Kocha Garmond anatuhujumu hivi hivi! Mchezaji wake Guede mpaka sasa haendani kabisa na mfumo wa uchezaji wa Yanga!! Yaani hana tofauti na mtangulizi wake Hafiz Konkoni!
Kitendo cha kumuanzisha kwenye hii mechi kitasababisha timu kuelemewa wakati wote! Maana siyo mkabaji! Hana kasi ya uchezaji awapo uwanjani! Muda mwingi anasubiri aletewe mpira!!
Bora hata angeanza Mzize anayekosa magoli ya wazi, huku akijituma na kuwasumbua mabeki! Dah!! Hii ni kamari ya hatari sana kocha ameamua kuicheza.
Naahidi kumuomba huyu Guede msamaha hapa jukwaani baadaye, iwapo ataonesha maajabu kwenye hii mechi. Ila kiukweli ataisababisha timu kucheza pungufu kwa muda mwingi kutokana na aina yake ya uchezaji.