Familia ya watu 10 kutumia milioni 3 kwa mwaka kwa manunuzi ya vyakula

Familia ya watu 10 kutumia milioni 3 kwa mwaka kwa manunuzi ya vyakula

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Kuna mama alituekeza maisha ya familia yake. Yeye na mume wake wamebarikiwa kupata watoto wanne. Walichukua jukumu la kulea watoto wawili wa ndugu waliofiwa na wazazi wao. Msichana wa kazi na kijana wa shamba.

Waliamua kuondoka mjini miaka mitano iliyopita baada ya kununua eneo la ekari tano kando ya mji na kujenga makazi yako. Wamefanikiwa kuzungusha uzio katika eneo lao lote. Ndani wanafuga kuku wa kienyeji 200 na bata 70. Wanalima mboga kama nyanya, vitunguu, mchicha, bilinganya, hoho nk.

Watoto wanasoma mjini, hivyo asubuhi kuna gari ya kupeleka watoto wanne wadogo shule kwani wakubwa wanasoma vyuoni na hurudi nyumbai wakati wa likizo. Usafiri wao ni pick up double cabin. Asubuhi inabeba pia na mboga za kupeleka sokoni baada ya watoto kushushwa shuleni.

Yule mama anasema tangu amehamia ‘kijijini’ kama anayoita mwenyewe, budget yake ya chakula imeshuka sana. Kila siku wanachinja kuku mmoja kutoka bandani wakiongeza na mboga kutoka katika bustani yao.

Vyakula anavyonunua ni sukari, mafuta ya kula, unga wa ngano, mchele na unga wa mahindi. Hata wakiamua kubadilisha mboga badala ya kuku hununua nyama ya ng’ombe au samaki kutokana na mauzo ya mboga kila siku.

Kulisha familia ya watu 10 kwa milioni 3 kwa mwaka na kila mtoto anapata mayai asubuhi, mchana kuna uhakika wa nyama na jioni chakula kizuri ni mafanikio.

Ninapenda kuishi mjini, zile harakati za umesikia uvivu wa kupika kuna chips mayai hapo mbele, kuna shishi kebab au kuna biryani mtaa wa pili, kuyakosa haya inahitaji moyo.
 
Labda kama wana chanzo kingine cha mapato

kuku 200 wa kienyeji-wanalishwa nini? mimi ninao 30 tu wananitoaga jasho ongeza bata 30 weeeeeee

hala kila siku wanakula kuku mmoja

siseme wewe ni muongo ,nahisi kuna some hiden information especial kwenye sources of income

all in al maisha ya kijijini ni mazuri kama ardhi yake ipo vizuri kwa mazao
 
labda kama wana chanzo kingine cha mapato
kuku 200 wa kienyeji-wanalishwa nini? mimi ninao 30 tu wananitoaga jasho
ongeza bata 30 weeeeeee
hala kila siku wanakula kuku mmoja
siseme wewe ni muongo ,nahisi kuna some hiden information especial kwenye sources of income
all in al maisha ya kijijini ni mazuri kama ardhi yake ipo vizuri kwa mazao
Nimeongelea budget yao ya chakula na matumizi ya eneo la ekari tano sijaongelea vipato vyao vingine.

Sijasema hata watoto wanne wanasoma shule gani inawezakeana wakawa wanasoma Feza na baba ni Mkurugenzi wa Shirika.
 
labda kama wana chanzo kingine cha mapato
kuku 200 wa kienyeji-wanalishwa nini? mimi ninao 30 tu wananitoaga jasho
ongeza bata 30 weeeeeee
hala kila siku wanakula kuku mmoja
siseme wewe ni muongo ,nahisi kuna some hiden information especial kwenye sources of income
all in al maisha ya kijijini ni mazuri kama ardhi yake ipo vizuri kwa mazao
Maisha ya kijijini ukijipanga unapiga ela sema kuishi kule kunahitani moyo.

Mimi nina ndugu yangu alihangaika town akaona umri unaenda hatoboi akaamua kurudi bush, shamba lipo zaidi ya heka 100 akachagua eneo analoweza limudu akapanda mikahawa mipya ya zamani akaondoa, hapo hapo anapandaga maharage na mahindi, akapanda miti heka za kutosha, akajenga banda anafunga ng'ombe 21 na mbuzi 14 na kuku wa kutosha.

Miti uwa anachagua eneo anauza kwa wanaokata mbao au kiwanda cha chai kwa ajili ya kukaushia majani ya chai wanamlipa kati ya 20 to 50 mls kutokana na ukubwa wa eneo maana wao wananunua kwa eneo sio idadi ya miti.

Ana ela anaishi vzuri ila bado mimi sijashawishika kuishi kijijini maana bado naona kuna mambo anayakosa.
 
Maisha ya kijijini ukijipanga unapiga ela sema kuishi kule kunahitani moyo.
Mimi nina ndugu yangu alihangaika town akaona umri unaenda hatoboi akaamua kurudi bush, shamba lipo zaidi ya heka 100 akachagua eneo analoweza limudu akapanda mikahawa mipya ya zamani akaondoa, hapo hapo anapandaga maharage na mahindi, akapanda miti heka za kutosha, akajenga banda anafunga ng'ombe 21 na mbuzi 14 na kuku wa kutosha.
Miti uwa anachagua eneo anauza kwa wanaokata mbao au kiwanda cha chai kwa ajili ya kukaushia majani ya chai wanamlipa kati ya 20 to 50 mls kutokana na ukubwa wa eneo maana wao wananunua kwa eneo sio idadi ya miti.
Ana ela anaishi vzuri ila bado mimi sijashawishika kuishi kijijini maana bado naona kuna mambo anayakosa.
Matajiri wengi ambao wanaweza kuhitajika na shughuli zao za kila siku mjini huishi vijijini.

Porini unahitaji mtaji kuishi, ukiwa na uwezo majambazi pia watakuweka tagert.

Ukijiweza katika eneo la ekari 30 weka na nyumba za wafanyakazi.

Na uwe na usafiri wa watoto wao kwenda shule au wakihitaji hospitali.
 
Matajiri wengi ambao wanaweza kuhitajika na shughuli zao za kila siku mjini huishi vijijini.

Porini unahitaji mtaji kuishi, ukiwa na uwezo majambazi pia watakuweka tagert. Ukijiweza katika eneo la ekari 30 weka na nyumba za wafanyakazi. Na uwe na usafiri wa watoto wao kwenda shule au wakihitaji hospitali.
Sasa shida watoto wake wanasoma kule kule kijijini, na umeme Tanesco waliweka nguzo na transformer halafu wakasepa mwaka wa pili sasa hawaunganishi watu sema yeye kafunga solar.

Mwaka jana kanunua trakta la kilimo usafiri anao.

Yuko vizuri sema bado mazingira hayanishawishi
 
Sasa shida watoto wake wanasoma kule kule kijijini, na umeme Tanesco waliweka nguzo na transformer halafu wakasepa mwaka wa pili sasa hawaunganishi watu sema yeye kafunga solar.
Mwaka jana kanunua trakta la kilimo usafiri anao.
Yuko vizuri sema bado mazingira hayanishawishi
Uzuri wa kuishi shambani ni kuwa unaendeleza eneo lako na huhitaji kuhama. Watotot na wajukuu pia watalikuta na kuliendeleza.

Wengi wetu ujanani hatuwazi maisha baada ya kustaafu, unaamka huhitajiki kokote kule zaidi ya kwenda ibadani kama unapenda.
 
Sasa shida watoto wake wanasoma kule kule kijijini, na umeme Tanesco waliweka nguzo na transformer halafu wakasepa mwaka wa pili sasa hawaunganishi watu sema yeye kafunga solar.
Mwaka jana kanunua trakta la kilimo usafiri anao.
Yuko vizuri sema bado mazingira hayanishawishi
Kijijini ukiweza kuchimba kisima uwe na uhakika wa maji umemaliza. Unaweaka vyoo vya ndani na maisha yanaendelea. Sola ni pesa yako zipo zinazoweza hata kuendesha freezer na vyakula visiharibike.

Ukishazoea maisha haya hutaki kurudi mjini. Nilimltemebelea rafiki hangu nje ya Kampala yeye amejenga bomba la maji ya bafuni linapita jikoni. Jiko ni la kujengea la mkaa. Akiwasha jiko asubuhi watu wote mnapata maji ya moto ya kuoga.

Wanahimiza watu waoge kipindi hicho hasa wakati wa baridi.
 
Kijijini ukiweza kuchimba kisima uwe na uhakika wa maji umemaliza. Unaweaka vyoo vya ndani na maisha yanaendelea. Sola ni pesa yako zipo zinazoweza hata kuendesha freezer na vyakula visiharibike.

Ukishazoea maisha haya hutaki kurudi mjini. Nilimltemebelea rafiki hangu nje ya Kampala yeye amejenga bomba la maji ya bafuni linapita jikoni. Jiko ni la kujengea la mkaa. Akiwasha jiko asubuhi watu wote mnapata maji ya moto ya kuoga. Wanahimiza watu waoge kipindi hicho hasa wakati wa baridi.
Yes ana sola iko vzuri ana kila kitu kwake sema mazingira ya kule bwana kuna vitu kama ulivyosema vya kawaida ila ndivyo vinafanya mjini kupendwe.

Kupanga ni kuchagua
 
labda kama wana chanzo kingine cha mapato
kuku 200 wa kienyeji-wanalishwa nini? mimi ninao 30 tu wananitoaga jasho
ongeza bata 30 weeeeeee
hala kila siku wanakula kuku mmoja
siseme wewe ni muongo ,nahisi kuna some hiden information especial kwenye sources of income
all in al maisha ya kijijini ni mazuri kama ardhi yake ipo vizuri kwa mazao
Mdau unaniangusha yaani kuku 30 tu wanakutoa jasho wakati hata debe 1 la pumba hawamalizi kwa wiki na unawakatia majani ya kutosha au unazungumzia wa kuku wa kisasa?
 
Mdau unaniangusha yaani kuku 30 tu wanakutoa jasho wakati hata debe 1 la pumba hawamalizi kwa wiki na unawakatia majani ya kutosha au unazungumzia wa kuku wa kisasa?
Ukifuga kuku wa kienyeji, unafanya urafiki na mama ntilie, ugali uliobaki na ukoko wa wali una bei yake na wewe unapata chakula cha mifugo.
 
labda kama wana chanzo kingine cha mapato
kuku 200 wa kienyeji-wanalishwa nini? mimi ninao 30 tu wananitoaga jasho
ongeza bata 30 weeeeeee
hala kila siku wanakula kuku mmoja
siseme wewe ni muongo ,nahisi kuna some hiden information especial kwenye sources of income
all in al maisha ya kijijini ni mazuri kama ardhi yake ipo vizuri kwa mazao
Kuku hawasumbui kwenye kula kama utawafuga nusu huria,kwakua wanaeneo kubwa wala usiwaze,mm pia ninao kuku,Bata ,kanga,na sungura ,ninacho kifanya nawapa Chakula asubuhi tu, baadae ya hapo nawaachia wakatafute na maisha yanasonga
 
Yes ana sola iko vzuri ana kila kitu kwake sema mazingira ya kule bwana kuna vitu kama ulivyosema vya kawaida ila ndivyo vinafanya mjini kupendwe.
Kupanga ni kuchagua
Kuishi porini principal ya kwanza ni kunua vitu jumla, vya wiki na vya mwezi. Huwezi kuchoma mafuta kisa huna kibiriti.
 
Kuishi porini principal ya kwanza ni kunua vitu jumla, vya wiki na vya mwezi. Huwezi kuchoma mafuta kisa huna kibiriti.
Kweli kabisa.
Yeye anaishi kwenye kijiji kabsa kuna maduka na like 3 kms kutoka hapo kuna center ya kijini ambapo kuna mawakala wa benki na huduma nyingine
 
Back
Top Bottom