Muhongo sijui atarudi kufundisha mliman?
Hivi nani anasimamia shughuli za serikali?
PAP means doesn't exist
Genius yule. Embu ingia Facebook account yake uone aliandika nini tarehe 13 mwezi huu, ndio utajua huu mchongo kachonga nani. Lowassa hawezekaniki!naona safari ya matumaini ya bw mamvi sasa imenyooka kutoka monduli hadi magogoni. anachekeleaje!
...... Hapa ndio utaona Busara za Mk.were, ingawa akili za darasani nusu kijiko, ila busara za pwani zinamsaidia kupisha upepeo.
Kijamaa kimekaa kimya utafikiri kilikuwa hakijui kilichokuwa kinaendelea, na inawezekana kilishiriki. lakini utaanzia wapi sasa kumuunganisha?
Hapa wenye midomo mirefu, midomo imewahukumu, kuanzia Muhongo, maswi, Werema hadi Pinda.
Ni wakati muafaka Chenge akajiuzulu kule kwenye KATIBA pia.
PAC said:Mwanzo wa kunukuu.
"…kubadili Waziri Mkuu sio jambo la ajabu. Ndugu Rashid Mfaume Kawawa alikuwa Waziri Mkuu wangu kwa muda mrefu. Hakuwa amefanya kosa lolote; lakini nilitaka kumbadili na kuteua Waziri Mkuu mwingine. Nilimwita, nikamwambia hivyo. Tukakaa pamoja mimi na yeye, tukashauriana na kukubaliana nani anafaa kushika nafasi yake. Nikamteua Hayati Edward Moringe Sokoine. Najua kuwa watu wa aina ya Rashidi Kawawa ni adimu sana Duniani, hawazaliwi kila siku; hata hivyo
ni jambo la kushangaza kidogo kwamba viongozi wetu wa Mageuzi, hata bado hatujafa, wanaona kuwa ni kosa kuwakumbusha kuwa vyeo walivyonavyo ni dhamana.
Wanadhani kuwa Uwaziri ni Usultani; ukishakuwa Sultani utakufa sultani! Nadhani wanakosea. Nchi hii imewahi kung'oa Masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia Masultani wa kuchaguliwa, tutapanda mbegu ya Masultani wa kuzaliwa. Narudia; kumbadili Waziri Mkuu sio jambo la ajabu. Anaweza kujiuzulu, anaweza kufukuzwa Nchi isitikisike. Lakini
huwezi kumtimua Rais wa Nchi bila kuitikisa Nchi yenyewe. Ni vizuri jambo hili likatamkwa waziwazi na likaeleweka sawasawa. Maana watu wengine wananong'ona nong'ona kuwajibika kwa Rais kana kwamba ni jambo la mchezo mchezo tu. Kulazimika kumchukulia hatua Rais wa nchi ni mkasa na balaa kwa Nchi yeyote ile."
Mwisho wa kunukuu.
Ni kweli Mkombozi Bank ni ya kanisa na moja ya dhambi katika kanisa ni wizi na udanganyifu. Ifahamike kwamba bank hii inaendeshwa sawa na bank zingine chini ya usimamizi na miongozo kutoka central bank.
Kama kuna statutory/regulatory requirements ambazo Mkombozi Bank haiku comply wakati wote wa kufunguliwa kwa accounts na kufanya hizo transactions in question, naomba ziwekwe hapa tujadili. Vinginevyo hatutatukuwa tukiwatendea haki tukiwahukumu kuwa ni wakosa wakati hakuna kosa lililobayana ambalo wao kama bank wamelifanya.
Kuhusu askofu Kilaini na mwenziye, ni kwwli fedha walipokea. Mwenye ushahidi kwamba ffedha hizo walizipokea kwa niaba ya kanisa ama kanisa liliwatuma kuwa na huo ubia, aweke hapa. Kinyume na hapo ifahamike kwamba Kilaini ni viongozi wa kanisa lakini wao si kanisa. Ndiyo maana sheria imebainisha ni wakati gani mtumishi atahesabiwa kafanya kosa la kikazi linalomhusisha mwajili anayemwakilisha, ni wakati gani anakuwa ame commit personal offence, hata kama ni mtumishi.
NINAOMBA TUZITENDEE HAKI DHAMIRA ZETU KWA KUCHAMBUA HOJA KATIKA MISINGI YA UKWELI SAHIHI BADALA YA EMOTIONS NA MISUKUMO YA UTASHI WETU.
Tuko pamoja.
umeme umekatwa,sitaki kuamini kuna nguvu za kifisadis....
Mpaka sasa nasema subiri. Movie haijaisha.
Kwa ufisadi huu ndipo ninapoona China waliona mbali,ni kugongwa chuma tu!
baada ya zitto na deo kusoma taarifa ya kamati ya pac waziri mkuu mizengo pinda hana kosa wala hajatajwa popote kuwa kaiba au katengeneza mazingira ya kuiba bado pinda anabakia na heshima yake ya uadilifu
waliyo iba pesa ya umma wawajibike wote pia ambao kamati ya zitto haijawataja iwataja maana kuna walichota bilioni 73 kwa mifuko na mabegi ambao hawa kutajwa ni vizuri wangetajwa na wao
Hivi nani anasimamia shughuli za serikali?
Muhongo kama waziri angesimamia hizo pesa zisitolewe kutoka kwenye account,aondoke tu akafundishe folds na faultsDalali kivipi?, unaweza kuwa Dalali bila kupata chako?, Muhongo kapata ngapi ya udalali?, hebu onyesha makosa ya Muhongo yako wapi?
yeye kaingia Wizarani kakuta kuna kesi isiyoisha na Mkono kila siku anakula pesa za Tanesco hakuna kinachofikia muafaka,
kama waziri akawakutaniaha Wadai na Wadaiwa wamalize tofauti zao, yeye kakaa pembeni, sasa ulitaka Muhongo kama Waziri afanye nini, azidi kumgawia Mkono pesa ya uwakili wakati issue inaweza kuisha kwa Mdai na Mdaiwa kukutana?
Wizi wa ESCROW UPO NA KWELI PESA YA WANANCHI IMEIBIWA, NA KUNA WATU WANAPASHWA KUWAJIBISHWA, LAKINI NI MKITENDO CHA AIBU KWA MTU KAMA Zitto, kutafuta mwanya wa kumuingiza Muhongo Kwenye hiyo report Muhongo anafit vipi vipi kama sio kwa interest za Zitto na Genge lake? yaani bila Muhongo huo wizi usingefanyika?
aibu mahakama kuu kuweka katazo kuzuia kashfa
ya kampuni ya IPTL ya uchotwaji wa zaidi ya
mabilioni kwenye akaunti ya Tegeta
Escrow.