Esther Matiko ahoji tofauti ya mishahara kwa askari magereza na askari polisi licha ya kuwa wote wapo wizara moja

Kumbe wanaolipwa mishahara midogo ni wengi ila kila siku wanasimangwa walimu
Polisi wa form four +cheti Cha polisi na mwalimu wa form four +cheti Cha ualimu walioanza kazi tarehe 30-06-2015 mwalimu ana mshahara mkubwa kuliko polisi na psssf amechangia Hela nyingi huku polisi hajawekewa hata mia mbovu.

Polisi ana gari wakati mwalimu ana pkpk
Polisi ana nyumba, Mwl ana kiwanja...au geto lipo lenta



CCM oyee
 
Kuwa cheo kimoja sio sababu ya kupata mshahara sawa, kitu cha msingi ni lini alikipata cheo. Kuna suala la "Salary Incliment" kwa wale tuliosoma Cuba watakua wamenielewa.
Hawawezi kukuelewa kwa sababu iliyotajwa ni Basic Starting Salary kwenye hicho cheo kwa Polisi na Magereza.Hiyo "Incliment" nadhani ulimaanisha "Increment" haihusiki.
 
Usipovuta mibangi yako unakuwaga na akili kiasi chake. Rushwa ni tabia ya mtu. Endelea kupunguza mibangi yako maana nilishasema akili kichwani mwako zipo ila mibangi ndio inayokuharibu
Hahahahaha sister umeanza, nadhani karibu Makonda anaingia Mbeya, UWT mjipange
 
Asisahau kuhoji pia utofauti uliopo kati ya mshahara wa mbunge na mwalimu
 
Rushwa ni tabia yako.
Kuna watumishi wanalipwa mamilioni lakini wanakula rushwa.
Huko huko polisi kuna Watumishi wanapokea mshahara chini ya huo lakini wamejitenga na rushwa
rushwa za buku mbili mbili za road ndio tatizo achana na zile rushwa za kibabe
 
Sasa hao wengine wapo na hali gani?
 
Aisee 🤣
 
Niliamua kuacha kazi nikiwa na cheo kikubwa,leo hela anayolipwa afisa wa police mwenye nyota mbili ndio namlipa dereva wangu.
 
Doh ndo maana
 
Nchi hii watu wana mishahara midogo Sana, Leo sukari 5000!
Huo mshahara nilikuwa napata 2007! Kipindi hcho bei ya Lita ya diesel 1200! -1800! Sukari kilo buku!
Na nilikuwa msera tu, na nikaona hautoshi!
Sasa polisi analipwa 900k! Asomeshe, alipe Kodi, Ada, na Ana miriki ka IST! Hapa kuna ujambazi na umafia wa kutisha! Sasa nimeelewa kwanini Yule kijana wa, Maldini mtwara, makachero waliamua kumpoteza kwa sindano ya sumu! Kisa milioni 33!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…