FT: Ken Gold 0-1 Yanga | NBC Premier League | Sokoine Stadium | 25.09.2024

Dakika 12
Goal Baccaaaaaaaaaaa⚽️
 
Dakika 12
Goal Baccaaaaaaaaaaa⚽️View attachment 3106592View attachment 3106595
 
Coach Gamond ashauriwe atumie 2 strikers badala mfumo huu anaotumia striker mmoja na viungo wengi. Ana 4 strikers Dube, Mzize ,Musonda na Beleke haitaji kuwa na hofu ingawa lengo lake kutumia viungo wengi ni ili atawale mchezo hasa eneo la kati japo hufanikiwa sana kutawala pale kati shida inakuwa kumalizia mashambulizi maana mshambuliaji mmoja aliyemuweka mbele akipelekewa mpira anajikuta anakabwa na mabeki 3 sio ajabu kuona washambuliaji wake kukosa magoli ya wazi sababu mshambuliaji mmoja kufunga mbele ya walinzi 3 au 4 anawapa mtihani sana hata ikitokea huyo mshambuliaji akitaka kutaka kutoa assist inabidi atafute kiungo mmoja wapo aje kusaisia kugunga ndicho kinachooneka Yanga hata anayeongoza kwa kufunga magoli pale Yanga ni kiungo mshambuliaji Azizi K.

Mfumo huo wa kutumia mshbuliaji mmoja ndio Gamond anautegemea hata leo na Kengold ndio alioutumia na si mshambuliaji Wala kiungo aliyefunga goal Bali ni beki Boka .

Pia eneo la kiungo uwingi wa viungo waliosajiliwa Yanga panaonyesha pia pana ushindani mkali wa kugombea namba zimeanza tetesi wachezaji kununiana Coach Gamondi na bench la ufundi liimarishe mawasiliano mazuri kati yao ili waweze kupasiana vizuri bila vinyongo vya kugombea namba vinatakavyochangia na kukosa umakini uwanjani bali watatakiwa wawe makini kwa kufunga magoli nafasi zinapopatikana kuliko hii tunayoshuhudia ya kukosa magoli ya wazi kabisa wakati mwingine ni sababu ya wachezaji kutokuwa na team work nzuri maana Yanga imeshaonyesha ikiwa kwenye form yake nzuri inaweza kufunga magoli mengi ndio maana Kuna kipindi ikaoneka kama Yanga sasa huko CAF CL itafika mbali sana , sasa kwa mwendo huu Kengold unamfunga goli Moja huku unakosa magoli mengi , hata mechi na Kagera Sugar Yanga ilishinda 2 huko pia ilikosa magoli mengi ilijirekebisha kwenye mechi juzi dhidi ya CBE ya Ethiopia kwenye CAF Cl kufuzu kwenda makundi kwa ushindi wa 6-0 , kama Yanga inajiandaa kuja kutukutana na vigogo huko CAF makundi yakianza isiwe na mwendo wa kusua sua leo , Timu kama Al Ahly ya Misri imeshinda kombe la CAF CL mara 13 na huko kwao Misri imekuwa bingwa wa nchi mara 44 , na timu zote za CAF pot 1 zimeshachukua ubingwa wa CAF zaidi ya mara Moja , Yanga Tz ubingwa imeshinda mara 30 tu ndio rekodi yake kubwa , inapojiandaa kwenda kukutana na hao vigogo muda huu inatakiwa ijitengenezee muendelezo wa ushindi mzuri kwenye ligi ya NBC ili kuiweka timu katika Hali ya kujiamini zaidi kukabiliana na yeyeto hasa makundi ligi ya mabingwa itakapoanza.

Kila la kheri Yanga,Coach Gamond & GSM
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…