Uchaguzi 2020 Freeman Mbowe, Zitto Kabwe, Godbless Lema na Boniface Jacob waachiwa kwa dhamana

Uchaguzi 2020 Freeman Mbowe, Zitto Kabwe, Godbless Lema na Boniface Jacob waachiwa kwa dhamana

Baada ya mabeberu kuandika twitter
"we mbuzi waachie huru mbuzi wenzako"
Leo wameachiwa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jamani mwenzenu Tundu Lisu ana hamu ya kwenda kwao Belgium, wenzenu wame-miss kwa siku nyingi. Ile shughuli ukishazoea huwezi kuiacha jamani mswalie mtume! Kuweni na huruma.
Na wewe unaamini umeandika kitu kwenye jamvi la GT? Pole sana, Embicile ana afadhali
 
Shime shime, turudi kwenye jambo letu sasa la MAANDAMANO YASIYO NA KIKOMO hadi kieleweke.
 
Continue to rest in eternal peace mwl JK Nyerere missing you babu huku mambo magumu sana yani siku ukiamka hata kwa bahati mbaya tu unaweza usiamini yanayi endelea , ile keki ulio iacha inaliwa kwa ubaguzi sana, na kwaulinzi mkali ole wao waandishi na mafarisayo...
 
Inatakiwa waongeze jitihada ili vijana wao ambao nao wako ndani waachiwe. Vijana wa Bavicha, Mdude n.k. wote wanastahili kupiganiwa kama viongozi walivyopiganiwa.

Amandla...
 
Askari wa hapo Darisalama alituambia Jana tarehe mbili kwamba hao viongozi wa vyama vya upinzani wamekamatwa kwa kupanga maandamano na ugaidi.

Makosa ya ugaidi kwa inchi yetu hayana dhamana. Je, kwanini hawa wanaachiwa? Au tuhuma za ugaidi yalikua makosa ya kutunga?

Au tumeogopa kelele za mabeberu?
 
Watanzania zaidi ya 80% waliompigia kura Magifuli naamini wangependa hilo kundi la viongozi wabinafsi na wenye uchu wa madaraka kwa njia yoyote ile, wangefunguliwa mashtaki ya uhaini
 
Mkuu OKW BOBAN SUNZU ni wakati wa kujitafakari kama kweli upinzani ulikuwa na nafasi ya kushinda! Zifuatazo ni baadhi ya sababu, nyingi zimejadiliwa sana humu jamvini, ambazo kimsingi hao viongozi wasingekuwa na uhalali wa kuhamasisha maandamano yasiyo na kikomo, kushinikiza Uchaguzi Mkuu urudiwe:

√ Mbowe mwenyewe amekuwa akiamru wabunge wake wasusie vikao vya bunge, hasa vya bajeti. Wapiga kura walisikia na kuona;
√ Mbowe na karibu kundi zima la viongozi wa upinzani wamekuwa/wakaendelea kudai Serikali ya CCM ilikuwa inajishughulisha na maendeleo ya vitu. Wapiga kura wamewasikia, wakaona vitu (miundo mbinu na huduma za afya) jinsi vilivyonavyoboreshwa. Wamevitumia kiasi cha kuamini viongozi wa Serikali ya CCM. Kwenye sanduku la kura wapiga kura wameonesha imani hiyo;
√ Mbowe, huyo huyo, kama kiongozi wa Chama Kikuu cha Upinzani, kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, 2019. Hivyo basi Upinzani ukakosa wawakilishi kwenye Serikali za Mitaa, ambako ndiko kwenye nguvu ya ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu, 2020. Wagombea wao wakakosa msaada ngazi hiyo na kufanya kampeni kams watoto wakiwa. Upweke huo ukajibiwa kwenye sanduku la kura;
√ Ni Mbowe huyo huyo alishinikiza Lissu awe Mgombea wa Urais kupitia chama CHAKE, wakati akijua madhaifu yake. Wapiga kura wakahudhuria kampeni zake za majivuno, kero, matusi nk. Baada ya hapo wamemwadhibu kwenye sanduku la kura;
√ Viongozi wakuu wa CHADEMA na ACT-Wazalendo wakaingia kwenye Uchaguzi Mkuu na nia ya kisanii ya kuungana, kumbe nyuma ya pazia, Mbowe huyu huyu, ana agenda yake ya siri, kumtosa Mgombea Urais kupitia ACT-Wazalendo. Wapiga kura (wanachama na wafuasi wa ACT-Wazalendo) wakasikia na kuona usanii huo. Kwenye kura wakamjibu Mbowe na kundi lake; na
√ Mgombea wa Urais, kupitia CHADEMA, alipofungiwa na NEC kutokuendelea na kampeni kwa siku kadhaa, Mbowe alijitokeza hadharani kulaani vyama vya upinzani vilivyoshiriki kupiga kura hiyo kuwa ni mamluki wa CCM. Viongozi wa vyama hivyo, wanachama na wafuasi walisikia, wakaona na kujibu kwenye sanduku la kura.

Uchaguzi Mkuu 2020, ulikuwa Huru na wa Haki kwa 100% kwa sababu kuu zifuatazo:
1) Wapiga kura walishiriki mchakato wote (kujiandikisha, kushiriki na kupiga kura) kwa uhuru kabisa na kutumia haki yao.
2) Wagombea nao kwa Uhuru, walitumia Haki yao kushiriki katika kinyang'anyiro hicho, kwa kuomba kuteuliwa na vyama vyao, kupitishwa na Tume, kufanya kampeni na hatimaye kushiriki wenyewe kupiga kura.

Kitendo cha viongozi hao kuhamasisha maandamano yasiyo na kikomo, sasa yanalaaniwa kila kona ya nchi na kila kundi katika jamii. Sasa ni wazi kuwa viongozi hao hawakuwa na nia njema katika Taifa bali wao kuingia madarakani kwa njia yoyote ile, ikiwemo umwagaji damu. Sheria za nchi, baada ya wananchi kuwaadhibu kwenye sanduku la kura, nazo zitawaadhibu.

cc: wafuasi wa upinzani humu JF
Mkuu maelezo mengi yanini . kwa Mara ya kwanza tuliona marundo ya kura feki zilizotikiwa magufuli yakizagaa mitaani. Lini umewahi ona kitu kama hicho kabla
 
Vipi yule polisi na shahidi wake waliopeleka ushahidi wao Tbc badala ya mahakamani
- KumbukiziMTAFUTANO.jpg
 
Ningekua mimi ni Mungu yani Magufuli angenitambua!

Huwezi ninyanyasia watu wangu kwenye Nchi yao halafu unaniletea unafiki kwenye nyumba yangu ya Ibada na huku mikono yako imejaa damu zisizo na Hatia. Ningemnyoosha haswa.

Bahati yake mimi siyo Mungu.
Hapo bado hujatambua huyo Mungu hayupo tu?
 
Hapo bado hujatambua huyo Mungu hayupo tu?
Mungu yuko haijalishi hoja na matukio ya kumpinga yako kiasi gani. Mambo mengine usihitaji uthibisho maana ndicho unachotakaga.

Tuendelee na siasa,

Tupe updates za hapo USA kuhusu uchaguzi, Biden hapiti kweli?
 
Back
Top Bottom