TANZIA Edward Lowassa (Waziri Mkuu Mstaafu na Mgombea Urais wa CHADEMA 2015) afariki dunia

Mwenyezi Mungu ampe pumziko la Amani. Huwezi kuandika simulizi la siasa za Tanzania na changamoto za utawala wake bila kuweka mchango na nafasi ya Lowassa katika chama tawala na katika upinzani. Nawaombea faraja familia, ndugu na Jamaal kufuatia msiba huu. Raha ya milele umpe Ee Bwana na Mwanga wa milele umuangazie apumzike kwa Amani, Amina.
 
So sad,mwenyezi Mungu ampe pumziko la amani,ni njia ya wanadamu wote.Nichukue nafsi hii binafsi kuipa pole familia ya mh Lowasa,ndugu jamaa na marafiki.
 
Kwani komredi alikuwa bado Chadema hadi kufariki kwake?

Mie Nijuavyo alirudi nyumbani baada ya nyumbani kunoga, so viongozi wa CDM huu msiba hauwahusu.
Tupo kwenye maridhiano huu msiba unawahusu sana chadema hasa ikizingatiwa marehemu aliwahi kusajiliwa kwa mkopo mwaka 2015 kabla kurejea lumumba FC .
 
Waziri Mkuu Mjiuzuru?
Unat
Huyo waziri mkuu hakustaafu, Bali alijiuzulu kwa kashfa, Sasa bendera inapepea nusu mlingoti kwa kipi? Au ni kisiasa zaidi?
Ndio maana siku zote napingana na wanaCHADEMA Kwa sababu hawatumii akili kwenye hoja zao na hii comment ni mfano tosha wa akili za CHADEMA.

Nakupa ufafanuzi hapa ili utambue Kwa nini tunasema aliyestaafu na sio aliyejiuzulu na kama utaendelea kuwa mbishi wa kutokuelewa nitakushangaa.

Kwanza, katiba haijatoa muda wa kikatiba wa mtu aliyechaguliwa kama Waziri mkuu tofauti na Urais hivyo kipindi cha muda wowote atakaohudumu Waziri mkuu atakuwa kastaafu. Je, Waziri mkuu anatakiwa kustaafu baada ya muda gani?

Pili, Kuna mstari mwembamba sana unaotafautisha kujiuzulu na kustaafu na kujiuzulu Kwa lugha nyepesi ni kustaafu mapema. Tuachane na sababu iliyofanya Lowassa kujiuzulu tuje kwenye kujenga picha kubwa zaidi hivi Lowassa angeomba kujiuzulu Kwa sababu ya ugonjwa kutokana na umri mkubwa ,je Bado ungesema aliyejiuzulu au aliyestaafu?

Tatu, kitafsiri kustaafu ni neno linalotumika kuashiria ukomo wa mtu kwenye nafasi yake na Lowassa alikoma kwenye nafasi hiyo ndani ya kipindi na Kwa kuwa katiba haikueleza Waziri mkuu anatakiwa kukaa muda gani kisheria basi inatosha kusema alistaafu.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe. Apumzike Kwa Aman
 
Aamin mzee mwanakijiji .
 
Yeah! Inafikirisha sana....huenda hili lisingeepukika.

Anyway yote ni maisha tu.
 
Ila inasemekana ni tajiri sana ni bilionea sasa kapata wapi mali yote hiyo na kazi yake alikua mtumishi wa umma? Alikua anafanya biashara gani huko serikalini?
Huyo katoka kwenye familia ya kitajiri tangu akiwa mtoto na biashara amefanya sana tu, si aina ya watu ambao walihitaji kujitafuta sana ili watoboe kama ilivyo kwa makupuku wengi hapa Tz.

Ni kama ilivyo kwa Mbowe tu.

Mtu wa pekee ambaye utakuwa sahihi kushangaa utitiri wa mali alizojilimbikizia ni JK kwasababu hata historia ya familia yake inakataa.
 
Mungu akulaze mahala pema peponi Mzee wangu Edward Ngoyayi Lowassa, Byee byee Baba Lowassa.

Mwaka 2015 nilikuwa supporter wako mkubwa sana, hakika nilikufuata toka CCM na kukupigia kampeni mitandaoni na majukwaani upate kura kwani niliamini ulikosa haki yako CCM wakati ule, ingawa wengi tulikuwa CCM ila ulipata kura zetu 2015, CCM wengi tuliumia sana, yote sasa ni historia, nilikupenda kama mwanasiasa shupavu katika CCM na nje ya CCM, busara zako zilikuwa za hali ya juu sana, ni mwanasiasa uliyejua kudhibiti sana ulimi wako, umeondoka Lowassa ila moyoni mwangu uko hai daima sitakusahau asilani, ulijaa wema sana na mchapakazi wa kweli.

Mungu akulinde daima na milele yote, Amen


View: https://youtu.be/8nibWz0XLlw?si=bx_vXZzJwZDEUXZl


View: https://youtu.be/RgKAFK5djSk?si=MCxe6lhOMuM56eM5
 
R.I.P Umepigania sana uhai wako lakini hamna namna nyakati zimekwenda na ashukuriwe aliye juu Kwa zawadi ya maisha.
 
Pole sana kwa mkewe kipindi chote hicho cha kupumua kwa mashine hakukata tamaa, Joseph haule alirejea EL yeye imeshindikana kazi yake Mola
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…