nyundo2017
JF-Expert Member
- Sep 7, 2017
- 1,439
- 861
Kwahiyo wamasai kwa mila zao hawataingia mbinguniKuna makosa aina mbili katika imani;
1) Kumkosea Mungu.
2) Kumkosea Mwanaadamu.
Kuna baadhi ya makosa mungu hasamehi mpaka ukamuombe msamaha uliemkosea kwanza, mfano Kulala na Mke/Mume Wa Mtu. Hapa kwa mungu kosa ni kuzini, kwa mwanaadamu umemchafulia haki yake inayotambulika mpaka mbinguni.
Msamaha kwa mungu unakubalika kwa kuapa kutokurudia tena kosa, sambamba na kurekebisha ulipo kosea (Mfano umefunga mtu gerezani kwa chuki, unapaswa kumwachia huru kwanza na kumpa fidia stahiki kwa kifungo ulichompa, halafu ndio unaomba msamaha kwa mungu na kuapa kutokurudia tena kufunga mtu asie na hatia - Ukiua mtu asie na hatia, unapaswa kukiri kosa na kuwaomba msamaha wana familia kwanza then unarudi kwa mungu kutubia na kuapa kutokurudia tena kuua).
Then walio dhulumiwa na kufungwa magerezani kwa chuki basi aliwaachia kabla ya kutubia dhambi zake?
Alikwenda kuwaomba msamaha familia za waliopoteza maisha yao kwa kivuli cha watu wasiojulikana?
Alirudisha haki za watu waliopewa kesi za uhujumu uchumi ili walipishwe fidia?
Alirudisha haki za watu waliobambikozwa KODI na MAKOSA iwe ya trafik barabarani n.k?