Gari wanazohitaji waTanzania hazipatikani dunia nzima

Mjerumani wa Jf katika ubora wako πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Hizo toyota century mnamiliki wangapi hapa bongo?

Zaidi nawaona kwenye raum, sienta, spacio n.k

Mbona sizioni barabarani? Kidogo naziona progress, brevis na crown.
Unazo waona nazo wabongo zipo katika level ya uchumi wao. Kilicho juu ya uchumi wao hawakiwezi. Kabla ya kununua gari lazima uchuje vitu vingi. Kuna Vitz zina bei sawa na BMW wanazomiliki machalii hapa bongo.. ila mtu anachukua zake tu Vitz anatulia, sio kwamba asingeweza nunua BMW ila mahesabu yake yamekataa.. kuiga kunya kwa tembo wengine hawataki
 
Hiyo engine ya 2JZ-GTE kutokana na mkataba ndio maana waliiminya kuachia nguvu yote na hiyo ilitokana mkataba. Wazungu wana fitina sana [emoji3][emoji3][emoji3]
Story za vijiweni hizo. Mnajazana ujinga na hypes.

Onesha huo mkataba, unahusu nini, unasemaje, kwa malengo gani?

Hiyo engine unaikuza tu. Haina uspecial wowote.

Kuna mwenzako aliita Aristo yenye hiyo engine performance car. Kwamba ameilinganisha na 911 turbo S.
 
Mie nakaa na mkatba kama nani.. jipitie link hapo chini mkuu

Motortrend
 
Wajapan mnamiliki gari za 2019 si ndio?

Au na nyie mnanunua hizo hizo za 2003?

Hivi C class ya 2003 unailinganisha na gari gani za Toyota hapa bongo?

Kwamba utapata stability, speed, handling bora zaidi ya hiyo c class?
Gari zilikuwepo kwa kazi hio, kina Celsior, Brevis, Progress na Lexus ES300 wote walikuwa wanakalisha!
 
Mjerumani wa Jf katika ubora wako [emoji3][emoji3][emoji3]

Ndio ukweli huo sijawahi kuona Mabilionea wana show off na hizo Toyota, tunaona tu Benz G wagon, Bwm , RR , na nyingi za Ulaya.. labda Dubai ndio tunaona mwarabu tena jangwani anafanyia mbwembwe huko,hizo Toyota .. , tuwe wakweli mioyoni kwetu hata huko Japani wenye nazo utaona wanasukuma Mjeruman, nionyeshe tajiri yoyote Japan asikuwa na gari ya Ulaya., kuanzia Waziri Mkuu wao mpaka mabilione wao wanasukuma Germany mashine.., na kwao ndio Kiwanda cha Toyota kilizaliwa.
 

Floyd Mayweather JR. Toyota Avanza
 
Ila vipi mziki Skyline GTR upoje ? nafatilia fatilia inaoneka ni chombo moja hadi leo wazungu wanaitamani
Wazungu wameshatengeneza gari zinachomoka kuliko hiyo skyline. Au unaposema "wanaitamani" unamaanisha nini?

Naipenda Nissan GTR Nismo.

Ndo gari pekee Japan naimezea mate.
 
Matajiri huwa wanakuwa na gari nyingi nyingi, na maskini vipi ? Alafu hapa ligi ni mjerumani na mjapan. Usilete na England, Italiano, India na USA.. mbona mnaunganisha nguvu Vs mjapan peke yake au mmesanda tayari ? Kuna legue yenu tuna wandalia Mjerumani vs Muingereza .. subirni kwanza
 
Wazungu wameshatengeneza gari zinachomoka kuliko hiyo skyline. Au unaposema "wanaitamani" unamaanisha nini?

Naipenda Nissan GTR Nismo.

Ndo gari pekee Japan naimezea mate.
Aah! Hata mimi napenda sana Ferrari , Astorn Martin, Bentley kidogo na RR.. haina shida.
 

Mwingereza hana kitu Sasa hivi Land Rover kitambo tuu imechukuliwa na TATA ya India, RR Imechukuliwa na BMW sasa sijui kuna nini huko Uingereza labda Bentley na sina uhakika kama ajauza shea yake Germany.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…