FT: Ethiopia 0 - 2 Tanzania | AFCON QUALIFICATION | Stade des Martyrs - DRC | 16-11-2024

FT: Ethiopia 0 - 2 Tanzania | AFCON QUALIFICATION | Stade des Martyrs - DRC | 16-11-2024

Msuvaaaa🙆🏼‍♂️🙆🏼‍♂️
Inagonda Mwamba
 
Tunahitaji Ushindi zidi ya Guinea ili kupita.
 
Match Day.
View attachment 3153868
KIKOSI CHA TANZANIA KINACHOANZA LEO
View attachment 3153869
Mpira ndio unaanza sasa.

Updates
Game on
05'
Tanzania wanafanya mashambulizi hafifu kidogo kwenye lango la Ethiopia.
Tanzania wanatawala game.

06'
Msuva anakosa goli la wazi kabisa hapa,
Amepata assist nzuri sana toka kwa Samatha.
Namna gani palee
Anakosaaaa tena.

08'
Ethiopia wanafanya shambulizi moja hapa lakini halileti matumaini.

10'
Mzizee anakosa tena hapa.
Taifa stars wako vizuri sana
0-0

14'
Game on.
Bado umiliki wa ball ni kwa Taifa stars
0-0

15'
Tanzania wanapata kona inapigwa na Miroshi.
Inapigwa inajaa kwenye kichwa cha Msuva...
Goooooooooooal ni goli hapa.
Chumaaaaaaaaa
Msuva anaipatia Taifa Stars goli la kuongoza.
0-1.

23'
Game imesimama kidogo kuna mchezaji wa Taifa stars yuko chini.
0-1

29'
Feiii
Anakosa.

30'
Goooooooooooal
Feisaliiii
Chuma cha pili. Baada yakupokea assist mujarabu sana kutoka kwa Mzize
0-2

34'
Ethiopia wanafanya shambulizi linatolewa nje, inakuwa kona wanapiga kona ya haraka haileti madhara yoyote kwenye lango la Taifa stars.
0-2

39'
Ethiopia wanapata free kick nje kidogo ya 18 inapigwa inatoka nje.
Goal kick

45'
Additional time 2'
Msuvaa, mpira unatolewa nje.
Taifa stars wanapata kona ya pili
Inapigwa inakuwa goal kick.

HT
Ethiopia 0 - 2 Tanzania.
==================
Kipindi cha Pili.

47'
Game on
Ethiopia wamefanya mabadiliko mawili yanaonekana kuwasaidia kidogo.
0-2

59'
Samatha na Msuva wanakosa nafasi ya wazi kabisa kabisa.
Namna gani hapa bana.
0-2

64'
Kibu Inn
Mzize Out
Miroshi Out
Mtasimgwa Inn

67'
Kumeibuka vurugu kidogo Uwanjani baada ya Samatha kupigwa kwenzi la kichwa na mchezaji wa Ethiopia.
Hussen Zimbwe akataka kujibu.
Mpira bado umesimama kidogo.
Kutuliza taharuki iliyoibuka hapa Uwanjani.

70'
Game on.
Kibuuuu amekosaaaa,
alikuwa tayari ni Offside

81'
Ethiopia wanakosa goli la wazi hapa.
Mabeki wa TANZANIA wanafanya uzembe.
0-2

84'
Mudathir Out
Samatha Out
Saaduni Inn
Ame Inn
0-2

90+5'
Msuva Out
Msindo Inn
Taifa stars wanapata kona haileti.
madhara

Full Time.
Ethiopia 0-2 Tanzania
Asante sana kwa updates
Huku nilipoTANESCO washafanya songombingo zao muda mrefu sana
 
Ni bora tu , GUINEA itoe sare na CONGO...
stars ije kupambana na Guinea Dar kwa ajili ya sare manake kumfunga CAMARA Dar itakuwa ngumu sana
 
Ni bora tu , GUINEA itoe sare na CONGO...
stars ije kupambana na Guinea Dar kwa ajili ya sare manake kumfunga CAMARA Dar itakuwa ngumu sana
Tushatolewa guinea imepata bao lala salama hatupindui kwa kamara hapa
 
Kama kawaida
Tukifungwa wanakaa kimyaaa
1000030473.jpg
 
Back
Top Bottom