FIFA Women's World Cup 2023 | Kombe la Dunia kwa Wanawake

FIFA Women's World Cup 2023 | Kombe la Dunia kwa Wanawake

Hao weshenzi wametufungia hio video tusione ni chuki au? Ukiwasha VPN inaonyesha pumbavu
 
Hata FIFA TV hawa weki highlights

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
FIFA huwa hawaweki chochote mpaka baada ya mwezi mzima tangu mashindano yaiseh wakati mwingine inawachukua hata miezi miwili. Jaribu kugoogle "Bein TV" ndiyo mimi hutumia kuangalia mashindano ya CAF na ya UEFA bure. Link yake kutokea huku imeziba michezo inayopendwa na watu wa huku ikiwamo hiyo World CUP.
 
Mchezo baina ya Uholanzi na South Afrika umeshaanza ingawa hadi nakuja kwenye compyuta Uholanzi ilikuwa inaongoza kwa bao 1-0 lililofungwa dakika ya tisa tu. Hata hivyo ndiyo mchezo umeanza ngoja tuone utakwishaje. Katika dakika hizi za kwanza Uholanzi wamekuwa kwa spidi kubwa na wamemiliki mpira sana. Hatujui kama hiyo itakuwa ni nguivu ya soda tu kabla dada zetu Banyana Banyana hawakunjua makucha yao.

Banyana Banyana wameanza kukiwasha sasa. Naona wameanza kuwa masimba jike wenye njaa. wameanza kuwakamia Uholanzi kama nini ingawa bado uholanzi wanatawala mchezo lakini wameanza pia kupoteza petroli.

Naona Uholanzi wameanza kuchoma mafuta tena na kuongeza mashambulizi kwenye lango la Banyana Banyana lakini bila madhara yoyote.

Hawa wasichana wa Banyana Banyana kweli wanalijua boli. Pamoja na kufungwa wana-control mpira vizuri sana. Mambo yanaweza kugeukia upande wao wakati wowote ingawa Uholanzi imeweka ulinzi mkubwa sana langoni mwao baada ya kupata bao mapema.

Mpaka Half-time mabao bado ni 1-0 huku Uholanzi ikiongoza. Hata Hivyo dakika za mwisho Banyana Banyana walilishambulia sana lango la Uholanzi na walimiliki mpira kwa kiwango kikubwa sana kiasi kuwa kipindi cha pili kinaweza kuwa chao.

Nimeshaona wasichana hawa wa uholanzi wakimwomba refa amalize mpira mara moja. Inaonyesha kuwa kipindi cha pili Uholanzi watakuwa defensive sana, wanaelekea kucheza na walinzi wengi sana kulinda goli lao moja.

Kipindi cha lala salama kimeshaanza. Tuwaombee sana dada zetu wa Banyana Banyana; wameanza kwa masmabulizi makali sana dhidi ya Uholanzi.

Uholanzi wamepata goli la pili mwanzoni tu mwa kipindi cha pili. Matumaini ya Banyana Banyana yanaanza kupungua japo wameonyesha mchezo mzuri sana. Good news! Bao hilo limekataliwa

Banyana Banyana hawaonyeshi kukata tamaa na wameanza tena kwa nguvu ile ile.

Uholanzi imetonesha kidonda kwa kuongeza bao la pili. Sasa kazi itakuwa ngumu sana kwa Banyana Banyana.

Baada ya kupata goli la pili, wanawake wa uholanzi wamekaza misuli sana kulilinda goli. Banyana Banyana wanapata wakati mgumu sana kupenyeza.

Tuko kwenye dakika za majeruhi na tayari Banyana banyana wameshakata tamaa. Ninachoogopa ni kwamba wasijekuruhusu goli la tatu kutokana na kukata tamaa. Ilivyofika dakika ya tisini nilikaribia kupata heart attack kwa masikitiko ila nikavuta bia moja baridi nikapona.

Haya jamani, mpira umekwisha na Uholanzi wameibuka kidedea kama ambavyo wale akina Sheikh Yahya wa mchongo niliopost hapo juu walivotabiri. Nasubiri FOX wapandishe video za highlights niziweke hapa. Mchezo unaofuata ni baina ya Marekani na Sweden ambao utachezwa saa 6 mchana saa za Tanzania.


Siku njema!
 
Mchezo baina ya Uholanzi na South Afrika umeshaanza ingawa hadi nakuja kwenye compyuta Uholanzi ilikuwa inaongoza kwa bao 1-0 lililofungwa dakika ya tisa tu. Hata hivyo ndiyo mchezo umeanza ngoja tuone utakwishaje. Katika dakika hizi za kwanza Uholanzi wamekuwa kwa spidi kubwa na wamemiliki mpira sana. Hatujui kama hiyo itakuwa ni nguivu ya soda tu kabla dada zetu Banyana Banyana hawakunjua makucha yao.

Banyana Banyana wameanza kukiwasha sasa. Naona wamanza kuwa masimba jike wenye njaa. wameanza kuwakamia Uholanzi kama nini ingawa bado uholanzi wanatawala mcheazo lakini wameanza kupoteza petroli.

Naona Uholanzi wameaza tena kuchoma mafuta tena na kuongeza mashambulizi kwenye lango la Banyana Banyana lakini bila madhara yoyote.

Hawa wasichana wa banyana Banyana kweli wanalijua boli. Pamoja na kufungwa wana-control mpira vizuri sana. Mambo yanaweza kugeukia upande wao wakati wowote ingawa Uholanzi imeweka ulinzi mkubwa sana langoni mwao baada ya kupata bao mapema.

Mpaka Half-time mabao bado ni 1-0 huku Uholanzi ikiongoza. Hata Hivyo dakika za mwisho Banyana Banyana walilishambulia sana lango la Uholanzi na walimiliki mpit=ra kwa kiwangu kikubwa sana kiasi kuwa kipindi cha pili kinaweza kuwa chao.

Nimeshaona wasichana hawa wa uholanzi wakimwomba refa amalize mpira mara moja. Inaonyesha kuwa kipindi cha pili Uholanzi watakuwa defensive sana, wanaelekea kucheza na walinzi wengi sana kulinda goli lao moja.

Kipindi cha lala salama kimeshaanza. Tuwaombee sana dada zetu wa Banyana Banyana; wameanza kwa masmabuliz makali sana dhidi ya Uholanzi.

Uholanzi wamepata goli la pili mwanzoni tu mwa kipindi cha pili. Matumaini ya Banyana Banyana yanaanza kupungua japo wameonyesha mchezo mzuri sana. Good news! Bao hilo limekataliwa

Banyana Banyana haonyeshi kukata tamaa na wameanza tena kwa nguvu ile ile.

Uholanzi imetoesha kidonda kwa kuongeza bao la pili. Sasa kazi itakuwa ngumu sana kwa Banyana Banyana.

Baada ya kupata goli la pili, wanawake wa uholanzi walikaza misuli sana kulilinda. Banyana Banyana wanapata wakati mgumu sana kupenyeza.

Tuko kwenye dakika za mejruhi na tayari Banyana banyana wameshaka tamaa. Ninachoogopa ni kwamba wasijekuruhusu goli la tatu kutokana na kukata tamaa. Ilivyofika dakaia ya tisini nilikaribia kupata heart attack kwa masikitiko ila nikavuta bia moja baridi nikapona.

Haya jamani, mpira umekwisha na Uholanzi wameibuka kidedea kama ambavyo wale akina Sheikh Yahya wa mchongo niliopost hapo juu walivotabiri. Nasubiri FOX wapandishe video za highlights niziweke hapa. Mchezo unaofuata ni baina ya Marekani na Sweden ambao utachezwa saa 6 mchana saa za Tanzania.


Siku njema!
Ripoti ya leo ni nzuri sana... Masikitiko ni kwa Banyana Banyana.
Hapana shaka watakuwa wamepata uzoefu fulani kwa fainali hizi...
 
Video ya highlights za mchezo wa Banyana Banyana na Netherlands ni hii hapa. Sitaeleza chochote zaidi ya nilivyopost hapo juu

 
Ripoti ya leo ni nzuri sana... Masikitiko ni kwa Banyana Banyana.
Hapana shaka watakuwa wamepata uzoefu fulani kwa fainali hizi...
Banyana Banyana wamecheza mchezo mzuri sana; muda wote kocha wa Netherlands alikuwa anasumbuliwa na presha kupanda na kushuka. Amemeza vidonge vingi sana kuponya maisha yake; ukimwambia mchezo urudiwe hatakubali kabisa.
 
Mchezo unaofuata ni baina ya Marekani na Sweden; utaanza saa sita mchana (saa za Tanzania). Nitajaribu kuleta progress report lakini kwa vile nitakuwa kwenye majukumu mengine ninaweza kupoteza events nyingine kwani sina uwezo wa kuwa kwenye TV, na kwenye computer mbili kwa pamoja.
 
images (38).jpeg


Huu uzi mtamu sana
 
Mchezo wa leo baina ya Sweden na USA ulikuwa mzuri sana na USA walicheza vizuri sana wakiutawala uwanja. Kwa jumula timu USA waliielemea sana Sweden, ila kama nilivyowahi kuandika huko nyuma, USA haina wafungaji. Baada ya Rose Lavelle kupewa kadi mbili za njano wakati wa makundi hakucheza mchezo huu na kusababisha timu imtegemee Lindsey Horan, na Alex Morgan zaidi has kwa vile Sophia Smith hana uzoefu. Sasa Ingawa wote ni wacheazji wawili, center forwad Alex Morgan hana shabaha langoni tena kama zamani (sijui labda baada ya kujifungua). Timu USA ilipata nafasi nyingi sana lakini zote zikapotea mpaka nikazimia, ndiyo maana nimechelewa kuandika post hii. Ama walikuwa wanapiga nje ya goli au walikuwa wanamlenga golikipa au walikuwa wanachelewa kutoa uamuzi hadi wanabanwa kushindwa kufunga. Hakuna mshambuliaji aliyetoa mashuti kama yale aliyokuwa akipiga Christen Press yanayomfuata kipa halafu yanapiga kona angani.

Baada ya dakika 90 wakaongezewa nyingine 30 nako hawakupata kitu. Zikaja mikwaju ya Penalty ambazo ndizo zilzioamua ubishi.

Sweden walipiga penalty moja nje, na penalty nyingine ikazuiwa na golikipa wa marekani, na hivyo kupata penaly tatu. Lakini sasa marekani ilivurunda sana kwa kutoa penalty mbili nje, yaani moja ya veteran Megan Repinoe ilikwenda nje kabisa, halafu nyingine ya Sophia Smith nayo ilikwenda nje hivyo timu zote zikamaliza penalty kwa 3-3 (utaona kuwa Marekani wafungaji ndio walikuwa pumba kabisa)

Sasa walipoingia kwenye kipindi cha penalty za moja moja, Marekani bado Kelley O'Hara naye alishindwa kufunga penalty moja kwa kugonga mwamba na na kuisababaisha Sweden kupata goli la ushindi lilioamuliwa kwa VAR kwa sababu golikipa Alyssa naeher alidaka mpira ukiwa umeshapita zaidi ya nusu ya msitali kama inavyoonekana picha hii hapa chini. Matokeo ya mwisho yakawapa Sweden ushindi wa 5-4

Ingawa timu ya Merakani niliyokuwa nashabikia imetolewa, ilicheza mpira mzuri sana leo kuliko walivyocheza na Ureno; wanatakiwa kujifunza jinsi ya kufunga kwani ushindi ni kupenyeza magoli nyavuni.

1691331806019.png

Goli lililoipa ushindi Sweden

Highlights za mchezo huo ni hizi hapa; kwanza ni mchezo wa dakika 120



Halafu mikwaju ya penalty.



Baada ya Banyana Banyana na Team USA kuondolewa, sasa nimebakiza timu nne tu za kushabikia kwa order hii: Nigeria, Jamaica, Morocco, Japan na Australia; usiniulize kwa nini. Mchezo unaofuata ni baina ya Nigeria na Uingereza ambao utachezwa kesho saa 4 na nusu asubuhi (saa za Tanzania)
 
hya jamani timu yangu pendwa ya Nigerai nayo imetolewa kwenye mtanange huu. Hata hivyo nakiri kuwa Nigerai ilicheza mchezo mzuri sana na waliilemea sana Uingereza. Yaani goli la Uingereza lilishambuliwa kwa nguvu kama nyuki. Nawapa sifa sana magolikpa wote wa Uingereza na Nigeria kwani kuna wakati beki wa Nigera alifanya makosa ambayo nusura yasababisha bao ndani ya box lakini golikipa wa Nigeria akalipangua. Mchezaji wa uingereza Lauren James (wa Mwananchi B) alipewa red card mwishoni mwa dakaika ya 89 kwa kumkanyaga mchezaji wa Nigeria kwa makusudi. Mpaka dakika tisini mpira ulikuwa bado ni droo ya 0-0.

Hivyo zikaongezwa dakika 30 ambazo pia hazikubadili matokeo na kuingia matuta ya penalty.

Timu zote zilipoteza kick ya kwanza kwa kupiga nje. Hata hivyo uingereza ilipata kick zote nne zilizobaki wakati Nigeria ilipoteza kick la pili pia. Sasa kwa vile Uingereza ndiyo ilikuwa inaanza kupiga penalty, ilipopata penalty ya nne zbasi Mchezo ukaisha na kuiacha Nigeria ikipiga penaly nne tu na kuishia kupata mbili, hawakuruhusiwa kupiga penalty ya tano kwa vile isingebadilisha matokeo..

Pamoja na kutolewa nje ya mashindano haya, kweli Nigeria walicheza boli zuri sana ambalo hata mimi sikulitegemea, Leo wamecheza vizuri zaidi ya siku walivyoifunga Australia, yaani standard yao kwa leo ilikuwa ya juu sana.

Dakika 120 za mchezo



Mapigo ya Penalty

 
Mchezo wa mwisho kwa leo iulikuwa baina ya Australia na denmark, na kama ilivyotarajiwa Australia imeibamiza denmark mabao 2-0. Ingawa nimeshapoteza timua tatu katilkka list ya timu zangu pendwa za S.Africa, USA, Nigeria, Jamaica, Morrocco, Australia, na Japan, Australia imenifuta machozi kwa leo. Nitaleta Video hapo baada ya Fox kuzipandisha.



Michezo ya kesho itakuwa kati ya Colombia na Jamaica hapo kesho saa 5 asubuhi (saa za Tanzania pamoja na ule kati ya Ufaransa na Morroco saa 8 mchana (saa za Tanzania)
 
Mpaka sasa bado Colombia na Jamaica wanamenyana, mchezo ni mkali sana kwa pande zote mbili ingawa Colombia wanaelekea kuwaelemea Jamaica. Ndiyo sasa tu wameanza kipindi cha pili; nilichelewa nusu ya kipindi cha kwanza. Nitaingalia baadaye kwa vile niliurecord kwa kujua nitauchelewa.

Mashambulizi ya Colombia kwenye dakika ya sita ya kipindi cha pili imezaa matunda na hadi sasa hivi Colombia inaongoza 1-0.

Mchezo umedumaa sasa. Mashambulizi yamepungua, umebakia kuchezewa katikati tu kwa vile Colombia imeamua kuimarisha ulinzi wa golia lake na hivyo kupunguza kasi ya kushambulia huku pia ikidhibiti mashambulizi kutoka Jamaica.

Colombia wamezidi kuwa wakali wa kulinda golia lao; Jamaica wanatawala sana mchezo na wanajaribu kushambulia lakini Ulinzi wa Colombia hauna utani kwenye kuzuia mashambulizi hayo. Zimebaki dakika saba tu kumaliza ngwe ya dakika tisini. Miujiza hujitokeza dakika za mwisho kwa hiyo bado hope ipo.

Ngoma imekwisha na Colombia ameibuka kidedea kwa 1-0. Dada zangu wa Jamaica "wamekufa kiume." Ngoja niwasubiri Fox watuwekee video nizilete hapa.

Highlights za mchezo huo ni hizo:

 
Mpira wa wanawake unavutia sana kuliko mpira wa wanaume. Kwanza wana spidi sana na wanatumia ufundi mwingi mno; hawatumia maguvu kama wanaume. Kama unapenda burudani ya mpira, basi lazima vigezo vyako viwe spidi na mbinu. Ndiyo maana huwa nayafuatilia mashindano haya kwa uzito sawa na yale ya wanaume. Hata mwaka 2019 nilijaribu kuyafuatlia kwa karibu na kuweka record zake hapa 2019 FIFA Women's World Cup
 
Back
Top Bottom