Ray C alizidiwa kiuno hadi na Fifi Moto bwana. Taji lake lilikuwa hatarini kama Fifi angeamua kudumu humo.
Jide mlia machozi alikuwa ndio SI unit ya muziki wa bongo kwa wanawake. Wimbo wa kwanza tu akaenda kutumbuiza na Kora Awards huko Kusini mwa Afrika.
Yaliyokuja baada ya hapo ni kisanga.
Alipambana na kila aina ya presha ya wadau wa muziki bongo, kwanini nisimuite Komando?
Aliwaweka mbali zaidi washindani wake kwa Distance kubwa sana kwa kuchanganya Lugha za neno Nakupenda kutoka mataifa mbalimbali.
Tukamuita Mama Some Food nae hakutuacha tuzubae kwa kutufungulia mgahawa, nahisi ndio alikuwa msanii wa kwanza kuwa na biashara inayoonekana na kuwa na maana.
Tumesahau hata aliponunua prado? Na baadae akaja kumuuzia produza Lamar. Ikafikia hatua Marehemu Ngwair akaimba kwenye ngoma yake "Sikiliza" akiwahusia mabinti kuhusu kumiliki Prado kama Lady Jay Dee?
Huyu Mkurya atanimalizia wino kwa kuandika.
Maua yake hayatoshi hata niseme niyanunue kwa gharama za pesa zote zilizoko B.O.T