Freeman Mbowe: TRA walinidai Kodi Bilioni 2, Wakafunga akaunti zangu zote za biashara mpaka binafsi, Wakachukua hela

Freeman Mbowe: TRA walinidai Kodi Bilioni 2, Wakafunga akaunti zangu zote za biashara mpaka binafsi, Wakachukua hela

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
172031437_3925544254203904_5146527358487816551_n.jpg

Nilifungiwa akaunti zote za bank za kampuni yangu. Nikafungiwa akaunti zote za biashara. Hata akaunti yangu binafsi ya mshahara wa ubunge ilifungwa toka mwaka 2018, nikazuiwa kupokea mshahara ambao ni haki yangu kisheria" Mhe.Freeman Mbowe akizungumza na wanahabari.

My Take:
Natengua msamaha nilioutoa kwa Magufuli

====

MBOWE: NILITUMIWA MADAI YA KUDAIWA KODI NIKIWA JELA

Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema alitumiwa madai ya kudaiwa kodi ya Tsh. Bilioni 2, kwenye email binafsi akiwa jela ambapo alishindwa kuiona.

Barua pepe ya kwanza ilimtaka kupeleka malalamiko ndani ya siku 30 kama hakubaliani nayo, kwa kuwa alikuwa jela hakuweza kuijibu, wakatuma nyingine kusema kuwa kwa kuwa amekaa kimya ameonekana kukubaliana nayo.

Alivyotoka jela, akadaiwa kodi ambayo amedai kuwa haikuwa sawa kwa kuwa ili biashara ilipe kodi ya Tsh. Bilioni 2 lazima iwe imetengeneza faida ya Tsh. Bilioni 12 kwa mwaka, na biashara yake ni ndogo isingeweza kutengeneza faida hiyo.

Ili Mamlaka ya mapato kuipata kodi hiyo walifungia akaunti zake zote ikiwemo aliyokuwa anapokelea mshahara wa ubunge. Kwa sababu hiyo aliondoka nchini ili kutafuta fursa za kuwekeza nchi nyingine.
 
Kama hakufata sheria..alitaka iweje!!! Kama alifata aende mahakamani..

Ila nawashangaa wengi.. maneno mengi kama vile uongozi wote umebadilika ukaja mpya kutoka sijui safari ipi.. na sheria za nchi zimekutwa..

Waendelee tu kuongea...........
 
Halafu Mbowe anataja kua Hayati Magufuli alikua na upendeleo wa kindugu, neportism, anaweza kutupatia ushahidi kua kulikua na upendeleo huu na huu wa kindugu wakati wa Magufuli?

Tupate ushahidi wa ndugu zake na Magufuli ambao aliwapendelea na hawakua na sifa kwenye nafasi za kiutumishi.

Hii kampeni ya ukabila inapigiwa chapuo sana na makabila ya kaskazini. Wanajitahidi kutaka kufukia tabia yao ya ukabila nchi hii. Mfano, Kimei amejaza wachaga CRDB.

Ukabila umejaa CHADEMA, chama kinaongozwa na kabila moja tu, Mwenyekiti mchaga, katibu mkuu, wakurugenzi wote, kuanzia fedha, itikadi, na kadhalika.

Huu uzushi wa ukabila ambao chadema mnamtungia Magufuli na mmeshindwa kuleta ushahidi usiopingika wa ukabila wa Magufuli ni kutaka kufunika tabia yenu ya kikabila.

Angalia wabunge viti maalum wa Chadema waliopita, 50 walikua wachaga na watu wa kaskazini.

Mbowe achana na hoja ya ukabila dhidi ya Magufuli, hakuna ushahidi, chama chako kina ushahidi wa ukabila.
 
Back
Top Bottom