Feisal Salumu: Nimeondoka Yanga kutokana na manyanyaso, nilizungumza na Rais wa Yanga kwa saa 6, nikamwambia nataka kuondoka

Feisal Salumu: Nimeondoka Yanga kutokana na manyanyaso, nilizungumza na Rais wa Yanga kwa saa 6, nikamwambia nataka kuondoka

watu wengi ambao mnauelewa mdogo wa kufikiri mnarukia kwenye cheap issues lakini hamtizami tatizo kuu. wachezaji wengi hasa wa kitanzania wana changamoto ya elimu kutokana na mfumo uliopo wa maisha yetu kwamba shule ikikushinda unakimbilia mpira na kipaombele ni kupata pesa tu bira kutizama mustakabari mzima wa maisha.

maana yake mpira haukua kama ajira rasmi. na hapo TFF na baraza la michezo liliunda sheria na kanuni za kulinda haki za wachezaji na vilabu. Lakini kwakua soka letu limeshakua TFF na baraza la michezo linatakiwa liunde chombo rasmi kinachojitegemea kwaajili ya kusikiliza kesi zinazowahusu wachezaji na vilabu vya mpira.

hilo halijafanyika hivyo ni kasoro kwasababu wachezaji wetu wandani hawana uwezo wa kumudu gharama za kwenda CAS badala yake wangeweza kufungua kesi katika mahakama za michezo hapahapa Tanzania.

wapo wachezaji wengi tu wanachangamoto kama alizonazo Feisal lakini kwasababu ya ukubwa wa Jina alilonalo Feisal ndio maana linatizamwa kwa ukubwa lakini ukweli wapo wengi.

so ni muda muafaka sasa wa Rais wa TFF kushirikiana na Waziri wa michezo kuanzisha mchakato wa mahakama ya michezo.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Feisal laani inamuandama.

Timu za Yanga na Simba si za kuzichezea, angeondoka kwa kufuata taratibu na si kwa kujifanya mjuwaji.

4e60009438e942acad4e267c17a6febd_350533381_963882314760569_6674677573109426796_n.jpg



Bandiko alihusiani na hii thread.
 
Tusi NI neno ambalo litamkera mtu, Kama Hersi alijibu neno la hovyo yeye akidhani ni jepesi basi limemkera mama na mtoto. Na Kama hakutukana kwa nini Fei anasema Eng. alimuomba msamaha? Kuwa wa mwisho ni hiari ya mtu mkuu.
Kwa hiyo ni kweli Hersi alimtukana Mama Fei akamuita andazi na ndio maana akamuomba msamaha?! Andazi?! Andazi?! Andazi?!
 
Mimi najiuliza,huyu Hersi si ni mwajiriwa wa GSM? Kama yeye ni mwajiriwa huo mkataba wake wa ajira angekuwa anafanyiwa haya mazonge angeweza kudumu hapo GSM.Tunasahau point ya msing ya Fei kuwa anacholilia ni hatma ya maisha yake na watu wanatanguliza ushabiki na upenzi wao wa Team.

Fei ana hoja asikilizwe.
Nakazia asikilizweeee [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 

"niliambiwa na viongozi wa Yanga kuwa nauza mechi iliniuma sana na nikipokuwa nawapigia simu hao viongozi waliokuwa wanatamka hayo maneno hawapokei simu yangu.

"Viongozi walikua wanamtukana mama yangu na kutoa matusi ya kumnyanyasa hata ingekua ni wewe ndugu mwandishi usingekubali kutukaniwa mzazi"

"Kula ugali kwa sukari sikula saivi nilikula kipindi kile timu bado ilikua ipo chini kiuchumi na kuna muda tulicheleweshewa mishahara lakini Mama aliniambia vumilia mwanangu maana alikua ni mpenzi wa mkubwa wa Yanga.

"Mama kuna muda mwingine alinipa pesa yake tulipokua tumecheleweshewa mshahara."

Mwandishi: Tueleze umepitia manyanyaso gani?

"Naambiwa nauza mechi, viongozi wananitukana na nikiwaambia familia wanasema nivumilie.

"Mama yangu alikuja Dar wakamtukana na kuanza kumpa maneno ya kejeli."

"Huyo huyo Raisi anatuma watu wamtukane mama yangu wanamuita mama yangu andazi "

Wanitukane Mimi lakini siyo mama yangu maana mama yangu ni pepo yangu"

"Nimekaa masaa sita na Engineer Hersi kuwa hapa nilipofikia nataka niachane na Yanga na Hers alisema kuwa bado anahitaji huduma yangu"

Raisi: anampigia simu mama na mama aliniambia niende kusaini mkataba na mama alimwambia mpe Fei mkataba wa miaka miwili"

Hers aliongeza mwaka mmoja badala ya miaka miwili"

"Mimi sijui kiingereza walinipa mkataba wa miaka mitatu"

"Signing fee sijapewa kwa wakati nilipewa kidogo kidogo tena kwa kutumiana meseji za vitisho"

"Nataka kukusanya milioni 60 niende CAS na watanzania wengi wananichangia na utaratibu umeanza tunasubiri invoice"

"Unajua yanga ni taasisi kubwa na Mimi ninawapenda wanayanga nilimwambia hers ata Kama alinikosea Ila nilimwambia tukae chini tumalizane na hers alikili makosa yake lakini Mimi nilitaka tuachane nikatafute maisha sehemu nyingine"

"Nilimwambia eng Hers bmkubwa alikuambia Miaka miwili lakini ukanipa mitatu lakini hers hakunijibu"

"Familia yangu wanaipenda Yanga lakini kilichonitoa Yanga ni manyanyaso"

"Hakuna timu inayonitaka na ndiyo maana nilitaka kuvunja mkataba niende kutafuta maisha yangu pengine"

"Tumekaa na familia yangu niliona Bora tuvunje mkataba na niliwaomba viongozi tuachane nilichangiwa pesa na familia"

"Mimi siwezi kula dhuluma siwezi kula pesa ambayo siifanyii kazi na ndiyo maana wakituma pesa zinarudi"

"Mimi sipendi hizi kelele nataka hili Jambo liishe na nafsi yangu haitaki kucheza Yanga na ndiyo maana nilikaa nao chini viongozi chini tuyamalize nikatafute maisha sehemu nyingine"

",Kama Jambo litakua haliishi ni bora nikae nyumbani maana ndiyo mwenyezimung atakua amepanga hivyo" kipaji kuisha.

"Hers anasema nauza mechi kun pass moja nilimpa Mayele aongeze magoli mbele ya kipa lakini Mayele alikosa hapo Hers akaanza kusema kuwa nauza mechi"

"Nilimtafuta GSM aje kutafuta suluhu lakini hakupokea simu zangu lakini aliposikia sakata Hili ndiyo akaanza kunitafuta na Mimi sikupokea simu yake"

"Nilikutana Hers akasema kuwa anataka nirudi Yanga nilikataa basi akaniambia niende CAS"

"Hers anadharau kubwa sana na Msolwa alikua ni mkarimu sana"

"Watu hawajiulizi ni kwa nini Fei hajaondoka katika kipindi kile Cha Yanga ngumu lakini nimeondoka kipindi hiki kizuri".

"Mimi nina matatizo na Raisi wa club Sina Tatizo na club Ila hers ndiyo Raisi wa club ndiyo Nina tatizo nae"

"Mpaka Sasa hela haijatosha Ila nashukuru Watanzania wameshanichangia kiasi cha shilingi milioni tisa (9)

"Mimi Nina rafiki na ndugu na wengine wapo humo humo ndani ya klabu ya yanga ndiyo walinichangia kurudisha pesa ili nivunje mkataba."

"Naitakia kila la heri Yanga katika fainali yake huko Algeria na nitaiombea Dua mungu ifanye vizuri"

"Mimi nimeongea yote lakini nafsi yangu haitaki kurudi kabisa Yanga sc"
Safi sana Feisal kwa kupigania haki yako... inshaallah utawashinda hawa watesi wako.
 
watu wengi ambao mnauelewa mdogo wa kufikiri mnarukia kwenye cheap issues lakini hamtizami tatizo kuu. wachezaji wengi hasa wa kitanzania wana changamoto ya elimu kutokana na mfumo uliopo wa maisha yetu kwamba shule ikikushinda unakimbilia mpira na kipaombele ni kupata pesa tu bira kutizama mustakabari mzima wa maisha.

maana yake mpira haukua kama ajira rasmi. na hapo TFF na baraza la michezo liliunda sheria na kanuni za kulinda haki za wachezaji na vilabu. Lakini kwakua soka letu limeshakua TFF na baraza la michezo linatakiwa liunde chombo rasmi kinachojitegemea kwaajili ya kusikiliza kesi zinazowahusu wachezaji na vilabu vya mpira.

hilo halijafanyika hivyo ni kasoro kwasababu wachezaji wetu wandani hawana uwezo wa kumudu gharama za kwenda CAS badala yake wangeweza kufungua kesi katika mahakama za michezo hapahapa Tanzania.

wapo wachezaji wengi tu wanachangamoto kama alizonazo Feisal lakini kwasababu ya ukubwa wa Jina alilonalo Feisal ndio maana linatizamwa kwa ukubwa lakini ukweli wapo wengi.

so ni muda muafaka sasa wa Rais wa TFF kushirikiana na Waziri wa michezo kuanzisha mchakato wa mahakama ya michezo.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
Naunganaa na wee. Uko sahihi
 
Feisal laani inamuandama.

Timu za Yanga na Simba si za kuzichezea, angeondoka kwa kufuata taratibu na si kwa kujifanya mjuwaji.

View attachment 2642385


Bandiko alihusiani na hii thread.
Ushabiki bana. Fei ameshasema hana tatizo na Yanga ana tatizo na Hersi, ila bado unaiingiza Yanga. Au Hersi ndo Yanga? Mnasahau kuwa kunaweza kuwa na tabia binafsi za viongozi ambazo sio tabia za club. Hapa Hersi anatakiwa aulizwe una tatizo gani binafsi na Fei? Maana anasema ana shida na wewe sio Yanga.
 
Back
Top Bottom