Faida na hasara za kuoa mwanamke msomi na mtumishi

Faida na hasara za kuoa mwanamke msomi na mtumishi

Mwamba maarifa yanapoishia ndio mwanzo wa kuangamia kwako.
#Hekima kutambua ufanye lipi kwa wakati fulani .. ukiwa na hii silaha Kuna matatizo huwa sio matatizo Hadi pale tunapoyatafsiri kwa mapana yetu binafsi😁😁
 
Ukioa mke msomi akaajiliwa akipangiwa dodoma ukimpigia video call usiku lazima uone kivuli chenye madevu au chenye kitambi kinavaa kondomu
[emoji16][emoji16][emoji1787][emoji1787]
 
Watoto wenu wa kike msiwasomeshe
Inasikitisha sana kiukweli kabisa kuna watu wameoa wanawake hawana elimu na mambo ni yale yale. Hii mentality tunayozidi kujijengea mi huwa naona inategemea na muhusika tu iwe msomi au hakwenda shule, all in all niishie hapo ila kusema kuoa mke ambaye hajasoma ni kujidanganya watu tuombe kupata kilicho chema tu.
 
Inasikitisha sana kiukweli kabisa kuna watu wameoa wanawake hawana elimu na mambo ni yale yale. Hii mentality tunayozidi kujijengea mi huwa naona inategemea na muhusika tu iwe msomi au hakwenda shule, all in all niishie hapo ila kusema kuoa mke ambaye hajasoma ni kujidanganya watu tuombe kupata kilicho chema tu.
Ieleweke si wote waliosoma wana hayo mapungufu wala si wote ambao hawajasoma ndo wake bora ila asilimia kubwa ya wanawake waliosoma wana hizo tabia. Unaweza ukawa na bahati ukapata aliesoma na akakufaa na unaweza ukawa na mkosi ukampata ambae hajasoma na akawa na changamoto vile vile.
 
Ieleweke si wote waliosoma wana hayo mapungufu wala si wote ambao hawajasoma ndo wake bora ila asilimia kubwa ya wanawake waliosoma wana hizo tabia.
Hapo sawa na bila shaka ndo umeweka kitu ambacho nilitaka kiwe hivyo kwamba kwendana na tafiti asilimia kubwa ndiyo imeonekana wasomi wana hizo shida. Umeeleweka.
 
At the same time wazazi wangu wa kike mashangazi etc wamesoma Sana na Bado ndoa zao nahisi ziko vzr japo siwezi kujua Siri za ndani ila hawajaachwa.
Ndoa ni makubaliano lakini wanaopenda kudhalilisha wanawake ndiyo wanaopiga kelele saaana.

Siku zote kuna wanaume wazuri na wabaya na wanawake wazuri na wabaya.
 
Nimeipenda na 3 ila ukweli mwanamke mzuri ni yule anamjua Mungu maana kwa uongozi wa neno la Mungu litamfanya ajue nafasi yake bila hivyo kuoa msomi asiyemjua Mungu ni sawa na kukumbatia bomu ambalo litalipuka na kukupata madhara maishani mwako.
 
Ni ndoto za wanaume wengi kuoa mwanamke mrembo na mwenye kipato ili wasaidiane kutengeneza familia bora ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba nzuri,kusomesha watoto kwenye shule bora n.k Hapo ndipo baadhi ya vijana hufikiria kuoa wanawake wasomi wenzao wenye kazi nzuri. Lakini kabla ya kufikiria kuoa mke msomi na mwajiriwa( hasa serikalini) ni vema ukajua faida na hasara zake.

Tukianza na faida
1. Mke mwajiriwa atakusaidia kuongeza kipato kwa maendeleo ya familia.
2. Pindi hali yako ya kiuchumi ikienda vibaya,familia inaweza isiyumbe na km itayumba basi ni kidogo.
3. Kazi/cheo cha mkeo kinaweza kuleta heshima fulani ndani ya familia.

Hasara zake:-
1. Kuna baadhi ya wanawake akichangia hela yake kununua kitu mfano kiwanja usishangae siku mkikosana akakudhalilisha kwamba kiwanja kanunua yeye,au nyumba kajenga yeye.

2. Wanawake waliosoma na wenye kazi wengi wao (SI WOTE ) huwa si watiifu kwa waume zao hasa ikitokea kipato chake ni kikubwa kuliko mme.

3. Jiandae na mivutano ya haki sawa. Kuna baadhi ya wanawake wasomi huigeuza ndoa kuwa sehemu ya kufanya uanaharakati. Hali hii inaweza kuibua mivutano ya mara kwa mara.

4. Ndoa kuongozwa na vichwa 2. Maandiko yanasema, "Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe" Efeso 5:23.

Kuna baadhi wanawake wakisha soma na kuwa na ajira nzuri hujipa mamlaka ndani ya nyumba. Baadala ya mume kuwa sauti ya mwisho kimaamuzi atataka yeye awe msemaji wa mwisho. "In nature"wanaume hatuko tayari kutawaliwa na mwanamke hapo inaweza kuwa chanzo cha ndoa yenu kusambaratika.

5. Ndugu wa mke kukudharau/ kutokupa heshima unayostahili hasa km familia yao ni ya kishua na wasomi.Hebu fikiria mkeo ni mkuu wa kitengo muhimu aafu wewe Mwalimu wa shule ya msingi( mfano tu), Usishangae kwa baadhi ya matukio ukawa wa mwisho kupewa taarifa. Tena usiombe iwe familia ya Kihaya( kidding).

6. Watoto wakigundua mama yao anapesa nyingi kuliko baba heshima yao kwako inaweza shuka na usishangae kuona shida zao nyingi wanamalizana na mama yao. Hapa usipokuwa makini unaweza jikuta km umetengwa ndani ya nyumba yako.
Kuna afande ni rafiki angu hiki kimemkuta,watoto hawana time nae kabisa.

7. Usitegemee neno pole na kazi au kupokewa mzigo utokapo kazini. Mwanamke mwenye kazi anajiona hata yeye ni mtafutaji. Hivyo anaweza asione sababu ya kukupokea kwani hata yeye katoka kutafta huo mkate.

8.Kuleta ubosi kitandani. Wanawake wengi wenye kazi na mabosi hujisahau na kuleta ubosi wao hadi nyumbani. Hivyo mkiwa faragha usishangae kauli za kibabe na wengi wao hawawezi kuwa romantic.

Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo mengi nimejifunza kwa brother angu aliyeoa Daktari mwenzake mwenye cheo kikubwa kuliko yeye na kwa baadhi ya wafanyakazi wenzangu.

NB: Niko tayari kurekebishwa.
 

Attachments

  • 1656855231872.jpg
    1656855231872.jpg
    181.9 KB · Views: 43
Oa mke yule unayemweza kumuhandle uliyemzoea . Sio kazi inambadilisha mke ni wewe unambadilisha mkeo aweke ukuta kwako.

Unaoa mtu unaye mwona anakufaa nyie mnaoa wanawake wanaowasaidia na ningumu kuwaheshimu .
Mwanaume huwa anapaswa kutunza familia yake sio kutunziwa ila siku hizi nyie mnataka muheshimiwe na mnatunziwa familia.

Wazazi wetu walikuqa fair na squre hutunzi familia unaheshimu mke na mke anakuheshimu
 
Smart911 Unasemaje katika hili
Kikubwa maelewano, though mahusiano mengi ambayo mwanamke yupo juu kielimu na kiuchumu kuna kadharau fulani hivi kapo kwenda kwa mwanaume wake...

Mpishano kidogo utasikia tafuta hela... hahahaha...
Kama yule aliyekuaga vice presidaa kipindi kilichopita...
 
Kikubwa maelewano, though mahusiano mengi ambayo mwanamke yupo juu kielimu na kiuchumu kuna kadharau fulani hivi kapo kwenda kwa mwanaume wake...

Mpishano kidogo utasikia tafuta hela... hahahaha...
Kama yule aliyekuaga vice presidaa kipindi kilichopita...
🤣🤣🤣Yule lazima ukae chini
 
Back
Top Bottom