Tetesi: Edward Lowassa na Frederick Sumaye mbioni kurejea CCM

Tetesi: Edward Lowassa na Frederick Sumaye mbioni kurejea CCM

Hao jamaa wakirudi tu CCM, kama watapokewa basi hata CCM itakuwa imezidi kujishusha hadhi, na pia Mbowe ndio atakua amefungashiwa virago rasmi chadema.
 
Sisiemu ya JK sikuipenda sababu ya watu kama lowassa na niliaminishwa sana ma watu wa ndani na nje ya sisiemu kuwa ni fisadi, chadema ikiwa mstari wa mbele!
Kwa kweli kukinusuru chama, wasimpokee yeye wala sumaye.
Uliaminishwa na CHADEMA kwamba Lowassa ni fisadi, ukaamini? Lakini huamini kama Magufuli, Mkapa, Kikwete, Chenge, Ngeleja, Muhongo na Tibaijuka ni mafisadi! Lowassa na hilo kundi la pili wote wametajwa na CHADEMA. Lakini zombie wewe umeamua kuamini Lowassa ni fisadi kwa kuwa hayupo tena CCM, huku hauamini hilo kundi la pili kuwa ni mafisadi kwa kuwa yapo CCM.
 
Tatizo kubwa la hawa wawili ni makabila yao.
Kwenye makabila hayo unafiki ni laana mbaya saana na aghalabu kumpata mtu mzima muwongo,pia husimamia wanachokiamini.Daima kwao nyeupe ni nyeupe tu.
 
Kuna jamaa mpaka leo huwa ananiambia kuwa yeye anaamini Lowassa alipelekwa CHADEMA kama mamluki kusaidia kukiua kwa ndani... Kama ni kweli kwani hiyo kazi ishatimia mpk arudi?
Si kweli kuwa lowasa alitumwa chadema, alikwenda kwa uamuzi wake mwenyewe. Lakini marando aliwahi kusema kuwa jamaa wa tiss wanaweza kukutumia bila wewe kutambua kuwa unawatumikia.
 
Si kweli kuwa lowasa alitumwa chadema, alikwenda kwa uamuzi wake mwenyewe. Lakini marando aliwahi kusema kuwa jamaa wa tiss wanaweza kukutumia bila wewe kutambua kuwa unawatumikia.
yawezekana..
 
Hao jamaa wakirudi tu CCM, kama watapokewa basi hata CCM itakuwa imezidi kujishusha hadhi, na pia Mbowe ndio atakua amefungashiwa virago rasmi chadema.
CCM itakuwa haija shuka hadhi Chadema ndio itakuwa imeshuka kihadhi na kimapato sababu hao na rafiki zao ndio walikuwa wachangiaji wakubwa na ndio waliwezesha Chadema kupata madiwani wengi na Wabunge .
 
Wameshamaliza kazi waliyotumwa kuifanya. Itakuwa safi sana. Na akirudi CCM tu CHADEMA watamrudisha tena kwenye orodha ya mafisadi. Shauri yake [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Siasa za Bongo yaani raha sana !!!
Hahahahaa!
Watamrudisha tena kwenye orodha ya mafisafi,
Ni hakika watazunguka nchi nzima na kusema huyo ni fisadi papa.
 
Uliaminishwa na CHADEMA kwamba Lowassa ni fisadi, ukaamini? Lakini huamini kama Magufuli, Mkapa, Kikwete, Chenge, Ngeleja, Muhongo na Tibaijuka ni mafisadi! Lowassa na hilo kundi la pili wote wametajwa na CHADEMA. Lakini zombie wewe umeamua kuamini Lowassa ni fisadi kwa kuwa hayupo tena CCM, huku hauamini hilo kundi la pili kuwa ni mafisadi kwa kuwa yapo CCM.
Licha ya kuaminishwa, kuna kitu unasahau, COMMON SENSE!
Utendaji kazi pia wa JPM nimeuona kwa miaka kama 10 hivi, UMETUKUKA.
Tafuta nyuzi za zamani humu jf kabla lowassa hajahamia chadema akiwa sisiemu UNIELEWE nilivyokuwa nampinga, sijawahi mkubali lowassa! Hata Salary Slip na MUSSA ALLAN toka wakiwa na mzee wao akiwa sisiemu na wao wakimpigia debe na sisiemu niliwapinga!
Sio mnafiki kama nyie.
 
Kuna jamaa mpaka leo huwa ananiambia kuwa yeye anaamini Lowassa alipelekwa CHADEMA kama mamluki kusaidia kukiua kwa ndani... Kama ni kweli kwani hiyo kazi ishatimia mpk arudi?
Yo yo yo Chadema walikuwa na matumaini hewa kuwa mgombea uraisi wao hewa Lowasa atashinda na akishindwa atakataa matokeo na atakiinukisha na kuitumbukiza nchi kwenye vita.Wafadhili koko wa Ndani na nje waliamini hivyo kuwa Lowasa na seif Sharif Hamad wakishindwa lazima wakatae matokeo na kuitumbukiza nchi vitani ya wewnyewe kwa wenyewe.Lowasa na seif sharif Hamad wakapiga chenga ya mwili ukawa na wafadhili koko wao wa nje ya nchi hadi Leo hawaamini kilichotokea Tanzania bara na Zanzibar na hawana hamu na CCM wanajua chama CCM ni chama dume kisichosomeka.!!!!!! Lowasa na seif Sharif Hamad wakirudi CCM poa tu .Mission accomplished
 
Lowasa, Sumaye, Kingunge n.k. wakirejea CCM kutokea CHADEMA sitashangaa kusikia kauli kutoka kwa Mwenyekiti wetu kwamba "acha waende kwakuwa hawakuwa na msaada wowote" na kwamba "sisi tulishasema siku nyingi kwamba ni mafisadi".

Siasa za Tanzania ni sawa na biashara nyingine inayoingiza kipato (ruzuku) hasa pale inapoendeshwa na mfanyabiashara mzoefu dizaini ya Mbowe. Haitakiwi jazba kwenye eneo la biashara. Wanaopandwa jazba ni washabiki na waandamanaji wasioijua biashara yenyewe.
Hongera mkuu kwa kuongea ukweli tupu.
 
Back
Top Bottom