Edwin Mtei aliposikitishwa na Tundu Lissu kumtusi Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere

Edwin Mtei aliposikitishwa na Tundu Lissu kumtusi Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere

Nyerere kafanya mazuri mengi, na ana makosa mengi tu.

Na alilalamika watu wanaangalia makosa yake, wanaacha kuangalia mazuri.

Hapo napingana naye, watu wanatakiwa waaangalie makosa ya viongozi. Bila kuangalia makosa ya viongozi hawawezi kuyarekebisha.

Mazuri hayahitaji kurekebishwa sana, hivyo hayatakiwi kupewa kipaumbele katika kuangaliwa.

Nyerere ninamuheshimu kwa mengi mazuri aliyofanya.

Lakini, nikisikia kuna mwanasiasa anamkosoa Nyerere, nashukuru kwamba kuna mtu ana uthubutu wa kumkosoa Nyerere.

Mtei hakueleza Tundu Lisssu alisema nini.

Sitaunga mkono kumtusi Nyerere. Nyerere alikuwa ni kati ya viongozi waliojiheshimu na kuheshimu watu sana, sana tu. Angeweza kuwa dikteta mkubwa lakini hakuamua kufanya hivyo.

Ukitaka kuelewa umuhimu wa Nyerere, na alivyojiheshimu, linganisha kauki za Nyerere na za Magufuli halafu uone tofauti. Kama rais Mwinyi alisema yeye ni kichuguu na Mwalimu Nyerere ni mlima Kilimanjaro, basi Magufuli ni punje moja ya mchanga!

Lakini, Nyerere katika siasa, alifanya makosa mengi tu. Hata yeye mwenyewe alikubali hilo.

Sasa kama Nyerere mwenyewe alikubali kwamba alifanya makosa (mfano alikubali utaifushaji wa mashamba makubwa ulikuwa na mapungufu makubwa, serikali iliyachukuwa bika ya kuwa na uwezo wa kuyaendesha).

Mtu kama huyo ambaye mwenyewe kakubali makosa, kwa nini wengine wasimseme makosa yake?
Ok.. Nyerere ana makosa lakini si kwa ukali na lugha ile aliyotumia Lisu katika kumkosoa!

Yani kwa akili ya Lisu, alimuweka Nyerere kwenye kapu moja na kina Msukuma,

Kwangu mimi Lisu ni msomi anaetumia usomi wake kudanganya wapumbavu.
 
Mtu yeyote anayemlaumu Nyerere kwa kuchakachua kura Znz au baadhi ya maamuzi yake aseme hapa angekua yeye angefanyaje.

Znz imekua ally kwa ajili ya usalama. Tungekua na usalama huo huo kama ingekua inaongozwa na mtu wa cham tofauti na chake? Wewe ungekua ndiyo kiongozi ungefanyaje?

Nataka mjue kua chochote ambacho aliamua huo uamuzi ulikua ni best option kati ya options zote zilizopo. Vijiji vya ujamaa, vita n.k hizo zote zilikua ni best options kuliko zote zilizokuepo.
 
Nyerere kafanya mazuri mengi, na ana makosa mengi tu.

Na alilalamika watu wanaangalia makosa yake, wanaacha kuangalia mazuri.

Hapo napingana naye, watu wanatakiwa waaangalie makosa ya viongozi. Bila kuangalia makosa ya viongozi hawawezi kuyarekebisha.

Mazuri hayahitaji kurekebishwa sana, hivyo hayatakiwi kupewa kipaumbele katika kuangaliwa.

Nyerere ninamuheshimu kwa mengi mazuri aliyofanya.

Lakini, nikisikia kuna mwanasiasa anamkosoa Nyerere, nashukuru kwamba kuna mtu ana uthubutu wa kumkosoa Nyerere.

Mtei hakueleza Tundu Lisssu alisema nini.

Sitaunga mkono kumtusi Nyerere. Nyerere alikuwa ni kati ya viongozi waliojiheshimu na kuheshimu watu sana, sana tu. Angeweza kuwa dikteta mkubwa lakini hakuamua kufanya hivyo.

Ukitaka kuelewa umuhimu wa Nyerere, na alivyojiheshimu, linganisha kauki za Nyerere na za Magufuli halafu uone tofauti. Kama rais Mwinyi alisema yeye ni kichuguu na Mwalimu Nyerere ni mlima Kilimanjaro, basi Magufuli ni punje moja ya mchanga!

Lakini, Nyerere katika siasa, alifanya makosa mengi tu. Hata yeye mwenyewe alikubali hilo.

Sasa kama Nyerere mwenyewe alikubali kwamba alifanya makosa (mfano alikubali utaifushaji wa mashamba makubwa ulikuwa na mapungufu makubwa, serikali iliyachukuwa bika ya kuwa na uwezo wa kuyaendesha).

Mtu kama huyo ambaye mwenyewe kakubali makosa, kwa nini wengine wasimseme makosa yake?
Kukosoa na kutukana vitu viwili tofauti kabisa mkuu.
 
Nyerere alibariki matokeo ya uchaguzi Zanzibar kuchakachuliwa mwaka 1985.

Idris Abdul Wakil alishindwa kupata kura za kutosha, akiwa mgombea pekee.

Matokeo ya kweli yalifika mpaka Daily News, yakionesha Wakil kashindwa.

Nyerere akaamuru serikali itoe matokeo tofauti yanayoonesha Wakil kashinda.

Tangu wakati huo CCM imekuwa ikiiba kura Zanzibar.

Kwa huo mfano mmoja tu, Nyerere alifanya udanganyifu.

Sipo upande wa Nyerere wala wa Tundu Lissu, wote wana mapungufu.

Nipo katika kutafuta ukweli.
[emoji2315]
giphy.gif
 
Kukosoa na kutukana vitu viwili tofauti kabisa mkuu.
OK. Sawa.

Kukosoa kunaishia wapi na kutukana kunaanzia wapi?

Tundu Lissu katoa maneno gani ambayo ni ya kutukana, na si ya kukosoa.

Mimi sikumbuki vizuri maneno halisi.

Tuyachambue maneno halisi. Tukiongozwa na fact.

Kwa mfano. Mtu akisema "Nyerere hayawani" kwangu hii si fact. Ni kashfa.

Ila mtu akisema "Nyerere muuaji, alimrubuni Kassim Hanga arudi kutoka Guinea, kisha akamrubuni Kassim Hanga aende Zanzibar huku akijua kule Hanga anaenda kuuawa na Karume", hapo kuna a factual basis ya kumuita Nyerere muuaji.

Sasa maneno halisi aliyosema Tundu Lissu, ukiacha habari za watu wengine za uchambuzi wa maneno aliyosema Tundu Lissu, ni yapi?

Tuyachambue maneno aliyosema Tundu Lissu, tuangalie kama yana fact au hayana fact au ni kashfa au ni matusi.
 
Ok.. Nyerere ana makosa lakini si kwa ukali na lugha ile aliyotumia Lisu katika kumkosoa!

Yani kwa akili ya Lisu, alimuweka Nyerere kwenye kapu moja na kina Msukuma,

Kwangu mimi Lisu ni msomi anaetumia usomi wake kudanganya wapumbavu.
Wanasiasa karibu wote wanatumia exaggeration katika sanaa yao.

Hiki ni kitu cha kuwa makini nacho sana.

Hata wewe.

Kwa nini unasema Tundu Lissu alimuweka Nyerere kundi moja na Msukuma? Alisema Nyerere ni sawa na Msukuma?
 
OK. Sawa.

Kukosoa kunaishia wapi na kutukana kunaanzia wapi?

Tundu Lissu katoa maneno gani ambayo ni ya kutukana, na si ya kukosoa.

Mimi sikumbuki vizuri maneno halisi.

Tuyachambue maneno halisi. Tukiongozwa na fact.

Kwa mfano. Mtu akisema "Nyerere hayawani" kwangu hii si fact. Ni kashfa.

Ila mtu akisema "Nyerere muuaji, alimrubuni Kassim Hanga arudi kutoka Guinea, kisha akamrubuni Kassim Hanga aende Zanzibar huku akijua kule Hanga anaenda kuuawa na Karume", hapo kuna a factual basis ya kumuita Nyerere muuaji.

Sasa maneno halisi aliyosema Tundu Lissu, ukiacha habari za watu wengine za uchambuzi wa maneno aliyosema Tundu Lissu, ni yapi?

Tuyachambue maneno aliyosema Tundu Lissu, tuangalie kama yana fact au hayana fact au ni kashfa au ni matusi.
Mzee Mtei, mtu mzima mwenye heshima yake ilibidi ajitenge na maneno ya Lissu kama ifuatavyo.....


Tundu Lissu.. "yule Nyerere aliishi maisha ya ulaghai,udanganyifu na vitisho kama vile majambazi/matapeli Papaa Musofe na Alex Massawe!?"

Hayo ni maneno kayatamka Tundu Lissu, mpaka leo hakuomba radhi kuwa mdomo ulikuwa kwenye overspeed.
Leo naye ati anataka urais.
 
OK. Sawa.

Kukosoa kunaishia wapi na kutukana kunaanzia wapi?

Tundu Lissu katoa maneno gani ambayo ni ya kutukana, na si ya kukosoa.

Mimi sikumbuki vizuri maneno halisi.

Tuyachambue maneno halisi. Tukiongozwa na fact.

Kwa mfano. Mtu akisema "Nyerere hayawani" kwangu hii si fact. Ni kashfa.

Ila mtu akisema "Nyerere muuaji, alimrubuni Kassim Hanga arudi kutoka Guinea, kisha akamrubuni Kassim Hanga aende Zanzibar huku akijua kule Hanga anaenda kuuawa na Karume", hapo kuna a factual basis ya kumuita Nyerere muuaji.

Sasa maneno halisi aliyosema Tundu Lissu, ukiacha habari za watu wengine za uchambuzi wa maneno aliyosema Tundu Lissu, ni yapi?

Tuyachambue maneno aliyosema Tundu Lissu, tuangalie kama yana fact au hayana fact au ni kashfa au ni matusi.
Kwamba Karume alimwambia Nyerere ampeleke Hanga huko Znz? Au Nyerere alioda Karume amuue Hanga na yeye ndiye atakayemfikisha Hanga kwa Karume?
 
Wanasiasa karibu wote wanatumia exaggeration katika sanaa yao.

Hiki ni kitu cha kuwa makini nacho sana.

Hata wewe.

Kwa nini unasema Tundu Lissu alimuweka Nyerere kundi moja na Msukuma? Alisema Nyerere ni sawa na Msukuma?
Ungesikiliza kwanza hizo crip ndio ujue akili za Lisu zikoje
 
Mzee Mtei, mtu mzima mwenye heshima yake ilibidi ajitenge na maneno ya Lissu kama ifuatavyo.....


Tundu Lissu.. "yule Nyerere aliishi maisha ya ulaghai,udanganyifu na vitisho kama vile majambazi/matapeli Papaa Musofe na Alex Massawe!?"

Hayo ni maneno kayatamka Tundu Lissu, mpaka leo hakuomba radhi kuwa mdomo ulikuwa kwenye overspeed.
Leo naye ati anataka urais.
Nyerere hakudanganya na kuendeleza utawala wake kwa vitisho?

Twende na facts.
 
  • Thanks
Reactions: Pep
Kwamba Karume alimwambia Nyerere ampeleke Hanga huko Znz? Au Nyerere alioda Karume amuue Hanga na yeye ndiye atakayemfikisha Hanga kwa Karume?
Huo ni mfano wa kuonesha kwamba kikitu kikiwa fact,mtu kusema fact si kashfa.

Karume alimuomba Nyerere ampeleke Hanga Zanzibar, Nyerere akamrubuni Hanga atoke Guinea alipokuwa kajificha arudi Tanzania. Hanga alipofika Tanzania Nyerere akamrubuni Hanga aende Zanzibar. Akijua Hanga anaenda kuuawa na Karume huko.

Hanga akaenda Zanzibar, akauawa.
 
Nyerere hakudanganya na kuendeleza utawala wake kwa vitisho?

Twende na facts.
I challenge you ,huyo mtaalam wa matusi Tundu Lissu aseme hivyo tena kwa Magufuli leo.
Kama ataiona Tanzania itakuwa mjaaliwa.

Fact ni kwamba alimlinganisha Mwalimu na matapeli!
Hilo la kwamba Mwalimu aliendesha utwala wake kwa vitisho anzisha mada kuhusiana na hilo ambalo ni tofauti na mada hii.
 
Hilo bandiko lipo humu humu JF ana mzee mtei aliandika mwenye maana ni member humu
Tundu Lissu na rekodi yake ya kisiasa, ati sasa naye anautaka Urais.
...............

APR
17

EDWIN MTEI ASIKITISHWA NA ALAANI KITENDO CHA TUNDU LISSU KUMTUKANA BABA WA TAIFA, MWL. NYERERE

Nilimsikiliza Mheshimiwa Tundu Lissu na nasikitika kwamba sikubaliani naye jinsi alivyoeleza shutma juu na dhidi ya Mwalimu Julius Nyerere, Baba na Muasisi wa Taifa letu.

Inajulikana na umma wa Watanzania, kwamba mimi binafsi, kama Waziri wa Fedha, nilitofautiana na Mwalimu, nikajiuzulu Uwaziri Decemba,1979, nikimwomba ateuwe Mtanzania mwingine atakayeshauri mambo ya Uchumi na Fedha. Lakini tuliendelea kuwasiliana kwa maelewano bila chuki, na hata aliniteuwa niwe Mwakilishi wa Tanzania na Afrika inayoongea Kiingereza katika IMF (Shirika la Fedha Duniani) chini ya miaka mitatu baadaye Novemba, 1972.

Nimekuwa na mawasiliano na maelewano mazuri sana na Mwalimu hata baada ya kuasisi CHADEMA, Julai 1992 na tulipokamilisha Katiba na Sera za Chadema, nilimtembelea Nyumbani kwake Butiama nikampa azisome ajionee jinsi tulivyonuia kuwahudumia Wananchi wetu. Hata siku moja siwezi kumtusi Muasisi wa Taifa letu. Iwe ni mwiko pia kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo kumtusi Baba wa Taifa.

Ningewashauri uongozi wa Chadema na hasa Vijana wa M4C (Vuguvugu la Mabadiliko) tuendelee na uhamasishaji : kwa umakini, tukiwa na huruma kwa wanyonge maskini wa kutupwa, tukijiandaa kwa umakini na kiutaalamu Sera na Mikakati ya kuwakomboa toka katika umaskini wa kutupwa kwa kutumia nguvu ya umma (Peoples Power) tukitumia mikakati sahihi: kwani Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke:

Mikakati na Sera sahihi ikiwa ni kutumia misingi ya Uchumi na Miundombinu tulionayo licha ya uhalisia dhoofu tulioridhi; tukiwaenzi walioijenga na kuturidhisha kwa unyofu wao.

Roho ya Julius Nyerere ilale mahala pema Peponi. Amen!

With all due respect to Hon. Tindu Lissu, this smacks BAD TASTE.


Edwin Mtei,

Founder Chairman of CHADEMA.
 
Binafsi sijawahi kumwelewa kiviile mzee wetu Nyerere,Kuna maamuzi mengi ya kiboya aliyafanya na kuficha ukweli, hakuwa muwazi na alikuwa mbinafsi sana, aliona yeye ndo Yuko sahihi tu na watanzania wote no maboya. Ni Kama kagame anavyoiongoza Rwanda
Nyie madogo kuweni na heshima kidogo japo hata kwa Baba Wa taifa, hizo schoolboy politics zitawaletea shida,
 
I challenge you ,huyo mtaalam wa matusi Tundu Lissu aseme hivyo tena kwa Magufuli leo.
Kama ataiona Tanzania itakuwa mjaaliwa.

Fact ni kwamba alimlinganisha Mwalimu na matapeli!
Hilo la kwamba Mwalimu aliendesha utwala wake kwa vitisho anzisha mada kuhusiana na hilo ambalo ni tofauti na mada hii.
Nyerere katapeli watu ana degree ya pili , wakati ana degree ya kwanza.

Unaelewa hilo?
 
  • Thanks
Reactions: Pep
Back
Top Bottom