Feisal Salum Feitoto amekosa mzazi

Feisal Salum Feitoto amekosa mzazi

Ongeeni muongeavyo lakini kuanzia viongozi, mashabiki wa utopolo huwa mna roho za kichawi na kimasikini na wengi wenu hamna akili.
Fei toto amesha sema hataki kuendelea kukaa yanga kwa sababu kapata timu iliyo bora kwake kimaslahi lakini mmemgangania tu.

Simba walimuachia Samata kwenda mazembe baada ya kuona kule mazembe atapata maslahi kwa manufaa ya maisha yake lakini nyinyi hamta kumuachia Fei kwa ajili manufaa ya maisha yake badala yake nyinyi mnataka atumike kwa ajili ya maslahi yenu tu.
Ni aibu kwa mazee mazima yanayo jiita masomi kutumia nguvu kubwa kumiharibia ndoto kijana mdogo kama fei eti kwa ajili ya kumkomoa.
Hiyo timu mbona haijitokezi mezani kama Mazembe?!!!
 
Kwani ukimpa mtanzania maslahi yake kwa wakati kuna tatizo gani? Kwann lazima avumilie, apate shida? Haiwezekani akapewa fedha za kumwaga mapema tu? Ni lazima ateseke kwanzaaaa?
 
Ongeeni muongeavyo lakini kuanzia viongozi, mashabiki wa utopolo huwa mna roho za kichawi na kimasikini na wengi wenu hamna akili.
Fei toto amesha sema hataki kuendelea kukaa yanga kwa sababu kapata timu iliyo bora kwake kimaslahi lakini mmemgangania tu.

Simba walimuachia Samata kwenda mazembe baada ya kuona kule mazembe atapata maslahi kwa manufaa ya maisha yake lakini nyinyi hamta kumuachia Fei kwa ajili manufaa ya maisha yake badala yake nyinyi mnataka atumike kwa ajili ya maslahi yenu tu.
Ni aibu kwa mazee mazima yanayo jiita masomi kutumia nguvu kubwa kumiharibia ndoto kijana mdogo kama fei eti kwa ajili ya kumkomoa.
Samatta alivunja mkataba na Simba Kwa njia ya Feisal?
 
Mbwana Samatta amekulia katika viunga vya Mbagala huko ndiko kuliko mtambulishan katika uga wa kandanda. Historia ya huyu mchezaji haikuwa rahisi kutoboa hadi kufikia hapo alipofikia. Kuna kipindi alikuwa anakosa hata sh. 200 ya nauli ya kumpeleka mazoezi. Waliokuwa karibu yake walimsaidia pesa ya nauli. Sina haja ya kueleza mengi kuhusu mchezaji huyu aliyecheza African Lyon kwa miaka miwili kuanzia 2008 hadi 2010 alipohamia club yake pendwa ya Simba SC. Kila mtu anayefuatilia na asiyefuatilia soka katika nchi hii anamjua Mbwana Samatta.

Ifahamike hapa, lengo sio kumzungumzia Mbwana Samatta, ila tu nataka nikukumbushe au niwakumbushe wachezaji wa Kitanzania njia alizopitia Mbwana Samatta.

Ndio, baada ya kuwika na African Lyon, 2008-2010 Mbwana Samatta alisajiliwa na Simba SC kwa ada ya usajili ambayo ni siri hadi leo lakini moja ya kipendele katika mkataba wake ilikuwa ni lazima Simba SC wampatie gari mpya aina ya Toyota Mark II Grand GX 110.

Siku zikaenda zikarudi lakini team yake ya Simba hawakutimiza ahadi ya kumpatia gari ambayo walimuahidi, Toyota Mark II Grand GX 110. Kumbuka kipindi hicho Samatta alishaanza kuteka mioyo ya wana Msimbazi wa uhodari wake wa kupachika nyavu… nini kilitokea??

Mbwana Samatta, AKAGOMA. Hii ilikuwa ni mwaka 2011 mwanzoni hapo club ya Simba inakabiliwa na mechi ngumu mbeleni dhidi ya TP Mazembe katika ligi ya Mabingwa Afrika.

Hapo ndipo akaibuka Kenny Mwaisabula Maarufu kama “MZAZI’’ huyu ni mmoja katika ya watu walimsaidia Mbwana Samatta katika makuzi ya kisoka. Hata zile mia mbili mia mbili za nauli za kwenda kwenye mazoezi Mbwana Samatta amepatiwa sana na huyu “MZAZI”

Kenny Mwaisabula, ‘’MZAZI’’ kupitia gazeti la Mwanasporti na kupitia ukaribu aliokuwa nao na Mbwana Samatta alimsihi sana kijana wake asigomee mazoezi wala mechi za Simba. Katika Makala yake hiyo ‘’MZAZI’’ alimuomba Mbwana Samatta aendelee tu kucheza mpira ipo siku atapata kile anachotaka kupitia huo mpira, cha msingi asiache mazoezi na aongezee bidii kwenye mechi kwani kwa kufanya hivyo ipo siku atapata na atakuwa na uwezo wa kununua Zaidi gari mia moja kama hiyo aliyoahidiwa na Simba.

Haikuishia hapo, ‘’MZAZI” akakaa na Mbwana Samatta nakumueleza kuwa Simba SC wapo kwenye ligi ya mabingwa Afrika na kama ataendelea kugoma hawezi kupata chance ya kucheza michezo hiyo mikubwa Zaidi kwa upande wa vilabu barani Afrika.

Ndipo Samatta akamsikiliza ‘’MZAZI’’ Kenny Mwaisabula. Akarudi Kambini. Mechi ya kwanza Simba akacheza na TP Mazembe ugenini tarehe 20/03/2011 na Samatta akiwa ndani Simba akafungwa 3-1 pale Lubumbashi.

Mechi ya pili pale taifa Mnyama anakufa tena 3-2 dhidi ya TP Mazembe magoal ya Simba yalifungwa na SHija Mkina dakika ya 58 kwa Assist ya Mbwana Samatta na goal la pili la Simba lilifungwa na Mbwana Samatta mwenyewe dakika ya 70. Hii mechi Mbwana aling’aa sana. Mwingine aliyeng’aa sana kwenye mechi hii ni Mganda Patrick Ochan. TP Mazembe wakaondoka na majina mawili, Patrick Ochan na Mbwana Samatta. Mwaka huo huo 2011, Mbwana Samatta na Patrick Ochan wakatua TP Mazembe.

Bila ushauri wa ‘’MZAZI’’ Mbwana Samatta angeendelea kugoma na angeendelea kugoma sidhani kama TP Mazembe wangemuona akiwa kwao Mbagala alisubiri GX 110 aliyoahidiwa na Simba SC.

Baada ya hapo wazungu wanasema ‘’the rest is history’’ kila mtu anajua ukwasi wa Captain Diego Mbwana Samatta, niliyecheza nae pale Mbeya viwanja vya MBATTA kipindi cha utoto wetu.

Bahati mbaya sana ndugu yetu Feisal Salum Abdallah ‘’FEITOTO’’ amekosa mtu kama ‘’MZAZI’’ katika carrier yake ya kucheza mpira, mtu ambaye anaona mbali na kukitazama mbali kipaji cha FEITOTO. Huyu mtu amekosekana katika maisha ya Feitoto. Watu walionyuma ya Feisal kwasasa ni wale watu ambao wamefikiri leo tu na sio kesho na kesho kutwa na huyu mchezaji.

Ndio, hakuna ubishi ya kuwa FEITOTO ameibeba sana Yanga katika mabega yake na anastahili kupata donge nono katika mshahara wake lakini njia alizotumia ni kama tu zile Hasira za mkizi. Timu yake ya YANGA inakaribia kuanza kucheza michuano ya kimataifa lakini yeye hayupo kikosini. Na bila shaka hii michuano ya Kombe La Shirikisho la Afrika ingekuwa ni Platform kwake kujitangaza kimataifa Zaidi na huenda angepata team nzuri nje ya Nchi ambayo ingekidhi mahitaji yake mara Zaidi ya watu wanaomrubuni kwasasa.

Naamini kabisa FEITOTO angekuwa na ‘’MZAZI’’ angeshauriwa aendelee kucheza huku akiendelea kubargain juu ya maslahi yake mapya kitu ambacho team yake ya YANGA wasingeshindwa kusimsikiliza.



Feisal Amekosa mtu kama Kenny Mwaisabula.



Nawasilisha.



N.B;

FEISAL SALUM FEITOTO RAMADHANI SINGANO A.K.A MESSI ANAOMBA UPOKEE SIMU YAKE ANAKUPIGIA
Kila mtu ana njia yake., acheni kuwatapeli local talents
 
Feisal atafute team hata uarabuni atalipwa vizuri kuliko yanga wanamlisha mihogo tu
 
Ajamaliza chochote kubalini utopolo ni kikundi kilicho jaa wachawi.
Hili suala la fei viongozi wa utopolo wangekuwa na akili wangetumia busara tu kumuachia dogo asepe na sio kumngangania ili kumkomoa.

Kama ni suala la kufuata sheria Utopolo ndo mabingwa wa uvunjanji wa kanuni za soka ndani ya nchi hii.
Kama ndo hivo Kuna haja gani ya kua na mikataba???
 
Kwa mujibu wa vipengele vya mkataba alicho kifanya Fei ni sawa ila TFF imeliamuwa hili suala kisiasa na sio kikanuni.
Kuna nafasi ya feisal kwenda kwenye vyombo vya juu zaidi kudai haki yake acha tuone itakuaje akifanya ivyo
 
Kama ndo hivo Kuna haja gani ya kua na mikataba???
Ndo hapo sasa ushangae yaani mchezaji akitaka kuondoka wakati wowote timu imuachie sasa kuna haja gani ya kusaini miaka miwili, mitatu, mnne n.k. watu hawaelewi kwamba mchezaji na timu ni pande tofauti kwaiyo kila upande una haki ya kusimamia masilahi yake. Kama mchezaji akitaka kuondoka na timu ikakataa basi mchezaji anawajibika kuendelea kutumikia mkataba wake mfano feisal na yanga au timu ikataka kumtema mchezaji na mchezaji akakataa kuondoka basi timu inawajibika kumlipa mshahara na stahiki zake zote kwa mujibu wa mkataba mfano barcelona na de jong
 
Mbwana Samatta amekulia katika viunga vya Mbagala huko ndiko kuliko mtambulishan katika uga wa kandanda. Historia ya huyu mchezaji haikuwa rahisi kutoboa hadi kufikia hapo alipofikia. Kuna kipindi alikuwa anakosa hata sh. 200 ya nauli ya kumpeleka mazoezi. Waliokuwa karibu yake walimsaidia pesa ya nauli. Sina haja ya kueleza mengi kuhusu mchezaji huyu aliyecheza African Lyon kwa miaka miwili kuanzia 2008 hadi 2010 alipohamia club yake pendwa ya Simba SC. Kila mtu anayefuatilia na asiyefuatilia soka katika nchi hii anamjua Mbwana Samatta.

Ifahamike hapa, lengo sio kumzungumzia Mbwana Samatta, ila tu nataka nikukumbushe au niwakumbushe wachezaji wa Kitanzania njia alizopitia Mbwana Samatta.

Ndio, baada ya kuwika na African Lyon, 2008-2010 Mbwana Samatta alisajiliwa na Simba SC kwa ada ya usajili ambayo ni siri hadi leo lakini moja ya kipendele katika mkataba wake ilikuwa ni lazima Simba SC wampatie gari mpya aina ya Toyota Mark II Grand GX 110.

Siku zikaenda zikarudi lakini team yake ya Simba hawakutimiza ahadi ya kumpatia gari ambayo walimuahidi, Toyota Mark II Grand GX 110. Kumbuka kipindi hicho Samatta alishaanza kuteka mioyo ya wana Msimbazi wa uhodari wake wa kupachika nyavu… nini kilitokea??

Mbwana Samatta, AKAGOMA. Hii ilikuwa ni mwaka 2011 mwanzoni hapo club ya Simba inakabiliwa na mechi ngumu mbeleni dhidi ya TP Mazembe katika ligi ya Mabingwa Afrika.

Hapo ndipo akaibuka Kenny Mwaisabula Maarufu kama “MZAZI’’ huyu ni mmoja katika ya watu walimsaidia Mbwana Samatta katika makuzi ya kisoka. Hata zile mia mbili mia mbili za nauli za kwenda kwenye mazoezi Mbwana Samatta amepatiwa sana na huyu “MZAZI”

Kenny Mwaisabula, ‘’MZAZI’’ kupitia gazeti la Mwanasporti na kupitia ukaribu aliokuwa nao na Mbwana Samatta alimsihi sana kijana wake asigomee mazoezi wala mechi za Simba. Katika Makala yake hiyo ‘’MZAZI’’ alimuomba Mbwana Samatta aendelee tu kucheza mpira ipo siku atapata kile anachotaka kupitia huo mpira, cha msingi asiache mazoezi na aongezee bidii kwenye mechi kwani kwa kufanya hivyo ipo siku atapata na atakuwa na uwezo wa kununua Zaidi gari mia moja kama hiyo aliyoahidiwa na Simba.

Haikuishia hapo, ‘’MZAZI” akakaa na Mbwana Samatta nakumueleza kuwa Simba SC wapo kwenye ligi ya mabingwa Afrika na kama ataendelea kugoma hawezi kupata chance ya kucheza michezo hiyo mikubwa Zaidi kwa upande wa vilabu barani Afrika.

Ndipo Samatta akamsikiliza ‘’MZAZI’’ Kenny Mwaisabula. Akarudi Kambini. Mechi ya kwanza Simba akacheza na TP Mazembe ugenini tarehe 20/03/2011 na Samatta akiwa ndani Simba akafungwa 3-1 pale Lubumbashi.

Mechi ya pili pale taifa Mnyama anakufa tena 3-2 dhidi ya TP Mazembe magoal ya Simba yalifungwa na SHija Mkina dakika ya 58 kwa Assist ya Mbwana Samatta na goal la pili la Simba lilifungwa na Mbwana Samatta mwenyewe dakika ya 70. Hii mechi Mbwana aling’aa sana. Mwingine aliyeng’aa sana kwenye mechi hii ni Mganda Patrick Ochan. TP Mazembe wakaondoka na majina mawili, Patrick Ochan na Mbwana Samatta. Mwaka huo huo 2011, Mbwana Samatta na Patrick Ochan wakatua TP Mazembe.

Bila ushauri wa ‘’MZAZI’’ Mbwana Samatta angeendelea kugoma na angeendelea kugoma sidhani kama TP Mazembe wangemuona akiwa kwao Mbagala alisubiri GX 110 aliyoahidiwa na Simba SC.

Baada ya hapo wazungu wanasema ‘’the rest is history’’ kila mtu anajua ukwasi wa Captain Diego Mbwana Samatta, niliyecheza nae pale Mbeya viwanja vya MBATTA kipindi cha utoto wetu.

Bahati mbaya sana ndugu yetu Feisal Salum Abdallah ‘’FEITOTO’’ amekosa mtu kama ‘’MZAZI’’ katika carrier yake ya kucheza mpira, mtu ambaye anaona mbali na kukitazama mbali kipaji cha FEITOTO. Huyu mtu amekosekana katika maisha ya Feitoto. Watu walionyuma ya Feisal kwasasa ni wale watu ambao wamefikiri leo tu na sio kesho na kesho kutwa na huyu mchezaji.

Ndio, hakuna ubishi ya kuwa FEITOTO ameibeba sana Yanga katika mabega yake na anastahili kupata donge nono katika mshahara wake lakini njia alizotumia ni kama tu zile Hasira za mkizi. Timu yake ya YANGA inakaribia kuanza kucheza michuano ya kimataifa lakini yeye hayupo kikosini. Na bila shaka hii michuano ya Kombe La Shirikisho la Afrika ingekuwa ni Platform kwake kujitangaza kimataifa Zaidi na huenda angepata team nzuri nje ya Nchi ambayo ingekidhi mahitaji yake mara Zaidi ya watu wanaomrubuni kwasasa.

Naamini kabisa FEITOTO angekuwa na ‘’MZAZI’’ angeshauriwa aendelee kucheza huku akiendelea kubargain juu ya maslahi yake mapya kitu ambacho team yake ya YANGA wasingeshindwa kusimsikiliza.



Feisal Amekosa mtu kama Kenny Mwaisabula.



Nawasilisha.



N.B;

FEISAL SALUM FEITOTO RAMADHANI SINGANO A.K.A MESSI ANAOMBA UPOKEE SIMU YAKE ANAKUPIGIA

Nimekuwa na jambo la kujifunza!
Nashukuru mno
 
Ndo hapo sasa ushangae yaani mchezaji akitaka kuondoka wakati wowote timu imuachie sasa kuna haja gani ya kusaini miaka miwili, mitatu, mnne n.k. watu hawaelewi kwamba mchezaji na timu ni pande tofauti kwaiyo kila upande una haki ya kusimamia masilahi yake. Kama mchezaji akitaka kuondoka na timu ikakataa basi mchezaji anawajibika kuendelea kutumikia mkataba wake mfano feisal na yanga au timu ikataka kumtema mchezaji na mchezaji akakataa kuondoka basi timu inawajibika kumlipa mshahara na stahiki zake zote kwa mujibu wa mkataba mfano barcelona na de jong
Unapoteza muda wako bure kumuelimisha empty set
 
Yule mpiga kelele aliyeachwa nilisikitika majuzi anasema kwa madaha. Eti feisal huendi kokote unabaki hapa hapa.

nikaamini alivyosemaga pale yanga wenye akili ni wawili ni kweli maana hata yy kashakosa akili alivyoenda huko.
Mzee Mpili juzi kapeleka watu polisi baada ya kuzidiwa hoja, alikwenda kijiwe chale magomeni mwembechai akasema Feitoto hatacheza mpira akatokea mtu akamjibi hivi wewe huo uwezo unaomtishia feitoto unafikiri ni wewe peke yako unao hebu acha mambo ya akaweka tusi Mzee kakasirika kaenda polisi ila polisi wakaona kesi ya kipuuzi wakampuuzia kurudi wakamwambia kama huwezi matani usiwe unatania
 
Pointi zako zimejaa uongo Sammata aliposajiliwa Simba aliweka masharti ya gari lakini Simba hawakutimiza na yeye hakuchezea Simba inasemekana alienda ureno baada ya Simba kufanya vibaya ikabidi wamfate wampe gari walilomwahidi hovyo akajiunga Simba baada ya miezi sita mechi yake ya kwanza ilikuwa na Mazembe akafanya vizuri yeye na Ochan , Mazembe walipoleta ofa Simba wakamruhusu
 
Hap
Ongeeni muongeavyo lakini kuanzia viongozi, mashabiki wa utopolo huwa mna roho za kichawi na kimasikini na wengi wenu hamna akili.

Fei toto amesha sema hataki kuendelea kukaa yanga kwa sababu kapata timu iliyo bora kwake kimaslahi lakini mmemgangania tu.

Simba walimuachia Samata kwenda mazembe baada ya kuona kule mazembe atapata maslahi kwa manufaa ya maisha yake lakini nyinyi hamta kumuachia Fei kwa ajili manufaa ya maisha yake badala yake nyinyi mnataka atumike kwa ajili ya maslahi yenu tu.

Ni aibu kwa mazee mazima yanayo jiita masomi kutumia nguvu kubwa kumiharibia ndoto kijana mdogo kama fei eti kwa ajili ya kumkomoa.
Hapo na wewe unajiona binge la mwandishi na mtoa ushauri kumbe yote uliyoandika hapa no uhalo mtupu...
 
Pointi zako zimejaa uongo Sammata aliposajiliwa Simba aliweka masharti ya gari lakini Simba hawakutimiza na yeye hakuchezea Simba inasemekana alienda ureno baada ya Simba kufanya vibaya ikabidi wamfate wampe gari walilomwahidi hovyo akajiunga Simba baada ya miezi sita mechi yake ya kwanza ilikuwa na Mazembe akafanya vizuri yeye na Ochan , Mazembe walipoleta ofa Simba wakamruhusu
Uongo uko wapi Sasa!?
 
Feisal au fei toto ni mchezaji wa kawaida sana. Nawaza huyu kijana angekuwa anafanya mambo anayofanya chama ingekuwaje!!!

Watanzania sisi huwa tunaamua tu kumpaisha mtu na fei tumeamua tu kumpaisha ila hana tofauti na viungo wengi wazawa nchini.

Ww angalia mtu kama mandonga, piere, dokta shika na wengineo tuliwapaisha bila sababu za msingi, hata Fei anapitia eneo hili ila sema yeye yupo kwenye football.

Nimemuangalia sana huyu dogo ila sijaona ana kitu cha tofauti na wachezaji wengi wazawa nafikiri ni upepo wa kupaishwa tu umeamuangukia .
 
Back
Top Bottom