Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)

Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)

UPDATE: Korea Kusini

Kasi ya maambukizi inazidi kuongezeka nchini humo huku visa vipya 70 vikiripotiwa.

Mpaka hivi sasa, Korea Kusini imekwisharipoti visa takribani 833 na vifo saba (7).
 
Habari!

Karibu kwa ajili ya kujuzwa na pia kupata taarifa (masasisho) mbalimbali ya kile kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus) almaarufu kama "kirusi cha Wuhan" kutoka nchini China.

Katika uzi huu utapata kufahamu mambo mbalimbali hususani hali ya ongezeko na ukuaji, jitihada zinazofanyika kukabiliana na kirusi hiki na mengine mengi yanayoibuka duniani kote katika muda wowote kuanzia sasa.

Nikukaribishe sana!

====

Coronaviruses in virusi vinavyopatikana zaidi kwa wanyama, lakini katika matukio machache virusi hivyo ninavyoitwa Zoonotic, Kisayansi, vinaweza kuambukizwa kutoka kwa mnyama kwenda kwa binadamu.

Virusi hivi vinaweza kuwafanya watu wakaugua, mara nyingi katika sehemu ya juu ya mfumo wa upumuaji sawa kabisa na mafua ya kawaida.



Virusi husambaa kutoka kwa binadamu mmoja hadi mwingine kwa njia ya hewa kwa kukohoa au kupiga chafya, kugusana na mtu mwenye virusi hivyo.

Njia nyingine ni kugusa kitu au sehemu yenye virusi na kisha kujigusa mdomo, pua au macho kabla ya kunawa na mara chache huambukiza kupitia kinyesi.

Dalili za kuwa umepata virusi hivi ni pamoja na pua kudondosha mafua mfululizo, kuumwa kichwa, kukohoa, kupata homa na muwasho katika koo ila kwa wenye kinga ndogo ya mwili kama wazee au watoto wanaweza kupata Nimonia (Pneumonia).

Hakuna Kinga ya virusi hivyo kwa sasa, ila usambaaji wake kwa binadamu unaweza kupunguzwa kupitia kuosha mikono yako mara kwa mara kwa maji na sabuni na epuka kugusa macho, mdomo na pua kwa mikono isiyooshwa.

Pia, unaweza kupunguza usambazaji wake kwa kukaa mbali na mtu aliyethibitika kuwa na maambukizi. Ukianza kuona dalili hizo unashauriwa kumuona daktari.

Ukithibitika kuwa na maambukizi ya virusi hivyo, funika mdomo na pua yako wakati wa kupiga chafya au kukohoa na safisha sehemu au kitu ulichokigusa.

====

Kirusi hiki cha Corona, kinaaminika kuwa kilianza katika soko la bidhaa za baharini mwishoni mwa mwaka 2019, katikati ya Jiji la Wuhan, China ambalo lilikuwa linauza nyama ya porini.



Kirusi hicho ni sehemu ya familia ya kirusi corona ambacho kinauhusiano na virusi vya SARS na MERS ambavyo vilisababisha milipuko siku za nyuma.

Kirusi hiki kimeenea katika miji mingine ikiwemo Beijing na Shanghai, pia katika maeneo mengine duniani kama Marekani, Thailand, Korea Kusini, Japan, Australia, Ufaransa, Malaysia, Vietnam, Taiwan, Singapore, Nepal, Macau, Hong Kong na Canada.

Mpaka sasa kwa mujibu wa taarifa zilizopo ni kuwa, idadi ya watu wapatao 2045 wamegundulika kuwa na kirusi hiki huku wapatao 633 wakipatikana kwa siku ya jana pekee.

324 kati ya hao 2045 wako katika hali mbaya zaidi (critical condition) huku idadi ya waliokufa kutokana na kirusi hicho ikifikia 56 nchini China.

====

Hapo awali, China ilitoa tahadhari kuwa kirusi hiki kinaweza kusambaa kwa watu wengi zaidi.

Waziri wa Kamisheni ya Afya ya Taifa nchini China, Ma Xiaowei, akizungumza na vyombo vya habari, alisema kuwa, uwezo wa serikali wa kufahamu kirusi hiki kipya ni finyu na hawajui hatari zinazoweza kuambatana na kubadilika kwa kirusi hiki. [VOA]

Ma Xiaowei alisema muda ambao kirusi hiki cha corona huchukuwa hadi kujitokeza ni kati ya siku mmoja hadi 14, na kuwa kirusi hiki kinaambukiza hata wakati kinajijenga mwilini, kitu ambacho kilikuwa tofauti kwa homa kali ya mafua, SARS, kirusi corona kilichoibuka China na kuua takribani watu 800 duniani mwaka 2002 na 2003.

Mpaka sasa juhudi zilizokwisha kufanyika ili kudhibiti kuenea kwa kirusi hiki ni pamoja na katazo la usafirishaji na kusafiri na kusitisha matukio ya sherehe kubwa. China imetoa makatazo kadhaa ya kusafiri katika maeneo yaliyoathiriwa vibaya sana katika nchi hiyo ili kuzuia kuenea kwa kirusi hicho.

Muendelezo wa haya pamoja na yatakayokuwa yakijiri tutapata kuyafahamu kwa kina.

Baki hapa!

====

SASISHO: Februari 22; Hubei imeripoti visa vipya 630 pamoja na vifo vipya 96 kutokana na virusi vya Corona mkoani humo. Mpaka sasa visa takribani 78,754 vimeripotiwa ulimwenguni huku idadi ya waliokufa kutokana na virusi vya Corona ikifikia 2,460 duniani kote.

Takwimu hizo ni kulingana na ripoti rasmi.

SASISHO: Februari 21; Wizara ya afya ya China imeripoti visa vipya 397 nchini humo pamoja na vifo vipya takribani 109 huku vifo 106 kati ya hivyo vikitokea katika mkoa wa Hubei pekee.

Virusi vya Corona hadi sasa vimekwishapoteza maisha ya watu wapatao 2,360 duniani kulingana na takwimu rasmi huku visa takribani 77,812 vikiripotiwa ulimwenguni kote.

SASISHO: Februari 20; Vifo vipya 115 vimeripotiwa Hubei nchini China huku visa vipya 411 vikiripotiwa mkoani humo.

Idadi ya visa vyote ulimwenguni imefikia 76,188 hadi sasa huku watu wapatao 2,245 wakipoteza maisha.

Wagonjwa takribani 11,728 wako mahututi huku wagonjwa wapatao 15,827 wakipata nafuu. na kuruhusiwa kutoka hospitalini.

SASISHO: Februari 19; Hubei nchini China imeripoti vifo vipya 108 kutokana na virusi vya Corona huku visa vipya takribani 349 vikiripotiwa mkoani humo.

Kulingana na takwimu rasmi, jumla ya visa 75,640 vimeripotiwa ulimwenguni huku idadi ya waliokufa kutokana na virusi vya Corona ikifikia 2,121 hadi sasa.

SASISHO: Februari 18; Vifo vipya 132 pamoja na via vipya 1,693 vimeripotiwa Hubei nchini China huku maeneo mengine ndani ya China yakiripotiwa kuwa na visa vipya 48 pamoja na vifo vipya viwili (2).

Watu wapatao 2,010 wamekufa kutokana na virusi vya COVID-19 huku watu zaidi ya 75,000 wakibainika kuwa na maambukizi ya virusi hivyo ulimwenguni.

SASISHO: Februari 17; Hubei imeripoti visa vipya 1,807 pamoja na vifo vipya 93 kutokana na virusi vya COVID-19.

Nchini China, nje ya mkoa wa Hubei vimeripotiwa vifo vipya vitano (5) pamoja na visa vipya 79, kulingana na wizara ya afya nchini humo.

Mpaka sasa, watu takribani 1,873 wamekufa kutokana na virusi hivyo huku visa zaidi ya 73,000 vikiripotiwa duniani kote.

SASISHO: Februari 16; Hubei imetangaza vifo vipya 100 kutokana na virusi vya COVID-19.

Pia, visa vipya 1,933 vimeripotiwa mkoani humo huku idadi ya walioambukizwa virusi hivyo ikipindukia 70,000 ulimwenguni kote.

SASISHO: Februari 15; Hubei imeripoti ongezeko la vifo 139 ambavyo ni sawa na ripoti ya siku iliyopita pamoja na visa vipya 1,843 mkoani humo huku jumla ya waliokufa kutokana na virusi vya Corona (SARS-CoV-2) wakifikia 1,666.

SASISHO: Februari 14; Hubei imetangaza vifo vipya 139 pamoja na visa vipya 2,420 vya COVID-19.

Ripoti ya leo inapelekea ongezeko la visa vyote ulimwenguni kufikia 66,887 huku idadi ya waliokufa kutokana na virusi hivyo ikifikia 1,523.

SASISHO: Februari 13; Mkoa wa Hubei nchini China umetangaza vifo vipya takribani 116 pamoja na visa vipya 4,823 mkoani humo.

Idadi ya visa vyote nchini China imefikia 64,627 huku idadi ya visa vyote ulimwenguni ikifikia 65,210.

Jumla ya watu 1,483 wamekufa kutokana na virusi hivyo nchini humo na 1,486 duniani kote.

SASISHO: Februari 12; Mkoa wa Hubei nchini China umetangaza vifo vipya 242 kutokana na virusi vya Corona.

Visa vipya 14,840 vimeripotiwa mkoani humo na kufikisha visa 60,016 duniani kote.

Idadi ya waliokufa kutokana na virusi hivyo kwa mujibu wa ripoti rasmi mpaka sasa wamefikia 1355 ulimwenguni huku idadi kubwa ya vifo hivyo vikitokea nchini China.

SASISHO: Februari 11; Mkoa wa Hubei umeripoti vifo vipya 94 pamoja na visa vipya 1,638.

Katika mkoa huo pekee, idadi ya vifo imeongezeka mpaka kufikia 1,068.

Kutokana na ongezeko la vifo 94, jumla ya vifo vyote mpaka sasa kutokana na virusi vya Corona ni 1,112 duniani kote huku watu takribani 44,754 ulimwenguni wakigundulika kuwa na maambukizi ya virusi hivyo.

SASISHO: Februari 11; Shirika la afya duniani WHO limetangaza kuupatia jina jipya ugonjwa mpya unaotokana na virusi vya Corona.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO, ugonjwa huo sasa utaitwa COVID-19.

SASISHO: Februari 10; Idadi ya vifo kutokana na virusi vya Corona yafikia 1013 ulimwenguni.

Mamlaka ya afya ya mkoani Hubei imeripoti kuwa watu 103 zaidi wamekufa kwa ugonjwa wa Corona katika mkoa wa Hubei Jumatatu, na kuongeza idadi ya vifo katika mlipuko wa janga hilo kufikia 974 mkoani humo.

Visa vipya takribani 2,097 vimeripotiwa katika mkoa huo.

SASISHO: Februari 9; Mkoa wa Hubei nchini China umeripoti visa vipya 2,618 pamoja na vifo vipya 91.

Kutokana na ongezeko hilo, idadi ya vifo duniani kote imefikia 904 huku zaidi ya watu 40,000 wakibainika kuwa na maambukizi.

SASISHO: Februari 8; Idadi ya vifo imeongezeka mpaka kufikia 719 huku zaidi ya watu 34,000 wakigundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkoa wa Hubei nchini China ambao ndiyo kitovu cha mlipuko wa virusi vya Corona umeripoti vifo vipya 80 pamoja na visa vipya 2,841.

SASISHO: Februari 7; Idadi ya waliokufa kutokana na virusi vya Corona yaongezeka mpaka kufikia 638.

China imethibitisha vifo vipya 73 pamoja na visa vipya 3,143 kwa siku ya jana pekee. Vifo vipya 69 pamoja na visa vipya 2,447 ni katika mkoa wa Hubei pekee.

SASISHO: Februari 6; Mkoa wa Hubei nchini China umeripoti vifo vipya 70 na visa vipya 2,987 vya virusi vya Corona.

Idadi ya jumla ya vifo vyote imepanda mpaka kufikia 564 huku visa vyote vikiongezeka mpaka kufikia 27,648 duniani kote. Wagonjwa wapatao 911 wamepata nafuu.

SASISHO: Februari 5; Jumla ya visa vote kutokana na virusi vya Corona yafikia 23,858 mpaka sasa huku idadi ya vifo ikifikia 492 kutoka 426 ikiwa ni ongezeko la vifo 66.

China bara pekee ni jumla ya visa 23,648 na idadi ya vifo ni 490.

SASISHO: Februari 4; Ripoti mpya yaonesha ongezeko la visa mpaka kufikia 19,852 duniani kote huku idadi ya vifo ikifikia 426 mpaka sasa.

Jumla ya visa 19,668 pamoja na vifo takribani 425 ni ndani ya China bara pekee.

SASISHO: Februari 3; Watu karibu 17,500 wamekwisha thibitika kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona duniani kote huku watu takribani 362 wamepoteza maisha kutokana na virusi hivyo.

SASISHO: Januari 30; Idadi ya vifo kutokana na virusi vya Corona yafikia 169.

Hili ni ongezeko la vifo 37 toka ripoti ya mwisho ya vifo 132 ilipotoka huku vikiripotiwa visa vipya zaidi ya 1000. Vifo 162 kati ya hivyo ni kutokea mkoa wa Hubei pekee.

SASISHO: Januari 28; Idadi ya vifo kutokana na virusi vya Corona imeongezeka kutoka 106 hadi 131.

Taarifa ya vifo vipya 25 ni kutoka katika mkoa wa Hubei pamoja na visa vipya takribani 840 kwa siku ya jana pekee (Januari 28).

SASISHO: Januari 27; Idadi ya vifo kutokana na virusi vya Corona (Coronavirus) imekwisha fikia 106 hivi sasa kutoka idadi iliyoripotiwa mara ya mwisho ya 82.

Mkoa wa Hubei, China pekee umeripoti visa vipya takribani 1291 na vifo vipya 24.

Wagonjwa wapatao 690 wana hali mbaya zaidi.

SASISHO: Beijing, China imetangaza kifo cha kwanza kabisa katika jiji hilo kutokana na kirusi cha Corona, mwanamume wa miaka 50 aliyekuwa amesafiri kwenda Wuhan tarehe 8, Januari na kurejea jijini Beijing tarehe 15. Idadi ya vifo imefikia 82.

SASISHO: Kifo kingine kimeripotiwa kutokana na kirusi cha Corona katika mkoa wa Hainan nchini China. Hicho ni kifo cha kwanza kabisa katika mkoa huo. Jumla ya vifo kutokana na kirusi hicho ni 81 mpaka sasa.

SASISHO: Idadi ya vifo nchini China kutokana na virusi vya Corona imeongezeka na kufikia 80 mpaka sasa huku idadi ya wenye maambukizi ikifikia zaidi ya 2700 ikijumuisha Hong Kong, Macau pamoja na Taiwan.
mbona idadi ya wafu ndogo sana. kumbe kawaida tu
 
Kawaida tu,inazidiwa Hadi na kipindupindu banah..
mbona idadi ya wafu ndogo sana. kumbe kawaida tu
nyi nanyi fateni uzi kwa mtililiko mpk chini muone
toka nipate akili sijawai ona ugonjwa wa mlipuko unaosambaa kwa kasi km huu na kuua watu wengi kwa muda mchache hivi halafu mpk ss mataifa hayajui yafanyaje
yaani
hayajui jinsi gani ya kuzuia kusambaa
hayajui hata mataifa mengne yameupata vp
hawajui tiba yake
hawajui kinga yake
na hawajui lini watapata kinga /dawa

halafu mnasema eti kawaida tu wakati hayo mafua ya ndege hayafui dafu kwa ugonjwa huu hata EBOLA cha mtoto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We ndo be smart
Sio kila kitu unahisi utakavyo
Jamaa kakuelezea kimakini sana ila huelewi, shida ni ww

Sent using Jamii Forums mobile app
Kaeleza nini ? Hebu dadavua , kwamba kitoweo mtumie tokea miaka ya 30 huko kije kilete madhara 2020 ?? Almost miaka 100 ??? And you are buying into that idea ???

Alafu sio mtu mmoja n taifa, mfano wake ungekua na maana kama angeathirika mtu mmoja tu , taifa Hilo Hilo waathirika Zaid ya watu 70000, in space of two months, kwann wasidhurike muda woooote huo ?? Be smart like your smartphone bro

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pengine popo walipata ugonjwa ambao hawakuwahi kuupata kabla ambapo ugonjwa huo ukikutana na mwili wa bina adamu unasababisha madhara kama tunayoyaona sasa Nimejaribu tu kueka sawa ila sija maanisha maana hata mm naamini kuna uwezekano wa maradhi ya maabara.....

Sent using Jamii Forums mobile app
Hili ni wazo lako , na kama wamepata ugonjwa ambao hawakui kuupata , hata huo utakua man made , Mungu haumbi tena , alishamaliza , kiumbe kipya kinachokuja chenye uhai n mikono ya binadamu... Mengine hua n genetic modified yaweze kua lethal zaid

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nyi nanyi fateni uzi kwa mtililiko mpk chini muone
toka nipate akili sijawai ona ugonjwa wa mlipuko unaosambaa kwa kasi km huu na kuua watu wengi kwa muda mchache hivi halafu mpk ss mataifa hayajui yafanyaje
yaani
hayajui jinsi gani ya kuzuia kusambaa
hayajui hata mataifa mengne yameupata vp
hawajui tiba yake
hawajui kinga yake
na hawajui lini watapata kinga /dawa

halafu mnasema eti kawaida tu wakati hayo mafua ya ndege hayafui dafu kwa ugonjwa huu hata EBOLA cha mtoto

Sent using Jamii Forums mobile app
vipi mbona unatokwa povu mkuu, we tulia uugue corona, na inakuja
 
Mkuu tusizunguke sana katika jambo ili..
Nini msimamo wako juu ya chanzo cha ugonjwa huu?, ni silaha za kibaiolojia ama ni moja ya janga la asili tu kama yalivyo mengine?.

Sent using Jamii Forums mobile app
Si janga la asili , labda nikuulize , Kwani Mungu bado anaendelea na uumbaji ??

Hawa wadudu ni mikono ya binadamu, wanafanya genetic modifications wanayaachia , shida inakua kama hivi.... Kuna kitabu kama nikikumbuka nitakileta hapa..kinahusu Mossad..shirika la kijasus la Israel.. virusi vya Ebola walikua navyo kabla hata havijawahi reportiwa popote dunia kama vimeleta maafa , na hata hapa naamini Wana magonjwa mengine mengi tu deadly na lethal kuliko hata huu..ni swala la muda tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nyi nanyi fateni uzi kwa mtililiko mpk chini muone
toka nipate akili sijawai ona ugonjwa wa mlipuko unaosambaa kwa kasi km huu na kuua watu wengi kwa muda mchache hivi halafu mpk ss mataifa hayajui yafanyaje
yaani
hayajui jinsi gani ya kuzuia kusambaa
hayajui hata mataifa mengne yameupata vp
hawajui tiba yake
hawajui kinga yake
na hawajui lini watapata kinga /dawa

halafu mnasema eti kawaida tu wakati hayo mafua ya ndege hayafui dafu kwa ugonjwa huu hata EBOLA cha mtoto

Sent using Jamii Forums mobile app
Ebola inachinja acha utani , sema huu unasambaa kama umeme

Sent using Jamii Forums mobile app
 
UPDATE: Iran imeripoti visa vipya vinne (4) pamoja na vifo vipya vinne (4). Jumla, visa 47 pamoja na vifo 12 vimeripotiwa hadi sasa huku vyanzo vingine vikidai kuwa idadi ni kubwa zaidi.
 
NEWS ALERT: Iranian lawmaker claims at least 50 people have died of coronavirus in the city of Qom; the official death toll stands at 12. [ILNA]

The lawmaker added that he has urged the minister of health to quarantine the city. ILNA reports that, last night alone, 7 people in Qom died of coronavirus.
 
UPDATE: Italia

Visa vipya 38 vya COVID-19 vimeripotiwa nchini humo na kufikisha jumla ya visa 193 nchi nzima huku wanne (4) wakipoteza maisha hadi sasa kutokana na virusi hivyo.
 
UPDATE: Bahrain imeripoti kisa cha kwanza cha COVID-19 nchini humo. Kisa hicho kikiwa ni raia wake aliyerejea nchini humo akitokea nchini Iran.

Wizara ya afya nchini humo imetangaza kuwa, wale wote wenye dalili za homa, kukohoa na kushindwa kupumua vizuri, kuhakikisha wanajitenga na wengine na kisha kupiga simu namba ya dharura (444).
 
Ebola inachinja acha utani , sema huu unasambaa kama umeme

Sent using Jamii Forums mobile app
mi nafikiri huu ugonjwa pia unaweza kuwa ni wa mda tu kama magonjwa mengine ya mlipuko, tatizo dunia ya sasa media ndo zinafanya mambo yanakuzwa. bila media tatizo lingeisha kimya kimya, mbona epidemics zinatokea miaka mingi na kuisha zenyewe. yani pia ni mabadiliko ya hali ya hewa, kuna baadhi ya bacteria na virus huwa wanaishi kwenye viipindi tofauti vya hali ya hewa, hali ya hewa ya kipindi hicho ikiisha na vyenyewe vina potea. nahisi pia ndo maana hii kitu haionekani africa kwa sababu ya hali ya hewa iko tofauti. tropical na equitor kuna joto sana, flue virus hawapendi kuishi kwenye joto.
 
UPDATE: Korea Kusini imeripoti kifo kipya nchini humo kinachohusishwa na COVID-19. Mpaka sasa, idadi ya waliokufa kutokana na virusi vya COVID-19 nchini humo imefikia 8.
 
ila pia nahisi kwa waafrika tulivo less protected, wale jamaa wameisha utest huu ugonjwa kwa waafrika kitambo na wameona waafrika hawaugui, na siamini kama ni kweli huu ugonjwa haujawahi kujaribishwa huku, wachina ni wajanja sana na wako fasta fasta sana katika kutrace tatizo, so kumuambukiza mtu mweusi ili waone reaction ni option ambayo lazima waifanye kwa siri bila kukwambia
 
mi nafikiri huu ugonjwa pia unaweza kuwa ni wa mda tu kama magonjwa mengine ya mlipuko, tatizo dunia ya sasa media ndo zinafanya mambo yanakuzwa. bila media tatizo lingeisha kimya kimya, mbona epidemics zinatokea miaka mingi na kuisha zenyewe. yani pia ni mabadiliko ya hali ya hewa, kuna baadhi ya bacteria na virus huwa wanaishi kwenye viipindi tofauti vya hali ya hewa, hali ya hewa ya kipindi hicho ikiisha na vyenyewe vina potea. nahisi pia ndo maana hii kitu haionekani africa kwa sababu ya hali ya hewa iko tofauti. tropical na equitor kuna joto sana, flue virus hawapendi kuishi kwenye joto.
Trump alisema mpaka mwezi April utakua umeisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ila pia nahisi kwa waafrika tulivo less protected, wale jamaa wameisha utest huu ugonjwa kwa waafrika kitambo na wameona waafrika hawaugui, na siamini kama ni kweli huu ugonjwa haujawahi kujaribishwa huku, wachina ni wajanja sana na wako fasta fasta sana katika kutrace tatizo, so kumuambukiza mtu mweusi ili waone reaction ni option ambayo lazima waifanye kwa siri bila kukwambia
Kwa Muingiliano ulipo kati ya Africa na China , waafrica wanao enda huko kibiashara n wengi Sana , mpaka sasa tuko salama , Hilo eneo lenyewe la Huwan..waafrica wako kibao ila mpaka sasa wako salama wote , huenda ukatupita pembeni huu ugonjwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom