Familia: Hayati Magufuli aliongoza sala na nyimbo kabla ya kifo chake, alipakwa mafuta matakatifu. Pia aliombewa na Mufti

Familia: Hayati Magufuli aliongoza sala na nyimbo kabla ya kifo chake, alipakwa mafuta matakatifu. Pia aliombewa na Mufti

Kuna makosa aina mbili katika imani;

1) Kumkosea Mungu.

2) Kumkosea Mwanaadamu.

Kuna baadhi ya makosa mungu hasamehi mpaka ukamuombe msamaha uliemkosea kwanza, mfano Kulala na Mke/Mume Wa Mtu. Hapa kwa mungu kosa ni kuzini, kwa mwanaadamu umemchafulia haki yake inayotambulika mpaka mbinguni.

Msamaha kwa mungu unakubalika kwa kuapa kutokurudia tena kosa, sambamba na kurekebisha ulipo kosea (Mfano umefunga mtu gerezani kwa chuki, unapaswa kumwachia huru kwanza na kumpa fidia stahiki kwa kifungo ulichompa, halafu ndio unaomba msamaha kwa mungu na kuapa kutokurudia tena kufunga mtu asie na hatia - Ukiua mtu asie na hatia, unapaswa kukiri kosa na kuwaomba msamaha wana familia kwanza then unarudi kwa mungu kutubia na kuapa kutokurudia tena kuua).

Then walio dhulumiwa na kufungwa magerezani kwa chuki basi aliwaachia kabla ya kutubia dhambi zake?

Alikwenda kuwaomba msamaha familia za waliopoteza maisha yao kwa kivuli cha watu wasiojulikana?

Alirudisha haki za watu waliopewa kesi za uhujumu uchumi ili walipishwe fidia?

Alirudisha haki za watu waliobambikozwa KODI na MAKOSA iwe ya trafik barabarani n.k?
Kwahiyo wamasai kwa mila zao hawataingia mbinguni
 
Kumbe unaweza ukafanya ubaya wa kila aina alafu ukiumwa ukahisi kamba inaenda katika unatubu na kuingia mbinguni..
Kama ndio hivyo huyu Mungu atakuwa wa upendeleo sana..

28 Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.
29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.
30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.
31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Basi Yesu akawaambia, Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu.

Mathayo 21:28-31
 
Msemaji wa familia ya hayati Magufuli amesema mpendwa wao kabla ya kufa alibahatika kuongoza sala ya maombi ya kumuombea pamoja na nyimbo.

Pia alipata sakramenti ya toba na mafuta matakatifu.

Kadhalika Mufti wa Tanzania sheikh Zubeir alimuombea.

Katika maisha ya binadamu hii ni neema kubwa ambayo watu wengi huikosa wawapo kufani.

Binafsi sitaomboleza kwa kuvaa nguo nyeusi bali nitavaa nguo nyeupe kwa ajili ya shukrani kwa Mungu kwa maisha ya John hapa duniani.

Maendeleo hayana vyama!
Ilikuwaje Mufti tu ndiyo alikuwepo Kumuombea lakini Roman Catholic Cardinal Ruwa'ichi Thadeo hakuwepo au hata tu wa Madhehebu mengine? Nayasubiri Majibu ya Wanafamilia Ndugu au kama unaweza Kuwajibia pia itapendeza. Why Mufti was the Special One to him especially on his last Prayers before he died?
 
Hii sasa ni blah blah! Huyo mtu, siku zote alizokuwa anaumwa, alifichwa! Hizo SAKRAMENTI alipewa na wauguzi wake?
Waendelee kutuongopea hapa hapa Duniani tu. Huko alikoenda hakuna KUONGOPEANA!
barakoa3.jpg


Kazi ipo!​
 
28 Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.
29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.
30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.
31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Basi Yesu akawaambia, Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu.

Mathayo 21:28-31
Kumbeeeee.. basi Biblia inatufundisha tusiwe wema mpaka tukikaribia kufa ndio tutubu
 
Ilikuwaje Mufti tu ndiyo alikuwepo Kumuombea lakini Roman Catholic Cardinal Ruwa'ichi Thadeo hakuwepo au hata tu wa Madhehebu mengine? Nayasubiri Majibu ya Wanafamilia Ndugu au kama unaweza Kuwajibia pia itapendeza. Why Mufti was the Special One to him especially on his last Prayers before he died?
Alikuwepo Pengo na Padri Makubi.
 
Nje ya mada Padre kwanini kwenye ibada ya leo pale uwanjani askofu na mapadre walivaa majoho meupe badala ya zambarau kama tunavyowaonaga kwenye ibada za mazishi
Zambarau ni rangi ya maombolezo. Leo ilikuwa sikukuu ya kumwaga rais wetu alietutoka.

Tunachukulia kifo kwa mtazamo tofauti, ni Safari kutoka hatua moja kwenda nyingine nzuri zaidi. Hivyo badala ya kuhuzunika tunasherekea mwenzetu kutoka katika hatua moja ya chini kwenda hatua ya juu zaidi.
 
CCM ni waongo sana.
Wanataka kutuaminisha kuwa mwenyekiti wao ni mtu Safi,tusikumbushie makosa yake.
Angesema neno kuhusu uchaguzi mkuu wa 2020 na wasiojulikana tungeelewa.
 
Back
Top Bottom