Full Time: Coastal Union 0-1 Simba SC | Mkapa Stadium | Mshindi wa tatu | 11/08/2024

Ubora wa Coastal naona kama imepungua sana msimu huu, sijui labda mbeleni waje wabadilike. Ila sijaiona ile Coastal ya msimu uliopita walikuwa wanautulivu na usahihi mkubwa wa pasi na walikuwa na ukuta na kiungo imara sana.
Wana timu nzuri ila wamekutana na giant wa Tanzania
 
Hawa wachezaji wa simba wakifika golini ni kana kwamba kila mtu anataka afunge aweke jina mapemaaa
 
Hii simba bado kabisa. Hata kama mechi haina umuhimu, lakini kwa upande wet mashabiki inamaana kubwa sana kukiamini kikosi.
 
Nimeelewa kwanini Simba wanataka kutafuta forward mwingine. Mukwala ana haraka sana ya mafanikio. Atulize kichwa chake na awe anaangalia walio kwenye clear chances. Simba hatutaki kujua kafunga nani, ila tunataka kushinda tena kwa idadi kubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…