Nitengeneze defence team ya nini ? Niipeleke nchi za nje kwenye nchi huru ya nje ya nchi ya Zanzibar nchi ya watu wengine?
Mkuu huu utetezi wako una makengeza,
Ni butu pia unaugua degedege kimashiko.
Unasema Visiwani ni Nchi nyingine,
Swadakta, -na inao hao uliowataja wooote,
Waziri wa Sheria,ma-Jaji, Mahakam nk.
Pengine unayo hoja,
Lakini,U-mpofu kuona kuwa hilo shauri halikuwa Siri.
Liliendeshwa kama mashauri mengine ya kisheria.
Utaniambia vyombo vyote vya Kisheria vilikuwa likizo na kuwa isingewezekana kuiona ni dosari kuliendesha shauri hilo kule kwa mujibu wa Sheria?
Pili,
Iwapo hukumu hiyo isingekuwa halali,
Huyo mkosaji unadhani kitu gani kinamfanya awe mafichoni?
Je, matusi yake, majivuno na dhihaka zake unadhani pangekalika hapa?
Jamaa yako kaufyata anajua akileta za kuleta lupango itamhusu na hayupo anaepumua wa kulizuia hilo.
Anyway, yawezekana wengine hatuelewi kidogo ila, busara ya kawaida haingii kichwani na msimhadae ajitokeze mwenzenu kama kweli yuko mbali akae hukohuko huku akija watu wanae wanataka Fweza zao na kizuri zaidi anamjua vizuri 'Sister Doo wa Bumbwini'🤪
Nawasilisha.