Fundisho la Utatu haliingii akilini kabisa, mnaoamini mmetoa wapi mbona Biblia iko wazi kabisa?

Tayari nimekujibu post # 209. Kitu asilia hakina chanzo, na wewe unajua hivyo.

Huo mfano wako ni wa kiporojo zaidi kuliko uhalisi. Hauna afya ya mjadala wetu. Rudi kwenye hoja ya uwepo wa Mungu au la.

Hoja yangu ilijengwa katika msingi wa "Licha ya Mungu" kwa kuwa natambua uwepo wa Mungu. Nisingefanya hivyo, ningekuwa nimeikubali kizembe hoja dhaifu. Hata hivyo, kwa nini unakerwa na hiyo sentensi?
 
Kumbukumbu la Torati 6:4 Sikiza, Ee Israeli; BWANA, Mungu wetu, BWANA ndiye mmoja.

1 Yohana 5:8 Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.

Utatu Mtakatifu ni Mungu Mmoja katika Nafsi Tatu. Hatuna Mungu Watatu. Tuna Mungu Mmoja katika Nafsi Hai Tatu.
 
Kwanza hakuna jina la Mungu linaitwa Jehova, Mungu hana Jina
 
Ukishasema kitu asilia hakina chanzo, ushakubali kwamba chanzo si kitu cha lazima.
 
Yohana 1:1
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

Yohana 1:2
Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

Yohana 1:3
Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
Kwanza anza na maandiko hayo halafu ubishe kuhusu Mungu katika nafsi zake. Mimi naamini Mungu ni mmoja ambaye hujigawanya katika nafsi tofauti kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake.

1 Yohana 5:6
Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu.

1 Yohana 5:7
Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.

1 Yohana 5:8
Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.
Kumbuka Mungu alishasema hawezi kututokea sisi tumuone kama alivyo katika ubinadamu wetu maana tukimuona kutokana na dhambi tutakufa, hivyo alikuja kama mwanadamu ili tuishi naye na kukombelewa kutoka dhambini. Yesu alikuwa binadamu kwa asilimia mia moja na mwanadamu asilimia mia moja.
 
So mungu yesu pale msalabani alikua anamlilia nani!?..na aliyemtia mimba Maryam nani!?..na neno wa yohana ni nani,na aliyemtuma yesu nani!?
 
Kama wewe. Ni mkristo na hujui Baba,mwana na Roho mtakatifu Imani yako imetindikiwa kwa sababu hapo ndipo penye Imani ya mkristo.Hata Yesu akawaambi wafuasi pokeeni roho mtakatifu na kila mtakaye msamehe dhambi na mbinguni imefutwa.Yoh 20:22-23.
Hii ilikuwa siku ya Pentecoste ambapobwatu 3000 walibatizwa
 
Nimeamrishwa kupigana na watu wote mpaka waseme La ilah ila Allah Muhammad rasul allah
Sasa Huyo allah mpaka akuambie upigane kusambaza imani ya MUDI NA MAARABU WENZIE MBONA MAYAHUDI WAMEMUSHINDWA MPAKA LEO!!!TATIZO SISI SIO MAARAABU MWAMBIE HUYO allah na MUDI SISI TUNASEMA YESU NI MUNGU NA HAKUNA ANAEWEZA KUTUPIGA NA SIFA YA MUNGU WETU NI UPENDO!!!!
 
πŸ˜‚πŸ˜‚,Mambo ya imani hayalazimishwi, maana ni vitu za kubuni,, kuna wanaoabudu mtu kama wewe, kuna wanaoabudu ng'ombe, etc,,
Kila mtu yuko huru kuabudu chochote
 
Nimeamrishwa kupigana na watu wote mpaka waseme La ilah ila Allah Muhammad rasul allah
Hebu mndenge pata ilimu!
Uislamu [emoji56][emoji56]
[emoji116][emoji116]
: ΩˆΩŽΩƒΩŽΨ°ΩŽΩ°Ω„ΩΩƒΩŽ Ψ£ΩŽΩˆΩ’Ψ­ΩŽΩŠΩ’Ω†ΩŽΨ§ Ψ₯ΩΩ„ΩŽΩŠΩ’ΩƒΩŽ قُرْؒنًا ΨΉΩŽΨ±ΩŽΨ¨ΩΩŠΩ‘Ω‹Ψ§ لِّΨͺΩΩ†Ψ°ΩΨ±ΩŽ Ψ£ΩΩ…Ω‘ΩŽ Ψ§Ω„Ω’Ω‚ΩΨ±ΩŽΩ‰Ω° ΩˆΩŽΩ…ΩŽΩ†Ω’ Ψ­ΩŽΩˆΩ’Ω„ΩŽΩ‡ΩŽΨ§ وَΨͺΩΩ†Ψ°ΩΨ±ΩŽ ΩŠΩŽΩˆΩ’Ω…ΩŽ Ψ§Ω„Ω’Ψ¬ΩŽΩ…Ω’ΨΉΩ Ω„ΩŽΨ§ Ψ±ΩŽΩŠΩ’Ψ¨ΩŽ ΩΩΩŠΩ‡Ω ۚ ΩΩŽΨ±ΩΩŠΩ‚ΩŒ فِي Ψ§Ω„Ω’Ψ¬ΩŽΩ†Ω‘ΩŽΨ©Ω ΩˆΩŽΩΩŽΨ±ΩΩŠΩ‚ΩŒ فِي Ψ§Ω„Ψ³Ω‘ΩŽΨΉΩΩŠΨ±Ω

[ ASH-SHUURA - 7 ]
Na namna hivi tumekufunulia Qur'ani kwa Kiarabu ili uwaonye watu wa Mama wa Miji na walio pembezoni mwake. Na uhadharishe na Siku ya Mkutano, haina shaka hiyo. Kundi moja litakuwa Peponi, na kundi jengine Motoni.
: ΩˆΩŽΨ£ΩŽΩ†Ψ°ΩΨ±Ω’ عَشِيرَΨͺΩŽΩƒΩŽ Ψ§Ω„Ω’Ψ£ΩŽΩ‚Ω’Ψ±ΩŽΨ¨ΩΩŠΩ†ΩŽ

[ ASH-SHUA'RAA - 214 ]
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.


claims!; Saudi author Muhammad al-Arifi Wahab Cleric said:

ARABS are the true Muslims and the true descendants of Prophet Muhammad (pbuh)..

"Nonβ€”Arabs who without shame, called themselves Muslims are just plain Converts whom are lowly cowards with unhonourable souls That were overwhelmed with ease by the Swords of Allah, thus they deserved to be called as our Dogs."
 
So mungu yesu pale msalabani alikua anamlilia nani!?..na aliyemtia mimba Maryam nani!?..na neno wa yohana ni nani,na aliyemtuma yesu nani!?
Alikuwa Anamlilia Mungu Akiwa Ktk Hali yake ya Ubinadamu Kamili!
Sema Mungu Hawezi!
 
JEHOVAH ni MUNGU Baba na sio Yesu (MUNGU Mwana).
MUNGU alimwambia Musa amwite JEHOVAH . Na Musa hakuwahi kuiona sura ya MUNGU , kwa hiyo huyo ndiye MUNGU Baba - haonekani
Musa aliabudu dini gani?
 
πŸ˜‚πŸ˜‚,Mambo ya imani hayalazimishwi, maana ni vitu za kubuni,, kuna wanaoabudu mtu kama wewe, kuna wanaoabudu ng'ombe, etc,,
Kila mtu yuko huru kuabudu chochote
Jamaa anatulazimisha tuamini anachoamini ndio nashangaa
 
Kwanza hakuna jina la Mungu linaitwa Jehova, Mungu hana Jina
Umesoma Mungu hana jina kulingana kitabu gani!
Andika huo mstari hapa? Mm nitakuonyesha mistari yenye kuonyesha Mungu ana jina!
 

Inategemea Allah unamuita katika kitu gani. Na pia jifunze kuwa Uislamu hauamini katika miujiza kama nyie. Tunaamini atakalotaka Mola ndio litakalotokea sio kulazimisha wewe unavyotaka. Keep Allah out of you nonsense.
 
Nilijibu hoja hiyo post # 209.
Uliandika hivi.

"Mungu ni asili. Licha ya asili, sijakubali kwamba chanzo sio kitu cha lazima."

Unaelewa hapa umekubali kwamba chanzo si kitu cha lazima?
 
Alikuwa Anamlilia Mungu Akiwa Ktk Hali yake ya Ubinadamu Kamili!
Sema Mungu Hawezi!
Kama mungu alikua katika Hali ya ubinadam,alikua akimlilia nani Sasa!?..maana huko akaako mungu haikuwepo alikua galilaya
 
Uliandika hivi.

"Mungu ni asili. Licha ya asili, sijakubali kwamba chanzo sio kitu cha lazima."

Unaelewa hapa umekubali kwamba chanzo si kitu cha lazima?
Unaweza kufafanua kukubali kwangu katika hiyo post?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…