GEITA: Wananchi wavamia kituo Cha Polisi, wawili wauawa

GEITA: Wananchi wavamia kituo Cha Polisi, wawili wauawa

Taarifa ya Polisi inaonyesha hao ni wazazi, je ni kweli au si kweli?
Kuhusu watu wangapi katika matukio hayo wengi huwa wanaenda na upepo tu pasipo kuujua ukweli.
Wanaweza wakaanzisha wawili lakini mamia wakafuata mkumbo. Kwani wezi anavyopigwa mitaani watu wote huwa wanajua hata kilichoibwa au aliyeibiwa? Si hufuata tu zile kelele za tuhuma
Mimi naamini Raia wewe nawe amini police hukatazwi
 
Vijana wawili wamefariki dunia hii leo Septemba 11, 2024 baada ya wananchi 800 kuvamia na kufanya vurugu katika kituo cha polisi Lulembela wilayani Mbogwe mkoani Geita vurugu zilizoanzia katika eneo la mnada wa Lulembela baada ya watu wawili kuonekana wakiwa wamebeba watoto wawili na wananchi waliokuwa katika mnada huo kuwahisi kuwa ni wezi wa watoto na kuanza kuwashambuilia, ndipo akatokea Mtendaji wa Kata akawabeba kwenye pikipiki na kuwakimbiza katika kituo cha Polisi Lulembela.

Ambapo baada ya watu hao kufikishwa katika kituo cha polisi, wananchi hao walifika katika kituo hicho na kuwataka askari polisi wawakabidhi watuhumiwa hao ili wawaue na Askari walijaribu kuwaelimisha na kuwaeleza ni kosa na si vizuri kujichukulia sheria mkononi lakini walikaidi na baada ya askari kuona hali hiyo ya kuhatarisha maisha ya watu na mali za serikali walitumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya watu hao na iliposhindikana walitumia silaha za moto kwa kupiga risasi juu ili watu hao watawanyike

"Mbali na kushambulia kituo hicho kwa mawe na kutaka kuingia kwa nguvu ndani ya kituo hicho, wananchi hao walichoma moto gari moja lenye namba za usajili T.440 ATW aina ya Toyota Cardina lililokuwa limeegeshwa nje ya kituo hicho na katika vurugu hizo watu wawili wamepoteza maisha, mmoja ni mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 18 hadi 20 na wa pili ni msichana aitwaye Teresia John mwenye umri wa miaka 18, mwanafunzi wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Lulembela ambaye nyumba yao inatazamana na kituo hicho cha Polisi," imeeleza taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa, "Hata hivyo, ilibainika kuwa watu waliokuwa wamebeba watoto hao ni Emanuel John (33) mkazi wa Kigamboni Lulembela ambaye alikuwa amembeba mtoto wake aitwaye Ikram Emanuel mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi kumi na moja na wa pili anaitwa Ng'amba Leonard (24) ambaye alikuwa amembeba mtoto aitwaye John Emanuel mwenye umri wa miaka miwili na miezi nane, Mama wa watoto hao aitwaye Rachel Luhende (22) amethibitisha kuwa watoto hao ni wakwake na walikuwa kwa wifi yake ambapo baba yao mzazi na mjomba wao walikwenda kuwachukua,".

#EastAfricaRadio
Polisi hawana weredi na kazi yao. Their souls RIP.
 
Wengine tunajicho pevu sana.

Kuna nadharia mbaya juu ya polisi kwa wananchi. Polisi jitafakalini ni kweli mna silaha za moto ila nguvu ya raia hawajawahi kuogopa hizo silaha!

kule Mganza-Chato kituo kilichomwa mwaka jana leo na sababu kuu ilikuwa ni polisi kukamata na kutesa kijana hadi kupelekea umauti. Kwanini anafanya hivi wakati mnajua sheria zipo?

Jukumu lenu ni kulinda usalama wa raia na mali zao na sio kutoa HUKUMU.

Hii imepelekea jamii imekosa imani na polisi sio jamii tu hadi familia zenu hazina upendo kabisa.
UPolisi umekuwa kama kazi ya shetani? Badilikeni dunia tuliyopo usatarabu kwanza ndio maana kuna sheria za Nchi.

Polisi mkishupaza shingo hakuna atakayebaki salama . Mtaua badaye mtauana.
 
Ni suara la muda tu!! Utasikia hao marehemu walijinyonga wenyewe. Chura endelea kuziba mackio yako soon watanganyika wata ya zibua tu.wananchi 800.
All the best.
 
Watu 800 hawawezi kukosea
Sio kweli.

Watu ni wajinga sana.

Kuna uvumi kuwa kuna watu wanateka watoto ili kutoa figo.
Hapa nilipo sungusungu wamepuliza kipyenga na kutoa taarifa kuwa kuna watoto wawili wametekwa, ili hali, hakuna familia waliopotelewa na mtoto.

Kwa hiyo, kuna uwezekano mkubwa hizi taarifa ni uvumi tu. (rumours)
 
Ukute hao waliouwawa hawakuwa na hatia yoyote ni kama yale ya Akwelina 💔
Ndo uhalisia huyo binti alieuwawa nyumba yao ipo karibu na kituo kwahiyo probably alikua kwenye perimeter ya nyumba yao au alisogea kituoni kuona kuna nini.

Unajua sisi wananchi kuna mambo huwa hatuelewi pengine ni uelewa mdogo wa sheria, katika kujichukulia sheria mkononi kuna mazingira polisi hata akikuua hataulizwa maana kuna mazingira sheria imemruhusu polisi afanye hivyo mfano wa sheria hiyo ni Sect 21(2) CPA cap 20 RE 2022 hapo anaruhusiwa kutumia nguvu na ikiwezekana kuua kwaajili ya kutetea uhai wake au uhai wa mtu mwingine.

Sasa ni vyema tukaepuka mazingira flani flani ya sisi kuonekana ndo tulikua wahalifu, juzi tu hapa aliuwawa Mandojo kwenye hizi hizi Mob justice, leo tena mtu anataka auwawe kisa kabeba mtoto wake
 
Acha ujinga,Unategemea Serikali ikili kuwa walikuwa wanaiba Watoto huku upepo ulivyo sasa nchi nzima inawalaumu Polisi hawafanyi kazi watoto wanaibiwa.
Polish na Serikali hapo wanafunika kombe mwanaharamu apite
huna akili polisi huwa hakili mtu kuwa na kosa ama hapana

mahakama ndo huamua, kuna majirani wanao mfahamu huyo mama kama hao n watoto wake ama hapana

hatuhitaji polisi ndio aseme hao ni watoto wa hao jamaa ama hapana

huna akili kama ngosha wenzako unaongozwa na hisia tu
 
Ndio maana wazungu wanadharau ngozi nyeusi, wangefanya hata utafiti wa chap chap kabla ya kuamua. "No research no right to speak ".
 
Back
Top Bottom