Full Text: Ripoti ya PAC Bungeni kuhusu Tegeta Escrow Account

Full Text: Ripoti ya PAC Bungeni kuhusu Tegeta Escrow Account

Baada ya Zitto na Deo kusoma taarifa ya kamati ya PAC Waziri mkuu Mizengo pinda hana kosa wala hajatajwa popote kuwa kaiba au katengeneza mazingira ya kuiba bado Pinda anabakia na heshima yake ya uadilifu

waliyo iba pesa ya umma wawajibike wote pia ambao kamati ya zitto haijawataja iwataja maana kuna walichota bilioni 73 kwa mifuko na mabegi ambao hawa kutajwa ni vizuri wangetajwa na wao
 
Aibu kubwavkwa wote waliorefusha midomo kumshambulia Kafulila, ukweli aibu hii itawaandama mpk mwisho wa Maisha yao.
 
matutusa wa lumumba wakiongozwa na wafu wao MSALANI & FaizaFoxy WAMEPIGWA GANZI au WAMEGANZISHWA! huwezi kuwaona kwenye uzi huu. wamejifungia lumumba pamoja na vibaraka wao wanauguliwa kipigo kizito walichopigwa leo kutoka kwa kamanda Zitto

Thubutuuuuuu yao, wadanganye waje wauone moto. Nao ni majizi tu
 
Last edited by a moderator:
P.A.C oyeee!
images
 
yeye ni dalali wa PAP na JR,Kuwatumia Zitto,Mengi na Mkono ili kupangua ufisadi wake,ni hoja dhaifu

Dalali kivipi?, unaweza kuwa Dalali bila kupata chako?, Muhongo kapata ngapi ya udalali?, hebu onyesha makosa ya Muhongo yako wapi?

yeye kaingia Wizarani kakuta kuna kesi isiyoisha na Mkono kila siku anakula pesa za Tanesco hakuna kinachofikia muafaka,

kama waziri akawakutaniaha Wadai na Wadaiwa wamalize tofauti zao, yeye kakaa pembeni, sasa ulitaka Muhongo kama Waziri afanye nini, azidi kumgawia Mkono pesa ya uwakili wakati issue inaweza kuisha kwa Mdai na Mdaiwa kukutana?

Wizi wa ESCROW UPO NA KWELI PESA YA WANANCHI IMEIBIWA, NA KUNA WATU WANAPASHWA KUWAJIBISHWA, LAKINI NI MKITENDO CHA AIBU KWA MTU KAMA Zitto, kutafuta mwanya wa kumuingiza Muhongo Kwenye hiyo report Muhongo anafit vipi vipi kama sio kwa interest za Zitto na Genge lake? yaani bila Muhongo huo wizi usingefanyika?
 
Last edited by a moderator:
Hakuna Waziri Mkuu Yeyote Chini Ya Kikwete atabaki salama.

Honestly Pinda Is Inocent.

Mkilazimishia ataondoka .. Huyo ajae .. ATAKUWA SALAMA?
 
Ni kweli Mkombozi Bank ni ya kanisa na moja ya dhambi katika kanisa ni wizi na udanganyifu. Ifahamike kwamba bank hii inaendeshwa sawa na bank zingine chini ya usimamizi na miongozo kutoka central bank.
Kama kuna statutory/regulatory requirements ambazo Mkombozi Bank haiku comply wakati wote wa kufunguliwa kwa accounts na kufanya hizo transactions in question, naomba ziwekwe hapa tujadili. Vinginevyo hatutatukuwa tukiwatendea haki tukiwahukumu kuwa ni wakosa wakati hakuna kosa lililobayana ambalo wao kama bank wamelifanya.

Kuhusu askofu Kilaini na mwenziye, ni kwwli fedha walipokea. Mwenye ushahidi kwamba ffedha hizo walizipokea kwa niaba ya kanisa ama kanisa liliwatuma kuwa na huo ubia, aweke hapa. Kinyume na hapo ifahamike kwamba Kilaini ni viongozi wa kanisa lakini wao si kanisa. Ndiyo maana sheria imebainisha ni wakati gani mtumishi atahesabiwa kafanya kosa la kikazi linalomhusisha mwajili anayemwakilisha, ni wakati gani anakuwa ame commit personal offence, hata kama ni mtumishi.

NINAOMBA TUZITENDEE HAKI DHAMIRA ZETU KWA KUCHAMBUA HOJA KATIKA MISINGI YA UKWELI SAHIHI BADALA YA EMOTIONS NA MISUKUMO YA UTASHI WETU.

Tuko pamoja.

Kosa kubwa la mkombozi ni kutoa kiasi kikubwa cha fedha kwa mara moja kinyume na sheria ya Bank kuu.
 
Haya tena ''tumbili'' leo kakamata mwizi kumbe ukali wote ule sio bure. Ama kweli '' A graceful giraffe cannot become a monkey''

Kafulila alitakiwa kwenye ndoa yake ya juzi apate '' zawadi ya ushindi'' hata hivyo kwa mabinti wa siku hizi mhhhh
 
labda tujikumbushie report ya richmond ni wap lowasa alitajwa kaiba ........?
 
Naona kama siamini amini kama atajiuzulu.....

Hata asipojiudhuru, kitendo cha kutolewa pendekezo na kamati na pendekezo kuungwa mkono na wabunge kwa kushangilia na kupiga makofi tayari reputation yake imeishuka sana kama si kuisha kabisa.
Ni aibu kubwa kwake kitaifa na kimataifa. Hata hivyo ni mtu wa hovyo, alitakiwa asome alama za nyakati na ajiondoe mapema. Kitendo cha kusubiri hadi atolewe mapendekezo na kamati ni aibu kubwa sana kwake.
Hata hivyo acha yamfike yaliyomfika, viongozi wengi wa Afrika yetu hii ni wagumu wa kuelewa mambo, hata hawajifunzi kutoka kwa wenzao wa nchi zilizoendelea.
Wenzetu huwa hawasubiri hatua hizi.
Ukijiondoa mapema unajijengea heshima, ukisubiri hatua za namna hii inahesabika umefukuzwa so inakuwa ni aibu.
Wanatutia aibu sana hawa.
Shame on them.
Wapi Faizafoxy, Mwanakijiji, Pasco, Ritz.......
 
Hahahahahaaaaa upo? Nakukumbuka sana ulivyokua Unakataaa na kuutetea huu wizi. Kazi unayo, maana suala sio kujibika suala ni ukiukwaji wa kanuni na taratibu.

Mpaka sasa nasema subiri. Movie haijaisha.
 
Back
Top Bottom