Fifa XI 2015, kulikoni wachezaji EPL?

Fifa XI 2015, kulikoni wachezaji EPL?

Waingereza huwa wananichekesha sana... Wanasema wao ndio walianzisha mpira huku duniani, Sasa wenzao Wamarekani wanawacheka, wanawaambia kwanini mnasema mlianzisha mpira wakati hamshindi chochote kwenye mashindano ya kimataifa yama World Cup au Europe Cup... Wenzao wamarekani wanasema tulianzisha Basketball na kweli Olympics zote wao ndio wanachukua Gold Medal...

Ifike mahali Uingereza wakubali kwamba wao ni vilaza kwenye mpira ila ni media tu inawabeba... Sasa yule wanayemwita White Pele Runinga hajawahi kuchukua kiatu cha mfungaji bora hata mara moja kwenye ligi yao... Wanachukua wageni tu kutoka nchi zingine..
uingereza hakuanzisha mpira,aliuboresha tu
 
tofautisha uzuri wa ligi na uzuri wa timu.ligi ya hispania haisisimui ni ya timu mbili na inajulikana kbisa bingwa ni nani
Hata mgao wa pesa ya matangazo ya television ni real mad na barca ndo team zinapata mgao mkubwa kuliko team zingine..ligi bora team mbili? Hapa nasubiri bonge ya match..liverpool vs Arsenal.
 
Suarez,Nolito,Bale,Benzema,Iniesta,Ramos,Marcelo,Alves,Turan,Vidal,Serg roberto,asee ni wengi mno bado sijataja makipa
hazard,sanchez,ozil,kane,calwalker,kante,mane,yaya toure,aguero,kompany,montero,de gea,koscielny,silva,na dogo wa liverpool
 
ukitoa messi,ronaldo,neymar kuna wachezaj gan wa ajabu la liga?

We la liga uangalii, kwahiyo mi sitaki kupigizana na wewe kelele. Mtaalamu Rio Ferdinand kakubali mafundi wamejaa Spain, wewe umeona Ronaldo na Messi tu? Sibishani na watu wasiojua mpira. Bye!!!
 
We la liga uangalii, kwahiyo mi sitaki kupigizana na wewe kelele. Mtaalamu Rio Ferdinand kakubali mafundi wamejaa Spain, wewe umeona Ronaldo na Messi tu? Sibishani na watu wasiojua mpira. Bye!!!
mi naangalia sana la liga,ila inaniboa,yaan kitimu mpaka dk ya 20 kitaongoza kwa goli 2 dhidi ya barca au madrid,dk ya 60 utakuta kmeshapgwa 5
 
ligi haibebi kombe,timu ndiyo inabeba kombe,mashindano ya mtoano ni tofauti na ligi

umejifanya hujaelewa alafu ukatoa jibu... sasa jibu umelipata wapi wakati hujaelewa swali??

Sijasema utofautishe ligi na mechi za mtoano.. usibadilishe swali

Kwa hakika umeelewa vizuri tu, na jibu unalijua sema hujalipenda au haulitaki
 
Mkuu hivi ulishawahi kuangalia Seville vs malaga labda,villareall vs bilbao,atletico Madrid vs Valencia unaangaliaga hii mipira lakini.
wananilisha sana mikeka yangu,naangalia..lakin huwez linganisha na everton vs spurs,leicester vs everton,thoumpton vs leicester,westbrom vs leicester..uingereza patam
 
Mkuu hivi ulishawahi kuangalia Seville vs malaga labda,villareall vs bilbao,atletico Madrid vs Valencia unaangaliaga hii mipira lakini.
Mpira kwangu ndo kilakitu..napenda sana na ujua mpira...ligi zote naangalia.
 
Hata mgao wa pesa ya matangazo ya television ni real mad na barca ndo team zinapata mgao mkubwa kuliko team zingine..ligi bora team mbili? Hapa nasubiri bonge ya match..liverpool vs Arsenal.
aminia mkuu ligi timu zingine zinzshindwa kulipa mishahara halafu bado tuiite ligi.timu zao 4 au tano hatukatai ni nzuri ila kwa ligi hawana.
 
Tusibishane kwa maneno matupu kwani kila mtu anajua kuongea
Tuangalie takwim tokea mwaka 2000 hadi 2015

Ni ligi ipi timu zao zimechukua Champion league mara nyingi

Ni ligi ipi imetoa mchezaji bora wa dunia mara nyingi

Ni ligi ipi kati ya hizo imebeba kombe la Uropa league mara nyingi

Ni ligi ipi kati ya hizo imebeba kombe la super cup mara nyingi

Ni nchi ipi kati ya hizo imechukua kombe la dunia na euro

hapo tutakata mzizi wa fitina
umeulza ni ligi ipi..kwa hyo jibu langu ni sahihi,ligi haichukui kombe
 
aminia mkuu ligi timu zingine zinzshindwa kulipa mishahara halafu bado tuiite ligi.timu zao 4 au tano hatukatai ni nzuri ila kwa ligi hawana.
Hii itachukua miaka mingi kama fifa hawataacha chuki zao dhidi ya Epl...england kuna wachezaji wazuri sana amini maneno yangu..mesut ozil..kun aguero..sio wa kukosa.
 
aminia mkuu ligi timu zingine zinzshindwa kulipa mishahara halafu bado tuiite ligi.timu zao 4 au tano hatukatai ni nzuri ila kwa ligi hawana.
wana timu tatu tu,na hyo ya tatu ishachoka,ki-sevilla man city kakibutu kwelikwel,manake angekiacha wangechonga kwel
 
wana timu tatu tu,na hyo ya tatu ishachoka,ki-sevilla man city kakibutu kwelikwel,manake angekiacha wangechonga kwel
huwezi linganisha epl na la liga au hata bundesliga ambapo timu moja imefanya ligi ya mamaake.
 
ronaldo mbona hakufanya upuuzi wa kufunga magoli 50 uingereza?

Uingereza wanavunjana miguu kila siku! sio rahisi kufunga magoli 50, lazima wakuvunje miguu..... hiyo inawezekana la liga tu, ambapo unakuwa free kucheza mpira ,......unamwona Neymah anavyoleta burudani..
 
Uingereza wanavunjana miguu kila siku! sio rahisi kufunga magoli 50, lazima wakuvunje miguu..... hiyo inawezekana la liga tu, ambapo unakuwa free kucheza mpira ,......unamwona Neymah anavyoleta burudani..
wanavunjana miguu au watu wanashona njia hazipitik?
 
Back
Top Bottom