Enyi Manabii wa kizazi kipya ni kweli mmepewa nguvu na Mwenyezi Mungu, au ni ushirikina tu?

Enyi Manabii wa kizazi kipya ni kweli mmepewa nguvu na Mwenyezi Mungu, au ni ushirikina tu?

1. Logical consistency kwa maana ya kuwepo kwa mantiki isiyojikanganya wala kupingika kwa kuonekana ina uongo. Kwa mfano, tukijua kuwa square root ya 2 ni kazima iwe ndogo kuliko 2, ukioewa jibu lolote lililo kubwa kuliko 2 kama square root ya 2, jibu hilo litakosa logical consistency na kanuni hiyo ya kwamba square root ya 2 ni kazima iwe ndogo kuliko 2.

. Huwezi kupata maneno yasiyo jichanganya kutoka kwenye utafiti wa binadamu, labda uazishe Mwenyewe huo uthibitisho, hata Ukifanya uthibitisho wewe Mwenyewe karne hii, miaka ijayo binadamu watakao zaliwa, watapinga uthibitisho wako...
 
Nafuu wangetumia mababu zao katika kuomba labda ningeamini. Huyu Mungu wa Israeli na mwafrika haingii akilini.
 
Nafuu wangetumia mababu zao katika kuomba labda ningeamini. Huyu Mungu wa Israeli na mwafrika haingii akilini.
😄😄, Inafikirisha sana, lakini binadamu hatutaki kuelewa kabisa kuhusu hao wanaojiita manabii... Kila kukicha makinisa yao yanazidi kufurika
 
. Huwezi kupata maneno yasiyo jichanganya kutoka kwenye utafiti wa binadamu, labda uazishe Mwenyewe huo uthibitisho, hata Ukifanya uthibitisho wewe Mwenyewe karne hii, miaka ijayo binadamu watakao zaliwa, watapinga uthibitisho wako...
Sawa, naelewa hilo. Nimesoma Godel's Incompleteness Theorems. Baically kila uthibitisho utahitaji assumptions ambazo haziwezi kuwa ndani ya mfumo huo wa uthibitisho, na msururu huo hauna mwisho, ukienda level moja deeper, utakutana na tatizo la kuthibitisha assumptions mpya upya, hivyo hivyo, ad infinitum, ad nauseam.

Ndiyo maana watu wakamtengeneza Mungu ili awe chanzo cha yote, asiyehitaji uthibitisho, asiyeweza kuthibitishika. Hii ni "Deus Ex Machina", hadithi ya "Mungu kamaliza kila kitu" ya kusimamisha uchunguzi bila kuumaliza, wakati habari hatujaimaliza na Mungu hayupo.

Kimsingi, habari ya kuwepo kwa Mungu ni kusema "Bwana wee, tumetafuta majibu mpaka tumechoka, hapa tumchomeke Mungu tu kaumba hivi, kesho tukiamka tutaendelea kutafiti, tukipata majibu yanayotuonesha ukweli mwingine, tutajiongeza hapo, na tutakapokwama, tutamchomeka Mungu tena.

Hii habari inaitwa "God of The Gaps".

Watu kutoweza kuwa na narrative yoyote ambayo iko fully logically consistent ni ushahidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo. Angekuwepo, angeumba ulimwengu wenye kueleweka na kutupa logically consistent explanation ya ulimwengu ambayo ingetuonesha uwepo wake bila contradiction yoyote, popote, kwa yeyote.

Hilo tatizo ulilolitaja, kutoweza kupata maneno yasiyojichanganya kutoka kwenye utafiti wa watu, huo nao ni ushahidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingekuwa mkatili hivyo kutuumba katika ulimwengu ambao hatuwezi kupata kitu kilicho fully logically consistent.
 
Sawa, naelewa hilo. Nimesoma Godel's Incompleteness Theorems. Baically kila uthibitisho utahitaji assumptions ambazo haziwezi kuwa ndani ya mfumo huo wa uthibitisho, na msururu huo hauna mwisho, ukienda level moja deeper, utakutana na tatizo la kuthibitisha assumptions mpya upya, hivyo hivyo, ad infinitum, ad nauseam.

Ndiyo maana watu wakamtengeneza Mungu ili awe chanzo cha yote, asiyehitaji uthibitisho, asiyeweza kuthibitishika. Hii ni "Deus Ex Machina", hadithi ya "Mungu kamaliza kila kitu" ya kusimamisha uchunguzi bila kuumaliza, wakati habari hatujaimaliza na Mungu hayupo.

Watu kutoweza kuwa na narrative yoyote ambayo iko fully logically consistent ni ushahidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo. Angekuwepo, angeumba ulimwengu wenye kueleweka na kutupa logically consistent explanation ya ulimwengu ambayo ingetuonesha uwepo wake bila contradiction yoyote, popote, kwa yeyote.

Hilo tatizo ulilolitaja, kutoweza kupata maneno yasiyojichanganya kutoka kwenye utafiti wa watu, huo nao ni ushahidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingekuwa mkatili hivyo kutuumba katika ulimwengu ambao hatuwezi kupata kitu kilicho fully logically consistent.

• Nimepitia vitabu vyako ingawa si kwa ujumla,
Deus ex machina - Wikipedia, Deus ex machina" hii ina inazungumzia masuala ya mungu kuwa ni hadithi au kazi ya sanaa, au kutatuliwa kwa tatizo kwa njia isiyo ya kawaida au ya ghafla au bila vielelezi maelezo ya kutosha(kuhusu uthibitisho wa Mungu) .

• Godel's Incompleteness Theorems, lakini pia naye huyu nimepitia, huyu ni kama Kiranga tu, Kwa sababu anahisi kuna vitu vilifichwa kuhusu ukweli wake,, huyu mwana hisabati bado hajanishawishi kuhusu uthibitisho,

• Lakini uelewa wangu, Hii njia isiyo sahihi au isiyoaminika ya kumaliza/kuthibitisha hadithi au uwepo wa kitu hapo zamani na inaweza kusababisha upotezaji wa ubunifu au mantiki katika hadithi.

• je una kitabu kingine cha kidunia kinazungumzia haya masuala ya fact????
 
Mambo ambayo yanaweza thibitisha kuwa ni vitabu vya mungu :-
• Mafundisho: Ujumbe wa Biblia na mafundisho yake, kama vile maadili, amri za Mungu, na maelezo ya historia ya kidini, unaweza kuifanya ionekane kama kitabu takatifu.

• Historia na Utamaduni: Katika jamii nyingine, Biblia inaweza kuonekana kuwa takatifu kutokana na umuhimu wake wa kihistoria na kiutamaduni, hata kama haichukuliwi kama Neno la Mungu.

• Uthibitisho wa Kiroho: Baadhi ya watu wanaweza kusema kwamba wamepata uzoefu wa kiroho na maelezo yanayopatikana katika Biblia, na hivyo kuiona kama kitabu takatifu kwao
Biblia inasapoti slavery,Huo nao unasema ni utakatifu?
 
Biblia inasapoti slavery,Huo nao unasema ni utakatifu?
• Swali la kama Biblia inaunga mkono utumwa, na ikiwa hilo linakwenda sambamba na utakatifu, limejadiliwa kwa kina na wasomi na watu wenye imani tofauti. Ni muhimu kuelewa kwamba muktadha wa utamaduni, historia, na tafsiri unahusika katika kuelewa maandishi matakatifu.

• Wakati maandiko ya Agano la Kale yanajumuisha sheria zinazohusu utumwa, inapaswa kuzingatiwa kwamba muktadha wa wakati na tamaduni zilikuwa tofauti sana na muktadha wa leo. Sheria hizo hazimaanishi kwamba Biblia inaidhinisha au inapendekeza utumwa kama tunavyouelewa katika muktadha wa kisasa.

• Vile vile, mafundisho ya Agano Jipya juu ya upendo, haki, na usawa vimechukuliwa na wengi kama msingi wa kutetea haki za binadamu na kupinga utumwa. Kwa hiyo, wakati sehemu za Biblia zinaweza kuonekana kutoa mwongozo kuhusu utumwa katika muktadha wa kihistoria,

Ni muhimu kutafsiri maandiko hayo kwa kuzingatia mafundisho yote ya kiroho, kimaadili, na kijamii yanayopatikana katika maandiko matakatifu. Watu wanaweza kuwa na mitazamo tofauti kuhusu jinsi ya kuelewa na kutumia maandiko hayo kulingana na imani zao na muktadha wao wa kitamaduni.
 
Mambo ambayo yanaweza thibitisha kuwa ni vitabu vya mungu :-
• Mafundisho: Ujumbe wa Biblia na mafundisho yake, kama vile maadili, amri za Mungu, na maelezo ya historia ya kidini, unaweza kuifanya ionekane kama kitabu takatifu.

• Historia na Utamaduni: Katika jamii nyingine, Biblia inaweza kuonekana kuwa takatifu kutokana na umuhimu wake wa kihistoria na kiutamaduni, hata kama haichukuliwi kama Neno la Mungu.

• Uthibitisho wa Kiroho: Baadhi ya watu wanaweza kusema kwamba wamepata uzoefu wa kiroho na maelezo yanayopatikana katika Biblia, na hivyo kuiona kama kitabu takatifu kwao
Sasa umeniandikia nini hiki!!

Huu ndiyo uthibitisho?
 
🤔🤔, Nikisema na wewe unipe uthibitisho kuwa Mungu hayupo utatoa..?
Dhana ya uthibitisho ipo kwa vitu vilivyopo.

Wewe ukisema mimi namiliki bunduki kinyume cha Sheria, you've burden of proof, kuithibitisha kwamba ni kweli namiliki bunduki kinyume cha Sheria.

Sasa Mungu asiekuwepo mimi nathibitishaje kuwa hayupo, wakati hayupo?
 
Kumuaminisha mtu kuwa kuna Mungu halafu yeye na misingi yake hairuhusu kuamini kuhusu Mungu ni jambo gumu sana tena sana ....ni Bora ubaki na unacho kiamini kaka
Kwanza kabisa, siongelei imani, imani kila mtu ana au hana yake, hiyo ni haki ya kikatiba, ni haki ya utu imeandikwa katika Universal Declaration of Human Rights tangu December 10 1948.

Siongelei imani, naongelea kutafuta ukweli.

Imani unaruhusiwa kuamini vyovyote unavtotaka, ukweli au uongo.

Kutafuta ukweli ni lazima tuangalie ukweli uko wapi na tuachane na uongo.

Umeelewa tofauti hapo?
 
Dhana ya uthibitisho ipo kwa vitu vilivyopo.

Wewe ukisema mimi namiliki bunduki kinyume cha Sheria, you've burden of proof, kuithibitisha kwamba ni kweli namiliki bunduki kinyume cha Sheria.

Sasa Mungu asiekuwepo mimi nathibitishaje kuwa hayupo, wakati hayupo?

. OK, Uthibitisho wa namna hiyo huwezi ukaupata hata iweje....

. Kumbuka hapa duniani, hakuna kitu chenye uthibitisho.
 
. OK, Uthibitisho wa namna hiyo huwezi ukaupata hata iweje....

. Kumbuka hapa duniani, hakuna kitu chenye uthibitisho.
Hapa duniani hakuna kitu chenye uthibitisho au uthibitisho wa mungu kuwepo ndiyo haupo hapa duniani?
 
Jamani itoshe kusema majibu ya haya majadiriano yote majibu yake yapo kwenye biblia.
kila kitu kilishatabiriwa kwenye biblia kuhusu mlipuko wa manabii wa uongo na watafanya maajabu na ishara kubwa..ndo kama hizi tunazoziona.
Tuzipimeni hizo roho kama zinatoka kwa Mungu Jinsi ya kuzipima ni kumwamini Yesu kristo kama bwana na mwokozi wetu.
 
Back
Top Bottom