Faida 04 za kijana kuoa ukiwa na miaka 20

Faida 04 za kijana kuoa ukiwa na miaka 20

Wala hakuna tatizo, kwani wataishi maisha hayo hayo.

Tatizo ni mafunzo mabaya tunayowapa watoto pengine toka kwa wazazi au kwenye mitandao juu ya ueleo wa maisha. Kijana hataki kuoa mpaka ajiandae. Na kujiandaa kwa tafsiri ya mitandao inamaanisha awe na mjengo pengine na gari na kazi ya maana ya kuajiriwa. Wengine hutamka kabisa kuwa siolewi na mwanaume aliyeajiriwa serikalini katika kazi "A" au "B". Hizi ni fikra mbovu!

Anzeni maisha pamoja, mkiwa na kitanda kimoja, sufuria 4 na n.k mkajua kuna siku mnaweza lala njaa na siku za mafanikio. Yote mnayabeba pamoja.

Wengi nawafahamu wameoa mwaka wa kwanza chuo kikuu na mpaka leo maisha yanakwenda. Maisha ni wewe tu.
SAwa
 
Ukomavu wa utu uzima unaanza mtu akifikisha miaka 20. Utu uzima unaanza akifikisha miaka 13. Kimsingi mwenyezi Mungu hatambui kitu mnachokiita Teenagers/Adolescents au foolishage. Miaka 13~19 ni mtu mzima anayejianaa kuoa akihitimu 20s.

Ziko faida nyingi wazazi wakiwaandaa vijana wao kukomaa ili kufikia miaka 20 wawe na uwezo wa kuoa.

1: Ni umri sahihi wa ukomavu wa kijana kukaa na mke. Anaoa akiwa amekomaa bila kupitiliza.

2: Ana nguvu za kutosha kufanya masahihisho ya makosa akiwa bado anamwili wenye nguvu.

3: Akifikisha miaka 40, yaani mtu mzima mkomavu mtoto wake anakuwa na miaka 20. Mtu mzima.
Anawahi kutua majukumu ya malezi na kusomesha.

4: Anabaki na muda mwingi wa kuendelea kumfurahia mke wake ukubwani huku watoto wakiwa wameshajitegemea. Kumbuka wewe ni mwili mmoja na mkeo sio na watoto wako. Watoto ni wapitaji tu unepewa na Mungu uwavushe.

Ni hayo tu.
Du, uwezo wenu wa kufikiri ndio umefikia huku wakuu
 
kwa kusoma kama ulivoandika look so simple but in reality tunadanganyana why?

1. MATURITY
Umri wa miaka 20 kwa mtoto wa kiume anakua maturity "physical" but not ""Mentaly so hawezi kuhimili mikiki ya ndoa.
Umri wa Miiaka 20 tunategemea aoe kijana wa kike wa miaka 20 au chini ya hapo ambao kimtazamo akili zao wote hawa ni za kitoto bado hawawezi kupambanua mambo katika upana wa kufanya ndoa iwe "STABLE" matokeo ni kesi za kupigana, kuchitiana na utoto toto mwingi mwisho wa siku kuwapa mzigo wazazi hata kuachana.

2. ECONOMIC STABILITY
Kwa asilimia kubwa kwa vijana wengi wa kiume umri wa miaka 20 ndo kwaanza wapo chuo au wanajitafuta ukiachiliana mbali kupima uwezo wao wa kufua nazi kupimia nyenzo tofauti tofauti i mean wako PEAK in sexual drive...So my point is ni ngumu kukuta yupo kiuwezo kifedha wa kumtunza MKE na watoto kwa jamii yetu kama hii ya KITANZANIA.

3. LIFE EXPERIENCE and EXPOSURE
hahaha nimecheka kwa kuwa najua kuna watu wanaweza kuona kama sio point ya msingi lakini ina umuhimu wake..Taasisi ya ndoa kwa kijana wa kiume wa kitanzania ili uindeshe vizuri basi lazima uwe umepitia changamoto mbalimbali za kimaisha na kuweza kuzibakabili kimwili,kiakili na hata kiroho kuna kauzoefu flani lazima upate utaopima ujasiri na uwezo wa kutatua mambo kwenye maisha, sasa kwa kijana wa miaka 20 HAHAHAHA Ndo kwaaanza wengi akili zao zinakua zipo stage1 of maturity ni shida tupu alafu uje umpe ndoa asee ni vichekesho.

CONCLUSION
Kwangu mimi BIG NO kwa misingi na mifumo ya jamii zetu za kiafrika miaka 20 kwa kijana wa kiume kuingia kwenye NDOA.
Hizo point tatu ni muhimu ila ni mtu mwenyewe kuamua. Hayo ni matatizo ya wazazi sio watoto husika.
Du, uwezo wenu wa kufikiri ndio umefikia huku wakuu
Asante mkuu ila haya ni maarifa ya zamani sana.
 
Anaweza maisha nikufanya na sio kujaribu . Rafiki yangu wa sasa kakijana tu kanaitwa dogo ameoa 18 mke ana 17 wote walianza maisha hayo hapa mjini na wote waliajiriwa kama wafanya usafi wa kaanz akodogo kidogo wakasave sasa hivi wana kimgahawa chao kinaingiza ml 3 kwa siku kama hutaki acha wanapika chipsi kuanzia saa sita mpaka sanane usiku na amewaakiri wafanyakazi wakumsaidia kupeleka chipsi kutengeneza kachumbari hadi now mwenzako sio yeye . Maisha sio yakuogopa na uchaguzi
sawa
 
Back
Top Bottom