Fursa nchini Morocco: Biashara ya mbuzi inalipa sana

Fursa nchini Morocco: Biashara ya mbuzi inalipa sana

Hao waliokufanyia ubaguzi labda uliwaudhi , mbona mimi nimekaa nao miaka 5 sijaona ubaguzi wowote ?? Tena kuna wakati naumwa nilikuwa na rafiki yangu akisoma mwendo wa masaa mawili na nusu kwa train na alikuwa akija kuniangalia
Itakuwa alieenda na mzungu wake
Akaona wanamchangakia zaidi kuliko yeye huwa wanajua mtu mweusi hatoi tip
 
Sio kwamba wafanyabiashara hawajui. Tatizo ni namna ya kuwasafirisha na gjarama zake. Hizi ndege za kuungaunga hadi Morocco sio rahisi. Miuondo mbinu ya usafirishaji wa meli poa migumu.
 
Kingine watanzania wavivu kutafuta masoko mengine,na hili la kingereza ni tatizo pia anashindwa kuconnect na watu wapya. Nnimetembelea sehem izo sijakutana na mtanzania kwenye biashara izo.
Watanzania ndio jamii ya watu ambao hufasiri kwa uchache zaidi.. yani unawezakuta katika mtaa ni mtu mmoja au hata watu 2 ndio wametoka nje ya mpaka wa Tanzania
 
Si kweli,mpaka mbuzi. Cha msingi uzifikishe salama. Mbuzi wanauzwa wengi
Mkuu, kuna vitu navijua vizuri sana kwenye biashara hiyo, kusafirisha mbuzi wazima ni biashara kichaa,unaweza kusafirisha,ila sahau kuhusu faida,kwanza waarabu wanachagua sana sana!! Ukimpelekea mbuzi mkubwa sana hanunui, ukimpa aliyenona sana hanunui, waarabu wanapenda mbuzi wadogo,ambao hawajakomaa, angalau ukipeleka nyama kwanza wateja ni wengi, pia ni vigumu kidogo kuanza kuchambua nyama ya mbuzi wa miaka miwili kwenye cold room lenye miili ya mbuzi 2000, kikubwa ni uaminifu, ukipata mteja akakwambia sitaki mbuzi wazee wewe jiongeze, kuna waarabu hawanunui mbuzi sababu tu ya rangi yake, mwingine akiona tu hata mkwaruzo kwenye ngozi hanunui, jifunze zaidi mkuu,nipo kwenye hiyo industry,so najua 1i-2-3
 
Mkuu, kuna vitu navijua vizuri sana kwenye biashara hiyo, kusafirisha mbuzi wazima ni biashara kichaa,unaweza kusafirisha,ila sahau kuhusu faida,kwanza waarabu wanachagua sana sana!! Ukimpelekea mbuzi mkubwa sana hanunui, ukimpa aliyenona sana hanunui, waarabu wanapenda mbuzi wadogo,ambao hawajakomaa, angalau ukipeleka nyama kwanza wateja ni wengi, pia ni vigumu kidogo kuanza kuchambua nyama ya mbuzi wa miaka miwili kwenye cold room lenye miili ya mbuzi 2000, kikubwa ni uaminifu, ukipata mteja akakwambia sitaki mbuzi wazee wewe jiongeze, kuna waarabu hawanunui mbuzi sababu tu ya rangi yake, mwingine akiona tu hata mkwaruzo kwenye ngozi hanunui, jifunze zaidi mkuu,nipo kwenye hiyo industry,so najua 1i-2-3
shukran...
 
anzia ubalozi wa Morocco hapa tz wakupe details zaidi. Au cheki na ubalozi wa tz huko Morocco ili wakupe info sahihi
 
Tanzania si nasikia tuna export nyama ya mbuzi huwa wanapeleka wapi?

Nahisi ni either Oman au Saudi, Ila nyama ya mbuzi ni dila sana uarabuni, kule sio sana kula nyama ya ng'ombe, wao ni mbuzi na kondoo tu. bado sana hatujawa serious kwenye hiyo ishu, Saudi, Oman, UAE, Qata, Kuwait, Bahrain, Morocco, Tunisia, Algeria yani soko lipo kubwa sana ila sisi tu tumelala
 
Kwa umri wangu huu mdogo nimepata fursa ya kutembelea baadhi ya nchi hapa Afrika,ktk fursa hii nimebahatika kwenda nchi ya Morocco.

Nilienda Morocco kupitia Mali kwa Tombouctou Airport ya Mali to Duarzazate airport ya morocco.
Nikiwa Morocco nimetembelea majiji tofauti tofauti km unavyojua tunaojitafuta kila tulipo tunaangalia furasa, kati ya majiji niliotembea ni pamoja na Nador, Tetouan na Tangier(mji wa kibiashara sana,maana hapa watu utoka ulaya kuja kufanya biashara hapa).

Kuna fursa nimeliona Morocco, kwa mtu mwenye connection na mtaji unaweza ukaifanya. Morocco biashara ya Mbuzi inalipa sana, kule wanapenda sana nyama choma hasa ya mbuzi, wazungu wanatoka Spain kuja kununua mbuzi Morocco. Mbuzi mwenye ubora mzuri anauzwa hadi laki tano(500,000/=)kwa ela ya kitanzania na wakati mwingine mbuzi zinakuwa hadimu bei upanda.

Kule Waarabu wana hela, hawalili bei kiasi hicho. Kama anahitaji atachukua. Lkn mbuzi wengi sana wanaenda ulaya, nimeona niwasanue kwa hili.
Wale siyo waarabu ni moors
 
Kwenye nchi za kiarabu ikiwemo Morocco,kuna kiwanda kikubwa tu cha kuchakata nyama kinachomilikiwa na muhindi mkoani Arusha huwa kinafanya uchakataji na usafirishaji nyama (ya mbuzi tu) kwenda huko, kiwanda kina uwezo wa kuchakata hadi mbuzi mia tano kw sikuna bado wanasema soko mzigo hautoshi, ni biashara nzuri ila inahitaji mtaji mkubwa,, wat3ja huwa wanatoa order ya kuanzia mbuzi 100 na kuendelea,nilishajaribu kutafuta wateja huko kupitia Go4worldbusiness.com na nikawapata wengi tu, issue ni vigezo na masharti yanakuwa mengi huku mtaji pia ukiwa changamoto, asante kwa kutusanua tena.

mkuu mtaji kama ngapi unaohitajika kwa kuanzia?
 
Back
Top Bottom