Fisi aliyeuawa kwa risasi 49, wananchi wagawana nyama

Fisi aliyeuawa kwa risasi 49, wananchi wagawana nyama

Donnie Charlie

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2009
Posts
16,908
Reaction score
19,123
Fisi.jpg

Fisi huyo aliyeua mtoto wa mwaka mmoja na nusu baada ya kuvamia nyumba katika Kijiji cha Kangeme wilayani Kaliua alijeruhi pia watu watatu ambao inaelezwa wanaendelea vizuri.

Diwani wa kata ya Zugimlole, Ramadhan Balikeka amesema kuwa wananchi waligawana nyama na haelewi walienda kufanya nini.

"Watu baada ya fisi kuuawa walidai watamshughulikia na kuchukua nyama huenda walienda kuila,"amesema.
Balikeka amesema kuwa tukio la fisi huyo na namna alivyokuwa mahiri kukwepa risasi, limehusishwa na imani za kishirikina, wananchi wakidai ni fisi wa aina yake.

Katika taarifa yake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Safia Jongo alisema kuwa fisi huyo alivamia kwenye nyumba katika kijiji hicho na kuua mtoto wa mwaka mmoja na nusu na kujeruhi watu watatu.

Pia aliongeza kuwa polisi na askari wanyamapori walimuua baada ya kutumia risasi arobaini na tisa.

Kwa mujibu wa Diwani Balikeka, tukio hilo la fisi ni la kwanza mwaka huu katika kata yake.

Chanzo: Mwananchi

 
huyo jamaa ni mtata sana!

kuna siku moja gari ilichomoka exaust ikabidi nishuke ili niifunge na kamba.

niko chini ya gari naskia mtu anacheka..nikajua ni msela kwenye gari kule ndo anacheka!

nikawa namuuliza wee fala unacheka nini??!!nikaona anazidi tu.

nikatoka chini ya gari na tochi yangu!kumulika hivi pembeni wako fisi wawili nyuma yao wanakuja fisi wengine km 7 hivi..mahali kioo cha gari kilibaki nilipita pale..maana lile fala kule lililoki milango ya gari!!siku zote usisafiri na mtu muoga kabisa nahisi huyu fala angekuwa anajua kuendesha gari angeacha niliwe siku ile..nilipita sehemu ambayo hata kuku hawezi kupita.

kumbe ile kucheka walikuwa wanaitana ukoo mzima ili wapate dinner ya pamoja(dinner ndio mimi).sitasahau hiyo siku
 
huyo jamaa ni mtata sana!
kuna siku moja gari ilichomoka exaust ikabidi nishuke ili niifunge na kamba...
niko chini ya gari naskia mtu anacheka..nikajua ni msela kwenye gari kule ndo anacheka!...
Acha uoga umeshaingia VB kwenye gari unatakiwa kurelax maana hawawizi kuvunja kioo.na huyo kenge ungemshusha tu
 
huyo jamaa ni mtata sana!
kuna siku moja gari ilichomoka exaust ikabidi nishuke ili niifunge na kamba...
niko chini ya gari naskia mtu anacheka..nikajua ni msela kwenye gari kule ndo anacheka!
nikawa namuuliza wee fala unacheka nini??!!nikaona anazidi tuuu...
Ulimfanya nini jamaa aliyelock milango ili iwe fundisho kwake na watu wenye tabia kama hii?
 
huyo jamaa ni mtata sana!
kuna siku moja gari ilichomoka exaust ikabidi nishuke ili niifunge na kamba...
niko chini ya gari naskia mtu anacheka..nikajua ni msela kwenye gari kule ndo anacheka!
nikawa namuuliza wee fala unacheka nini??!!nikaona anazidi tuuu....
dah! jamaa alishakutoa sadaka
 
Back
Top Bottom