Duru za Siasa: Matokeo ya Uchaguzi Marekani

Duru za Siasa: Matokeo ya Uchaguzi Marekani

Kama kweli hacking ya Warusi ndo ilimfanya Trump ashinde, iweje sasa Hillary aongoze kwenye popular vote?

Hao Warusi ndo waliompa ushindi wa popular vote huyo bibi?

Nawaza tu mi mbeba maboksi.....
 
Kama kweli hacking ya Warusi ndo ilimfanya Trump ashinde, iweje sasa Hillary aongoze kwenye popular vote?

Hao Warusi ndo waliompa ushindi wa popular vote huyo bibi?

Nawaza tu mi mbeba maboksi.....
Upuuzi tu,obama alitaka ashinde yule kigagula ili alinde na kuendeleza kila kitu chake alichofanya. Lkn lingine tukubaliane ingawa wengine hapa hawatakubali..! Obama akili zake ni zilezile za kiafrica,ukiangalia alivyokuwa ameshupaa ktk huu uchaguzi huku akiwa uongozini amethibitisha uafrica wake.

Madai ya hacking pia yanatokea wakati marekani ikiwa chini ya Rais mweusi na sasa kuthibitisha uwezo wake mdogo wa kufikiri kashupaa kweli kumtishia putin wakati yeye anaondoka ikulu. Hata hili la kuhonga watu waandamane kushinikiza wapiga kura wa electrol college wabadili matokeo ni upuuzi ule ule. Trump asingepata kura 270 bado angeidhinishwa na congress ambayo nayo inadhibitiwa na republican.

Kwa akili ya kawaida tu ambayo haihitaji kuwa umesoma kujua mambo waliyofanya huyu bibi na obama yamewaaibisha sana ktk huu uchaguzi. Lkn si wao tu hata wachambuzi wetu wa hapa nao wametia fora ktk kuuchambua huu uchaguzi us. Hasa mag3 ambae anaamini trump hana akili lkn wakati huo huo anajua km trump ni tajiri mwenye utajiri wa zaidi ya dollar billion 4. Yaani sijui waafrika sijui tuna akili gani!!? Hv mtu asiye na akili anawezaje kutajirika?? Huwezi kutenganisha uwezo mkubwa wa kufikiri na utajiri haya ni mambo ya kijiweni..!!
 
Kama kweli hacking ya Warusi ndo ilimfanya Trump ashinde, iweje sasa Hillary aongoze kwenye popular vote?

Hao Warusi ndo waliompa ushindi wa popular vote huyo bibi?

Nawaza tu mi mbeba maboksi.....
Hapa nichangie kidogo tu bila kujadili mengine

Uchaguzi wa US ni wa aina yake. Kwa mfano, Wisconsin na Michigan zingeabaki Democrat, Trump akashinda zote isipokuwa NH, uchaguzi wote wa US ungeamuliwa na congressional district ya Maine

Kwa maana 'EV 1' zaidi ingetoa mshindi, bila kujali ukubwa wa EC zoote au Popular vote

2. Hillary angeweza kushinda California na Trump akapata kura 10 na isingeabadilisha matokeo ya leo

3. Swing state zinaamua nani awe Rais, haihitaji influence ya nchi nzima.

Hivyo uchaguzi wa US upo katika mfumo tofauti. ndio maana asiyelewa anaweza kusema mfumo wa Electoral college inazuia state kubwa kuchagua Rais, akiwa haoni state ndogo zinazoweza kuchagua Rais

Ni senti moja
 
Upuuzi tu,obama alitaka ashinde yule kigagula ili alinde na kuendeleza kila kitu chake alichofanya. Lkn lingine tukubaliane ingawa wengine hapa hawatakubali..! Obama akili zake ni zilezile za kiafrica,ukiangalia alivyokuwa ameshupaa ktk huu uchaguzi huku akiwa uongozini amethibitisha uafrica wake.

Kuna siku Rais Obama aliwaambia Wamarekani weusi kuwa wakimchagua Trump itakuwa ni tusi binafsi kwake (personal insult). Yaani POTUS anapiga siasa za kibaguzi??

Akawa akifanya Press conference kabla ya uchaguzi anaonyesha hasira zake za wazi kwa Trump bila kujali kuwa yeye ni Rais.

Yeye na mke wake walitumia mda wao mwingi kumkampenia Hillary na kumkashifu Trump utadhani Rais Obama alikuwa kwenye re-election.

Legacy aliyokuwa anahangaika kuilinda ni legacy ya kufeli. Hakuna cha maana alichowafanyia wananchi waliomchagua halafu anazunguka kila kona kuwaambia mgombea gani wamchague!

Alizungumza hadharani kuwa Trump hawezi kuwa mgombea wa Republican kipindi cha primaries, Trump akawa mgombea. Badala ya kutulia, akaropoka tena, akadai Trump hawezi kushinda Urais, akashinda. Ni bora angekaa kimya angeonekana mwenye busara kuliko kujifanya anajua akili za wananchi zilipo.


Madai ya hacking pia yanatokea wakati marekani ikiwa chini ya Rais mweusi na sasa kuthibitisha uwezo wake mdogo wa kufikiri kashupaa kweli kumtishia putin wakati yeye anaondoka ikulu. Hata hili la kuhonga watu waandamane kushinikiza wapiga kura wa electrol college wabadili matokeo ni upuuzi ule ule. Trump asingepata kura 270 bado angeidhinishwa na congress ambayo nayo inadhibitiwa na republican.

Rais Obama aliambiwa awaambie waandamaji waache kuandamana kwa kuleta fujo na kusababisha uharibifu, yeye kwa kuweka siasa mbele akazidi kuwachochea.

Mara anataka report ya 'Russia hacking' kabla hajaondoka madarakani. Waliomtangulia kipindi kama hiki walikuwa wametulia hawana mbwembwe. Yeye hataki kukubali kuwa wananchi wamemchoka na hawataki kumsikia bado anahangaika kucheza 'Russian Card' tena wiki nne kabla hajaondoka madarakani!

Electors walitishiwa vifo, Rais Obama hajasikika kulaani na kukemea vitendo hivyo kwa sababu electors waliotishiwa ni wa Republican, cha ajabu alimhurumia gaidi aliyejeruhi watu Ohio State University!!


Kwa akili ya kawaida tu ambayo haihitaji kuwa umesoma kujua mambo waliyofanya huyu bibi na obama yamewaaibisha sana ktk huu uchaguzi. Lkn si wao tu hata wachambuzi wetu wa hapa nao wametia fora ktk kuuchambua huu uchaguzi us. Hasa mag3 ambae anaamini trump hana akili lkn wakati huo huo anajua km trump ni tajiri mwenye utajiri wa zaidi ya dollar billion 4. Yaani sijui waafrika sijui tuna akili gani!!? Hv mtu asiye na akili anawezaje kutajirika?? Huwezi kutenganisha uwezo mkubwa wa kufikiri na utajiri haya ni mambo ya kijiweni..!!

Nadhani wachambuzi wa Tanzania walikuwa wanazoa habari kwenye Liberal media za US ambazo zilikuwa biased kwa Trump. Pengine kwa kujua au kutokujua kuwa zile media companies kubwa duniani haziwezi kuandika au kusema uongo.

Rais Obama amekuwa kama viongozi wa nchi za Kiafrica, sijui haamini matokeo au haoni kama mda wake umeisha? Au anadhani akiondoka madarakani bado atakuwa na influence, pengine anatafuta legacy!..sasa hivi dunia nzima imeelekeza macho kwa Trump na yeye bado anatafuta kukaa kwenye headlines kwa habari ambazo hazina kichwa wala miguu.
 
3. Swing state zinaamua nani awe Rais, haihitaji influence ya nchi nzima.

Braza, I'm a US politics junkie. Yote hayo nayaelewa fika kabisa.

Wakati Trump anaenda kupiga kampeni WI, MI, na PA, wale so called "experts" walimbeza na kusema he has no snowball's chance in hell of winning them let alone winning the whole thing.

Hillary hata kampeni hakupiga kule WI kwa sababu aliamini hilo jimbo ni true-blue kwa Democrats. GOP mara ya mwisho kushinda huko kwenye urais ilikuwa 1988, kama sijakosea.

Simply put, Trump outworked her. Kuna nyakati bibi alikuwa hata hapigi kampeni kwa wiki nzima eti sijui akijiandaa na debates mara sijui akipumzika. Wakati yeye Hillary anapumzika Trump alikuwa kwenye campaign trail.

Ndo maana mimi binafsi naikataa hoja ya Warusi sijui ku influence huu uchaguzi. Hicho ni kisingizio tu. Kisingizio cha team Hillary ambao nahisi hawataki kukubali kuwa walikuwa outworked na outsmarted na team Trump.

Warusi hawaku stuff ballots kwenye mashine za kupigia kura. Na ndo maana hata unaona Hillary kapata kura nyingi za popularity.

Uchaguzi mkuu wa Marekani, kwa mfumo wanaotumia, huwa ni wa kimkakati zaidi. Na ndo hapo Trump alipowazidi akili team Hillary.

Kuilaumu Urusi ni jitihada tu za ku deflect lawama.
 
Kwa kifupi tu. Sikubaliani na suala la kuhusisha ubovu wa kitu ama mtu na uafrika. 'Ubovu' wa Obama ni wake yeye kama yeye.

Niliwahi kusema huko siku za nyuma kuwa Obama anaendeshwa na White Power 'inayomiliki' White House. Nakuhakikisha 'kuchanganyikiwa ' kwa Obama ni kuonyesha jinsi White power ilivyo'data' kwa maamuzi ya Wamarekani wa vipato vya kati na chini waliyochukua ya kumpiga chini HRC. Pale, Obama, anaamrishwa kaseme hiki ama kile!! Aliwahi kukiri kuwa hakutaka kumuondoa Comrade M. Ghadaffi bali alikuwa'pressurised' kuruhusu jambo hilo.
 
Mwaalimu wangu hapa Jukwaani Nguruvi3, hivi unaona jinsi demokrasia ya wenzetu (US) ilivyo na mushkeli. Sasa watu kwa uhuru wao wa kidemokrasia waliamua kutompa kura Hillary Clinton lakini kwa kitendo hicho wamepigwa fine. Sasa hapo hauoni kuwa demokrasia zetu na zao mapungu ni yale yale tofauti 'rangi' tu!?
===========
Four Washington state electors who broke their pledge to vote for Democratic candidate Hillary Clinton are each being fined $1,000, after 3 chose to vote for ex-Secretary of State Colin Powell, and one for Native American tribal elder Faith Spotted Eagle.
They will all be fined next week, and have 60 days to pay, according to the spokesman for Washington Secretary of State Kim Wyman, who spoke to the AP. He added that an appeals process is being formulated in case of a challenge.

This is the first time anything like this has happened in the state in 40 years, when one elector went rogue and voted for Ronald Reagan instead of Gerald Ford, who won in Washington but lost the general election to Democratic candidate Jimmy Carter in 1976. It was that year that the penalties for going rogue were signed into law, but 2016 is the first year they will be enforced.
Washington state’s rogue electors make history – fined $1,000 for not voting Clinton
 
Mwaalimu wangu hapa Jukwaani Nguruvi3, hivi unaona jinsi demokrasia ya wenzetu (US) ilivyo na mushkeli. Sasa watu kwa uhuru wao wa kidemokrasia waliamua kutompa kura Hillary Clinton lakini kwa kitendo hicho wamepigwa fine. Sasa hapo hauoni kuwa demokrasia zetu na zao mapungu ni yale yale tofauti 'rangi' tu!?
===========
Four Washington state electors who broke their pledge to vote for Democratic candidate Hillary Clinton are each being fined $1,000, after 3 chose to vote for ex-Secretary of State Colin Powell, and one for Native American tribal elder Faith Spotted Eagle.
They will all be fined next week, and have 60 days to pay, according to the spokesman for Washington Secretary of State Kim Wyman, who spoke to the AP. He added that an appeals process is being formulated in case of a challenge.

This is the first time anything like this has happened in the state in 40 years, when one elector went rogue and voted for Ronald Reagan instead of Gerald Ford, who won in Washington but lost the general election to Democratic candidate Jimmy Carter in 1976. It was that year that the penalties for going rogue were signed into law, but 2016 is the first year they will be enforced.
Washington state’s rogue electors make history – fined $1,000 for not voting Clinton
Mkuu sijui umeelewaje hii habari ambayo naweza kusema haina details za kutosha ndiyo maana umefikia conclusion ukiongozwa na Prejudice dhidi ya Demokrasia ya US na Pengine Clinon

Kabla sijafafanua ningependa kupata japo ufahamu kuhusu maswali haya
1. Ni nani amepigwa faini na faini ilihusu nini na ipo katika sheria au nje ya sheria?
2. Kwanini Texas hawakupigwa faini lakini Washington wamepigwa?
3. Faini hizo wanalipa kwa nani, state au kwa chama husika?
4. Ingetokea California au Ohio, utaratibu upi ungetumika?
 
Mwaalimu wangu hapa Jukwaani Nguruvi3, hivi unaona jinsi demokrasia ya wenzetu (US) ilivyo na mushkeli. Sasa watu kwa uhuru wao wa kidemokrasia waliamua kutompa kura Hillary Clinton lakini kwa kitendo hicho wamepigwa fine. Sasa hapo hauoni kuwa demokrasia zetu na zao mapungu ni yale yale tofauti 'rangi' tu!?
===========
Four Washington state electors who broke their pledge to vote for Democratic candidate Hillary Clinton are each being fined $1,000, after 3 chose to vote for ex-Secretary of State Colin Powell, and one for Native American tribal elder Faith Spotted Eagle.
They will all be fined next week, and have 60 days to pay, according to the spokesman for Washington Secretary of State Kim Wyman, who spoke to the AP. He added that an appeals process is being formulated in case of a challenge.

This is the first time anything like this has happened in the state in 40 years, when one elector went rogue and voted for Ronald Reagan instead of Gerald Ford, who won in Washington but lost the general election to Democratic candidate Jimmy Carter in 1976. It was that year that the penalties for going rogue were signed into law, but 2016 is the first year they will be enforced.
Washington state’s rogue electors make history – fined $1,000 for not voting Clinton
Mkuu naona bado unatafakari hoja hapo juu.

Nichangie hoja kwa maana mbili, kwanza, dhana ya uchaguzi na pili dhana ya demokrasia

Kwa hoja yako' waliopigwa faini wameonewa' wana uhuru wa kumchagua wamtakae'

Mantiki yako inaongozwa na hoja hizi
1. Wamepigwa faini kwasababu ya kutompigia kura Hillary Clinton,ni kukiuka Demokrasi
2. Kwamba, wana uhuru lakini kuna mizengwe inawekwa kwavile wamekwenda kinyume
3. Kwamba faini waliopigwa inatoka kwa Democrats
4. Kwamba, electors wapo huru kumchagua wamtakaye
5. Hayo 1-4 ni ukiukwaji mkubwa wa demokrasia kama tufanyavyo sisi

Majibu ya dhana ya hoja zako
1. Uchaguzi mkuu wa Marekani:
Kama tulivyojadili utaratibu upo ngazi za vyama,state na federal

Tulisema kuiba kura hakuwezekani kitaifa ingawa inaweza katika county au state

Kila state ina bunge na senate,uchaguzi wa N.Carolina ni tofauti kwa utaratibu S.Carolina

Ndio maana yapo malalamiko(voter suppression) NC tusiyoyasikia South Carolina

Afisa tawala wa state( sec of state) ndiye msimamizi wa chaguzi katika ngazi ya state.

Huyu ni mtu wa tatu kwa wadhifa baada ya state Governor na Lieutenant

Ukisoma article kwa umakini faini wamepigwa na Washington sec of state $ 1000

Ni mara ya kwanza, si kwasababu ya Clinton bali utaratibu kutumika katika state husika

$1000 haikubuniwa, ipo sheria ya Bunge, kuanzia 1976 Reagan akiwania na Ford

1976 electors walimpigia Reagan na siyo Ford(alishinda state)ya Washington si kitaifa

Ndipo Washington state ikaweka utaratibu electors wampigie aliyeshinda state

Uchaguzi wa 2016 Clinton alimshinda Trump na electors waliwajibika kumpigia kura

Kwavile walikwenda kinyume na sheria, sec of state akawapiga faini, si Clinton Vs Trump

Kila state ina utaratibu unaoongoza electors wanavyokusanyika na kupiga kura

Kwa maana hiyo Maine na Nabraska wanatumia congressional district tofauti na Ohio

Article haikuwa na details kwa utaratibu na hivyo kudhani Dem na Clinton wanahusika

Kilichokuongoza ni dhana ya Clinton na Trump kuonyesha ''upendeleo au uonevu''

Kwa bahati mbaya uka igonore ukweli wa taratibu zilivyo, adhabu na nani katoa

Mwisho ukatoa conclusion Clinton/Dem wamekikuka misingi ya 'watu huru kuchagua'

2. Demokrasia tumeijadili, haiwezi kuwa uniform Duniani na hili tulikueleza kwa kina.
Demokrasia ni taratibu za jamii husika kupanga, kuamua kuchagua wanayokubaliana

Ukitazama uchaguzi wa US, utaiona demokrasia bila miwani wala lens

Unapolinganisha na kwetu inashangaza kwasababu hata tuliyokubaliana hautendi

Fuatilia tume ya uchaguzi ya US katika federal level, rudi katika state hadi county

Ukimaliza, ulinganishe na tume ya uchaguzi ya Tanzania ambayo mwenyekiti anateuliwa na mwenyekiti wa chama na kuapishwa na kwa kofia ya Urais ili mwenyekiti wa tume asimamie haki kati ya mwenyekiti alimteua na mtu mwingine!

Mkuu Chungwa na nazi koroma ni vitu viwili tofauti,kulinganisha ni kutafutia watu kicheko

Tusemezane
 
Asante sana Mwalimu wangu, kwa maelezo mazuri. Ni kweli wale wamepigwa faini kutokana na sheria inayoongoza hiyo state. Ila Sheria ile ni kandamizi na inakiuka Katiba ya Marekani ya uhuru wa kutoa maoni (kwa mujibu wa mmojawapo wa aliyepigwa faini). Malalamiko hayo hayakombali sana na Malalamiko ya kwetu hapa ya sheria ya "habari " na hata hii ya mtandao kuwa inakiuka Katiba yetu.

Kwa msingi wa tafsiri yako ya demokrasia (Demokrasia ni taratibu za jamii husika kupanga, kuamua kuchagua wanayokubaliana), ambayo nimeipenda kweli na ningemshauri iingizwe rasmi kwenye mtaala wa somo la uraia hapa kwetu; nadhani si sahihi kumlaumu Mheshimiwa rais juu ya kuteua na kuapisha Mwenyekiti wa Tume. Asilaumiwe kwa sababu hiyo ndiyo demokrasia(rejea tafsiri yako) yetu. Rais kafuata utaratibu tuliojiwekea kupitia wawakilishi wetu bungeni na tukaukubali. Sidhani kama kunasheria ambayo inamtaka mwenyekiti wa chama cha siasa wakati huo huo ni rais asishiriki kumteua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi hapa nchini. Hiyo sheria hapo, Mwalimu wangu. Watanzania kama tunahitaji sheria hiyo basi tutumie 'demokrasia ' yetu kuiweka.

Ndiyo maoni yangu hayo Mwalimu wangu wa hapa JF.
 
Asante sana Mwalimu wangu, kwa maelezo mazuri. Ni kweli wale wamepigwa faini kutokana na sheria inayoongoza hiyo state. Ila Sheria ile ni kandamizi na inakiuka Katiba ya Marekani ya uhuru wa kutoa maoni (kwa mujibu wa mmojawapo wa aliyepigwa faini). Malalamiko hayo hayakombali sana na Malalamiko ya kwetu hapa ya sheria ya "habari " na hata hii ya mtandao kuwa inakiuka Katiba yetu.

Kwa msingi wa tafsiri yako ya demokrasia (Demokrasia ni taratibu za jamii husika kupanga, kuamua kuchagua wanayokubaliana), ambayo nimeipenda kweli na ningemshauri iingizwe rasmi kwenye mtaala wa somo la uraia hapa kwetu; nadhani si sahihi kumlaumu Mheshimiwa rais juu ya kuteua na kuapisha Mwenyekiti wa Tume. Asilaumiwe kwa sababu hiyo ndiyo demokrasia(rejea tafsiri yako) yetu. Rais kafuata utaratibu tuliojiwekea kupitia wawakilishi wetu bungeni na tukaukubali. Sidhani kama kunasheria ambayo inamtaka mwenyekiti wa chama cha siasa wakati huo huo ni rais asishiriki kumteua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi hapa nchini. Hiyo sheria hapo, Mwalimu wangu. Watanzania kama tunahitaji sheria hiyo basi tutumie 'demokrasia ' yetu kuiweka..
Mkuu uhuru wa kutoa maoni, au kauli au kujieleza una mipaka yake.

Huwezi kusimama airport ukazungumzia 'mabomu' milipuko n.k. ukaachwa tu.
Huwezi kutishia maisha ukaachwa. Kwamba, uhuru wa maoni una mipaka inayolindwa kisheria

Pili,Rais hajalaumiwa kuteua tume na wala hakuna anayakataa utaratibu huo uliotumika miaka mingi

Kinachogomba ni utaratibu huo ulikuwa wa chama kimoja na hauja reflect hali ya sasa

Kwa msingi huo sisi tuliojiwekea utaratibu miongoni wanasema ni wakati tuutazame kwa mazingira tuliyo nayo. Kama hakuna matatizo uendelee, hiyo ndiyo demokrasia.

Ni lazima mfumo uliotumika miaka 50 uwe 'calibrated , tested and validated'

Kwavile hawana sababu za kutosha za kuwapa haki ya kutawala, hawataki.
Wamekataa katiba mpya,miongoni mwa mambo ni tume huru ya uchaguzi

Wanajua uwepo wa tume huru hawawezi kupata aslimia 40 ya Bunge au Urais. Wanajua walivyochokwa na wananchi na walivyoshindwa kutoa majibu miaka 50.

Tume iliyopo sasa unaweza kusema ni huru kwasababu tu ya kusema.
Kimantiki si huru kama tulivyoona miaka 10. Unakumbuka suala la electronics lilivyoisha bila majibu?

Kwasababu tume haikujua ifanye nini, ikaishia kurudisha bilioni 10+. Kila serikali ikitamka tume ipo nyuma ya tamko na kila aina ya aibu tuliyoona.

Waliostaafu nafasi zinawasuta wanasema kuna haja ya mabadiliko.
Hii ni baada ya kufaidika miaka mingi wakijua haikuwa sahihi, wafanye nini? 'mtumikie kafiri...'

Kwa mtazamo wa tume, mwenyekiti anapoteuliwa na mwenyekiti wa chama ambaye ana vyombo vya dola kama Polisi, TISS n.k. mwenyekiti wa tume uhuru wake unakuwa limited kama si hakuna

Si unakumbuka Jecha aliondolewaje ukumbini, alifikaje kituo cha TV, alililndwaje pamoja na kukiuka taratibu na amependekezwa apewe tuzo. Hili tu huoni linakueleza kitu?

Tume huru ni lazima iwe na 'watch dog' mwingine kama Mahakama au Bunge.

Kwa sasa ipo chini ya serikali kwasababu mwenyekiti anawajibika kwa mteuzi hata kama hatukubali

Tazama US, katika federal level si zaidi ya watu 10, halafu kuna state level inayoratibu mambo yake hadi kufikia county. Chaguzi zinaamuliwa kituo cha kura hazisubiri kwenda kupangwa Washington

Kwa ukubwa wa Marekani ambapo Texas pekee ni kubwa kama Tz na California ikaribia population ya Tz, matokeo ya uchaguzi uwe wa house, senate, au President tunayapata usiku mmoja

Tanzania yanakusanywa yakasomwe Dar es Salaam, hivi hapa kuna ulinganifu kweli

Nimalizie kwa kusema kutafuta hoja za kulinganisha Tz na US katika demokrasia ni ngumu kuliko kutafuta sindano katika gunia la pumba za mpunga.
 
WIKI HII KATIKA SIASA ZA US

KURA YA BARAZA LA USALAMA

US imekwepa kupiga kura katika kikao cha baraza la usalama kwa suala la ujenzi wa makazi Israel katika ardhi ya Wapalestina. Suala hilo limeleta mtafaruku kiasi cha baadhi kupotosha ukweli

Kuanzia wakati wa Reagan hadi Obama sera ya Marekani ni kupinga Israel kujenga makazi katika maeneo yanaoelezwa kuwa ni ya Wapalestina.

Msimamo upo katika kinachoitwa'two state solution'

Ukweli ni kuwa marais wote wa Republican na Democrat wamekuwa na msimamo huo.
Tofauti ni US kutotumia Veto kuzuia mswada ndani ya baraza kama ilivyozoeleka

Hilo linachagizwa na uhusiano mbaya kati ya Obama na Netanyahu toka mapema

Katika jitihada za kutafuta suluhu ya kudumu, Obama alimtuma VP Joe Biden Israel

Katika hali isiyotarajiwa, siku aliyofika ikatangazwa na serikali kupitia sheria za majiji ongezeko la ujenzi wa nyumba .Jambo hilo lilikuwa kama kibao cha uso kwa Marekani

Obama alimwalika BB Nyahu na kumpa mapokezi ya dharau kama majibu

Netanyahu akaendelea na mpango wa kutumia House na Senate ambako alialikwa kuhutubia 'joint session' ya mabunge hayo bila kushirikisha wizara husika au WH.

Majuzi mswada ukaandaliwa na ilitegemewa kuwepo kura ya Veto kama kawaida.

Israel kwa kutambua mtafaruku iliamua kumtumia Trump kuweka pressure kwa Obama

Hilo likatia chumvi katika kidonda, Ob akisema sera ni Rais mmoja kwa wakati mmoja

Wiki hii Trump alitangaza balozi wa US Israel David Friedman anajulikana kwa sera za kuhamisha Ubalozi wa US kwenda Jeruslem, ishara ya kutambua makao makuu ya Israel

Maamuzi ya kushtua ni uteuzi wa balozi na kushadidia kuhamishaa ubalozi Jerusalem

Jerusalem ni eneo lenye historia ya dini mbili za Ukristo na Uislam.

Ugomvi unaohusisha eneo hilo unahusisha eneo la kati na mashriki ya kati kwa ujumla

Ku 'abstain' Veto kunatoa fursa ya nchi za Ulaya kuingia kama msuluhishi wa mzozo
Msimmo wa EU ni two solution state zikikataa upauzi wa Israel usitishwe

Yote yanazidi kuweka sera za Trump za mambo ya nje katika majaribu makubwa

Mzozo wa mashariki ya kati ni 'complicated' una define sera nyingi na hasa ulinzi na usalama wa US

Tusemezane
 
TRUMP: ALIYOPINGA SASA ANAYATEKELEZA

Katika uzi wa chaguzi za awali US 'Primaries and caucus' tulieleza kuhusu mtifuano ndani ya Democrat na jinsi utavyowagharimu siku za baadaye. Ndilo lililotokea, tutafafanua

Kwa upande wa Republican, wagombea walijikita katika sera za Republican

Mgombea mmoja, Trump, alikuwa tofauti sana hadi kuitwa si 'Republican'

Kuna nyakati alisimamia sera zilizoonekana kuwa za Democrat

Trump aliweza kusoma saikiloji ya Wananchi, aktumia mbinu za pande zote kushinda

Hoja ya kurudisha uchumi katika 'rust belt' ilikuwa ya Ben Sanders akimtuhumu Clinton kwa mikataba ya TPP. Sanders alimshinda Clinton Michigan kinyume na matarajio

Hoja hiyo akaibeba Trump kama ilivyo na kutumia dhidi ya Clinton.

Trump kama Sanders akshinda ukanda huo

Hoja ya Wall street ilikuwa ya Sanders akimbana Clinton atoe scripts na emails

Hii ilionekana mwiba kwa Hillary na Wikileaks wakaona fursa wakati wa hacking
Trump akaitumia kusema Hillary ni crooked na amezungukwa na wall street

Hoja ya Clinton foundation ni ya Ben Sanders, akatuhumu foundation ya Clinton
Kama nyingine ilionekana mwiba kwa Hillary.
Trump akaichukua na kusema Hillary alitumia ofisi ya umma kwa foundation binafsi

Hoja ya Obamacare ilikuwa ya Sanders aliyesema ina mapungufu na kuongeza premiums
Trump akaichukua kama ilivyo na kuihusisha na Hillary Clinton healthcare plan

Hivyo Trump akawatumia Democrat kupata independents na Democrat akiwa na kundi la GOP lenye mrengo wake na GOP wasiopenda Dem kwa lolote

Hakuwa na sera bali alicheza na saikolojia kwa umakini sana. Kwa mfano, alitia hofu sana kuhusu usalama na ISIS akisema imesambaa nchi 28.

Hakueleza atamaliza vipi ISIS katika nchi hizo isipokuwa kujaza watu hofu

Kadri siku zinavosonga hoja zile zile alizosimamia sasa anaanza kuzikana
Hii maana yake ni kuwa alisimamia hoja kwa uchaguzi lakini si kwa dhati au uhalisia

Tazama Trump alivyobadilika kwa hoja tulizoorodhoshea bandiko linalofuata
 
TRUMP: ALIYOPINGA SASA ANAYATEKELEZA II

1. Trump akiwa S.Carolina na mtifuano na Ted Cruz mwezi Feb, alisema 'anawajua Goldman Sachs' wana control na Ted kama walivyo nayo kwa Hillary

Baada ya ushindi: Amenteua president wa Goldman Sachs kuongoza sera za uchumi
Bannon alikuwa insider wa Wall street na sec of Treasury Munchin ni Goldmans sachs

Hoja ya Wall street kuwa na control kwa wenzake ipo wapi ikiwa yeye amewaalika?

2. Clinton foundation: Alisema imetumika katika masilahi binafsi ndani ya ofisi ya umma

Trump foundation, ametangaza kufunga ingawa AG wa NY anasema ni hadi uchunguzi ukamilike. Muhimu hapa ni jinsi atakavyotenga makampuni yake na Urais wake

3. News: Trump alimshutum Clinton kwa kutokuwa na mikutano na wana habari akiwa

Baada ya ushindi:
Trump hajaongea na waandishi wa habari kwa siku zaidi ya 140 tangu July 27

4. Uchunguzi dhidi ya Clinton
Trump alisema atatafuta private investigator kuchunguza emails za Clinton

Baada ya ushindi:
Hana mpango wa kuendelea na uchunguzi na hakubaliani na uchunguzi wa 'hacking'

5. Wall street
Trump alisema Hillary amezungukwa na special interest watakaomnunua

Baada ya ushindi: Baraza lake tarajiwa lina donors wakubwa 6 kuliko record za karibuni

Trump anasema ni katika kuhakikisha wall street wana negotiate na wananchi!

6. Obamacare: Alisema ataifuta mchana wa siku ya kwanza WH

Baada ya ushindi:
Ata replace Obamacare na kuacha pre existing conditions.

7. Alizungumzia legitimacy ya Obama Rais kukiwa na mashaka na Urais miaka 5
Cheti cha Obama cha kuzaliwa kilitolewa. Alisema ni haki kuhoji

Baada ya ushindi:
Trump ansema wanaohoji hacking za DNC wana lengo la ku 'deligitimize' Urais
Amesahau ndilo amelifanya kwa miaka 5 akidai ni haki yake

8. Trump alisema atajenga ukuta kuzuia wahamiaji na gharama watalipa Mexico

Baada ya ushindi
Ataanza na kurudisha wahalifu na kujenga sehemu ya ukuta wa kusini
Atapeleka mswada wa comprehensive immigration reform

9: Trump alisema atahamisha ubalozi wa US kutoka Tel Aviv na kupeleka Jerusalem

Baada ya ushindi:
Kateua balozi mwenye nia hiyo, ingawa Trump anasema lengo ni 'two state solution'

10. Trump anasema kuzuia umiliki wa silaha ni kukiuka second ammendement

Baada ya uchaguzi
Wote watakaobainika wanachoma bendera moto watanyang'anywa Urais.

Hilo ni kukiuka uhuru wa kujieleza ulioelezwa katika katiba

Tusemezane
 
SAKATA LA HACKING

Obama na Putin
Asiyekubali ni Trump peke yake


Sakata la ''hacking'' linaloihusu US na tuhuma kwa Russia limeendelea kuchukua sura

Wiki hii intelligence community (IC) ilikutana na kamati za bunge
Hii ilikuwa katika kuwaeleza kwa kina nini hasa kimetokea

Obama Adm imechukua hatua za kuwaondoa wanadiplomasia wa Russia wanaotuhumiwa

Katika hali isiyo ya kawaida, Mabunge yanamuunga mkono Obama
Yamefikia kusema hatua anazochukua hazitoshi, zinahitajika kali zaidi

Spika Ryan na Senate Majority McNell wameeleza uhusika wa Russia

Rais Mteule Trump ndiye amebaki peke yake asiyekubali hilo na hata kutofautiana na vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo ni muhimu kwake katika maamuzi ya nchi

Trump atakutana na IC wiki hii kupata briefing ya nini kimetokea

Russia ilitarajiwa kujibu mapigo lakini Putin akasema hakuna hatua za kidiplomasia

Trump anajikuta katika wakati mgumu

Kwanza, hakubaliana na Intelligence zake, na pili haungwi mkono na senate au House

Tayari wapo wanaohoji kuhusu interest za Makampuni yake na Russia ikizingatiwa Sec of state ana uhusiano wa karibu na Putin

Atakapoingia oval office tarehe 20 Trump atakuwa na mambo mawili

Kwanza, kukubaliana na IC , Seanate na house kulinda masilahi ya US
Au
Kuegemea Russia na kutengeneza 'political damage' siku za kwanza

Tusemezane
 
PUTIN AKATAA KUJIBU MAPIGO

Trump asema 'ni smart'

Kinyume na matamko ya viongozi wa serikali na wana diplomasia, Rais Putin wa Russia amesema hatafukuza Wanadiplomasia wa US

Amewakaribisha watoto wa wanadiplomasia katika mkesha wa mwaka mpya Kremlin

Hili limeshangaza waliodhani Putin atajibu mapigo kwa kufukuza wanadiplomasia wa US

Putin ameelewa hatua za US zilikuwa za awali tu na huenda angejibu zingefuata nyingine

Putin ana habari za NSA kupitia Snowden aliye na info za kutosha ku embarass US

Kilichomzuia Putin ni baada ya FBI kutoa ushahidi zaidi wa kuhusika kwa Russia

Kwa upande mwingine maseneta wa Republican wamekuja juu kuhusu suala hilo

Putin anafahamu Spika na kiongozi wa Seneti(Republican) wanapokubaliana na Intelligence community kuna ushahidi mzito juu ya maelezo yatolewayo

Putin anatambua ushahidi huo ukitolewa utaweka Urais wa Trump katika wakati mgumu

1. Kwamba, ameingia Oval office kwa msaada kutoka Kremlin. Hili linaloudhi Wamarekani

2. Trump kujibu mapigo kutaongeza ufa kati ya Trump na Republican kama ilivyo

3. Kutakosekana maelewano kati ya Trump na intelligence community zake

4. Putin anahisi mataifa ya NATO yakaendelea kumtenga zaidi kwa ushawishi wa US

4.Putin anachelea huenda ''data'' za uhusiano wake na makampuni ya Trump au sec of state mtarajiwa yatakuwa wazi na kumsumbua Trump katika uongozi

Ni kwa namna hiyo, njia nzuri ya kuepuka 'diplomatic row' ni kuacha kuchukua hatua

Ndiyo maana Trump aliyesema jana 'it's time to move on' leo ame tweet akisema 'anafahamu Putin ni mtu smart'

Haya yanamaanisha ni smart kwasababu mzozo ni tatizo kwa Trump

Washauri wa Trump wanakaririwa wakisema uchunguzi lazima ufanywe na chombo kingine kitakachoteuliwa na Trump siyo IC ambayo imeingiliwa kisiasa

Swali wasilojibu ni kuwa , je, Trump ataendelea kupata daily briefing kutoa IC asizoamini?

Na kwamba kwanini atengeneze chombo cha uchunguzi akiwa yeye ni 'mtuhumiwa' ?

Na je, taarifa ya Comey aliyosifu ina tofauti gani na hii inayozungumzia Russia?

Tusemezane
 
Just hold on President Elect Trump, you have 19 days to go.

The people are getting really exhausted by nasty decisions from a failed and worst US Pres. ever in history.

19 days to stop hearing from those leaders still whining on election results

19 days to start forgeting about an incumbent Pres. who think he knows what everybody else is thinking and think he could still win a third term against a Pres. Elect he jointly campaigned so hard against.

19 days for US to start making progress again

19 days for the real change and real hope not the fake change and hope that Pres. Obama ran on.

19 days for the whole world to learn how to put aside politics on every way of progress.

19 days for US leaders to quit pulling 'Russian card' everytime things are not moving in their favor. That is pure weakness.

19 days for US and Russia to start working together and trading again. Potential US-Russia relationship is being attacked by a few group of people and the good thing is that PEOTUS knows it.
 
'HACKING'

Ushahidi umetolewa na IC kuhusu hacking ya Russia. Hoja inayoungwa mkono na pande zote

Hoja kubwa si hacking au kubadilisha matokeo, ni kitendo cha Russia kuingilia uchaguzi

Trump amesema anazo taarifa kuhusu hacking ambazo watu wengine hawanazo
Atazitoa kati ya Jumanne na Jumatano

Wakati huo huo atakuwa na mkutano na wakuu wa IC kupata undani wa sakata

Utetezi wa Trump ni kuwa huko nyuma IC ilikosea kama ilivyokuwa kwa Iraq

Utetezi huu bado haulezi kama wamekosea sasa hivi ni wapi na eneo gani?

Kauli ya Trump kuwa ana habari nje ya zile za vyombo vya ulinzi na usalama ni tata saa

Kwasasa wengi wanasubiri kuona upande wa pili kutoka kwa Trump, na hili linaweza kumsumbua

Taarifa atakazotoa zitamsumbua kwa njia kadhaa

1. Kwanza athibitishe vyanzo na ushahidi wa kile atakachokuwa amepokea nje ya IC
2. Utakuwa ni mwanzo wa kutoaminiana na vyombo vya ulinzi na usalama
3. Kama hatakuwa na ushahidi mkubwa kuliko wa IC Trump itazidi kuondoa shaka kidogo iliyobaki

Kwa vile mada ni moto, Trump kwa mbinu zake ameamua kubadili mwelekeo wa mazungumzo

Kim Il Un wa Korea alisema katika mkesha wa mwaka mpya kuwa Korea ipo karibu kufanya ICBM
(Intercontinental ballistic missile)

Siku mbili baadaye Trump kajibu kwa Tweet 'It won't happen' Kwamba haitatokea

Hili ni kubadili mazungumzo ya hacking ambapo tayari anapata joto

Tweet yake haielezi atachukua hatua gani kwa sababu ina maneno matatu' na hivyo kuacha vyombo vya habari vikifanya speculations. Kwa uhakika tweet ililenga kubadili mazungumzo

Nini kitajiri wiki hii tutawahabarisha

Tusemazane
 
'HACKING'
Ushahidi umetolewa na IC kuhusu hacking ya Russia. Hoja kubwa si hacking au kubadilisha matokeo, ni kitendo cha Russia kuingilia uchaguzi

Huu ndio ushahidi unaouzungumzia?

1*T3Mpw-H1Wy0F621remdJAw.png


1*zb9geL4kG52nBTnHjEfi7w.png


Je USIC wametoa ushahidi wa kuhusisha Russia au serikali ya Russia mojamoja?

Kilichotolewa mpaka sasa ni ushahidi wa kudhaniwa tu na hii inatuonesha kuwa US hawana ushahidi wa kuhusisha Russia kwenye hiyo hacking iliyotokea kwa DNC au John Podesta.

Then USIC wanakuja wanatoa untraceable Tor IP addresses 876, hivi huo ni ushahidi ambao ni beyond reasonable doubt? IP addresses ambazo zinaweza kuwa 'spoofed' ndio ushahidi?.

Utetezi wa Trump ni kuwa huko nyuma IC ilikosea kama ilivyokuwa kwa Iraq.

Kwani ni uongo? Au kisa amesema Trump?

Utetezi huu bado haulezi kama wamekosea sasa hivi ni wapi na eneo gani?

Sir, unasubiri mpaka Trump akutafunie na hilo?

Hivi unafahamu kuna taarifa kwamba hiyo malware iliyotumika na huyo aliyewa-hack DNC na John Podesta unaweza kui-download hata wewe hapo ulipo tena bure na kuitumia?.

Ina maana kuwa mtu yeyote anaweza kui-download hiyo malware na kuitumia kutoka katika nchi yoyote duniani.

Kauli ya Trump kuwa ana habari nje ya zile za vyombo vya ulinzi na usalama ni tata sana
Kama watu wa nje ya USIC waliweza kupatia huku USIC wakikosea huko nyuma, hiyo inatakiwa ikufanye ufikiri kuwa sio kila wanachokisema ni cha ukweli hasa katika mazingira kama haya ambapo kabla ya Presidential debates walisema kitu hicho hicho then serikali ika-ignore.

Taarifa atakazotoa zitamsumbua kwa njia kadhaa

1. Kwanza athibitishe vyanzo na ushahidi wa kile atakachokuwa amepokea nje ya IC

Hapa ni kuzungumza Facts tu maana USIC leaders walioteuliwa na Rais Obama wanafikiri huo mtego ni mgumu kwa Trump ambaye anasifika na kuaminika kwa kuzungumza ukweli. Ndio maana aliwataka USIC kuwa na uhakika na wanachozungumza kwa sababu mpaka sasa hivi hamna cha maana walichoonyesha.

2. Utakuwa ni mwanzo wa kutoaminiana na vyombo vya ulinzi na usalama

Wala hata sio mwanzo wa kutoaminiana na vyombo vya ulinzi na usalama bali ni muendelezo.

Naamini hata Hillary Clinton haamini sana USIC kwa sababu walimfanya akapiga kura kuunga mkono vita ya Iraq, kura iliyom-cost kwenye uchaguzi miaka 16 baadae.

They have to be sure.

Trump ameshaona haja ya kufanya mabadiliko kwenye nafasi za juu kwenye US Intel. Agencies, alianza na CIA na naamini atabadilisha wengi.

3. Kama hatakuwa na ushahidi mkubwa kuliko wa IC Trump itazidi kuondoa shaka kidogo iliyobaki

Kwani USIC wametoa ushahidi usio na shaka? Hebu tuambie namna ushahidi walioutoa ulivyo wa uhakika.

Kwa vile mada ni moto, Trump kwa mbinu zake ameamua kubadili mwelekeo wa mazungumzo. Kim Il Un wa Korea alisema katika mkesha wa mwaka mpya kuwa Korea ipo karibu kufanya ICBM (Intercontinental ballistic missile). Siku mbili baadaye Trump kajibu kwa Tweet 'It won't happen' Kwamba haitatokea. Hili ni kubadili mazungumzo ya hacking ambapo tayari anapata joto

Mbona Trump anatweet karibu kila siku na mda mwingine mara nyingi kwa siku na kila akitweet anaamsha mazungumzo. Trump anapenda kutoa reaction yake kwenye Twitter kutokana na habari ambazo zinatengeneza headlines. Katika hiyo Tweet ni wazi alikuwa anampa taarifa Kim wa N. Korea.

Sasa utasema alivyo-tweet kuhusu China kufaidika zaidi ya US kwenye biashara baina ya nchi hizo mbili ni juhudi zake za kubadili mazungumzo? Angekuwa na nia ya kubadili mazungumzo angetuma tweets nne (4) baada ya hiyo ya North Korea chini ya masaa 13?

Tweet yake haielezi atachukua hatua gani kwa sababu ina maneno matatu' na hivyo kuacha vyombo vya habari vikifanya speculations. Kwa uhakika tweet ililenga kubadili mazungumzo
Vyombo vya habari kufanya speculations ni kitu cha kawaida, hawajaanza kufanya leo. Hata kipindi hiki cha Rais Obama wamefanya sana.

Kuhusu kuelezea hatua akakazochukua, Trump alishasema anaamini China inaweza kusaidia ku-deal na tatizo la North Korea na hakuwa na ulazima wa kutangaza hatua specifically akazochukua jana, au leo au hata kesho.

Nini kitajiri wiki hii tutawahabarisha
Ni kweli utatuhabarisha, maana unachukua huko kwenye liberal sources bila kuzichuja na kutuletea huku.

Hivi huoni kuwa hizi drama zitaisha within the next two weeks?
 
Back
Top Bottom