Gari namba MT 0128 Mali ya Jeshi la Magereza ikiwa na Wafungwa inatumika kupandisha Bendera za CCM katika nguzo za barabarani hapa Dodoma Mjini Leo

Bado tu kuambiwa ukitaka ajira au huduma yoyote serikalini lazima uonyeshe kadi yako ya CCM.
Watanganyika tusikubali huu ujuha
 
Una haraka ya Nini? Bado kidogo tu hapo October hivi vyombo vya umma vitakuwa vyenu chadema wakati rais ni tundu Lissu.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Hivyo ndivyo tulivyoambiwa vyama Vya upinzani lazima vifutwe
 
Umeona kadi ya gari inasomeka gari ya magereza? Mleta mada Mara ingine mnajitafutia jela bure

Hata traffic huwa haamini hi gari ya Nani kea kuangalia plate number sembuse wewe
 
Wanataka kuturudisha kwenye zama za ujima
Bado tu kuambiwa ukitaka ajira au huduma yoyote serikalini lazima uonyeshe kadi yako ya CCM.
Watanganyika tusikubali huu ujuha
 
Hii ni aibu sana.. shida ipo kwenye haya majeshi yetu. Kuna watu hawajielewi kabisa
 
Hata wewe unaweza kuwatumia wafungwa kwa shughuli yoyote ila kuna malipo unalipia, Sio kesi!
Mimi washanivunia sana mpunga
Kuwatumia unaweza ila kumbuka hao wafungwa wapo chini ya chombo cha dola ..ambavyo vyombo hivyo vya ulinzi havihusian na Mambo ya siasa.

Yani hata kama ni shughuli ya malipo sio kwenye siasa..tunakosea tujirekebishe.
 
Kuna tatizo katika hili la wafungwa kupandisha bendera za CCM mitaani ,

Au labda hawa wafungwa ni tawi la CCM kule gerezani,wajuvi tubarishane mawazo hapa??
 
Waache wapandishe, chama chenyewe ni cha wafungwa waliokosa uhuru wa kuamua zaidi ya kuamliwa na mtu mmoja,ndio maana watu wenye akili kama Membe wametoroka kwenye gerezaccm.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…