Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

1. Udini hautakufanya uonewe huruma.
2. Issue ya Udom hujui chochote, bora ukae kimya tu.
3. Funga bakuli lako, historia ya ukombozi wa TZ tunaijua pia.
Mjamaa,
Hapana haja ya matusi.

Mimi ningependa sana unieleze yaliyotokea UDOM kwani wewe unaifahamu vyema.

Kuhusu historia ya ukombozi unayoielewa wewe ni ipi?

Mimi ndiye niliyesahihisha ile ya Chuo Cha CCM Kivukoni kwa kitabu cha Abdul Sykes.
 
Mohamed kwani tunashindana? La hasha ni kuwekana sawa hoja zako nyingi zina ukakasi na si ajabu jukwaa limekuwa la moto.

Sisi tungefurahi ungewataja wazi wazi hao unasema walivunja EAMWS na pia uwataje wazi wazi waliofuta hiyo historia wa wapigania uhuru 'unaowataka'
Maswali..
1. Kwanini wafutwe??

2. Walikuwa na madhara gani hadi wafutwe?? Ni kweli ilikuwa chuki za kidini? Zilitoka wapi na zilisababishwa na nini??

3. EAMWS vision yake ilikuwa nini ili tupate sababu ya kukubali au kukataa kufutwa kwake..

4. Mohamed unafahamu kuwa ni rahisi sana kwa mwanafunzi kwa kiislam kusoma shule inayoendeshwa kwa misingi ya ukristo kuliko mwanafunzi wa ukristo kusoma shule inayoongozwa kwa misingi ya kiislam?? Unafahamu ni kwanin??

Nasubiri majibu ili niendelee na mjadala
 
Mohamed bado ana hoja nyingi za kujibu ila hatupi majibu ya kuridhisha ndio maana tunaona ni km anafanya ubabaishaji
 
Asante Mzee Mohamed, je kinapatikana kwa soft copy au ni hard copy pekee, na kama ni hard copy pekee nakipata sehemu gani? niko nje ya Dar Es Salaam
 
Kama unaamini wao walisukumwa na UDINI, haihalalishi nawe kuwa wao!! Busara ni kukemea UDINI, na sio kuendeleza UDINI eti kwa sababu zama hizo watu walitenda kwa kusukumwa na udini!!

Lakini kubwa zaidi, kama nilivyotangulia kusema hapo awali, Bibi Titi anatambulika kama mwanasiasa na sio kiongozi wa dini!! Bibi Titi anatambulika kama miongoni mwa waanzilishi wa UWT na sio mwanzalishi wa taasisi yoyote ya Kiislamu!!

As far as I know, hao waliojitokeza "leo hii: kumuenzi Bibi Titi sio Waislamu bali wana-CCM, na walienda pale kumwenzi Bibi Titi, ambae alikuwa mwanasiasa mwenzao!!

Hoja zako ningezimulia kidogo endapo hao walioenda kumuenzi wangekuwa ni Waislam, wanaoenda kumuenzi Mwislam mwenzao, halafu hapo akatokea Gaudensia Kabaka!!

Kinyume chake, walioenda ni wana-CCM!! Waliyeenda kumuenzi, anatambulika duniani kote kwa kupitia mrengo ule ule wa walioenda kumuenzi!! Ajabu, suala la wanasiasa kwenda kumuenzi mwanasiasa mwenzao unataka kuligeuza kuwa la kidini... wapi na wapi!!!
Nimesoma, na sijaona uhusiano wowote na mada inayoendelea hapa!!! Nilichokiona hapo ni maelezo yako ya kihistoria kuhusu uliyemtambulisha kama babu yako... Salum Abdallah, na Chinga Redrick Mchaulu!!

Sina shida na historia zako kwa sababu anayekerwa, na yeye aandike tu zake!! Shida yangu ni kuchanganya DINI na historia zako, na hata pasipo na historia husika!! Kama hii ya sasa, sioni uhusiano wowote wa wana-CCM kumuenzi Bibi Titi, halafu unaingiza udini as if huyo Bibi Titi alikuwa kiongozi wa Kiislamu!!
STILL HAKUNA UHUSIANO WOWOTE...

Unayanyamazia vipi uliyoyaona hayana na bado unatumia muda kutoa maelezo ambayo ni irrelevant?!

Ku-summarize hayo unayoona hayana maana, nieleze mantiki ya kuingiza udini kupitia suala la wanasiasa wa CCM kwenda kumuenzi wanayeamini ni mwenzao!!

Na kwa heshima na taadhima, na kuona hayana maana, basi ningekuomba UNIJIBU maswali yangu #1 hadi #6!! Muungwana akiombwa, sina shaka hutoa... naomba unijibu hayo maswali!!!
 
Anakimbilia kusema anaona "hazina maana"!!
Hapo ndio tunapopishana na yeye. Tunahitaji hoja zote zijibiwe kwa weledi mkubwa tuhuma anazotoa ni nzito kiasi kwamba inabidi azijibu kulingana na uzito wake wala sio juu juu.
 
Mzee Mohamed Shikamoo!
Bila shaka umewahi kusoma kitabu Cha Abubakari Ulotu ..Historia ya TANU,Mimi nilikisoma nikiwa darasa la Saba !
Nasikikitika huwa nakitafuta kwenye maduka ya vitabu sikipati!
Nakumbuka Bwana Ulotu alibainisha harakati za Watanganyika wakati wa kuijenga TANU maeneo mbalimbali ya Taanganyika!
Sikumbuki Kama alieleza kuwa watu wa Pwani ,na kwa maaana yako wewe Waislam! walidhulumiwa baada ya Uhuru!
Wewe unakizungumziaje Kitabu hicho !?
 
Asante Mzee Mohamed, je kinapatikana kwa soft copy au ni hard copy pekee, na kama ni hard copy pekee nakipata sehemu gani? niko nje ya Dar Es Salaam

Asante Mzee Mohamed, je kinapatikana kwa soft copy au ni hard copy pekee, na kama ni hard copy pekee nakipata sehemu gani? niko nje ya Dar Es Salaam
Kile...
Kitabu hiki kinapatikana Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro, Manyema na Mtambani.

Vilevile Elite Bookshop na Soma Bookshop.

Kwa Kiingereza na Kiswahili bei elfu kumi.

 
Hua nsmshangaa sana mzee wangu saidi kutaka kutuaminisha kua nyerere alikuja mjini akiwa hohehaheee [emoji1787][emoji1787][emoji1787].

Mtu alikua mwalimu tena enzi za ukoloni, utuaminishe kua alikua lofaa tuuu?.

Mbona huwa hasemi jinsi nyerere alivyo acha ualimu wenye malipo mazuri wakati huo ,ili kujiunga na harakatii?.

Yes, anatajwa sanaa nyerere pekee katika vitabu vya historia, lakini hiii haondoi uwezo wa hali, mali na akili alizo kua nao wakati huo
 
Asante Mzee Mohamed, je kinapatikana kwa soft copy au ni hard copy pekee, na kama ni hard copy pekee nakipata sehemu gani? niko nje ya Dar Es Salaam
Kl...
Samahani nimekuwekea kitabu cha Abdul Sykes.

"Kwaheri Ukoloni..." ipo soft copy ingia Google utakipata.

Samahani sana.
 
Chige,
Jibu nimekupa jibu hulitaki.

Unakuwa Shylock na ratili yake ya nyama anayodai kwa Bassanio.

Shakespeare "Merchant of Venice."

Umesoma historia ya babu yangu aliyepigania uhuru wa Tanganyika.

Babu yangu kaweka rekodi ya kihistoria ambayo hadi leo hajavunjwa nadhani Afrika nzima.

Kaongoza migomo mitatu 1947, 1949 na 1960 dhidi ya dhulma za Waingereza.

Mchochezi.
Hizi ni General Strikes.

Mgomo wa 1960 ndilo taji lenyewe ulidumu siku 82.

Unapata tabu kutambua achievement hizi na unasema ni, "rrelevant."

Lazima niheshimu fikra zako lakini kwangu nakutia kwenye mizani na kupata uzito wako.

Vyuo Vikuu wananisukuma niandike historia ya Salum Abdallah babu yangu.

Wanataka kujua kwa miezi mitatu wafanyakazi walikuwa wanajikimu vipi?

Nawagusia kuwa East Germany walitoa msaada wa fedha kwa TRAU halikadhalika chama cha wafanyakazi wa reli Uingereza.

Wananisukuma kila uchao niwape mswada wachape kitabu.

Wewe huoni chochote hapo wala hushangai kuwa babu yangu hajatajwa katika Labour politics za Tanganyika.

Haya ndiyo maswali nikijadiliana ba walimu wangu wa historia Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Unataka mimi nikujibu maswali yako.

Hapana.

Mimi niko darasani hapa nasomesha historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Jipime uwezo wako.

Je, ulikuwa unamjua Salum Abdallah?
 
Mzee humu kuna watu hawako tayari kupokea maarifa. Unahangaika nao wengine wakati wanakokotoa vya kuandika wanagugo kwanza, ninakushauri wengine waache usiwajibu, hawa wenye maswali yenye tija na wanaokubali hoja kinzani wakaielew ndio tunaowataka hapa
 
Vyovyote vile naamini kuna mapungufu mengi sana katika uandishi wa historia ya nchi ya Tanganyika na baadae Tanzania, mfano mwingine mzuri, shujaa wa mapinduzi ya Zanzibar ni yule Mganda Okello lakini leo historia imejaa na kumtukuza Mzee Karume!
Kwanini huyu mzee asiizungumizie hii historia ya Okello au kwakua Okello sio mvaa kanzu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Jamii zina jielezea zenyewe hakuna haja ya pepa wala nini hayo ni maandiko yako binafs na ibinafsi wako wa kidini..ila ukweli uko wazi jamii za pwani na za bara zipi zinaongoza kutilia maanani elimu?

#MaendeleoHayanaChama
 
1. Udini hautakufanya uonewe huruma.
2. Issue ya Udom hujui chochote, bora ukae kimya tu.
3. Funga bakuli lako, historia ya ukombozi wa TZ tunaijua pia.
Huyu tumpe jina la mzee kilizi..analialia anataka aonewe huruma na vi historia vyake uchwara..basi achuke nchi aifanye Islamic ili moyo wake ufurahi..fanatics

#MaendeleoHayanaChama
 
Huyu mzee anataka kutuharibia amani ya nchi..apigwe ban ya maisha humu..asilete hoja zake potofu za kutaka kupandikiza chuki za udini kwa watanzania..fanatic mkubwa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mzee Said,Kama hutaki kujibu hoja yangu ya uzi no. 205 Basi pokea hata shikamoo!
 
Huyu mzee anataka kutuharibia amani ya nchi..apigwe ban ya maisha humu..asilete hoja zake potofu za kutaka kupandikiza chuki za udini kwa watanzania..fanatic mkubwa.

#MaendeleoHayanaChama
Sidhani kana anstahili ban,tuende Naye hivo,hata baadhi ya Waislam hawakubalini Naye!
Mengine anatusaidia Sana kujua (hata Kama hayana umuhimu Kitaifa) Kwa mfano tungejuaje kuwa Mama Maria Nyerere aliwahi kuuza mafuta ya Taa pale Kariakoo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…