Facts kadhaa zinazoufanya Mkataba wa Tanzania na Dubai juu ya Bandari kuwa batili. Tuwe nazo Makini

Facts kadhaa zinazoufanya Mkataba wa Tanzania na Dubai juu ya Bandari kuwa batili. Tuwe nazo Makini

Mkuu, kuhusu 'mapungufu' na 'madoa' ya kisheria kwenye hii IGA ambayo wataalam na wabobevu mbali mbali wamekuwa wakiyapazia sauti, nini maoni yako kama mwananchi?

-Kaveli-
Kila kifungu cha mkataba huo mi nakiangalia kwa namna 4 hadi 5.
1. Kazi ya IGA hii ni nini?
2. Maana ya kilichoandikwa
3. Dhahania ya kwanini kimeandikwa hivyo
4. Natumizi yake kwa ujumla wake
5. Kilichoandikwa ni matokeo ya majadiliano ya pande mbili zenye sifa ya kuvutia upande wake kwa kila mmoja.

Katika hali kama hiyo, hamuwezi kuwa na mkataba au makubaliano ambayo upande mmoja utakuwa umepata kila kitu. Ukisoma maoni mengi, wamejikita kwenye maana ya kilichoandikwa bila ku foresee kwanini au ilikuwaje hadi kikaandikwa hivyo.

Mpaka sasa, kwa vifungu vinavyopigiwa kelele mimi binafsi naona havina shida za hivyo. Na naamini, kuna upotoshaji wa kimaslahi kutoka kwa watu wachache halafu wengi wameunga tela kwa kufuata mkumbo.

Kuna viashiria vingi sana vinaonyesha kuwa kuna upotoshaji. Mfano, IGA inataja kiambatisho chenye maeneo ya kipaumbele katika utekelezaji kama phase I, lakini cha kushangaza opponents hawayataji hayo maeneo ila zaidi wanatuambia kuwa bandari imeuzwa mazima. Unajiuliza, sasa kama Tanzania ishatoa Bandari (yote), logic ya maeneo ya utekelezaji ya phase I yanakujaje?

Kuna hoja ya kwanini Bandari ya Zanzibar haipo. Huhitaji kuwa mfanyabiashara mkubwa kujua kuwa bandari ya Zanzibar sio economically viable kwa investor yoyote yule. Hivi Bandari ya Zanzibar utaifanya hub kwa ajili ya mzigo wa kwenda kuuza wapi? Au mtu anakwenda Lindi na kuwaambia hii Bandari yenu itachukuliwa na DP World! Hivi kwa akili za kawaida tu, DP ajenge au aendeleze Bandari Lindi kwa interest gani? Will it be economically viable?

Lakini pia, kwanini akili zetu zimejijenga kwenye kuvunja??

Kwenye hoja ya ukomo. Unamuuliza mtu, IGA imesema ukomo wake ni subject ya mikataba ya utekelezaji ambayo imetajwa, then unamuuliza je nini itakuwa maoni yako kama hiyo mikataba itakuwa imesema miaka 10, je baada ya miaka 10, IGA itaendelea kuwa hai? Hupati majibu. Au unamuuliza wewe ulitaka hicho kifungu cha ukomo kiwe vipi? Anakwambia kitaje miaka kama 10, 20, 30 etc, unamuuliza basis ya kuandika 10, au 20 au 30 ni nini? Hana majibu.

In short, mambo ni mengi.
 
Nakuuliza umepigwaje? Achana na maneno ya kijiweni.
Tuje kwenye ahadi zilizotolewa, gas ikifika dar itasaidia kwenye usalishaji wa umeme na umeme ungeshuka bei na ingeondoa kabisa kukatakata kwa umeme. Hilo la kwanza, ilitekelezeka?
 
Mambo yasiyo na mwelekeo pia ambayo ni fitinishi kama unayopenda kiposti mara kwa marq.
Hii ni definition yako au umeitoa wapi? Na kiwango cha mantiki ya post zangu unapima wewe? Wewe na nani?
 
Hii ndo ilikua suluhisho tupigane na polis wao adi kieleweke sema tumekua waoga sana
Hizi ni kauli za kuambiana kwa sasa. Kavu kavu kama alivyosema nshalla. Uzuri hata wao wana roho moja.
...WHEN THE SOFT WAY FAILS, THE HARD WAY IS INEVITABLE..
 
Habari za asubuhi wana JF,

Tunaendelea na hili jambo ambalo sasa lipo katika ngazi ya familia kabisa. Tunaulizwa majumbani mwetu. Kuna mambo kadhaa ambazo ni facts kabisa katika mkataba huu na zinaufanya ukose sifa.

Wao wanasema ni makubaliano tu, lakini makubaliano ni mkataba. Baadhi ya facts hizo nilizoziona ni hizi zifuatazo:

1. Makubaliano hayana ukomo. Kama ambavyo imeonekana kwa wengi, makubaliano haya hayaonyeshi muda maalum katika umilikishaji wa bandari zote kwa DPW.

2. Umilikishaji wa Bandari zote. Kwanini DPW wapewe bandari zote za Bahari, Mito na Maziwa katika iliyokuwa Tanganyika? Tumezichoka au tamaa ya watawala au kulambishwa asali?

3. Kutohusishwa kwa bandari za upande wa Zanzibar. Hili linasababisha mtanziko wa kikatiba kabisa (Constitutional Crisis). Sheria wanayosema inaipa TPA mamlaka ya upande ya iliyokuwa Tanganyika, imeipa TPA mamlaka ya Tanzania bara na Tanzania Zanzibar katika kifungu cha 2 cha sheria hiyo ya TPA.

4. Hakukuwa na ushindani katika kutafuta mwekezaji. Hiyo inaipa DPW nguvu ya kuinyanyasa na kuifanya kuwa wanyonge serikali ya Tanzania kupitia hiyo timu ya Hamza Johari. Lakini pia ni uvunjaji na ukiukaji wa sheria za nchi juu yw manunuzi ya umma na uwekezaji katika rasilimali asili za nchi.

5. Pesa yenyewe inayotajwa, siyo kiasi cha kuvutia. Hivi leo nchi hii inayokusanya 2+ T kwa mwezi kama mapato ya kodi tu, inawehuka na uwekezaji wa 2T? kiasi cha kuachia bandari zote kwa DPW?

6. Kukosekana kwa ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Hadi sasa hatuoni katika document na katika ufafanuzi, mahali popote ambapo ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imehusika katika kushauri na kuyabariki makubaliano haya. Hili pia linavunja katiba na sheria kadhaa za nchi.

7. Kukosekana kwa sahihi ya Katibu Mkuu-Uchukuzi. Sehemu ya sahihi ya Katibu Mkuu-Uchukuzi imesainiwa kwa niaba yake na hadi sasa hakuna ufafanuzi wowote juu ya hilo. Je, kama alikataa? Wenye tamaa wakalazimisha? Kwanini waziri alisaini kwa niaba ya Katibu Mkuu?

8. Tanzania kutakiwa kuijulisha Dubai juu ya uwekezaji mpya katika bandari au maeneo mengine. Hili ni dharau kwa nchi na kuikosesha nchi wawekezaji wapya ambao wangekuja na terms bora kuliko za DPW.

9. Utatuzi wa migogoro unaenda kinyume na sheria ya Natural Resources (permanent sovereignty).

10. Wananchi hatuyataki haya makubaliano. Hili nalo kisidharuliwe. Haya makubaliano yamekataliwa na wananchi.
haya umeyatoa unakojua mwenyewe
 
Hii ni definition yako au umeitoa wapi? Na kiwango cha mantiki ya post zangu unapima wewe? Wewe na nani?
CHADEMA mna matatizo vichwani. Mnadhani nchi ni Kaskazini tu. Ndo maana hamtakuja kuupata uraisbwa hii nchi mpaka kiama. Hamfai kabisa.
 
Kwamba HGA zote ni Non-disclosure?

-Kaveli-
Ndio, utaona tu kampuni sehemu inapiga kazi. Au watu mnahamishwa, basi.

Kule ngorongoro si wamasai walihamishwa! Uliuona huo mkataba? Tuanzie hapo..
 
Back
Top Bottom