Feisal Salumu: Nimeondoka Yanga kutokana na manyanyaso, nilizungumza na Rais wa Yanga kwa saa 6, nikamwambia nataka kuondoka

👉Nimenyanyaswa sana nikiwa Yanga,nimeambiwa nauza mechi na viongozi.

👉Nimekaa na Hersi na Makamu wake masaa 6 nikamwambia yanayonisibu dhidi yake akaniomba radhi akasema tusameheane nikamwambia nimekusamehe lakini nataka kuondoka.
Akasema sisi bado tunakuhitaji, nikamwambia mimi siwezi tena kuendelea na Yanga, naomba niondoke.

Akasisitiza nibaki nikamwambia basi wanipe siku 3 niongee na familia yangu.

👉Mkataba huu nilio nao wakati nasaini mama aliniambia nitasaini mkataba wa miaka 2 lakini Hersi akaniongezea ikawa 3 bila mimi kujua.

👉Mkataba uliandikwa Kingereza na mimi Kingereza sijui na nilikuwa pekeyangu. Wao walikuwa Saimon, Hersi, Arafat na Mdhamini.

👉Mama yangu ni mpenzi mkubwa sana wa Yanga na yeye ndiye aliyenipambania wakati Yanga mambo yakiwa mabaya alikuwa ananipa pesa yake mwenyewe.

👉Nimekula Ugali na Sukari wakati Yanga ikiwa na hali mbaya sio sasahivi.

👉Wanamtukana na kunyanayasa pepo yangu, mama yangu ndiyo pepo yangu mimi halafu anafananishwa na andazi kweli?

👉Nawapenda sana mashabiki wa Yanga na najua wananipenda pia, hawajui niliyopitia wanaambiwa uongo wanamtukana mama yangu na mimi mwenyewe.

👉 Simkimbii Hersi nimkimbie ili iweje Kwani Mimi nimeua? Nimekaa nae yeye na Makamu wake masaa 6

Kuna mtu alituita wachezaji wa Yanga takataka lakini akaja Yanga tukampokea vizuri, leo hii mtu huyo huyo anatuambia tunahujumu timu”

Ikitokea sitocheza tena mpira niko tayari lakini sio kurudi Yanga”

My Take
Msimamo wangu ni kwamba Yanga sio club ya kwenda mtu makini. Imejaa uhuni na wahuni
 
Suala la elimu ni kwa wote ndugu yaani Fei na Yanga. Mchezaji anaiongelea vibaya klabu kwamba ilikuwa inachelewesha mishahara mpaka anakula ugali na sukari lakini kutokana na klabu kuendeshwa kienyeji na kimihemko klabu inataka kumkomoa mchezaji na kuleta uswahili badala ya kuachana nae Kwa makubaliano.

Man U walipokejeliwa Tu na Ronaldo fasta wakaterminate mkataba Kwa makubaliano. Nyinyi waswahili mnataka mpaka mumuone kijana akitembelea ndala zilizotoboka ndio itakuwa furaha kwenu wakati kuna mengine anaongea ukweli kabisa.
 
Tayari kuna uzi humu umeshafunguliwa Moderator walipaswa kuunganisha uzi

 
Ingekuwa ndivyo angeondoka tangu siku alipokuwa analishwa ugali na sukari
 
Mwambie huyo binti Kazumari arudishe gari ya Feisal na akome kurubuni Watoto.
 
Tatizo sio hiyo miaka 3, tatizo lipo kwenye unyanyasaji uliendelea na amefanya kazi kwa shida.

Sikiliza mahojiano yake.

Fei yupo tayari arudi mtaani kuliko kufanya kazi na Eng Hersi. Alichofanyiwa na Eng. Hersi hataki kufanya naye kazi tena.
 
Ila haka katoto kafala sana.
 
Vipi baada ya kusaini mkataba, mbona vyombo vya habari viliandika miaka mitatu na yeye aliona hakulalamika??
Aache kutafuta huruma. Asuburi mashabiki wa simba wamchangie wakiamini atasaini kwao ili kutukomoa sisi Yanga.
Na wakati wanatangaza yeye kakaa upande wa kushoto huku akichekelea labda na kiswahili nacho hajui
 
Vipi baada ya kusaini mkataba, mbona vyombo vya habari viliandika miaka mitatu na yeye aliona hakulalamika??
Aache kutafuta huruma. Asuburi mashabiki wa simba wamchangie wakiamini atasaini kwao ili kutukomoa sisi Yanga.
Eti bana.
 
Vijana wa zenji Wana tabia kama zile za yule afwande wao [emoji2380]
Mnatumika kushikishwa ukuta sana ili muitoe YANGA ktk attention, uzuri ni kwamba YANGA msimu huu tuna beba makombe yote hadi wake zenu na mademu
Sasa hili povuu vepeee? Muache Fei aongee ukweli, km ni uongo bas wahusika waje wakanusheee
 
Ndo kilicho kuwepooo hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…