Facts kadhaa zinazoufanya Mkataba wa Tanzania na Dubai juu ya Bandari kuwa batili. Tuwe nazo Makini

Facts kadhaa zinazoufanya Mkataba wa Tanzania na Dubai juu ya Bandari kuwa batili. Tuwe nazo Makini

Midimay

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2015
Posts
3,036
Reaction score
5,039
Habari za asubuhi wana JF,

Tunaendelea na hili jambo ambalo sasa lipo katika ngazi ya familia kabisa. Tunaulizwa majumbani mwetu. Kuna mambo kadhaa ambazo ni facts kabisa katika mkataba huu na zinaufanya ukose sifa.

Wao wanasema ni makubaliano tu, lakini makubaliano ni mkataba. Baadhi ya facts hizo nilizoziona ni hizi zifuatazo:

1. Makubaliano hayana ukomo. Kama ambavyo imeonekana kwa wengi, makubaliano haya hayaonyeshi muda maalum katika umilikishaji wa bandari zote kwa DPW.

2. Umilikishaji wa Bandari zote. Kwanini DPW wapewe bandari zote za Bahari, Mito na Maziwa katika iliyokuwa Tanganyika? Tumezichoka au tamaa ya watawala au kulambishwa asali?

3. Kutohusishwa kwa bandari za upande wa Zanzibar. Hili linasababisha mtanziko wa kikatiba kabisa (Constitutional Crisis). Sheria wanayosema inaipa TPA mamlaka ya upande ya iliyokuwa Tanganyika, imeipa TPA mamlaka ya Tanzania bara na Tanzania Zanzibar katika kifungu cha 2 cha sheria hiyo ya TPA.

4. Hakukuwa na ushindani katika kutafuta mwekezaji. Hiyo inaipa DPW nguvu ya kuinyanyasa na kuifanya kuwa wanyonge serikali ya Tanzania kupitia hiyo timu ya Hamza Johari. Lakini pia ni uvunjaji na ukiukaji wa sheria za nchi juu yw manunuzi ya umma na uwekezaji katika rasilimali asili za nchi.

5. Pesa yenyewe inayotajwa, siyo kiasi cha kuvutia. Hivi leo nchi hii inayokusanya 2+ T kwa mwezi kama mapato ya kodi tu, inawehuka na uwekezaji wa 2T? kiasi cha kuachia bandari zote kwa DPW?

6. Kukosekana kwa ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Hadi sasa hatuoni katika document na katika ufafanuzi, mahali popote ambapo ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imehusika katika kushauri na kuyabariki makubaliano haya. Hili pia linavunja katiba na sheria kadhaa za nchi.

7. Kukosekana kwa sahihi ya Katibu Mkuu-Uchukuzi. Sehemu ya sahihi ya Katibu Mkuu-Uchukuzi imesainiwa kwa niaba yake na hadi sasa hakuna ufafanuzi wowote juu ya hilo. Je, kama alikataa? Wenye tamaa wakalazimisha? Kwanini waziri alisaini kwa niaba ya Katibu Mkuu?

8. Tanzania kutakiwa kuijulisha Dubai juu ya uwekezaji mpya katika bandari au maeneo mengine. Hili ni dharau kwa nchi na kuikosesha nchi wawekezaji wapya ambao wangekuja na terms bora kuliko za DPW.

9. Utatuzi wa migogoro unaenda kinyume na sheria ya Natural Resources (permanent sovereignty).

10. Wananchi hatuyataki haya makubaliano. Hili nalo kisidharuliwe. Haya makubaliano yamekataliwa na wananchi.
 
Habari za asubuhi wana JF.
Tunaendelea na hili jambo ambalo sasa lipo katika ngazi ya familia kabisa.
Tunaulizwa majumbani mwetu.
Kuna mambo kadhaa ambazo ni facts kabisa katika mkataba huu na zinaufanya ukose sifa.
Wao wanasema ni makubaliano tu, lkn makubaliano ni mkataba.
Baadhi ya facts hizo nilizoziona ni hizi zifuatazo:

1. Makubaliano hayana ukomo. Kama ambavyo imeonekana kwa wengi, makubaliano haya hayaonyeshi muda maalum katika umilikishaji wa bandari zote kwa DPW.

2. Umilikishaji wa Bandari zote. Kwanini DPW wapewe bandari zote za Bahari, Mito na Maziwa katika iliyokuwa Tanganyika?Tumezichoka au tamaa ya watawala au kulambishwa asali?

3. Kutohusishwa kwa bandari za upande wa Zanzibar. Hili linasababisha mtanziko wa kikatiba kabisa(Constitutional Crisis). Sheria wanayosema inaipa TPA mamlaka ya upande ya iliyokuwa Tanganyika, imeipa TPA mamlaka ya Tanzania bara na Tanzania Zanzibar katika kifungu cha 2 cha sheria hiyo ya TPA.

4. Hakukuwa na ushindani katika kutafuta mwekezaji. Hiyo inaipa DPW nguvu ya kuinyanyasa na kuifanya kuwa wanyonge serikali ya Tanzania kupitia hiyo timu ya Hamza Johari. Lakini pia ni uvunjaji na ukiukaji wa sheria za nchi juu yw manunuzi ya umma na uwekezaji katika rasilimali asili za nchi.

5. Pesa yenyewe inayotajwa, siyo kiasi cha kuvutia. Hivi leo nchi hii inayokusanya 2+ T kwa mwezi kama mapato ya kodi tu, inawehuka na uwekezaji wa 2T? kiasi cha kuachia bandari zote kwa DPW?

6. Kukosekana kwa ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Hadi sasa hatuoni katika document na katika ufafanuzi, mahali popote ambapo ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imehusika katika kushauri na kuyabariki makubaliano haya. Hili pia linavunja katiba na sheria kadhaa za nchi.

7. Kukosekana kwa sahihi ya Katibu Mkuu-Uchukuzi.
Sehemu ya sahihi ya Katibu Mkuu-Uchukuzi imesainiwa kwa niaba yake Na hadi sasa hakuna ufafanuzi wowote juu ya hilo. Je, kama alikataa? Wenye tamaa wakalazimisha?
Kwanini waziri alisaini kwa niaba ya Katibu Mkuu?

8. Tanzania kutakiwa kuijulisha Dubai juu ya uwekezaji mpya katika bandari au maeneo mengine.
Hili ni dharau kwa nchi na kuikosesha nchi wawekezaji wapya ambao wangekuja na terms bora kuliko za DPW.

9. Utatuzi wa migogoro unaenda kinyume na sheria ya Natural Resources (permanent sovereignty).

10. Wananchi hatuyataki haya makubaliano. Hili nalo kisidharuliwe. Haya makubaliano yamekataliwa na wananchi.
Mkataba mbona Una termination clause?
Unaweza iweka hapa tuone labda tatizo ni English na sio mkataba
Hebu weka Termination clause tukutafsirie
 
Mkataba mbona Una termination clause?
Unaweza iweka hapa tuone labda tatizo ni English na sio mkataba
Hebu weka Termination clause tukutafsirie
Ajabu, wewe peke yako ndie unaejiona msomi wa kujua kiingereza zaidi ya wanasheria waliosema mkataba una shida, na unayejua kutafsiri vipengele vya kisheria kwenye huo mkataba, ambaye hata sheria yenyewe hujaisomea!.

Idiot.

IGA inajieleza wazi kwenye objectives zake, kwamba, the aim of that particular agreement, is to set a legally binding framework kwenye maeneo ya operation, management, improvement, na development. Hapa ndipo panapoleta hizi kelele za sasa, wala sio kutumiwa kama mnavyodai kwenye uongo wenu.

Ndio maana mnaambiwa mwarabu yuko huru kuanza kazi zake toka October 2022 IGA iliposainiwa, mpaka hapo hiyo HGA yako haina maana tena, soma mkataba wote, sio nusu nusu, au kulishwa matango pori na Mbarawa ili mumtetee shangazi yenu.
 
Mkataba mbona Una termination clause?
Unaweza iweka hapa tuone labda tatizo ni English na sio mkataba
Hebu weka Termination clause tukutafsirie
Prove hiyo termination clause. Wewe, The Boss toka mwanzo unautetea huu mkataba kisa tu Rais ni muislamu. Kiti ambacho ni ujinga tu kukubali kitu kisichofaa kisa kiongozi unasali naye.
JPM alipingwa hadi na kina Fr. Kitima.
 
Hadi Hamza Johari mwenyewe alishindwa kuelezea ukomo hadi akasema itakuwepo kwenye mikataba. Ana uhakika gani na sisi tunathibitishaje kwamba itakuwepo kwenye mikataba husika kama haipo kwenye mkataba mama?
Mikataba yote itakuwa subsests za mkataba huu.
 
Prove hiyo termination clause. Wewe, The Boss toka mwanzo unautetea huu mkataba kisa tu Rais ni muislamu. Kiti ambacho ni ujinga tu kukubali kitu kisichofaa kisa kiongozi unasali naye.
JPM alipingwa hadi na kina Fr. Kitima.
Termination clause imesema very openly kuwa uhai wa IGA utaenda sambamba na uhai wa HGA..
Simply kuwa kama HGA mtasema ni miaka 25 na IGA ni miaka 25...
Mbona kitu chepesi kuelewa??
 
Termination clause imesema very openly kuwa uhai wa IGA utaenda sambamba na uhai wa HGA..
Simply kuwa kama HGA mtasema ni miaka 25 na IGA ni miaka 25...
Mbona kitu chepesi kuelewa??
Huo ni mtego. Unaingiaje kwenye mtego huku unajiona?
 
HGA ndio ilitakiwa kufuata IGA imesemaje na sio kukwepa kutaja kwenye IGA, eti itakuwepo kwenye HGA!
 
Hizo paragraph zote 10,ni lazima zijadiliwe kwa kina na ikibidi zibadilishwe, mkataba uwe na awamu kadhaa, miaka 5 kwanza, then pande zikae zione tunakwenda kwa faida au hasara, au je mapungufu ni yepi?, kwa akili timamu huwezi kujifunga kichwa kichwa, wasiwasi ni akili, za kuambiwa changanya na zako!, tunahitaji wawekezaji lakini twendeni kwa hatua.
 
Back
Top Bottom