Feisal Salum Feitoto amekosa mzazi

Ni Mchezaji Mzuri Ila waliomzunguka wanamuaminisha kuwa yeye ni zaidi ya Prime Zinedine Zidane
kama ni mchezaji mzuri mbona hanunuliwi hata kwa matimu magalasa tu ya kiarabu huko kama wenzake? bila faitoto yanga hawawezi kushinda mechi? tupa kule. watu hata kabla hawajafanikiwa kwenye maisha wanapanda mabega juuu, umepata kidogo tu mabega juu utafikiri mchungaji kimaro, dawa yake ni kuwaacha waendelee kwenye shimo waliloliendea kina kaseja tu. sasaivi hata timu ya balozi wa mtaani haiwezi kuwaita. mvumilivu hula mbivu. na usiwe na kibri kabla hujafanikiwa.
 
Acha kulialia. Mshauri huyo dogo asiye jielewa, afuate utaratibu. Hata huyo Samatta unayemtolea mfano, aliondoka simba kwa kufuata utaratibu;

Hao Tp Mazembe hawakumpa Samatta hela kwa siri, ili avunje mkataba na timu yake.
 
Mbeya unazungumzia uwanja mpaka uwanja Ngoma? Nimecheza pale na timu ya forest ya kina Hamis Chepelino. Akina Shaban Mtupa.!?
 
Acha kulialia. Mshauri huyo dogo asiye jielewa, afuate utaratibu. Hata huyo Samatta unayemtolea mfano, aliondoka simba kwa kufuata utaratibu;

Hao Tp Mazembe hawakumpa Samatta hela kwa siri, ili avunje mkataba na timu yake.
Sidhani kama atakuelewa jamaa mgumu kuelewa
 
Sahihi Kabisa Kaka ameshimdwa hata kujifunza kwa Luis Miquissone dogo analamba si chini ya 90M pale Club Al Ahly dogo alikiwasha sana hatua ya makundi Hadi akaonwq
90M [emoji3][emoji3][emoji3] sawa.
 
Mbeya unazungumzia uwanja mpaka uwanja Ngoma? Nimecheza pale na timu ya forest ya kina Hamis Chepelino. Akina Shaban Mtupa.!?
Sasa sisi tulikuwa tunacheza pale Mbatta, Samatta alikuwa hapendi kucheza uwanja ngoma... Aisee umenikumbusha mbali enzi za Saitama, Ghana Stars, Redstar, Mwanjelwa, Barcelona Mimi nimecheza na Misango Magae Diego.... Enzi zile tunacheza kaka yake Samatta, Mohamed ndio alikuwa maarufu,.. walikuwa wanakaa pale kota za polisi
 
Fei toto amesha sema hataki kuendelea kukaa yanga kwa sababu kapata timu iliyo bora kwake kimaslahi lakini mmemgangania tu.
Ingekua ni rahisi tu hivi mchezaji kuondoka maana yake mikataba isingekua na maana kwa sababu mchezaji akitaka tu kuondoka anasema anaondoka. Sheria ya mikataba haipo ivyo, yanga sio kwamba wamemzuia feisal kuondoka ila wanachotaka afate utaratibu hao tp mazembe walikaa na simba mezani wakamalizana.. Rage apewe phd ya heshima kwa kweli
 
Sure lazima kuwe Kuna "Mutual Agreement"
 
Aisee safi sana Umecheza na Misango Diego!? very good to know you. Rafiki wa dogo Chale dogo mmoja hv alikuwa anakiwasha balaa. Yule dogo alikuja kuchezea Prison na kina Yona Ndabila nafikiri ni askari magereza sasahivi.
Sasa mimi nimechezea Forest pale uwanja ngoma na kina Hamis Chepe,Robo Mwasalemba, Maja tulikuwa na mzungu pori enzi hizo.
Kwa kifupi Mbeya kulikuwa na vipaji vya hatari sana. Ni vile kulikosekana watu wa kuviendeleza
 
Yes, kaka Misango ni Afande kwa Sasa... That's good memory Yani nikienda Mbeya lazima niende pale kiwanja Ngoma japo siku hizi hawachezi pale... Cheppe what a talent sijui yupo wapi siku hizi
 
Yes, kaka Misango ni Afande kwa Sasa... That's good memory Yani nikienda Mbeya lazima niende pale kiwanja Ngoma japo siku hizi hawachezi pale... Cheppe what a talent sijui yupo wapi siku hizi
Nadhani ni askari somewhere.
Kile kipaji mpaka leo kinaniuma hakikutendewa haki mpaka kimepotea bure.
 
Acha kulialia. Mshauri huyo dogo asiye jielewa, afuate utaratibu. Hata huyo Samatta unayemtolea mfano, aliondoka simba kwa kufuata utaratibu;

Hao Tp Mazembe hawakumpa Samatta hela kwa siri, ili avunje mkataba na timu yake.
Nyinyi utopolo mbona ndo vinara wa uvunjifu wa kanuni za soka hapa nchini na mnafumbiwa macho?
Hili jambo viongozi wa utopolo wangetumia busara tu wakamuachia dogo akaenda na sio kufanya mambo kwa ajili kumkomoa ili wamuharibie kijana mdogo kama huyo , maana hata utopolo imekuwa ikivunja kanuni za soka lakini wamekuwa TFF imekuwa ikitumia busara na kuwastiri.

Kwani hiyo roho ya kichawi mmemfanyia feisal peke yake ,nyinyi wachawi simlisha haribu dili la ngasa kwenda Sudani ambalo linge mpatia pesa kibao ambazo zinge badilisha maisha yake?

Utopolo ni kikundi cha wachawi Mungu atasimama na fei mwisho atakishinda kikundi hichi kiovu cha kichawi na kilicho jaa fikra za kimasikini.
 
Kwa mujibu wa vipengele vya mkataba alicho kifanya Fei ni sawa ila TFF imeliamuwa hili suala kisiasa na sio kikanuni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…