Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #181
Mjamaa,1. Udini hautakufanya uonewe huruma.
2. Issue ya Udom hujui chochote, bora ukae kimya tu.
3. Funga bakuli lako, historia ya ukombozi wa TZ tunaijua pia.
Wewe unajua kipi mfano?
Mohamed kwani tunashindana? La hasha ni kuwekana sawa hoja zako nyingi zina ukakasi na si ajabu jukwaa limekuwa la moto.Jones...
Ikiwa tutakwenda kwa hoja ya chembelecho "udini," hutofika mbali na mimi nitakuwa nishakushinda.
Nitakuuliza wale watafiti waliowafuta Waislam kwenye historia ya TANU na ukitazama nyuma utakuta majina yao hawakusukumwa na udini kufanya hivyo?
Wale waliovunja EAMWS wakati wanajenga Chuo Kikuu hawakusukumwa na dini nk. nk.
Maryknoll kuwa walitoa tiketi sina taarifa hiyo lakini kwa kuwa wewe umesema nikakwambia itakuwa safari ya 1957 na nimesema hayo kwa ustaarabu kwa kuamini utakuwa unasema kweli.
Mohamed bado ana hoja nyingi za kujibu ila hatupi majibu ya kuridhisha ndio maana tunaona ni km anafanya ubabaishajiMMoohhaUSER=12431]Mohamed Said[/USER], hebu twende taratbu...
1. Bibi Titi Mohamed anafahamika katika historia ya Tanzania kama kiongozi wa Waislamu katika kada yoyote, au anatambulika kama mwana-siasa aliyepigania uhuru wa Tanganyika na Mwenyekiti wa UWT?
2. Huyo Gaudensia Kabaka alikuwepo kwenye sherere za kumuenzi Bibi Titi akiwa na kofia ya Utawa au akiwa na kofia ya Uenyekiti wa UWT?
3. Wale walioenda kumuona mtoto wa Bibi Titi, walikuwa ni viongozi wa Kiislamu au CCM?
4. Paliwahi kuwa na tuhuma kwamba Mwalimu Nyerere alifanya sahihi kumtia korokoroni Bibi Ti
5. Kwamba:-
Ni umoja upi huo ambao uliasisiwa na mama zenu?! Umoja wa Wanawake wa Kiislamu Tanzania, au Umoja wa Wanawake Tanzania?!
6. BInafsi, labda kwa kutokuwa na uelewa, sijapata kusikia Bibi Titi kuasisi Umoja wa Wanawake wa Kiislamu Tanzania bali nimesoma mara kadhaa kuhusu yeye na wenzake kuasisi Umoja wa Wanawake Tanzania! Sasa kama unazungumzia UWT, hivi hujisikii aibu kutoa kauli kama hiyo hapo juu?
Niwe mkweli Mzee Mohamed Said... nakuheshimu kutokana na umri wako na pia kutokana na maarifa yako lakini ukweli ni kwamba UNABOA!!!
Hivi unajisikiaje kila mada kuhusisha na udini?!
Ajabu yako sasa... mtoto wa Bibi Titi mwenyewe kafurahia ugeni lakini unakuja kuumia wewe na kuingiza udini! Ina maana unataka kusema wewe unamfahamu sana Bibi Titi, na una mahaba nae sana kuliko mtoto wake wa kumzaa?!
Badala ya mara kwa mara kuleta mada zinazoakisi udini, Hivi kama kweli una uchungu na imani yako, kwanini usitumie muda wako kuelimisha
Wazee wenu wewe na akina nani?
Mama zenu wewe na akina nani?
Kama hiyo "mama zetu" unamaanisha "mama wa Waislamu", tafadhali stop generalizing kwa sababu sio Waislamu wote wanapendezwa na huu ujinga wa mambo ya udini!!
Nilidhani ungesema hapo ndipo walipokuwa wakiimba qaswida, kusoma quran na maulidi kumuomba Mwenyezi Mungu!! Kumbe walikuwa wakiimba nyimbo za hamasa katika kupigania uhuru?!
Itoshe tu kusema kwamba, tumia elimu na maarifa yako kuhubiri umoja badala ya kuhubiri umimi na udini!! Sisi, na wengine miongoni mwetu ni Waislamu, tunamfahamu Bibi Titi kama miongoni mwa wapigani uhuru wa taifa hili!!
Tumefundishwa Bibi Titi alikuwa mwanamke shupavu katika harakati za kupigania uhuru, lakini HAKUNA popote tulipofundishwa alikuwa Mwanamke wa Kiislamu Shupavu katika kupigania Uislamu!!
And FYI, hata Madrasa nimesoma, tena Kurasini Dar es salam... mwendo mfupi tu kutoka Kariakoo lakini HATA SIKU MOJA hatukuwahi kufundishwa habari za Bibi Titi!!!
ACHA UDINI....
Asante Mzee Mohamed, je kinapatikana kwa soft copy au ni hard copy pekee, na kama ni hard copy pekee nakipata sehemu gani? niko nje ya Dar Es SalaamKilembwe,
Soma kitabu hicho hapo chini utaielewa historia ya John Okello.
Hakuwa shujaa wa mapinduzi.
Mashujaa viongozi walioweka mipango wote wametajwa katika kitabu hicho.
Okello katajwa kwa kazi maalum aliyopewa.
Alipomaliza kazi ile alifukuzwa kwa kuwa alikuwa bughdha.
Huyo aliyeshika kitabu jina lake ni Mohamed Omar Mkwawa au Tindo jina alilopewa na Mzee Karume.
Yeye ndiye aliyewavusha Wamakonde wakata mkonge kutoka Kipumbwi, Tanga kuingia Zanzibar kwa siri usku wa manane kwa kazi ya kuipigia kura ASP 1961 na 1964 kushiriki katika kuipindua serikali ya Mohamed Shamte.
View attachment 1986478
Kama unaamini wao walisukumwa na UDINI, haihalalishi nawe kuwa wao!! Busara ni kukemea UDINI, na sio kuendeleza UDINI eti kwa sababu zama hizo watu walitenda kwa kusukumwa na udini!!Nitakuuliza wale watafiti waliowafuta Waislam kwenye historia ya TANU na ukitazama nyuma utakuta majina yao hawakusukumwa na udini kufanya hivyo?
Wale waliovunja EAMWS na kuunda BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wakati wanajenga Chuo Kikuu hawakusukumwa na udini nk. nk.''
Nimesoma, na sijaona uhusiano wowote na mada inayoendelea hapa!!! Nilichokiona hapo ni maelezo yako ya kihistoria kuhusu uliyemtambulisha kama babu yako... Salum Abdallah, na Chinga Redrick Mchaulu!!Umesema twende taratibu unaniuliza ni wazee wangu gani waliopigania uhuru wa Tanganyika?
Nakuwekea hapo chini historia ya babu yangu Salum Abdallah ingia kwenye link hizo hapo chini:
SIKU BABU YANGU SALUM ABDALLAH ALIPOMKABILI FREDERICK MCHAURU KATIKA MGOMO WA WAFANYAKAZI WA TANGANYIKA RAILWAYS TABORA 1947
SIKU BABU YANGU SALUM ABDALLAH ALIPOMKABILI FREDRICK MCHAURU KATIKA MGOMO WA WAFANYAKAZI WA TANGANYIKA RAILWAYS TABORA 1947 Frederick ...mohamedsaidsalum.blogspot.com BABU YANGU SALUM ABDALLAH
Uncle Jei Jei: Tatizo Nyerere si muislam kwa dini wala mmanyema kwa kabila. Na kibaya zaidi, baba wa mwandishi huyu, a...mohamedsaidsalum.blogspot.com
STILL HAKUNA UHUSIANO WOWOTE...Tusimame hapa kwa kuwa umesema twende taratibu.
Hiyo picha hapo chini kulia ni Kassanga Tumbo na anefuata ni Salum Abdallah viongozi waasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) 1955 na chama hiki kilipigania uhuru wa Tanganyika bega kwa bega na TANU.
Mengine hayana maana kwa hiyo nimeyanyamazia.
View attachment 1986883
Anakimbilia kusema anaona "hazina maana"!!Mohamed bado ana hoja nyingi za kujibu ila hatupi majibu ya kuridhisha ndio maana tunaona ni km anafanya ubabaishaji
Hapo ndio tunapopishana na yeye. Tunahitaji hoja zote zijibiwe kwa weledi mkubwa tuhuma anazotoa ni nzito kiasi kwamba inabidi azijibu kulingana na uzito wake wala sio juu juu.Anakimbilia kusema anaona "hazina maana"!!
Asante Mzee Mohamed, je kinapatikana kwa soft copy au ni hard copy pekee, na kama ni hard copy pekee nakipata sehemu gani? niko nje ya Dar Es Salaam
Kile...Asante Mzee Mohamed, je kinapatikana kwa soft copy au ni hard copy pekee, na kama ni hard copy pekee nakipata sehemu gani? niko nje ya Dar Es Salaam
Hua nsmshangaa sana mzee wangu saidi kutaka kutuaminisha kua nyerere alikuja mjini akiwa hohehaheee [emoji1787][emoji1787][emoji1787].Huwa unatengeneza picha mbaya sana ya Nyerere kama mtu aliyesaidiwa sana na waislamu alipokuja Dar es Salaam. Kumbuka kuwa Nyerere alikuja Dar es Salaama siyo kama ombaomba, bali alikuja akiwa na digrii ya M.A kama mwalimu wa St Francis College. Kabla ya hapo alikuwa ameshafundisha St Mary's College huko Tabora (kwetu mimi na wewe); miaka hiyo ualimu ulikuwa ni kazi yenye hadhi sana. Asingejihusisha na siasa, Nyerere alikuwa ni mtu wa kuishi maisha mazuri tu wakati huo.
Mara zote unasema iwapo "wazee wetu" wa Dar es Salaama wasingemsaidia Nyerere lakini ulishasema wewe ni mtu wa Tabora, kwa hiyo uhusiano wako na watu wa dar es salaama ni dini zenu tu, na hapo ndipo tatizo lako lilipo.
Kl...Asante Mzee Mohamed, je kinapatikana kwa soft copy au ni hard copy pekee, na kama ni hard copy pekee nakipata sehemu gani? niko nje ya Dar Es Salaam
Chige,Kama unaamini wao walisukumwa na UDINI, haihalalishi nawe kuwa wao!! Busara ni kukemea UDINI, na sio kuendeleza UDINI eti kwa sababu zama hizo watu walitenda kwa kusukumwa na udini!!
Lakini kubwa zaidi, kama nilivyotangulia kusema hapo awali, Bibi Titi anatambulika kama mwanasiasa na sio kiongozi wa dini!! Bibi Titi anatambulika kama miongoni mwa waanzilishi wa UWT na sio mwanzalishi wa taasisi yoyote ya Kiislamu!!
As far as I know, hao waliojitokeza "leo hii: kumuenzi Bibi Titi sio Waislamu bali wana-CCM, na walienda pale kumwenzi Bibi Titi, ambae alikuwa mwanasiasa mwenzao!!
Hoja zako ningezimulia kidogo endapo hao walioenda kumuenzi wangekuwa ni Waislam, wanaoenda kumuenzi Mwislam mwenzao, halafu hapo akatokea Gaudensia Kabaka!!
Kinyume chake, walioenda ni wana-CCM!! Waliyeenda kumuenzi, anatambulika duniani kote kwa kupitia mrengo ule ule wa walioenda kumuenzi!! Ajabu, suala la wanasiasa kwenda kumuenzi mwanasiasa mwenzao unataka kuligeuza kuwa la kidini... wapi na wapi!!!
Nimesoma, na sijaona uhusiano wowote na mada inayoendelea hapa!!! Nilichokiona hapo ni maelezo yako ya kihistoria kuhusu uliyemtambulisha kama babu yako... Salum Abdallah, na Chinga Redrick Mchaulu!!
Sina shida na historia zako kwa sababu anayekerwa, na yeye aandike tu zake!! Shida yangu ni kuchanganya DINI na historia zako, na hata pasipo na historia husika!! Kama hii ya sasa, sioni uhusiano wowote wa wana-CCM kumuenzi Bibi Titi, halafu unaingiza udini as if huyo Bibi Titi alikuwa kiongozi wa Kiislamu!!
STILL HAKUNA UHUSIANO WOWOTE...
Unayanyamazia vipi uliyoyaona hayana na bado unatumia muda kutoa maelezo ambayo ni irrelevant?!
Ku-summarize hayo unayoona hayana maana, nieleze mantiki ya kuingiza udini kupitia suala la wanasiasa wa CCM kwenda kumuenzi wanayeamini ni mwenzao!!
Na kwa heshima na taadhima, na kuona hayana maana, basi ningekuomba UNIJIBU maswali yangu #1 hadi #6!! Muungwana akiombwa, sina shaka hutoa... naomba unijibu hayo maswali!!!
Mzee humu kuna watu hawako tayari kupokea maarifa. Unahangaika nao wengine wakati wanakokotoa vya kuandika wanagugo kwanza, ninakushauri wengine waache usiwajibu, hawa wenye maswali yenye tija na wanaokubali hoja kinzani wakaielew ndio tunaowataka hapaChige,
Jibu nimekupa jibu hulitaki.
Unakuwa Shylock na ratili yake ya nyama anayodai kwa Bassanio.
Shakespeare "Merchant of Venice."
Umesoma historia ya babu yangu aliyepigania uhuru wa Tanganyika.
Babu yangu kaweka rekodi ya kihistoria ambayo hadi leo hajavunjwa nadhani Afrika nzima.
Kaongoza migomo mitatu 1947, 1949 na 1960 dhidi ya dhulma za Waingereza.
Mchochezi.
Hizi ni General Strikes.
Mgomo wa 1960 ndilo taji lenyewe ulidumu siku 82.
Unapata tabu kutambua achievement hizi na unasema ni, "rrelevant."
Lazima niheshimu fikra zako lakini kwangu nakutia kwenye mizani na kupata uzito wako.
Vyuo Vikuu wananisukuma niandike historia ya Salum Abdallah babu yangu.
Wanataka kujua kwa miezi mitatu wafanyakazi walikuwa wanajikimu vipi?
Nawagusia kuwa East Germany walitoa msaada wa fedha kwa TRAU halikadhalika chama cha wafanyakazi wa reli Uingereza.
Wananisukuma kila uchao niwape mswada wachape kitabu.
Wewe huoni chochote hapo wala hushangai kuwa babu yangu hajatajwa katika Labour politics za Tanganyika.
Haya ndiyo maswali nikijadiliana ba walimu wangu wa historia Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.
Unataka mimi nikujibu maswali yako.
Hapana.
Mimi niko darasani hapa nasomesha historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
Jipime uwezo wako.
Je, ulikuwa unamjua Salum Abdallah?
Kwanini huyu mzee asiizungumizie hii historia ya Okello au kwakua Okello sio mvaa kanzu.Vyovyote vile naamini kuna mapungufu mengi sana katika uandishi wa historia ya nchi ya Tanganyika na baadae Tanzania, mfano mwingine mzuri, shujaa wa mapinduzi ya Zanzibar ni yule Mganda Okello lakini leo historia imejaa na kumtukuza Mzee Karume!
Jamii zina jielezea zenyewe hakuna haja ya pepa wala nini hayo ni maandiko yako binafs na ibinafsi wako wa kidini..ila ukweli uko wazi jamii za pwani na za bara zipi zinaongoza kutilia maanani elimu?Ruta...
Bahati mbaya hujui historia ya Waislam na juhudi zao katika elimu ndiyo maana unasema Waislam hatuthamini elimu.
Ni paper ndefu inataka ustahamilivu lakini ikiwa unataka kujua ukweli soma yote:
Huyu tumpe jina la mzee kilizi..analialia anataka aonewe huruma na vi historia vyake uchwara..basi achuke nchi aifanye Islamic ili moyo wake ufurahi..fanatics1. Udini hautakufanya uonewe huruma.
2. Issue ya Udom hujui chochote, bora ukae kimya tu.
3. Funga bakuli lako, historia ya ukombozi wa TZ tunaijua pia.
Huyu mzee anataka kutuharibia amani ya nchi..apigwe ban ya maisha humu..asilete hoja zake potofu za kutaka kupandikiza chuki za udini kwa watanzania..fanatic mkubwa.Mohamed Said, hebu twende taratbu...
1. Bibi Titi Mohamed anafahamika katika historia ya Tanzania kama kiongozi wa Waislamu katika kada yoyote, au anatambulika kama mwana-siasa aliyepigania uhuru wa Tanganyika na Mwenyekiti wa UWT?
2. Huyo Gaudensia Kabaka alikuwepo kwenye sherere za kumuenzi Bibi Titi akiwa na kofia ya Utawa au akiwa na kofia ya Uenyekiti wa UWT?
3. Wale walioenda kumuona mtoto wa Bibi Titi, walikuwa ni viongozi wa Kiislamu au CCM?
4. Paliwahi kuwa na tuhuma kwamba Mwalimu Nyerere alifanya sahihi kumtia korokoroni Bibi Ti
5. Kwamba:-
Ni umoja upi huo ambao uliasisiwa na mama zenu?! Umoja wa Wanawake wa Kiislamu Tanzania, au Umoja wa Wanawake Tanzania?!
6. BInafsi, labda kwa kutokuwa na uelewa, sijapata kusikia Bibi Titi kuasisi Umoja wa Wanawake wa Kiislamu Tanzania bali nimesoma mara kadhaa kuhusu yeye na wenzake kuasisi Umoja wa Wanawake Tanzania! Sasa kama unazungumzia UWT, hivi hujisikii aibu kutoa kauli kama hiyo hapo juu?
Niwe mkweli Mzee Mohamed Said... nakuheshimu kutokana na umri wako na pia kutokana na maarifa yako lakini ukweli ni kwamba UNABOA!!!
Hivi unajisikiaje kila mada kuhusisha na udini?!
Ajabu yako sasa... mtoto wa Bibi Titi mwenyewe kafurahia ugeni lakini unakuja kuumia wewe na kuingiza udini! Ina maana unataka kusema wewe unamfahamu sana Bibi Titi, na una mahaba nae sana kuliko mtoto wake wa kumzaa?!
Badala ya mara kwa mara kuleta mada zinazoakisi udini, Hivi kama kweli una uchungu na imani yako, kwanini usitumie muda wako kuelimisha
Wazee wenu wewe na akina nani?
Mama zenu wewe na akina nani?
Kama hiyo "mama zetu" unamaanisha "mama wa Waislamu", tafadhali stop generalizing kwa sababu sio Waislamu wote wanapendezwa na huu ujinga wa mambo ya udini!!
Nilidhani ungesema hapo ndipo walipokuwa wakiimba qaswida, kusoma quran na maulidi kumuomba Mwenyezi Mungu!! Kumbe walikuwa wakiimba nyimbo za hamasa katika kupigania uhuru?!
Itoshe tu kusema kwamba, tumia elimu na maarifa yako kuhubiri umoja badala ya kuhubiri umimi na udini!! Sisi, na wengine miongoni mwetu ni Waislamu, tunamfahamu Bibi Titi kama miongoni mwa wapigani uhuru wa taifa hili!!
Tumefundishwa Bibi Titi alikuwa mwanamke shupavu katika harakati za kupigania uhuru, lakini HAKUNA popote tulipofundishwa alikuwa Mwanamke wa Kiislamu Shupavu katika kupigania Uislamu!!
And FYI, hata Madrasa nimesoma, tena Kurasini Dar es salam... mwendo mfupi tu kutoka Kariakoo lakini HATA SIKU MOJA hatukuwahi kufundishwa habari za Bibi Titi!!!
ACHA UDINI....
Sidhani kana anstahili ban,tuende Naye hivo,hata baadhi ya Waislam hawakubalini Naye!Huyu mzee anataka kutuharibia amani ya nchi..apigwe ban ya maisha humu..asilete hoja zake potofu za kutaka kupandikiza chuki za udini kwa watanzania..fanatic mkubwa.
#MaendeleoHayanaChama