FIFA Women's World Cup 2023 | Kombe la Dunia kwa Wanawake

FIFA Women's World Cup 2023 | Kombe la Dunia kwa Wanawake

Ushindi wa Colombia sikuhutegemea kabisa... Hongera zao!
Hata mimi; nilikuwa na matumaini makubwa sana na Jamaica. Hata hivyo michezo ya mwaka huu ina surprises nyingi.

Ukiangalia vizuri utagundua kuwa Colombia walikuwa na mbinu nzuri sana za ushindi. Hawakutaka ushindi wa mabao mengi, hivyo baada ya kupata bao moja, mbinu yao ya kulilinda ilfanikiwa sana kwani baada hayo Jamaica ilipata tabu sana kufikia goli la Colombia na wala Colombia hawaksuahambulia tena lango la Jamaica japokuwa hiyo mbinu ni risky sana.
 
Mpira wa wanawake unavutia sana kuliko mpira wa wanaume. Kwana wana spidi sana na ufundi mwingi mno; hawatumia maguvu kama wanaume. Kama uanepnda burudani ya mpira, basi lazima vigezo vyako viwe spidi na mbinu. Ndiyo mnaana huwa nayafuatilia mashindano haya kwa uzito sawa na yale ya wanaume. Ndiyo maana hata mwaka 2019 nilijaribua kuyafuatlia kwa karibu na kuweka recod zake hapa 2019 FIFA Women's World Cup
Yaani wanawake Wana spidi kuliko wanaume na ufundi kuliko wanaume??? Hahaha acha bangi
 
Yaani wanawake Wana spidi kuliko wanaume na ufundi kuliko wanaume??? Hahaha acha bangi
Hujui mpira wewe kama unadhani tulioangalia mashindano haya kwa miaka takriban miaka 35 hatujui sifa za mpira. Nadhani unasumbuliwa na tatizo la misogyny, yaani kuamini kuwa wanawake ni inferior kwa wanaume.
 
Nlikua timu Jamaica sasa hivi nipo Sweden

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Hata mimi nilikuwa Timu Jamaica pia ila sasa nahamia Morocco. Ingawa nina wasiwasi kuwa watafungwa tu kwa vile Ufaranza ni timu ya tishio sana lakini lazime mtu upende chako. Mrocco ni sehemu ya Africa na ndio pekee wamebakia kwenye mashindano hayo.

Mpaka sasa bado mabao ni 0-0 ingawa Ufaransa imeanza kwa mashambulizi makali sana dhidi ya Morocco.

Ufaransa ina hawa wanawake wawili kwenye forward line ambao ni hatari sana: Eugenie na Kadiditou. Hawa wanawake ni laani sana uwanjani.

Angalia formationa za timu leo uwanjani kama zilivyotolewa na FIFA

1691493465356.png
 
Hujui mpira wewe kama unadhani tulioangalia mashindano haya kwa miaka takriban miaka 35 hatujui sifa za mpira. Nadhani unasumbuliwa na tatizo la misogyny, yaani kuamini kuwa wanawake ni inferior kwa wanaume.
Mpira nimeangalia na Nafwatilia, mpira ni mchezo wa wazi unachokisema si kweli
 
Kama ilivyotegemewa, haikuchukua muda kwa Kadidiatou kufanya mambo yake ya kuipatia Ufaransa goli la kwanza ndani ya dakika 19 tu. Mpaka sasa Ufaransa inaongoza 1-0
 
Mpira nimeangalia na Nafwatilia, mpira ni mchezo wa wazi unachokisema si kweli
Sitaki kubishana na wewe; sasa hivi focus yangu iko kwenye mpira unaondelea uwanjani ambao sidhani kama unaujua bali unasubili kusimuliwa matokeo.
 
Dah! Ufaransa imeanza mauaji kwani baada ya dakika tano tu wameongeza bao la pili; mpaka sasa Ufaransa inaongoza 2-0. Morocco wasijifanye kichwa cha mwendawazimu.

Kabla sijamaliza post, Ufaransa wameongeza bao la tatu kupitia Eugenie; hii sasa ni aibu. Ndani ya dakika 25 tu tayari mabao matatu. Sitaki kuishabikia Morocco tena kwani nitapata ugonjwa wa moyo bure: ninaisubiri Australia na Japan tu.

Morocco hawachezi kwa ile confidence waliyoonyesha kwenye michezo yao miwili ya mwisho wakati wa makundi. Sijui wanaigopa France kwa vile walikuwa colonial masters wao au vipi, ila kweli Morocco imeelemewa mapema sana.

Mchezo umepoa kidogo kwa vile inaonekana France imepunguza mashambulizi kwa makusudi ila wamebaki kuwadhiti Morocco ambao hawashambulii lango la France, kwa hiyo mcheazo unabaki katikati tu.

Kwa jumla spidi ya mchezo haisisimui tena kwani inaonekana mindsets za timu zimeshakamilika: Morocco hawana hamu ya kuendelea na mashindano haya, wakati Ufaransa imeshajiahakikishia nafasi ya kuendelea robo fainali.

Sasa hivi ni half time lakini nimekata tamaa na Morocco; nina wasi wasi kuwa wakibahatika kufunga goli moja tu, basi Ufaransa itafungulie mizinga mingine ya magoli. Ngoja tusubiri.

Kipindi cha pili kimeshaanza
 
Ndani ya Kipindi cha Pili Eugenia ameongeza tena bao jingine kwenye dakika za sabini hivi hivyo sasa Ufaransa inaongoza kwa 4-0. Utakuwa ni muujiza mkubwa sana kwa Morocco kurudisha mabao hayo manne na kuongeza moja la ushindi ndani ya dakika kumi zilizobaki.

Ndani ya dakika za majeruhi sasa

Mchezo umekwisha na Ufaransa kaibuka kidedea wa nguvu sana kwenye round of 16 kwa kuifunga Morocco 4-0. Round hii ilikuwa ngumu kwa timu nne zikiishia kwenye penalty Kicks lakini ufarasa imejisafishia njia mapema sana. Nasubiri rafiki zangu wa Fox watoe video niilete hapa.



Sasa Michezo ya robo fainali inayofuata ni kama ifuatavyo hata chini; kuna mapumziko ya siku mbili hadi Alhamisi


1691500020465.png
 
# TeamFrance ..,
Sasa hivi nina timu nne: France, England, Netherlands, na (Japan/Sweden kwa pamoja). Kwenye mchezo wa Japan/Sweden, ambazo zote ni timu nzuri, mshindi wa mechi hiyo ataweza kuingia fainali na huenda kuchukua kombe. Ufaransa pale kuna forwad line wawili (Diani Kadidioatou na Eugenie Le Sommer) wanajua kutafuta magoli. Halafu pale kuna midfielder ambaye ndiye ndiye mwanamke mrefu sana kwenye timu zote anaitwa Wendie Renard; anajua sana kuongoza timu nzima kimchezo. Kuishinda France inabidi wanawake hawa watatu wazimwe pumzi. Marekani ndiyo ilikuwa inajuwa kuwazima pumzi vizuri sana hadi wanakasirika, lakini sasa Marekani imeshatolewa kwa hiyo njia yao iko wazi sana.
 
Sheikh Yahya mwingine wa quarter finals



Nakubaliana naye kuwa Sweden itafungwa kwa vile imevuka kutokana na makosa ya strikers wa Marekani, siyo kwa sababu ya ufundi wao kama timu. Strikers wa Marekani ndio waliozamisha timu yao.
 
Mchezo unaofuata ni kati ya Uholanzi na Spain ambao utachezwa ijumaa saa 10 za usiku kwa saa za Tanzania. Amka mapema siku hiyo uuangalie kabla ya kwenda kazini. Utakuwa ni mchezo wa kuvutia sana ingawa Uholanzi inapewa nafasi kubwa sana ya kushinda bila kusahau kiuwa matokeao ya mwaka huu yamekuwa hayatabiliki - anayetegemea kushinda ndiye anayeweza kutolewa.
 
Samahani kidogo nilijasahau kuwa mimi ni modereta wa thread hii nikaishia kwenye nyama za kuchoma, bia na TV tu. Sasa nimerudi kwenye meza yangu

Mpaka kipindi hiki cha pili, mceazo kati ya Spain na Uhloanzi bao wako suluhu ya 0-0. Hata hivyo Spain imekuwa ineaielemea sana Uhloanzi kwa mashambuliz mengi na makali sana. Uholazi inabebewa vizuri sana na defence line yao ikiongoza na golikipa wao.

Kuna wakati Spain walifunga bao lakini likakataliwa

Kuanzia sasa nitakuwa kwenye keyboard hii kuleta updates kadri ninavyozipata.

Mshambuliaji wa Uholanzi amefanyiwa faulo kwenye box, kwa hiyo wanaelekea kupata penalty. Hapana, penalty hiyo imekataliwa baada ya kupitia VAR.

Mchezo ni mgumu sana ila Spain wamewalemea sana uholanzi kwa msambuliz. Goli la Uholanzi halina amani hata kidogo.

Spain wamepata penalty na kujipatia goli la kuongoza. hadi sasa matokea ni kuwa Spain ineongoza kwa 1-0 na zimebakti kama dakika nane tu pamoja na zile za majeruhi ili mchezo uishe. Mashinadno haya yana maajabu sana kuwa timu zilizotegemea sana ndizo zimeondolewa au kupata wakati mgumu sana. Inaelekea Uholanzi sasa hivi ni kwishney.

Zimebaki kama dakaika tatu na nawaona Uholazi wameshakata tamaa wala hawajishughulishi kufanya mashambuliz yoyote. Katika mcehzo wote Uholazi walikuwa wanauzia tu, hawakuwa washambuliaji kabisa, jambo lililonishangaza sana kulingana na kuwa walikuwa wanapewa uwezeiakno mkuba. Labda wamekula hela za makampuni ya kamari.

Mchezo uko kwenye dakika za mejeruhi sasa, na Spain wameimarisha ulizi wao sana ukizingatia kuwa hata fowardline ya Uholanzi ni dhaifu sana.

Astaghfirullah! Uholanzi wamesawazisha ndani ya dakika za majeruhi; sikuamini hivyo. Sasa ngoje nilete bia zaidi kujiandaa na dakika nyingine 30 za burudani ingawa Uholanzi hawachezi vizuri.

Haya sasa; dakia 90 official pamoja na zile za majeruihi ndiyo zimekwisha, na msimamo bado ni 1-1 ingawa marefa waliweka dakika nyingi sana za mejeruhi (zaidi ya robo saa) nadhani wakitegemea timu moja itaibuka kidedea lakini wapi. Ngoja sasa tusibiri muda wa nyongeza.

Wachezaji wamepewa muda kidogo wa mapumziko na kusikiliza mafundisho ya mbinu kutoka kwa waalimu wao kabla ya kuanza ngwe ya inayofuata.

Haya jamani; ngwe ya lala salama imeanza. Timu zote mbili zina tension kubwa sana ila naona Spain wameanza kwa kuwaheshimu Uholazi. Ile spidi waliyokuwa nayo kipindi cha kwanza imepungua sana, au labda wameishiwa petroli. Ila mashindano ya mwaka huu hayatabiliki hadi kipenga cha mwisho.
SPain imeanza tena kukiwasha lakini siyo kwa spidi ile ya kipindi cha kwanza.

Time zote zimefanya subs. Nilisoma kuwa Uholanzi ilimwondoa Damari na kuwemka Katarina kwenye safu ya Ulinzi. Spain nayo walimwondoa Eva na kuweka Esta kwenye safu ya ushambuliaji; Spain pia imefanya mabadiliko mengine ambayo majina ya wahusika ni ya kizungu sikuweza kuyakumbuka.

Sasa hivi dakika 15 za kwanza kwenye kipindi cha nyongeza zimekwisha; wachezaji wote wanapumzika dakika tano. Bado matokeo ni 1-1.

Kipindi cha pili cha dakika za nyongeza kimeanza; uholanzi ilfanya subsa za watu wenye majina ya kizungu tu. kwa hiyo timu zote mbile zimefanya subs mbili mbili.

Spain wanapata goli la pili kutokea kwa Salma aliyeingia kama sub kwenye kipindi cha pili. Mpaka sasa Spain inaongoza 2-1

Zimbeaki dakika tatu official pamoja na zile za mejeruhi.

Tuko kwenye dakika za majeruhi na matokeo hayajabadilika.

Mchezo umekiwasha Spain kaibuka kidedea kwa 2-1. Fox wakishaleta video nitazishare hapa. Mchezo ulikuwa mzuri sana kwangu hasa kwa vile nilikuwa sishabikii timu yoyote niliufurahia sana.


 
Back
Top Bottom