Freeman Mbowe alia ubaguzi katika mfumo wa elimu Tanzania

Kwenye issue ya ubovu wa elimu ningependa zaidi uzungumzie kule mwanafunzi anakopata maarifa yatakayomuwezesha kushindana na ulimwengu kwenye soko la ajira, usizungumzie matokeo yake yule anayepewa hayo maarifa anayatumiaje baada ya kupewa.

Kuhusu mfano wa ripoti uliyotoa hapa naona mfano wako hauko sahihi, nasema hivyo kwasababau huyo profesa inawezekana kabisa ana elimu nzuri na ya viwango hitajika, tatizo lake ni kuchanganya elimu yake na siasa, hapa ndipo alipofeli.

Lakini kama angekuwa anatakiwa aende kwenye inyerview kwa ajili ya kupata ajira, inawezekana kabisa angeiweka siasa pembeni abaki na elimu na maarifa yake ambayo yangemuewezssha kufanya vizuri kwenye interview hiyo.
 
Kwani mtoto unampeleka shule kwa lengo gani? ajue lugha na elimu na kukaa nayo nyumbani? au ajue lugha pamoja na elimu vitakavyo muwezesha kuyamudu mazingira atakayokabiliana nayo mbele ya safari yake ya kimaisha?
Nenda kule Zanzibar kwenye mahoteli ya kimataifa kama utawakuta hao unaowalazimisha wasome kwa kiswahili
 
Kuna dawa moja pekee.
Elimu yetu ifumuliwe moja kwa moja. Huko ndiko kwenye tatizo, siyo kwenye lugha.
 
Narudia kukusoma lakini sikuelewi.

- Hakuna mahali niliposema elimu ya msingi inaweza kumpa mtu ajira.

- Ushindani nimeuzungumzia kwa kuwataja wakenya kwenye interview kwenye soko letu la ajira, ili kuonesha vile ujuzi wao wa lugha pamoja na maarifa wanayopata kwenye vyuo vyao unavyowasaidia.

- Suala la ubaguzi, nakubaliana nalo ndio maana Mbowe ameamua kulizungumzia ili kuondoa dhana ya "aliyenacho" na "asiyenacho" kwenye elimu yetu, sasa hapa napo sijaona pointi yako.

Hicho kiswahili kama unaona kina maana, niambie kitakusaidia wapi kwenye kushindana kwenye soko la ajira kama sio kuishia kuwa mfagizi? hapa tuwe realistic, kama kweli mnataka kukibeba kiswahili, basi kibebeni kama pambo tu kwa wakati huu, lakini sio kiwasaidie kushindana kaenye soko la ajira hasa EAC.
 
"Kushindana na ulimwengu kwenye soko la ajira", hitaji ni moja tu, na siyo lugha. Ni kuwa na uelewa wa fani unayoitumikia (unayoombea kazi). Hakuna zaidi ya hapo.

Ponda ponda lugha, si hoja, mradi ujuwe unachokifanya.

'Surgeon' mzuri hahitaji kujua kiingereza safi sana ili aweze kufanya kazi yake ipasavyo.

Kwa bahati nzuri au mbaya umetumbukiza sababu nyingine inayoharibu elimu yetu..., SIASA.
 
Kuna dawa moja pekee.
Elimu yetu ifumuliwe moja kwa moja. Huko ndiko kwenye tatizo, siyo kwenye lugha.
Huko "kufumua" hakutahusisha na kubadilisha lugha? nionavyo kama "utaifumua" lakini bado lugha itumikayo ikabaki kiswahili naona tutaendelea kuzunguka pale pale.
 
Nae atuonyeshe mfano, anaongea kiingereza kilichonyooka? Au ni sawa na yule jamaa yangu aliyehojiwa na radio fulani ya Kenya, tulihesabu neno "actually" mara mia. Ni kweli lugha inatuendesha ila tukiweka Nia tutaweza.
Kwa kweli Lughba ya Kiingereza inatuangusha sana Watanzania.

Nilishangaa sana wakati fulani nikiwa West Afrika kikazi. Sikuona Mtanzania hata mmoja kwenye kundi lile nililokutana nalo. Jioni nilikuwa nikikutana nao, wao walikuwa wakipenda sana kunisikia mimi nikiongea Kiswahili cha Kitanzania. Lilikuwa ni kundi la Wakenya 12 wakifanyia UN., Wakiwa na jukumu maalum kwa nchi ya Ivory Coast na Liberia. Mimi nilikuwa huko kikazi kwa kupitia makampuni ya kimataifa.

Binafsi sioni mantiki ya Kiswahili kutumika kama lugha ya kufundishia masomo shule za msingi, halafu gjafla mwanafunzi akiingia Secondary lugja ya kufundishia masomo inageuka na kuwa Kiingereza.

Tuamue kukiweka Kiswahili kuwa somo maalum la Lugha lakini Kiingereza kiwe lugha ya kufundishia.

Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa hatuwezi kukiacha Kiingereza kwa sababu ndiyo Kiswahili cha Dunia.
 
Atayapataje hayo maarifa wakati yote yameandikwa kwa Lugha ambayo haimudu?¡
 
Huyu Mbowe anatakiwa awe na washauri wazuri.Naona anakurupuka tu.
 
Kama unazungumzia specialist ndio maana hupelekwa nje kujifunza, especially madaktari, na huko hukutana na walimu wazuri wa lugha wanaoweza kuwapa elimu yenye viwango.

Lakini usidharau umuhimu wa lugha kwa "kuponda ponda" hasa kwenye fani sensitive kama ya utabibu, bila daktari kumsikiliza mgonjwa na kumuelewa vizuri ni sawa na kutengeneza tatizo kubwa zaidi mbele ya safari.
 
Mbowe hataki kukuza lugha ya Kiswahili ili iwe lugha ya kitaaluma?
Mbona wachina, Wajapan, Warusi, Waswede, Wajerumani, wafaransa wanatumia lugha zao kufundishia watoto wao kwa nini kiswahili kisiweze?
Lugha yako ili iwe na nguvu, na kuwa nyenzo muhimu ya kupatia maarifa, ni lazima kuwa na maarifa makubwa katika jamii husika.

Kama hutengenezi dawa za kuwatibu watu na mifugo, hutengenezi vifaa tiba, hufanyi ugunduzi wowote wa kisayansi, hutengenezi machine yoyote, n.k; lugha yako haiwezi kuwa na nguvu ya kuhamisha maarifa kwenda kwa wanafunzi.

Mataifa uliyoyataja, yanajitegemea kwa kiasi kikubwa katika maarifa. Uswizi, zamani walikuwa wanatumia Kijerumani kama official language yao, japo wananchi wao walio wengi walikuwa wanaongea French. Baada ya maarifa kukua, sasa hivi official language yao ni Kifaransa.
 
Huyo anayejiita msomi, naye ni bure. Ni msomi wa kukariri.

Ajiulize:

Kwa nini nchini China, Uturuki, India, Ukraine, South Korea, Israel, Dubai, Qatar, kwa sasa vyuo vinavyotumia Kiingereza kufundisha vinazidi kuongezeka, na wanafunzi wengi wa kwenye mataifa hayo, kutoka familia zenye uwezo mkubwa wanapenda kuwapeleka watoto wao kwenye vyuo hivyo?
 
Ndugu Data! Mitanzania mingi ni mijinga Sana. Mi ni mwl English medium. Watoto wanaelewa Sana. Tatizo Mwl Nyerere watu walimdanganya kuwa ukiendelea na Kiingereza watu wataerevuka na watajua mengi ya nje watakupindua! Akabadili gia angani Kiswahili tu tofauti na nchi zilizotawaliwa na Mwingereza. Sasa ccm inafurahia cnn, bbc world, sky news etc wakiongea watz ni hola! Shenzi type!
 
Mbowe hataki kukuza lugha ya Kiswahili ili iwe lugha ya kitaaluma?
Mbona wachina, Wajapan, Warusi, Waswede, Wajerumani, wafaransa wanatumia lugha zao kufundishia watoto wao kwa nini kiswahili kisiweze?
Lugha inaendana na uchumi wa inchi,kama.uchumi wako ni takataka unategemea nani atajifunza lugha yako,atakuja kwako kuomba nini?huyo Rais wako akienda kutembeza bakuli unazani huwa anaomba kwa kiswahili?

Au anaomba kiubububu?
 
Kingereza ni lugha muhimu kwa nchi kama Tanzania na haiepukiki. Serikali iwekeze kupata walimu wazuri wa kiingereza liwe ni somo kama ilivyo sasa kuanzia chekechea. Nilikutana na jamaa mmoja anakijua kingereza vizuri. Alisoma kijijini kwetu shule hizi za kawaida na alipofika sekondari huko huko kijijini mwalimu wao wa kiingilishi akawa ni raia wa Marekani valentia.

Hivyo tusikimbilie Kiswahili kwa kukataa uwekezaji kwenye Kiingereza. Lugha zote mbili zitumike kufundishia kwa level ya msingi kingereza kiwe somo. Na ikifika sekondari kiswahili kiwe somo. Maneno haya ya wenye maslahi ya miradi ya ulaji kwenye lugha ya kiswahili yataligharimu taifa hili.

Ujumbe kwa Mbowe, CDM haiwezi kubadilika kama itaendelea kuwa na akili hizi hizi za MKT. Ni wakati umefika wapishe wengine wao wawe washauri tu. Waache tabia za ujasiriasiasa.
 
Huko "kufumua" hakutahusisha na kubadilisha lugha? nionavyo kama "utaifumua" lakini bado lugha itumikayo ikabaki kiswahili naona tutaendelea kuzunguka pale pale.
Hata kidogo.
Lugha ya kufundishia siyo tatizo kabisa. Kiswahili kimekua na kujitosheleza kabisa kuwa lugha ya kufundishia elimu iliyo bora kabisa.
 
Mkuu 'denooJ', niamini mkuu, ninaelewa ninachokizungumzia hapa.
Lugha siyo sehemu ya utaalam wowote hapa duniani, ni chombo tu, na kuna vyombo mbalimbali vinavyowezesha kupata matokeo mazuri.

'Surgeon' hahitaji kujua lugha kuwa 'surgion' mzuri hata siku moja. Anajua kazi yake, awe amejifunza kwa kichina, kihindu, kiingereza, kifaransa, n.k.

Lile swali langu naona umeliweka kapuni kwa maksudi mazima, kuhusu anayejifunza lugha kwa miezi mitatu na anayetumia lugha kwa miaka mitatu, bado asiweze kuitumia lugha hiyo.
 
Sipingi Kiswahili kinaweza kutumika, ila Kingereza ni muhimu zaidi, hivi leo utoke zako huko Musoma hujui Kiswahili ukifika Darisalama nani atakuelewa na kilugha,? je huoni faida ya kuongea lugha ya kikwenu pamoja na Kiswahili??? ... the same goes to English, nani atakuelewa ukitaka kupata kazi private sector ambapo ni waajiri wakuu ama ukitaka kazi nje ya nchi ama scholarship??? kwa nini tulimit horizon ya ajira kwa wahitimu?
 
Kiswahili si Lugha Mama 99% ya Watanzaniani Kihaya Kisukuma, Kiluguru, Kizigua, Kiha, Kimakonde nk.
 
Hebu nikumbushe hilo swali lako, mambo yalikuwa mengi wakati mwingine ni rahisi kusahau jambo.

Bado kwangu nakushauri usidharau umuhu wa lugha kwenye fani yoyote kama chombo cha mawasiliano, hicho ndio kiunganishi kikuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…