Faidika na darasa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

Faidika na darasa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

1. Kukusikia na kukuona
2. Kutaka kujua siri ya wewe kujua mambo na uwezo wako wa kujibu maswali bila kuhamaki na ku-panic
3. Kuna tetesi wewe ni MTU mkubwa Sana hapa TZ kwa maana ya wadhifa kitaifa ( sina ushahidi)
4. Kukuskia kwa maskio yangu ukiongelea juu ya serikali ya JPM. Juu ya uchumi wake baada ya miaka minne iliyobaki.
5. Ushauri wako juu ya maswala la kitechnolojia, kwann swala la internet likua ishu TZ wakati ilipaswa kuwa compulsory ili kusaidia ujuzi wa ziada katika kazi na Elimu. Nini kifanyike?

1) Si muhimu sana.
2) Soma.
3) Si kweli.
4) Nisome tu humu JF.
5) Technolojia inaweza kuifanya nchi ipige hatua ndefu kwa haraka kuleta maendeleo kama itatumika vyema na inaweza ikaifanyia nchi ipige hatua kumi nyuma na kuwa ni janga badala ya neema kama haitowekewa mikakati ya matumizi sahihi.

Miundo mbinu ya kusambaza teknolijia tuliyonayo Tanzania ni bora kuliko nchi nyingi sana duniani. Tumpongeze sana Jakaya Kikwete kwa kufanya jitihada hizo hadi kufikia kusambaza "mkonga" wa taifa wa "fiber optics" Tanzania nzima. Ni hatua kubwa sana kwa nchi inayoendelea.

Watanzania bado hatutumii hata asilimia 5 ya uwezo wa huo mkonga.

Kulikuwa na mikakati mizuri sana iliyoanzia wakati wa Kikwete kuhusu teknolijia ya "internet":

1) Mitandao ya mawasiliano imesambazwa Tanzania nzima
2) Kikwete aliamuru shule zote ziwekewe umeme kama si wa gridi basi japo wa solar au njia nyingine, moja ya mafanikio yake ni REA., ili kila shule iweze kufundishika kwa mbali kupitia "internet".
3) Mkonga wa Taifa.
4) Super Computer (zipo)

Utaona kuwa miundo mbinu tayari kwa kiasi kikubwa kuhusu hilo la kuifanya "internet kuwa "compulsory".

Ni matumaini yetu kuwa awamu hii italitimiza lengo hilo kwani kwa kiasi kikubwa miundo mbinu yake ipo.
 
Kama una Akili timamu, na unajielewa/unaejielewa.

Pamoja ya kuwa umepewa Uhuru wa kuuliza Swali lolote.

Kuna baadhi ya Maswali wewe mwenyewe binafsi huwezi kuuliza.

Sio kwamba umezuiliwa,

Jibu ni kwamba huwezi kufikiria kuuliza Swali kama hilo

kwa hiyo kuuliza ni ujinga? wewe sio yeye! jata hilo hujui?
 
Siwezi kuamini hilo la Makonda katika kuchukia Waislam kwani sijaliona.

Alichosema simply kunamaanisha anaposimama yeye na Mungu yupo nae, hakumaanisha kuwa yeye ni "Mungu".

On the other hand, wewe umekuwa fataani kwa hilo la Makonda, kwanini?
Kwa hiyo kwa akili yako unaaamini kuwa Makonda ni kipenzi cha waislam? Na anawapenda sana waislam?
 
kwa hiyo kuuliza ni ujinga? wewe sio yeye! jata hilo hujui?

Qur'an 28:
55. Na wanapo sikia upuuzi hujitenga nao na husema: Sisi tuna vitendo vyetu, na nyinyi mna vitendo vyenu. Salamun Alaikum, Amani juu yenu! Sisi hatutaki kujibizana na wajinga.
 
Nafikiri hapa mnashindwa kuelewa.

Hizi ni Lugha tu.

Hiyo isikutishe, ni Lugha tu kama wanazotumia Viongozi, hasa Marais.

Mfano, Rais anaposema,

"Kesho tutaitisha Kikao, au kadha wa kadha"

Haina maana kwamba kuna Marais Watano, hapana. Ni Rais yule yule mmoja, na hii yote ni kutokuonesha Ubinafsi.

Kwahiyo hali kadhalika kwa Mwenyezi Mungu ni hivyo hivyo kwa sisi WAISLAM.

Mwenyezi Mungu anapotumia Sisi kwa Muislam mwenye Imani hawezi kuwa na shaka hata kidogo, kama kuna Mungu mwingine zaidi ya Allah, kwakuwa tunamwamini Mungu mmoja ambae ni Allah.

Mwenyezi Mungu Mmoja yeye ndie alieishusha/ameishusha QUR'AAN lakini hakuonesha Ubinafsi.

Hebu angalia mfano hai,

INNAA ANZALNAAHU QUR'AANAN ARABIYYA, ikiwa na maana:-

Hakika SISI tumeiteremsha QUR'AAN ya/kwa Kiarabu.

Hapo haina maana QUR'AAN imetereshwa na Miungu wawili, watatu, watano, Hapana.

Ni lugha tu.

Kuna Aya nyingi kwenye QUR'AAN Mwenyezi Mungu ametumia wingi, Kwahiyo usistuke
Utetezi Wa kimadrasa

[emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Qur'an 28:
55. Na wanapo sikia upuuzi hujitenga nao na husema: Sisi tuna vitendo vyetu, na nyinyi mna vitendo vyenu. Salamun Alaikum, Amani juu yenu! Sisi hatutaki kujibizana na wajinga.
kwani hata mende kulabua mavi chooni anaona kwake ni ujanja na hekima lakini sisi tunamuona zwazwa [emoji4]
 
  • Thanks
Reactions: PNC
kwani hata mende kulabua mavi chooni anaona kwake ni ujanja na hekima lakini sisi tunamuona zwazwa [emoji4]
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. T'A SIN MIM, (T'.S.M.)
2. Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.

 
FaizaFoxy nisaidie pa kuanzia kumsaidia kaka yangu,

Alipendana sanaa na binti wa kiislam na mama wa binti anampenda sana broh (Mkristo)

Kaka yangu alimsomesha huyu binti (namwita shem mpaka kesho) ada ya 2nd na 3rd year chuoni.

Kaka amejipanga kupeleka mahari upareni ghafla mwezi wa 6 Baba wa binti akamtafutia binti yake mchumba wa kiislam na wakaoana.

Alikuwa anamtishia binti kuwa akiolewa na Mkristo basi baba yake hatomtambua tena kuwa ni mwanae na hata salamu asimpe mpaka aingie kaburini

Sasahv binti anataka hata leo aridi kwa kaka yangu.

Hiyo ni Haki kweli? Ni jambo la Busara?

Cc: Babu na mjukuu
Ni haramu binti wakiislam kuolewa na mkristo, ila binti anaweza olewa na muislam.
 
Utetezi Wa kimadrasa

[emoji1] [emoji1] [emoji1]
Sasa mwenzio ameuliza ili kutaka kufahamu upande wetu.

Na SISI hatuna hiyana/khiyana, inabidi tujibu/tumjibu ilivyo kwa upande wetu.

Ndio, utetezi wa Kimadrassah, na wa Kiarabu pia.

Ili muweze kupata Akili:-

LA'ALAKUM TA'AQILUUN.

Ambao wahusika wakuu ndio SISI
 
Kwanza kabisa kazisome sababu zilizopelekea Waislam kutokufaulu wakati Ndalichako yupo NECTA.

Nnapenda wote wafaulu kwani wanaofaulu vizuri katika nyanja zote mwishowe hufaulu zaidi kwa kuwa Waislam, Huo ni ufaulu wa mwisho kwa mwanaadam.
Mbona mimi nilifaulu...
 
Kweli Mkuu kwa mama aliegraduate 1982 kumuuliza swali kama hilo ni ukosefu wa maadili.
Kama ni kweli FF now atakuwa miaka kama 55 hivi ebu sometime tumpe heshima yake kwa kumuuliza maswali ya kutujenga.
Kiongozi, Umenena
 
Naomba unijibu swali hili/ maswali haya vizuri..... ni hivi according to history tunasimuliwa kwamba Muhammad alikuwepo miaka ya 1500 iliyopita na Yesu miaka 2000 iliyopita.. lakini mpaka kwenye miaka 1000 na 1800 Africa tulikuwa hatuwajui hawa watu na tulikuwa tukiishi kwa kufuata mila zetu... na kuna babu na bibi zetu walizaliwa na kufa kati ya miaka hiyo ile hali hawajawahi kutamka shahada.... kwanin Muhammad na Yesu hawajawahi kufanya ziara ya nchi nzima kufikisha ujumbe wa Allah?? Mpaka pale imeshakuwa too late... nafikir unanielewa nikisema ni too late... kwani Muhammad hawezi kuja kwa ajili ya umma wote miaka hiyo alafu ujumbe wake utufikie 1000 years later tena pasipo yeye mwenyewe. Je nini hukumu ya wale walioshi katika karne ya 7 mpaka karne ya 17 wakiwa hawaujui msikiti? Hawamjui Mungu wa kweli na walikukwa wanafanya shirki... je ina maana watu hawa wote wataenda peponi kwa vile walikuwa hawajafikishiwa meseji so zambi zao zote sio valid?? Kama watu hao waliishi tu bila kufuata mila za waarabu, je kuna uspecial gani kwa sisi wa karne hii??? (Kuna jibu hili huwa siriziki nalo, kwamba Mungu huwaadhibu watu wale aliowafikishia ujumbe wake, kama hili ndio jibu lenye mantiki basi nitakuwa simuelewi Mungu.... anawezaje kuwaacha watu waendelee kufanya zambi wa upande mmoja wakati alishazikemea upande mwengine na hii inaleta contradiction). Unafikir kama sio njaa za waarabu na wazungu.. zilizowasukumia kuja Africa kutafuta mali ghafi... je kungekuwa na hizi dini kwa utitiri kiasi hiki? Vile vile ni kwanin waislamu walikuwa hawaweki msisitizo kwenye Elimu ya secular miaka ya nyuma tofauti na hivi sasa..ambayo imepelekwa waislamu wasomi hasa hasa Tanzania kuwa wachache tukilinganisha na idadi yao???
 
Back
Top Bottom