Fahamu vitu vinavyotofautisha gharama za ujenzi kwenye majengo yenye kufanana mchoro

Fahamu vitu vinavyotofautisha gharama za ujenzi kwenye majengo yenye kufanana mchoro

Hii kitu naona mafundi wameshaachana nayo mda sana, niliona jamaa mmoja akifitisha geti ndio alikuwa anatumia sana kuweka level, na ni very precise!!!
kama huna dumpy level hiyo ni good option esp. kwa mafundi wetu wa uswazi
 
Hapa nitaelezea Sababu za msingi zinazosababisha majengo yanayofanana kujengwa kwa gharama tofauti.

Tuzungumzie mchoro wa nyumba ya vyumba vitatu vya Kulala kimoja kati ya hivyo ni master bedroom, sitting room, dining, kitchen ,public toilet na store.
Mchoro aliununua ndugu anaitwa Juma, baada ya Juma kununua Alitoa copy akawapa majirani zake wawili Hasani na John.

Hawa wote walijengewa na fundi mmoja ambae ni mimi. Lkn Kila mtu kutumia gharama tofauti kusimamisha boma.

SABABU ZA MSINGI ZA KUFANYA GHARAMA ZA UJENZI ZITOFAUTIANE :

1. location
2. Uimara
3.land type. (slop au tambalale)
4.soil type
5.nyakati.

HAPA NITAZUNGUMZIA UIMARA
Msingi wa nyumba imara utajengwa Kama ifuatavyo.
. Utachimbwa kwenda chini urefu WA mita moja au zaidi.
. Utaanza na zege yenye ratio nzuri kabla ya kujenga tofali
.Utajengwa kwa tofali imara
.Utawekewa Beam yenye kusukwa nondo na ratio nzuri
.Utamwagiliwa maji ya kutosha.
ILI HAYA YOTE YAFANYIKE LAZIMA UMPATE FUNDI MZURI.

Juma aliomba nyumba yake nimjengee kwa viwango hivyo, ndio maana nilitumia tofali nyingi,cement nyingi, nondo nyingi, mchanga mwingi, kokoto nyingi, ring za kutosha, maji mengi nk. Ktk kujenga msingi.

John alisema uwezo wake mdogo , yeye alihitaji tuchimbe futi moja kwenda chini baada ya hapo tujenge tofali, hakuishia hapo pia alisema tusiweke Beam.

Kilichotekea ni utofauti wa Tshs zaidi ya million nne kati ya hiyo misingi miwili.

Kiufupi Juma alitumia 6mil
John Tshs 2.8mil
Hasani Tshs 4mil.

Kilichotofautisha ni uimara WA kujenga msingi. Hawa wote ni majirani.

Mpaka tunamaliza boma Juma alitumia 18m
John 7m
Hasani 12m.
Nyumba zote hizi zikipigwa rangi vizuri hutoweza kujua madhaifu ya awali mpaka pale utakapoanza kuona nyufa (expansion joint)

Hoja yangu hapa ni kwamba unapotokea mjadala wa gharama za ujenzi LAZIMA tuzingatie vitu mhimu vinavyosababisha gharama kuwa kubwa au ndogo.

Ushauri.
1.Tusipende kukimbilia kununua nyumba wakati hujui ilijengwa kwa viwango vipi.
2.Jenga nyumba imara ogopa vya Bei cheee
3.Nyumba kuijenga si lelemama, ili kumudu anza mdogomdogo. Ukiwa na 5m anza hata msingi.

Ukihitaji fundi, usisite kunitafuta, Hakina utaenjoy service yangu.
0655173113


UPDATES
tuendelee na mjadala wetu. Hapo awali tulijadili jinsi namna gani uimara wa nyumba unavyoathiri gharama za ujenzi. Leo tujadili namna location inavyoathiri gharama za ujenzi.

NAMNA LOCATION INAVYOSABABISHA GHARAMA ZA UJENZI KUWA TOFAUTI.

Mungu aliumba ardhi ktk mionekano tofauti. Kuna tambalale, milima na mabonde.
Ujenzi ktk Eneo tambalale unagharama nafuu kulinganisha na Eneo lenye slope . Lakini pia ujenzi wa Eneo tambalale lililoko Chanika mkoni DSM Unaweza kuwa na gharama tofauti na ujenzi wa Eneo tambalale lililoko msasani mkoani DSM. Hivyo hivyo ujenzi wa DSM unagharama kubwa kuliko ujenzi wa Mbeya.

SABABU ZA KUTOFAUTISHA GHARAMA KATI YA ENEO TAMBALALE NA LENYE SLOP.

sanasana hapa kimbembe huwa ktk kujenga msingi wa nyumba.

Msingi uliotumia tofali 1500 katika eneo tambalale, msingi huohuo ukitaka kuujenga ktk eneo lenye slope unaweza kutumia tofali 2300 au zaidi kulingana na ukali wa slope.
Tukumbuke kwamba Kwa kadri tofali zinavyoongezeka ndivyo na material mengine yanavyozidi kuongezeka kitu ambacho hupelekea kuongezeka kwa gharama za fundi. Si ajabu kumalizia 10mil ktk msingi wa nyumba ya Vyumba vitatu ktk Eneo LA slope.

Hivyo basi kama hutaki kutumia gharama kubwa kwenye ujenzi epuka kununua viwanja vilivyo na slope.

Jambo lingine linaloathiri ktk location ni upatikanaji wa material.
Mfano mtu anaejenga mbezi beach atanunua tani 18 Za mchanga zaidi ya 450.000 Tshs wakati mtu wa Chanika atanunua Kwa 220,000tshs.

Pia boma utakalojenga kwa 8mil Mbeya, DSM utalijenga Kwa zaidi ya 15mil. Sababu Mbeya tofali ni cheap, labour ni cheap nk.

Kwa ujenzi imara na wakisasa tutafutane 0655173113

Hongera kwa elimu uliyoitoa kuhusiana na baadhi ya mambo ya msingi kuhusu ujenzi.Asilimia kubwa ya watu wanaogopa kuanza ujenzi moja ya sababu ikiwa ni kukosa uelewa kuhusu mchakato mzima wa ujenzi.

Mbali ya elimu ya darasani,elimu itokanayo na uzoefu kazini ni muhimu sana jambo ninaloliona kwako. Japo baadhi wameonekana kukushambulia ila kwa mtazamo wangu uzoefu ulionao ni muhimu sana hasa hasa katika fani ya ujenzi.
Ushauri wangu kwako ni kuendelea kujielimisha kwani kutokana ukuaji wa teknolojia zipo mbinu mpya za ujenzi zenye kupunguza gharama za ujenzi.

Ushauri wangu kwa wanaotarajia kujenga na wataalam wa ujenzi, wasifanye mambo kwa mazoea kwani zipo style nyingi za ujenzi zenye kutumia gharama ndogo kwa mfano matumizi ya interlocking block,semi prefabricated slab(hii ni aina mpya ya ujenzi wa slab(jamvi) yenye kutumia nondo kidogo na zege kidogo bila kuathiri ubora).

Pia ningependa kushauri wengi wetu tujenge tabia ya kuwatumia watalaamu katika hatua za mwanzo kabla ya kuanza ujenzi. Tumia wataalam kupata ushauri na wakuandalie ramani kulingana na mahitaji yako kwani hii inaweza kukusaidia kupunguza gharama zinazoweza kujitokeza baadae.

Mwisho kabisa kwako fundi naomba unieleweshe tiles nzuri zenye ubora ni zipi? Bei yake ikoje? Na katika box moja zinakuwa tiles ngapi na size gani?

Ahsante.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nondo mbili?? Nondo mbili wamezifungaje hao mafundi..
Kitaalamu ground beam au beam yoyote inahtaji angalau nondo 4 za kuanzia mm 12,kwenda mbele.. Kwa nn ziwe nondo 4..
Beam nyingi znazosukwa huwa ni mstatili au mraba.. Na mara nyingi hayo maumbo huwa yana pembe 4,kitaalamu kwenye pembe ya beam ndo eneo ambalo linakua zaidi lipo hatarini kwenye kupatwa na nyufa. Hvo wataalam wanshauri angalau kwenye kila pembe ya Beam ipate nondo moja. Hvo ukiwa na beam ya mstatili, au Mraba lazma uwe na nondo 4 znazocover eneo lote la beam..

Sababu ya pili ni kuwa ili uwezd kumaintain shape ya beam yako, pamoja na cover (uwazi unaoachwa kati ya outer surface ya beam na nondo) unatakiwa uekwe nondo 4 ili kila pande iwe na cover.. Sasa unapoeka nondo mbili inakua vigumu kuipata shape ya pembe 4 ya beam yako

Sent using Jamii Forums mobile app

Well explained, ila in some cases beams inawezekana kutumia nondo 3, mbili chini na moja juu zikizungushiwa stirups.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwa elimu uliyoitoa kuhusiana na baadhi ya mambo ya msingi kuhusu ujenzi.Asilimia kubwa ya watu wanaogopa kuanza ujenzi moja ya sababu ikiwa ni kukosa uelewa kuhusu mchakato mzima wa ujenzi.

Mbali ya elimu ya darasani,elimu itokanayo na uzoefu kazini ni muhimu sana jambo ninaloliona kwako. Japo baadhi wameonekana kukushambulia ila kwa mtazamo wangu uzoefu ulionao ni muhimu sana hasa hasa katika fani ya ujenzi.
Ushauri wangu kwako ni kuendelea kujielimisha kwani kutokana ukuaji wa teknolojia zipo mbinu mpya za ujenzi zenye kupunguza gharama za ujenzi.

Ushauri wangu kwa wanaotarajia kujenga na wataalam wa ujenzi, wasifanye mambo kwa mazoea kwani zipo style nyingi za ujenzi zenye kutumia gharama ndogo kwa mfano matumizi ya interlocking block,semi prefabricated slab(hii ni aina mpya ya ujenzi wa slab(jamvi) yenye kutumia nondo kidogo na zege kidogo bila kuathiri ubora).

Pia ningependa kushauri wengi wetu tujenge tabia ya kuwatumia watalaamu katika hatua za mwanzo kabla ya kuanza ujenzi. Tumia wataalam kupata ushauri na wakuandalie ramani kulingana na mahitaji yako kwani hii inaweza kukusaidia kupunguza gharama zinazoweza kujitokeza baadae.

Mwisho kabisa kwako fundi naomba unieleweshe tiles nzuri zenye ubora ni zipi? Bei yake ikoje? Na katika box moja zinakuwa tiles ngapi na size gani?

Ahsante.


Sent using Jamii Forums mobile app
Kuhusu ubora wa tiles inategemeana na toleo. Mfano kuna tiles za china ni imara na zimenyooka sana ,huwa hazipauki. Pia Kuna za kichina zinazopauka mapema. Tiles ambazo mara nyingi za uhakika ni za spain ambazo bei yake huanzia @45000 kwa box.
Kuhusu idadi ya tiles kwa box inategemeana na size (ukubwa) wa tiles . Cha Msingi angalia coverage area ya tiles kwa box. Mfano kunazinazo cover Sqm 0.6 - 1.5sqm
 
Kuhusu ubora wa tiles inategemeana na toleo. Mfano kuna tiles za china ni imara na zimenyooka sana ,huwa hazipauki. Pia Kuna za kichina zinazopauka mapema. Tiles ambazo mara nyingi za uhakika ni za spain ambazo bei yake huanzia @45000 kwa box.
Kuhusu idadi ya tiles kwa box inategemeana na size (ukubwa) wa tiles . Cha Msingi angalia coverage area ya tiles kwa box. Mfano kunazinazo cover Sqm 0.6 - 1.5sqm

Ahsante mkuu, kwa hio bei ya 45,000/=@box inaweza kucover sqm ngapi? Iwapo size ya tile ni 60cmx60cm au size nyingine?




Sent using Jamii Forums mobile app
 
upana wa bati linalotoka nje ya ukutu,vipimo standard vya kwenye ramani ni fut 2 hadi cm 80 na kwenye gables isipungue futi moja na isizidi cm 50
 
Mleta mada nakupongeza kwa kuipenda kazi yako. Ila nakuomba pia uwe unatumia ushauri wa wataalamu wa ujenzi. Namaanisha uchote maarifa kwa Architects, Engineer na Quantity Surveyor. Mie nimesoma ujenzi na nimepitia maelezo yako naona kama hayajajitosheleza pengine ni kutokana na ufahamu wa kitaalamu. Kwa mfano, nyumba sio lazima iwe na ground beam, kuna sababu hupelekea iwepo au isiwepo.kwa hiyo wakati mwingine mnaongezea gharama za ujenzi zisizokuwa za lazima kwa kigezo/kauli mbiu ya nyumba imara

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli japo Mimi siyo mtaalamu wa ujenzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu embu tusaidie hili kitaalam kabisa, kwanini nyumba ikishapigwa plaster, during curing process nyufa ndogo ndogo sana hutokea kwenye plaster?.

Kumbuka nyufa hizi hazikuwepo kwenye tofali kabla plaster haijapigwa.

Naomba majibu ya kitaalam. Ni nyufa ndogo ndogo

Sent using Jamii Forums mobile app
kuna sababu kadhaa but ni ngumu kupata specific cause lakini kiujumla husababishwa na mchanganyo kua laini sana au kulikua na vumbi so wakati inakauka itakua na ile contraction and expansion kutokana na joto,pili maji machafu au ratio ya cement kuzidi au kupungua nk nk but kitu muhimu mchanga usiwe na vumbi na usiwe rojo sana pia plaster au zege lisimwagwe wakati wa jua kali na curing iwe mda wote
 
Boss jaribu kufanya utafiti kidogo, hizo nyumba zenye chimney mara nyingi huwa wanatumia kuni as a source of energy, sasa kwa nyumba zetu hizi nani anatumia kuni ndani!?, nafikiri zile kitchen ventilation za umeme ndio zinatufaa zaidi ya traditional chimneys.
Na wanaotumia mkaa ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gharama inategemeana na ukubwa wa Jengo, aina ya udongo unapojenga, Kuna slop au tambalale na mkoa unaojenga.
Je kwenye jengo la ukubwa huu gharama itakuwaje?
Vyumba vya kulala vitano.
Sebule mbili @ chini na juu
Location: village
Aina ya udongo mixed sand and clay

Landscape. Tambarare



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kurahisisha maelezo ili kutoa mwangaza wa hili jambo, tuchukulie haya mambo.

-Mkoa Dar.

-Udongo ni kichanga.

-Eneo ni tambarare.

-Ukubwa wa jengo ni square meter225(15m×15m).

-Nyumba ni ghorofa moja.

-Paa litaezekwa kwa Slab.

-Mtindo wa nyumba ni vyumba viwili(kimoja master), sebule, Public toilet na Kitchen, vitu vyote vitakuwa kwenye kila floor, kama ujenzi wa apartment hivi. (Hivyo ground floor itakuwa hivyo, na 1st floor itakuwa nayo hivyo hivyo). Hakuna complication, muundo wa kawaida au kizamani!!

-Ngazi inategemea, ama ziwe ndani kuunganisha ground floor na 1st floor au ziwe nje kuondoa mwingiliano kati ya ground froor na 1st floor)


Nimekupa picha hapo.

Nadhani ufafanuzi wako utakuwa na manufaa kwa watu wengi ambao wana viwanja vidogo lakini maeneo mazuri au kutaka kubadilisha fashion za ujenzi. Na hilo ndio lengo langu na kwa kuwa nimeona picha hapo juu katika huu uzi ukisimamia kazi ya ujenzi wa ghorofa, nikavutiwa kuuluza hayo.
Akijibu haya nami nitajifunza mengi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ok. Shukrani kwa maelezo mazuri mkuu. Ukifanya skimming kama nyufa za aina tajwa hapo juu zilikuwepo kwenye plaster zitaendelea kutokea?. Kama curing process ilisha isha?
kuna sababu kadhaa but ni ngumu kupata specific cause lakini kiujumla husababishwa na mchanganyo kua laini sana au kulikua na vumbi so wakati inakauka itakua na ile contraction and expansion kutokana na joto,pili maji machafu au ratio ya cement kuzidi au kupungua nk nk but kitu muhimu mchanga usiwe na vumbi na usiwe rojo sana pia plaster au zege lisimwagwe wakati wa jua kali na curing iwe mda wote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom