Feisal Salumu: Nimeondoka Yanga kutokana na manyanyaso, nilizungumza na Rais wa Yanga kwa saa 6, nikamwambia nataka kuondoka

Feisal Salumu: Nimeondoka Yanga kutokana na manyanyaso, nilizungumza na Rais wa Yanga kwa saa 6, nikamwambia nataka kuondoka

👉Nimenyanyaswa sana nikiwa Yanga,nimeambiwa nauza mechi na viongozi.

👉Nimekaa na Hersi na Makamu wake masaa 6 nikamwambia yanayonisibu dhidi yake akaniomba radhi akasema tusameheane nikamwambia nimekusamehe lakini nataka kuondoka.
Akasema sisi bado tunakuhitaji, nikamwambia mimi siwezi tena kuendelea na Yanga, naomba niondoke.

Akasisitiza nibaki nikamwambia basi wanipe siku 3 niongee na familia yangu.

👉Mkataba huu nilio nao wakati nasaini mama aliniambia nitasaini mkataba wa miaka 2 lakini Hersi akaniongezea ikawa 3 bila mimi kujua.

👉Mkataba uliandikwa Kingereza na mimi Kingereza sijui na nilikuwa pekeyangu. Wao walikuwa Saimon, Hersi, Arafat na Mdhamini.

👉Mama yangu ni mpenzi mkubwa sana wa Yanga na yeye ndiye aliyenipambania wakati Yanga mambo yakiwa mabaya alikuwa ananipa pesa yake mwenyewe.

👉Nimekula Ugali na Sukari wakati Yanga ikiwa na hali mbaya sio sasahivi.

👉Wanamtukana na kunyanayasa pepo yangu, mama yangu ndiyo pepo yangu mimi halafu anafananishwa na andazi kweli?

👉Nawapenda sana mashabiki wa Yanga na najua wananipenda pia, hawajui niliyopitia wanaambiwa uongo wanamtukana mama yangu na mimi mwenyewe.

👉 Simkimbii Hersi nimkimbie ili iweje Kwani Mimi nimeua? Nimekaa nae yeye na Makamu wake masaa 6

Kuna mtu alituita wachezaji wa Yanga takataka lakini akaja Yanga tukampokea vizuri, leo hii mtu huyo huyo anatuambia tunahujumu timu”

Ikitokea sitocheza tena mpira niko tayari lakini sio kurudi Yanga”

My Take
Msimamo wangu ni kwamba Yanga sio club ya kwenda mtu makini. Imejaa uhuni na wahuni
 
Kama haya ndiyo mambo yanayopelekea aende CAS ili wavunje mkataba,ameula wa chuya.

1.Mama yangu ametukanwa
2.Viongozi waliniambia nimeuza mechi
3.Mama yangu anaitwa andazi.

Dogo ameulizwa ishu za kimkataba zilizofanya asitishe mkataba amebaki kujing'ata ng'ata tu.

ELIMU,ELIMU,ELIMU,ELIMU,ELIMU
Suala la elimu ni kwa wote ndugu yaani Fei na Yanga. Mchezaji anaiongelea vibaya klabu kwamba ilikuwa inachelewesha mishahara mpaka anakula ugali na sukari lakini kutokana na klabu kuendeshwa kienyeji na kimihemko klabu inataka kumkomoa mchezaji na kuleta uswahili badala ya kuachana nae Kwa makubaliano.

Man U walipokejeliwa Tu na Ronaldo fasta wakaterminate mkataba Kwa makubaliano. Nyinyi waswahili mnataka mpaka mumuone kijana akitembelea ndala zilizotoboka ndio itakuwa furaha kwenu wakati kuna mengine anaongea ukweli kabisa.
 
Tayari kuna uzi humu umeshafunguliwa Moderator walipaswa kuunganisha uzi

 
Suala la elimu ni kwa wote ndugu yaani Fei na Yanga. Mchezaji anaiongelea vibaya klabu kwamba ilikuwa inachelewesha mishahara mpaka anakula ugali na sukari lakini kutokana na klabu kuendeshwa kienyeji na kimihemko klabu inataka kumkomoa mchezaji na kuleta uswahili badala ya kuachana nae Kwa makubaliano.

Man U walipokejeliwa Tu na Ronaldo fasta wakaterminate mkataba Kwa makubaliano. Nyinyi waswahili mnataka mpaka mumuone kijana akitembelea ndala zilizotoboka ndio itakuwa furaha kwenu wakati kuna mengine anaongea ukweli kabisa.
Ingekuwa ndivyo angeondoka tangu siku alipokuwa analishwa ugali na sukari
 
Huyo Kazumari Unayemtukana hivi hata Yeye kaipata hii Taarifa kutoka Clouds FM ( Kipindi chao cha Michezo ) cha Asubuhi ya leo ambako walikuwepo Studioni na Mchezaji Feisal Salum Feitoto na ndiyo akaongea hivyo na mengineyo mengi tu.

Hujachelewa Kumuomba Radhi Jemedari Said Bin Kazumari kwa hivi Ulivyomtukana na Kumdhalilisha.
Mwambie huyo binti Kazumari arudishe gari ya Feisal na akome kurubuni Watoto.
 
Katoka hali ya kawaida ukifikiria utagundua kuwa hiyo miaka ilyoandikwa kwenye mkataba aliijua na aliridhika nayo. Nasema hivyo kwasababu baada ya Feisal kusaini mkataba wa kuongeza miaka Yanga, vyombo vya habari vikaripoti kuwa Feisal asaini miaka mitatu Yanga. Ina maana Feisal sio mfuatilia wa vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kiasi kwamba asijue kumbe maandishi yameenda kinyume na tulivyoongea mdomoni? Kwanini alilikalia kimya swala la muda wa mkataba kipindi chote hiko?
Tatizo sio hiyo miaka 3, tatizo lipo kwenye unyanyasaji uliendelea na amefanya kazi kwa shida.

Sikiliza mahojiano yake.

Fei yupo tayari arudi mtaani kuliko kufanya kazi na Eng Hersi. Alichofanyiwa na Eng. Hersi hataki kufanya naye kazi tena.
 
"niliambiwa na viongozi wa Yanga kuwa nauza mechi iliniuma sana na nikipokuwa nawapigia simu hao viongozi waliokuwa wanatamka hayo maneno hawapokei simu yangu.

"Viongozi walikua wanamtukana mama yangu na kutoa matusi ya kumnyanyasa hata ingekua ni wewe ndugu mwandishi usingekubali kutukaniwa mzazi"

"Kula ugali kwa sukari sikula saivi nilikula kipindi kile timu bado ilikua ipo chini kiuchumi na kuna muda tulicheleweshewa mishahara lakini Mama aliniambia vumilia mwanangu maana alikua ni mpenzi wa mkubwa wa Yanga.

"Mama kuna muda mwingine alinipa pesa yake tulipokua tumecheleweshewa mshahara."

Mwandishi: Tueleze umepitia manyanyaso gani?

"Naambiwa nauza mechi, viongozi wananitukana na nikiwaambia familia wanasema nivumilie.

"Mama yangu alikuja Dar wakamtukana na kuanza kumpa maneno ya kejeli."

"Huyo huyo Raisi anatuma watu wamtukane mama yangu wanamuita mama yangu andazi "

Wanitukane Mimi lakini siyo mama yangu maana mama yangu ni pepo yangu"

"Nimekaa masaa sita na Engineer Hersi kuwa hapa nilipofikia nataka niachane na Yanga na Hers alisema kuwa bado anahitaji huduma yangu"

Raisi: anampigia simu mama na mama aliniambia niende kusaini mkataba na mama alimwambia mpe Fei mkataba wa miaka miwili"

Hers aliongeza mwaka mmoja badala ya miaka miwili"

"Mimi sijui kiingereza walinipa mkataba wa miaka mitatu"

"Signing fee sijapewa kwa wakati nilipewa kidogo kidogo tena kwa kutumiana meseji za vitisho"

"Nataka kukusanya milioni 60 niende CAS na watanzania wengi wananichangia na utaratibu umeanza tunasubiri invoice"

"Unajua yanga ni taasisi kubwa na Mimi ninawapenda wanayanga nilimwambia hers ata Kama alinikosea Ila nilimwambia tukae chini tumalizane na hers alikili makosa yake lakini Mimi nilitaka tuachane nikatafute maisha sehemu nyingine"

"Nilimwambia eng Hers bmkubwa alikuambia Miaka miwili lakini ukanipa mitatu lakini hers hakunijibu"

"Familia yangu wanaipenda Yanga lakini kilichonitoa Yanga ni manyanyaso"

"Hakuna timu inayonitaka na ndiyo maana nilitaka kuvunja mkataba niende kutafuta maisha yangu pengine"

"Tumekaa na familia yangu niliona Bora tuvunje mkataba na niliwaomba viongozi tuachane nilichangiwa pesa na familia"

"Mimi siwezi kula dhuluma siwezi kula pesa ambayo siifanyii kazi na ndiyo maana wakituma pesa zinarudi"

"Mimi sipendi hizi kelele nataka hili Jambo liishe na nafsi yangu haitaki kucheza Yanga na ndiyo maana nilikaa nao chini viongozi chini tuyamalize nikatafute maisha sehemu nyingine"

",Kama Jambo litakua haliishi ni bora nikae nyumbani maana ndiyo mwenyezimung atakua amepanga hivyo" kipaji kuisha.

"Hers anasema nauza mechi kun pass moja nilimpa Mayele aongeze magoli mbele ya kipa lakini Mayele alikosa hapo Hers akaanza kusema kuwa nauza mechi"

"Nilimtafuta GSM aje kutafuta suluhu lakini hakupokea simu zangu lakini aliposikia sakata Hili ndiyo akaanza kunitafuta na Mimi sikupokea simu yake"

"Nilikutana Hers akasema kuwa anataka nirudi Yanga nilikataa basi akaniambia niende CAS"

"Hers anadharau kubwa sana na Msolwa alikua ni mkarimu sana"

"Watu hawajiulizi ni kwa nini Fei hajaondoka katika kipindi kile Cha Yanga ngumu lakini nimeondoka kipindi hiki kizuri".

"Mimi nina matatizo na Raisi wa club Sina Tatizo na club Ila hers ndiyo Raisi wa club ndiyo Nina tatizo nae"

"Mpaka Sasa hela haijatosha Ila nashukuru Watanzania wameshanichangia kiasi cha shilingi milioni tisa (9)

"Mimi Nina rafiki na ndugu na wengine wapo humo humo ndani ya klabu ya yanga ndiyo walinichangia kurudisha pesa ili nivunje mkataba"
Ila haka katoto kafala sana.
 
Vipi baada ya kusaini mkataba, mbona vyombo vya habari viliandika miaka mitatu na yeye aliona hakulalamika??
Aache kutafuta huruma. Asuburi mashabiki wa simba wamchangie wakiamini atasaini kwao ili kutukomoa sisi Yanga.
Na wakati wanatangaza yeye kakaa upande wa kushoto huku akichekelea labda na kiswahili nacho hajui
 
Vipi baada ya kusaini mkataba, mbona vyombo vya habari viliandika miaka mitatu na yeye aliona hakulalamika??
Aache kutafuta huruma. Asuburi mashabiki wa simba wamchangie wakiamini atasaini kwao ili kutukomoa sisi Yanga.
Eti bana.
 
Vijana wa zenji Wana tabia kama zile za yule afwande wao [emoji2380]
Mnatumika kushikishwa ukuta sana ili muitoe YANGA ktk attention, uzuri ni kwamba YANGA msimu huu tuna beba makombe yote hadi wake zenu na mademu
Sasa hili povuu vepeee? Muache Fei aongee ukweli, km ni uongo bas wahusika waje wakanusheee
 
Walishaongea kabla ya kusaini mkataba kwanza, kwahivyo yale mazungumzo Faisal ndo akayapeleka kwenye mkataba ambapo baadaye yaliyotokea ni kwa Hersi miaka mitatu na kwa Feisal ni miaka miwili.

Alikariri mazungumzo waliongea kabla ya kusaini mkataba wa Kingereza.
Ndo kilicho kuwepooo hapa.
 
Back
Top Bottom