Wamekwambia hawana chakula hao?!
Si wanaendesha bandari hapo msumbiji, nani kakwambia msumbiji wamepata soko la mazao?!
Zungumza facts za mkataba, achana na mengineyo, hewa hiyo
Hawana chakula kwao ni jangwa,Hakuoti kitu chochote wala kufuga chochote,zaidi ya ngamia,hawana
1.Kuku
2.Ng'ombe
3.Mbuzi.
4.kondoo
5Viazi,ndizi,Michele,matunda,nk
Badala sisi kuanzisha njia za kibiashara kunufaika kwao,twapoteza wakati bure,!nafasi hiyo ya vyakula akichukuwa wa nchi nyingine tutakuja lalamika.Hapo Zanzibar kuna soko kubwa la vyakula na mifugo na matunda,kutokana na mahotel ya kitalii,fursa hatuzitumii.
Kuna visiwa vya Ngazija,Mauritius,Madagascar,!fursa za vyakula kuuza kule,na mifugo,hatutumii.
Kama hivi sasa mbuzi amefika mpaka 170000,ng'ombe mpaka mamilioni,kwa ajili ya sikukuu ya Eid,dini inawahimiza watoe sadaka ya nyama!,bado visima watachimba vya maji.kusaidia kwenye matatizo ya maji,maana dini ya uislamu imehimiza kutoa sadaka ya maji,sisi tumekaa kubishana yasio na faida.Ukiwa na mbuzi 20 si tayari una 36milioni.Bado ng'ombe
Ukiwa nao 20,hujainuka kiuchumi.Na hapo bado waarabu hawajaanza Bandarini.Hawa waislamu waacheni waje,watuinue kiuchumi,siku kuu zao zote na siku za kawaida ni neema.Bado kipindi cha sikukuu ya mwezi wa Ramadani,wananua Michele kwa wingi,kwa kutoa sadaka.Bado hatujagusia wavuvi wa samaki,hawa ni walaji sana wa samaki,kwa wavuvi ni fursa hiyo.
Wakulima na wafugaji,kwa ujio wa hawa waarabu waislamu ni neema kwao.