Ubaya Ubwela
JF-Expert Member
- Jul 24, 2024
- 1,353
- 3,060
Aliyataka mwenyewe Kujifanya master Lissu alishamuheshimu na kusema atagombea urais na Umakamu mwenyekitiHuyu mzee watamuua kwa presha! View attachment 3195159
Hana hekima za kuhubiri demokrasia wakati yeye haongozi kidemokrasia anakumbuka kuhusu demokrasia anapokuwa nyuma ya mikamera hasa wakati wa chaguziMBOWE aache kutapa tapa....aache kulalama.....kila mwana chadema mwenye vigezo na sifa ana haki ya kuwa mwenyekiti.....hicho kiti hakijawekwa akae peke mpaka akiwa maiti...
Kwanini kila msimu wa uchaguzi CHADEMA kunazuka mtafaruku kwa wagombea webgine kana kwamba wanafanya jambo baya......
Na aliyewatafuta hao viongozi wa kiroho ni yeye mwenyewe Mbowe. Huyu kitenge naye si ndiyo wote wanufaika wa hela ya DP World kama alivyo Mbowe.Bila shaka Lisu hakuweka wazi jina la kiongozi wa kiroho, huyu kitenge sijui alitoa wapi hilo jina!!, anyway hakuna ubaya kwa kiongozi wa kiroho kupatanisha watu maana imeandikwa heri wapatanishi
...Mbowe kafanya madudu mengi Sana kwa Mgongo wa uwenyekiti wa chademaKweli tupu. Kuna pia wale ambao kwa namna moja au nyingine wanaamini kuwa hawajatendewa haki katika uongozi wake. Hii ni pamoja na Lissu mwenyewe ambae amesema wazi kuwa Mbowe alitaka kumtilia kauzibe kupitia Wenje. Kuna wale walioshindwa au mtu wao alishindwa ( k.m. Msigwa)chaguzi tofauti.
Na pia wako ambao kwa dhati kabisa wanaamini kuwa kuna haja ya kuibadilisha Chadema ili ionekane kuwa inampambania mtanzania wa kawaida. Hawa wa mwisho hawataki kabisa CDM ipasuke ila hawana jinsi.
Amandla...
Mkuu umeamua kudanganya kweupe kabisa. Kati ya Mbowe na Lissu nani anapata support ya CCM?Lissu anasifiwa sana na anapata support kubwa kutoka sisiemu.
Una uhakika sa hizi yupo ub eligiji au unajiropokea tu kama chiziMuda mwingi yuko ubelgiji sio.Tanzania hata sasa hivi hayuko nchini yuko ubelgiji
Haahaa kutamka neno demokrasia ni rahisi Sana, vitendo ndo kazi ..Sijawahi kumuona Mbowe akiwa under pressure, kumbe akiwa depressed anakuwa boya kiasi hichi, imagine huyu angaukwaa uraisi wa Tanzania angepiga marufuku hata neno UCHAGUZI na KATIBA. hata Mobutu Sese seko huko aliko angaionea huruma Tanzania.
Hii counter attack aliyofanyiwa na Lissu imemtoa mchezoni kabisa hadi analialia kama mtoto aliyebemendwa.Mbowe Anaona akiongeabhivyo Wanachama watamuonea Huruma
Kwa mujibu wa Lissu yupi ulisikiliza mahojiano yake ya jana? Mbona laiweka wazi hasa kilichomsukuma kugombea hicho kiti, Mbowe Mwenyewe ndo kafanya agombee hicho kiti, kwa kujifanya yeye ndo masterKwa mujibu wa maelezo yake, Lissu amesukumwa kugombea na hayo makundi aliyoyataja.
Pascal Mayalla zitto junior
Kwa maoni yangu Lissu hafanyi attacks bali sera na misimamo yake inawavua wengine nguo.Kampeni hasa za chama namaanisha wote mnajenga nyumba moja si vizuri kuanza kuchambana ,uchaguzi ndani ya chama wajikite kwenye hoja/sera na si attacks ...siasa za attacks ni Chama A kwenda Chama B.
Lissu ana attack viongozi wake sasa na kiongozi akiwa attacked lazima ajibu ili kuweka mambo clear na hapo ndipo yanapotokea malumbano.
Ukiona unasifiwa na adui basi jua unakosea...Lissu anasifiwa sana na anapata support kubwa kutoka sisiemu.
..Chadema bila mbowe kuondolewa kwenye uwenyekiti watakuwa na wakati mgumu Sana...Tetesi toka Twitter zinasema mwamba kalambishwa asali ya 12B + na bado anataka asali zaidi. Dr slaa kazungumzia hilo clubhouse ya Twitter anasema kapewa Taarifa na vijana wa system. Vijana wa system wameona wampe taarifa slaa
Video ya sauti ya Dr slaa akielezea watu wanavyolamba asali ipo hapo
View: https://youtu.be/lU_QbyAtMUM?si=w_g-bndY2v_e58vQ
..Mbowe anahubiri demokrasia huku mwenyewe akiikandamiza..mKwa mujibu wa Lissu yupi ulisikiliza mahojiano yake ya jana? Mbona laiweka wazi hasa kilichomsukuma kugombea hicho kiti, Mbowe Mwenyewe ndo kafanya agombee hicho kiti, kwa kujifanya yeye ndo master
Lissu mkuu kupitia Peter msigwa aka Dalali Kinyambe.Mkuu umeamua kudanganya kweupe kabisa. Kati ya Mbowe na Lissu nani anapata support ya CCM?
Hata na yeye ni mla rushwa , michango ya matibabu wamechanga viongozi wa chadema na wanacnhi ila invoice amezidai zote 800m kama zake huo ni wizi/utapeli kukosa uhadilifu.Kwa maoni yangu Lissu hafanyi attacks bali sera na misimamo yake inawavua wengine nguo.
Huwezi kusema nitaondoa rushwa na ubinafsi bila kuwaambia watu unaondoa rushwa ipi. Usipoonyesha viashiria vya rushwa maana yake unataka kuondoa kitu kisichokuwepo.
Kwa wingi wa tuhuma za Mbowe huwezi kusisema kistaarabu hata kidogo, huwezi kupaka paka mafuta mtu anayekiuka misingi ya Utawala bora
Lisu anaungwa mkono na watu gani vile? Kwamba Lisu alishinda uenyekiti CCM watafurahi sio?Kampeni hasa za chama namaanisha wote mnajenga nyumba moja si vizuri kuanza kuchambana ,uchaguzi ndani ya chama wajikite kwenye hoja/sera na si attacks ...siasa za attacks ni Chama A kwenda Chama B.
Lissu ana attack viongozi wake sasa na kiongozi akiwa attacked lazima ajibu ili kuweka mambo clear na hapo ndipo yanapotokea malumbano.
Ukiona unasifiwa na adui basi jua unakosea...Lissu anasifiwa sana na anapata support kubwa kutoka sisiemu.
Vichwa panzi kutiwaambia hata yale mateso aliyokuwa anapitishwa nyingi zilikuwa script za kaole sasa anachezeshwa game lisilo na director ndio ndio tunaona rangi yake halisiSijawahi kumuona Mbowe akiwa under pressure, kumbe akiwa depressed anakuwa boya kiasi hichi, imagine huyu angaukwaa uraisi wa Tanzania angepiga marufuku hata neno UCHAGUZI na KATIBA. hata Mobutu Sese seko huko aliko angaionea huruma Tanzania.
Mbowe amefimisika kisiasa anatumia mbinu za kijinga kabisa wakati wenzake wanapinga ufisadi na uhuni wa kisasa unaowasanabisha watanzania kukata tamaa ya kupiga kura .Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA @chadematzofficial Freeman Mbowe amesema kuna makundi yanayoratibu kufanyika mapinduzi ndani ya chama hicho na makundi hayo ndiyo yanayomsukuma Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bara, Tundu Lissu kugombea nafasi ya Uenyekiti.
“Kuna kundi linaloitwa diaspora (watanzania waishio ughaibuni) ni kundi dogo tu wala sio kusema ni diaspora wote wa Tanzania hili kundi dogo linalojaribu kupanga mapinduzi ndani ya CHADEMA wengine hata hatuwajui tunawaona tu kwenye majina ya mitandaoni wanajiita Tanzania Diaspora ni kundi ndani ya Diaspora”
Mbowe ameeleza kuwa zaidi ya kundi hilo kuna kikundi kingine kinachoitwa Sauti ya Watanzania ambacho kinachoongozwa na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Wilbroad Silaa
“Kuna makundi ya watu kama Dkt. Silaa na kikundi kinachojiita Sauti ya Watanzania, Dkt. Silaa alikimbia CHADEMA mwenyewe akaenda Chama Cha Mapinduzi (CCM) akafungiwa Serena pale(Serena Hotel) baadae akahamishiwa Canada akapewa zawadi ya ubalozi.”
Mbowe ameongeza kuwa amekuwa akishangazwa na wanaomuunga mkono Lissu kuwa sio watu ambao ni wanachama kweli kweli hata hivyo anashindwa kuelewa kwa nini Dkt. Silaa hawekezi nguvu kwenye chama chake bali anawekeza muda na nguvu CHADEMA.
“Kazi aliyoifanya muda wote akiwa balozi(Dkt.Silaa) chini ya utawala wa Magufuli(Hayati Dkt. John Pombe Magufuli) ni kujaribu kuichonganisha CHADEMA na kutoa taarifa na mpaka kuandika kitabu cha uongo eti leo Dkt.Silaa ndiye anafanya kampeni ya Lissu kuchukua uongozi wa chama alisahau nini Dkt Silaa ambacho leo anakitaka”
Hata hivyo Mbowe ameongeza kuwa wengine wanaomuunga mkono Lissu ni pamoja na aliyekuwa Mbunge wa Iringa na Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa Mchungaji Peter Msigwa ambaye kwa sasa ni kada wa CCM.
Source: Jambo TV
Lisu anaungwa mkono na watu gani vile? Kwamba Lisu alishinda uenyekiti CCM watafurahi sio?
Mkuu hapa haujaeleweka, hii ni rushwa kivipi? Yaani mwanetu anaumwa yupo MNH tumemchangia. Akitaka kupewa risiti na invoice za malipo unataka lisome jina la nani? Unataka yasomeke majina yetu?Hata na yeye ni mla rushwa , michango ya matibabu wamechanga viongozi wa chadema na wanacnhi ila invoice amezidai zote 800m kama zake huo ni wizi/utapeli kukosa uhadilifu.