 Billion Dollar, na Budget ya Zanzibar ni 650Million na sisi tunachangia 450Million na wao wenyewe wanakusanya around 200Million.

Naomaba tutumie dollar kama evaluation currency specific kwa mjadala huu. Naomba utuambie serikali ya Tanganyika gharama zake za uendeshaji zitakuwa vipi, na gharama za serikali kuu ya Tanzania zitakuwa vipi?

Huko kwenye thread nyingine nilisema kwamba hakuna njia ya kupunguza gharama instead tutaongeza gharama. Sasa nyinyi orthodox wa serikali ya tatu hebu tuambieni hapa itakuwaje?
 
Mchambuzi, mzee hapa umechanganya mambo mengi sana kujaza paragraph. Bandiko lako hili umejikita sana kwenye Gharama za Muungano na kama unavyosimamia kwamba njia mbadala yake ni kuongeza serikali ya tatu, yenye Ikulu yake na Ving'ora vyake. Naomba twende taratibu, na tuchambue namba moja baada ya nyingine. Taratibu:

Kwa sasa Budget ya Tanzania ni 10 Billion Dollar, na Budget ya Zanzibar ni 650Million na sisi tunachangia 450Million na wao wenyewe wanakusanya around 200Million.

Naomaba tutumie dollar kama evaluation currency specific kwa mjadala huu. Naomba utuambie serikali ya Tanganyika gharama zake za uendeshaji zitakuwa vipi, na gharama za serikali kuu ya Tanzania zitakuwa vipi?

Huko kwenye thread nyingine nilisema kwamba hakuna njia ya kupunguza gharama instead tutaongeza gharama. Sasa nyinyi orthodox wa serikali ya tatu hebu tuambieni hapa itakuwaje?
Jibu hoja zangu zinazo base on fiscal autonomy framework, au njoo na ur own framework tujadili kero husika kiuchumi and public finance kwa manufaa ya washirika wa muungano;achana na hoja zisizokuwa na mashiko, hazina any framework kuzijadili;bila framework of analysis, hayo ma-GDP, bajeti, na analysis za serengeti advisors ni too junior kwa mjadala huu; isitoshe zimeshajibiwa na nguruvi3; what are your counter arguments? Anza kwa kukosoa my analytical framework, and how I have positioned the subnational gvnt ya zanzibar yenye autonomy na ile ya JMT isiyo na autonomy side by side;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom