CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 5,621
- 5,029
- Thread starter
-
- #21
Uchaguzi wa 2025 tayari CCM ilishashinda kabla ya Uchaguzi kuanza Pole sana " roho mbaya "Samia mwisho wake ni 2015.
Hayo mafeni yameletwa na chama gani? Hata yeye bado ataacha madeni mengi tu, kwa hiyo atakae chukua nchi baada yake na yeye ajisifu, sio? Ama hiyo mikopo atailipa kabla hajaondoka?
Ccm hata wakipewa miaka 1000 ngonjera ni hizi hizi.
niwapi kasifiwa Rais hapa,Chadema mtateseka sana kwa speed ya mama,Ninafikiri huyu ni Samia mwenyewe anajipigia promo..maana post zake ni kujikweza tuuu mwanzo mwisho.
Fanya kazi mama, ni wajibu wako. Huna sababu ya kujinadi kiasi hicho.
Kibaya kinajitembeza ila kizuri siku zote hujiuza.
CHADEMA kilishakufa kitambo sana,Chama kinakopa tangu lini wewe CHADEMA,
Madeni ni kwa maendeleo ya nchi,
Hayo madeni hata wewe yamekunufaisha kwa namna moja ama nyingine,
Hongera Sana Rais Samia tuko nawewe sana tu,
Toa sababu,Hakuna shaka mwenye account hii ni mwigulu nchemba
Ndio kodi zetu mkuu, tujipongezeKodi zetu hizo
Indelee kwa kasi zaidiKazi iendelee
Zimeongezwa mkuuHivi dau ni lile lile buku saba au wameongeza kidogo?!
Wakandarasi vicheko,Rais Samia Suluhu Hassan kimyakimya analipa madeni mbalimbali aliyoyakuta na kwa kuanza kwa mwaka huu pekee analipa madeni yenye Jumla ya TZS11.17623Trilioni,Mnapoambiwa Rais Samia huyu ni levels zingine muelewe na mumuombee mzigo huu ni mzito sana mabegani mwake na unahitaji neema ya Mungu,
1 . Mama ametoa TZS 111.41BL ili kuwalipa watumishi wa Serikali wanaoidai Serikali,malipo haya yataongeza ari na nguvu za watumishi hawa katika kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kuwatumikia Watanzania ambao ndio waajiri wao,
2. Mama ametoa Jumla ya fedha TZS 264.23BL kwaajili ya kuwalipa wakandarasi mbalimbali wa nje na ndani waliokuwa wanaidai Serikali ili kuongeza imani na uaminifu kwao katika kuendelea kutoa huduma kwa Serikali yetu ya JMT,
3. Mama ametoa Jumla ya fedha TZS 70.49BL kwaajili ya kuwalipa Wazabuni mbalimbali waliotoa bidhaa na huduma kwa Serikal,wote mtakumbuka Wazabuni wengi walikuwa wanalalamika kudaiwa mikopo benki naamini wamefuraha sasa na Wataendelea kutekeleza ilani ya CCM ya 2020-2025 bila kinyongo,
4. Mama ametoa TZS 2.17BL ili kuwalipa watoa huduma mbalimbali waliokuwa wanaidai Serikali kutoka katika Wizara mbalimbali,Hakika mama huyu anajicho la pekee kama hujaelewa unakwenda wapi na Rais Samia basi ni wazi wewe utakuwa hujui unakotaka kwenda,
5. Mama ametoa Jumla ya fedha TZS 67.93BL kwaajili ya hukumu na fidia mbalimbali ambazo Serikali inadaiwa baada ya kushindwa kesi mbalimbali ili kutengeneza imani kwa wawekezaji wa ndani na nje pamoja na watu binafsi,
6. Mama ametoa jumla ya fedha TZS 10.66Trilioni ili kulipia deni la Serikali pamoja na mikopo mingine hakika mzigo ni mkubwa ila kwa uwezo wa Manani kupitia Rais Samia tutafika tena kwa kuwahi,
View attachment 2003891
Naungana na wewe kwa 100% kwenye hilikutokana na Deni la taifa kupaaa, tinaiomba Serikali ihakikishe inadhibiti na kubana matumizi yasiyo ya lazima kwa mfano;
1. Safari za nje zisizo za lazima zizuiwe/zipunguzwe.
2. Vikao vya Bunge zipunguzwe, ratiba ya vikao iangaliwe upya kuanzia mwakani.
3. Matumizi ya magari ya V9/v8 ambayo ni gharama kubwa kuyahudumia,
4. Semina na vikao visivyo vya lazima vipunguzwe.
5. Mishara mikubwa kwa baadhi ya watendaji ipunguzwe, isiwe zaidi ya milioni 10 kwa mtendaji 1.
maana kuna baadhi ya taasisi za serikali watu wanalipwa hadi milioni 15 kwa mwezi.
Kama kweli Serikali yetu pamoja na watendaji wake wana uchungu na watanzania basi lazima wafanye kitu ili kuinisuru nchi na kuelemewa na madeni.
haiwezekani nchi imeandamwa na madeni mpaka puani halafu kuna baadhi ya watu/watendaji wanazidi kunyonya tu bila huruma.
hapana, tunataka kuona hatua zinachukuliwa haraka.
Tulisema tukaonekana wendawazimu, Leo nyie ndio mmethibitisha kuwa MNA matatizo makubwa, niwakumbushe tu kuwa jengeni mifumo na sio mtu, SSH akiondoka mtamsema pia. Samia hatoi pesa na wala haipaswi kutamkwa hivyo ila kwakua ujuaji mwingi hamtakubali
Ina maana wapinzania wakishika nchi hawatakopa .?Huwa naona kama wana ccm Sana matatizo makubwa, hayo madeni makubwa ni yameletwa na chama gani?
Daah madeni ya watumishi,tafuta namna nyingine ya kumpongezq mama,sio inshu ya madeni ,mwal.aliacha madeni,mwinyi aliacha madeni,mkapa aliacha madeni ,jk pia.hakuna ambae ataweza kuyamaliza au kutokukopa.tunachotaka maendeleo basi
Madeni yanaletwa na chama chochote makini. Kama hudaiwi maana yake wewe huna majukumu na hufai kuaminiwa.Huwa naona kama wana ccm Sana matatizo makubwa, hayo madeni makubwa ni yameletwa na chama gani?
Hataki tu kusikia Rais Kalipa madeni ya wazabuni, watushi, wakansarasi ili apate cha kuongeaIna maana wapinzania wakishika nchi hawatakopa .?
Madeni mpaka China na USA wanadaiwa. Hawapati madeni kwa nia ya kujifurahisha tu ni katika kutimizamalengo ya muda mfupi na mrefu.Samia mwisho wake ni 2015.
Hayo mafeni yameletwa na chama gani? Hata yeye bado ataacha madeni mengi tu, kwa hiyo atakae chukua nchi baada yake na yeye ajisifu, sio? Ama hiyo mikopo atailipa kabla hajaondoka?
Ccm hata wakipewa miaka 1000 ngonjera ni hizi hizi.
Unayohoja hoja mkuu ila usiogope deni ni stahimilivu kwa kipindi kifupi, chakati na kirefu hii ni kimataifa so relax nchi iko salama sana,kutokana na Deni la taifa kupaaa, tinaiomba Serikali ihakikishe inadhibiti na kubana matumizi yasiyo ya lazima kwa mfano;
1. Safari za nje zisizo za lazima zizuiwe/zipunguzwe.
2. Vikao vya Bunge zipunguzwe, ratiba ya vikao iangaliwe upya kuanzia mwakani.
3. Matumizi ya magari ya V9/v8 ambayo ni gharama kubwa kuyahudumia,
4. Semina na vikao visivyo vya lazima vipunguzwe.
5. Mishara mikubwa kwa baadhi ya watendaji ipunguzwe, isiwe zaidi ya milioni 10 kwa mtendaji 1.
maana kuna baadhi ya taasisi za serikali watu wanalipwa hadi milioni 15 kwa mwezi.
Kama kweli Serikali yetu pamoja na watendaji wake wana uchungu na watanzania basi lazima wafanye kitu ili kuinisuru nchi na kuelemewa na madeni.
haiwezekani nchi imeandamwa na madeni mpaka puani halafu kuna baadhi ya watu/watendaji wanazidi kunyonya tu bila huruma.
hapana, tunataka kuona hatua zinachukuliwa haraka.